Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Tanzania Kununua JET mpya lakini....

>> Wednesday, August 23, 2006

Naona inasemekana ile JET ya Raisi ilionunuliwa baada ya malumbano makali, imeonekana kuwa inasaidi kubana matumizi ya misafara ya Raisi. Hivyo imependekezwa inunuliwe Jet nyingine ili kuzidi kubana matumizi ya misafara ya Raisi.Habari hii hapa

Nisingependa kuiingilia habari hii ya ndege bado lakini ilinizingua kuona msafara unaobana matumizi ya nchi uliotokea kiwanja cha ndege kumuaga Raisi.
Dr Ali Mohamed Shein ,waziri mkuu Edward Lowassa, waziri wa ulinzi, Prof Juma Kapuya, waziri wa elimu, Prof Peter Msolla, waziri wa madini, Dr Ibrahim Msabaha, Waziri wa maji, Stephen Wassira, Utalii, Anthony Diallo , waziri wa nchi katika ofisi ya Raisi ,Kingunge-Ngombale Mwiru na kadhalika kadhaa. Hii imenikumbusha kile kipindi tulichokuwa tunatolewa mashuleni kwenda kujipanga Mabarabarani kumshangilia Raisi akipita. Labda walikuwa na kamkutano pale lakini ninamashaka na hili. Nahisi inawezekana lazima umchekee Raisi iliasije akahisi huko kwenye kambi lake kama huji kumchekea. Safari Njema Raisi!

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP