Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

IMANI YAKO ITAKUPONYA!UKIWA VUGUVUGU HUTA URITHI UFALME WA...

>> Friday, August 31, 2007

Kuna dini fulani zilinifundisha kitu muhimu sana kwenye maisha.
Ziliniambia kuwa karibu kila kitu kinahitaji sana na kinauhusiano sana na imani yako katika kitu hicho.

  • Ukiamini umekula chakula kichafu hotelini baada ya kugundua msalani kuchafu na ni pembeni ya jiko walilopikia na waliko wafadhili wale nzi wahitajio chakula kama wewe, unaweza kuharisha wakati huna vijidudu vilivyokududua.

Nilijifunza kuwa ukiamini kuwa kuna......... na ndio jibu , basi ni mpaka uamini kikwelikweli kuwa kalekadude ni ........ ndio katakuwa jibu.

Niliambiwa...
  • Imani yako ndio itakuponya.
Inamaana, ukiwa na imani haba, hata ukaokoka vipi, lakini kama hujaamini kisawasawa, jehanamu ilo karibu na ndio chobisi yako ukianza kinamna.
  • Nikaambiwa kuwa ni lazima uwepo ndani ya hekalu, au ,ujitoe kabisa chumbani, kwa sababu , mguu nnje-ndani = na uko nje.
DUH!
Nisikufiche!
Haka kakitu kako mawazoni sasa hivi.
Halafu nakaamini kikwelikweli......
  • Naamini ukitaka kale kakitu na kama unaamini kabisa nilazima ukapate kale ka....
  • Naamini kale kakitu utakapata hata kwa njia uifikiriayo sasa hivi, na sio ile ya mkato aliyokutonya mshikaji kuwa........
DUH!
Kumbe mshikaji ni wewe!
Nong'oneza tu njia ya mkato kama ni halali!

  1. Lakini , njia ndefu inafaraja zake.Inakusababishia kujua na kukasikilizia kale ka-utamu kunoga kinamna fulani.

Utakua unajua kwanini na kwa njia gani ambayo umekatolea jasho kukapata kale kakitu bila mjomba kukasaidia au yule mwingine kukupunguzia utandu kwa kudai kuwa; Simon bila mimi asinge......

Usiniulize lakini kama kale kakitu nimekapata tayari au bado!:-)
DUhh!
Najua kuna watu wana haraka sana hata katika..........!

DUH!
Sasaaa.........

Si imani yako itakuokoa?
Si imani yako itakuponza?
Swali :
Imani yako inaku.................?


Pata....

Read more...

UKIWA MVIVU KULIMA HALAFU UNASIKIA NJAA HARAKA!

Kama husikii njaa , huhitaji chakula!
Tatizo ni kama mvivu kutafuta chakula halafu unasikia njaa haraka!
Swali:

  • Si kuna utamu wa kula vya bure ndio maana watu kibao wanapenda vya bure?
  • Hivi kuna kitu cha bure?
Ijumaa njema!
Msikilize Tone Loc utagundua hata ukitumia kale kakitu unaweza kutoka bure....
JICHUNGE!

Read more...

Wachina wana akili!Waafrika je?

>> Thursday, August 30, 2007

Katika kipindi hiki ambacho China inazidi kuwa na nguvu!
Katika kipindi hiki ambacho wachina wameingia kisawasawa Afrika mpaka kwenye biashara za umachinga!
Katika kipindi hiki ambacho unasikia mpaka ni jinsi gani kila kona ya dunia inavyokiri kuwa Wachina wana akili....!

Ni rahisi kusahau kuwa cha zaidi wakifanyacho ni kugundua kasehemu waaminiko kana utamu na kukalamba kisawasawa.
Swali:

  • Si ni ukweli pamoja na watu kuzidiana akili(kama hicho kitu kipo) ,bado wengi tuwaitao majiniasi, siri yao kubwa ni ujuzi wao wakugundua pointi yenye utamu na kugundua jinsi ya kuilamba kwa nguvu zote?

  • Lakini si ni ukweli si kazi ngumu kugundua pointi yenye utamu karibu kwa mtu yeyote?

  • Tatizo si ni jinsi tu ya kugundua jinsi ya kuilamba nukta yenye utamu?

Niligongana na watu waliokuwa wanashabikia kuwa Wachina wanaakili sana.
Sipingi!
Nachojiuliza ...
Swali:
Kwani nani hana akili?

Ndio , ukifuatilia historia utagundua kuwa ni Wachina waligundua karatasi, poda za risasi, hata.....
Ndio , sasa hivi uchumi wao unakua kwa kasi ya ajabu. Inasemekana moja ya kazi ya wachumi wao kuu ni kupunguza kasi ya ukuaji wa uchumi ili kuweza kuudhibiti ukuaji.Kitu ambacho sisi katika nchi za Afrika tunajaribu kukuza uchumi wetu na hata kama haukui kisawasawa viongozi wetu hawakawii kutuambia uchumi unapaa.

Lakini katika historia pia utakuta jamii ya kichina , kizungu , na kiafrika vyote vilifanya makosa na mazuri yake.

Wazungu walistukia utamu uko wapi na wakaulamba kwa nguvu zote!
Wachina walishaustukia zamani lakini wakachemsha mpaka Wazungu wakawazidi na kuwatawala.

Swali:
  • Kama Mchina aligundua bunduki, unafikiri ilikuwaje Mzungu akaja kuwatawala kwa kutumia bunduki aliyogundua Mchina?
  • Si sisi waafrika wengi tulishindwa kwa Wazungu kutokana na wao kusaidiwa na kuwa na bunduki?
Nachojaribu kusema ni........

  1. Ikiwa Mchina aligundua bunduki na kuja kutawaliwa na mtu aliyejifunza kwa Mchina bunduki ni nini......

  1. Ikiwa Mchina aligundua karatasi.....na mpaka sasa anajifunza mambo mengi tu mengine watu wengine walioandika kwenye karatasi......

Naamini kuwa agunduaye si lazima afaidike zaidi ya aliyekopi jinsi ya kulamba.
Tatizo ni kwamba kila nukta B yenye utamu si lazima ilambwe kama nukta A.
AU?

Chakujiuliza:
  • Inakuwaje mchina anaweza kutoka kwao na kuwa machinga Afrika na kufanya umachinga kama wamachinga tulivyowazoea?

  • Je,kastukia kuna kautamu na kastukia kuwa wakalambavyo waafrika ni sawa ila yeye anaongeza nguvu tu?
  • Kwani sisi Waafrika tunakosea wapi?
Katika shule zote nilizotembelea na kusomea na mataifa karibu yote duniani, nilichogundua ni kwamba, hakuna hata moja huwezi kukuta Waafrika ambao ndio kiboko hapo darasani.

Katika kuongea na kujadiliana na watu duniani , ni rahisi kukutana na Waafrika wenye uwezo mkubwa wakufikiri na kufanya mambo na wako kila kona duniani wakionyesha maringo yao dingiridingiri mpaka chini.

Sasaaa........

Hivi pamoja na yote haya.......
Pamoja na ukweli tunajua utamu uko wapi......
  • Je, ni jinsi ya kulamba bado hatujajua , au ni spidi ya kulamba tuitumiayo ni ndogo kiasi cha kufanya tujikute tunaambulia kijisehemu kidogo tu cha pipi?
Hebu tujikumbushe Wachina......


Duh!

Basi bwana ngojea niache!

SIKU Njema!

Namuacha SUGAR DADDY akiendeleza kufagilia SOCA

Read more...

Si Umestukia Mungu Haongei na Miungu Haiongei Moja kwa Moja na Mtu wa Kawaida?

>> Wednesday, August 29, 2007

Dini karibu zote zimehitaji utashi wa mtu fulani na akili za mtu fulani kuwa kiunganishi cha watu na Mungu au Miungu yao.

Lakini....

Swali:
Imekuwaje Mungu na hii Miungu haijifungui kwa binadamu wote kirahisi mpaka watokee binadamu wengine kuwaelezea wengine maswala muhimu ya wokovu wa mioyo yao?

Lakini.....

  • Umestukia kuwa waletao dini chobisi na watambulikao kuwa ndio wanajua maswala haya, ndio wale pia wavaao vizuri, nyumba nzuri , wanakula vizuri kuliko wale watu wawalishao neno la Mungu au sentensi za Miungu?
Nakubali kuwa si miaka mingi sana iliyopita ilikuwa ni kawaida kutojua kusoma na kuandika. Ni kikundi kidogo cha waliojua kusoma na kuandika kilichopata maswala kutoka katika vitabu fulani na kutuletea katika jamii. Kikundi hiki kidogo kilitafsiri Mungu anasema nini, kutokana na ugumu wa kumuelewa Mungu na ugumu wa kuielewa hii Miungu.

Lakini...
Kumbuka kuna kikundi pia ambacho hakikuhitaji kujua kusoma wala kuandika kukupatia maswala ya Miungu au Mungu na kukusababisha ulete wale mbuzi na kuku kwa ajili ya kustawisha mihogo yako pale shambani, au hata kustawisha imani yako.
DUH!
Swali:
Inakuaje wengine wanajua mpaka siri za Mwenyezi wakati wengine hatujui?

Kweli labda kila mtu anakipaji chake cha kuelewa mambo fulani. Na Labda Mungu na Miungu pia huongea na watu fulani moja kwa moja kutokana na tofauti zao.
Swali:
Si unakumbuka kusali na kuswali eeh?
Hivi si tunaamini ni Mungu na Miungu hii ndio iliyotuumba wote ?

Nisikutishe lakini !
Labda wale wakutafsiriao kuhusu imani yako wanajua kuliko wewe kutokana na uzoefu na kuijua dini kuliko wewe.Labda wao wanaimani zaidi yako hivyo wanapata maono zaidi yako wewe na mimi.

DONDOO:
ushawahi kustukia kuwa asemekanaye ni wakwanza kustukia Mungu au Miungu , mara nyingi hutumia maneno kama....
  • Alioteshwa ndoto...
  • Alishukiwa....
  • Alitokewa na malaika
  • Ali....

Sijui kwanini lakini wanashukiwa watu mmoja mmoja katika dunia ya mamilioni.
DUH!
Ngoja niache haya maswala ya Mungu na Miungu!
Labda ni Mungu na hii miungu ndio ijuayo zaidi haya maswala!
Nakuachia wewe mwenyewe na ...
  • Shehe wako
  • Padre wako
  • Mchungaji wako
  • Bi kidude wako
  • Mzee Mghosi wako ................mwenyewe, haya maswala !

Turudi katika maswala ya dunia.......
Soca!
Ngojea nimuachie Machel Montano aseme..

Si unamkumbua Machel Montano alivyokuwa mtoto? Hebu furahi naye ndani ya SOCA


Read more...

Baada ya Kugundua Wakubwa Hutukana!

Utoto nishai!
Inahitajika ukue ilikugundua baadhi ya maswala ambayo wakubwa wanafanya na wakubwa husemekana kuwa ndio wanayajua.

Nakumbuka nilivyokuwa mtoto nilizani kuwa baba yangu ananguvu kuliko watu wengine wote.Niliamini kabisa anaweza kupiga watu wengine wote.Navyosimuliwa ni kwamba, nilipohudhuria msiba fulani wakati mdogo , nikiwa na familia, nilichoelewa ilikuwa ni kwamba baba kawapiga wote waliokuwa wanalia pale msibani.

Elezo hilo ni rahisi kulizungumzia kwa kastori kama hapo juu, lakini ukilichunguza....

  • Utagundua , mimi kama mtoto, nilikuwa tayari nimeshaelewa kuwa moja ya kazi ya baba ni kuchapa. Nafikiri pia hili lilitokana na kuamini kupiga ilikuwa sio kazi ya mama kwa kuwa mama yangu ni mpole asiyependelea hata kufinya ukiharibu mambo.Kwa busara yangu ya kitoto nishastukia kazi mojawapo ya baba.
  • Utagundua kuwa kizazi kikubwa tuishicho, kimekuwa katika mazingira ambayo mara nyingi kipigo na sababu ya kipigo havikuwa rahisi kuhusishwa.Tulikuwa tukijua tu nani anayetoa kipigo hata kama kosa si wakati wote tulilijua, na labda tungelijua kitu fulani ni kosa tusingefanya hicho kitu hata bila kuchapwa.
Swali:
Unafikiriaje maswala ya kuchapwa?
Mbona tumekuwa vizuri tu baada ya kuchapwa sana , au umedhurika?
Lakini hawa watoto wakuao sasa bila kuchapwa je?

Ukubwa nishai!
Unaamka tu siku moja unastukia eti wewe mkubwa.
Kama Mtized unastukia unaanza kupewashikamoo, mara jina linaanza kubadilika, baadhi ya watu wanaanza kukuita Mzee!

DUH!

Cha ajabu, si kweli wote waitwao mzee au wale wakubwa kwa umri na kwa... maana yake wamestukia ukubwa wao.

Na kwa bahati mbaya.....
  • Ukubwa haumaanishi busara.
  • Busara kwa mmoja inaweza ikawa ujinga kwa mwingine.
  • Busara mara nyingine inatokana na ufahamu wa mambo.Hii inamaana kama hujui unaweza ukatumia busara kufanya ujinga.(si unakumbuka maswala ya wenye busara kugawa almasi kwa malipo ya pipi?)

Lakini.....
Kuna ambao wamekulia mazingira ambayo ilikuwa kawaida kusikia wakubwa wakiongea kila aina la jambo.Kuna waliotukanwa tokea utotoni. Na tupo ambao tulifikiri wakubwa wanajua kila jambo kiasi kwamba waliyosema ndio ilikuwa ukweli.

DUH !
Sentensi mbili:

  • Zamani ilikuwa kidogo maswala mengine yamefichika. Wakubwa waliweza kusikiliza mpaka nyimbo ambazo kwa enzi hizo ilikuwa ni matusi , bila ya mtoto kustukia wimbo unasema nini. Kulikuwa hakuna mitandao vyanzo vya habari vingi ambavyo utaibia na kustukia mtoto anazaliwaje. Unakua ukiamini kunandege kamleta au mama kaenda kumnunua kutoka duka fulani yule mtoto.
  • Siku hizi bado kuna mambo mengi yamefichika kwa wengi. Wakubwa wanaweza kusikiliza mpaka nyimbo ambazo kwa enzi hizi ni matusi, bila ya mtoto kustukia wimbo unasema nini. Kuna mitandao na vyanzo vingi vya habari ambavyo utaibia na kutostukia mtoto anazaliwaje. Unakua ukiamini kunandege kamleta au mama kaenda kumnunua kutoka duka fulani yule mtoto.
Lakini labda niseme....
Kwa watu fulani ambao ni wengi kabisa, na ambao wanaweza kustukia na kugeuza mambo...

Ni vigumu kuwaficha mambo.
Mambo yako siku hizi nje nje sana.
Matusi yako wazi mno.
Cha ajabu ni kwamba tutukanwao hatuchukii tutukanwavyo matusi ya kikweli.

Mfano wa matusi yatuudhio ni :
  • Meno kama ngiri wewe!
Mfano wa matusi tutukanwayo kila siku watu wazima na akili zetu ni kama:
  • Mimi mwanasiasa nawaletea ari mpya na nguvu mpya!
  • Uchumi wa nchi unapaa!Wakati tunaona wananchi wakizama.
  • Salamu ; Habari za nyumbani! Jibu:Nzuri tu !Wakati unajua mambo nishai!
Swali:
Hivi mtu akiwa anakufanya wewe mjinga kila siku, hilo si tusi?

W
akubwa hutukana na wadogo huiga hata kabla ya kujua mkubwa alilosema ni tusi.
Nasikitika kuwa sina uhakika kuwa matusi waliyokuwa wanatukana wakubwa zamani kwa mafumbo ni bora kuliko siku hizi tutukanwapo hadharani hata bila aibu.
Swali:
Tunavyokua na kujua pia wakubwa katika angazao huongea matusi , inamaana nasi tukikua tutukane?
SIKU NJEMA!
Mpate Lord Kitchener akikupa kitu DR KITCH



Read more...

Demokrasia ya Bongo!:-(

>> Sunday, August 26, 2007

Wakubwa wana haki!
Wanyonge wanatafuta haki ingawa hakuna uhakika kuwa mnyonge anapata haki.

Lakini.....
Unakumbuka kuwa wakubwa waliwahi kuwa wadogo wasio na haki hata ya kukaa sana usiku au kujichanganya katika kijiwe bila kufukuzwa?
Swali:

  • Hivi historia inatufunza nini?
  • Hivi si bado yule dogo unamfukuza kidizaini?
  • Ukipata nguvu utaruhusu kusogelewa?
  • Wakati unanguvu unasogelewa?

DUH!

Mpate Lagbaja


Read more...

KESHO!

>> Friday, August 24, 2007

Kabla sijasema...
Mpate Mighty Sparrow


Umeanza Juzi eeh?
Lakini hivi unakumbuka kuwa hizi juzi ni siku tu?
Au..

  • Jana
  • leo
  • Kesho
  • Mtondogoo
Si zote siku tuuu?

Tatizo linakuja pale kuwa kila siku ifikapo , inamaana siku moja ya maisha yetu tukiwa hai imepita:-(

Sasaaa...
Jana nahisi uliipitisha vizuri.
mimi duh!
Ngojea lakini nikupe picha za siku ya kumuaga Allen....
Lakini nimestukia kunawatu dunia ya chobisi fulani mtakuwa mnawaza kwanini kuna picha fulani naziweka wakati hazioani na juzi wala jana yenu.
Duh!
Vumilia basi wakati wengine tuki......

Tulia na Chris Isaak
Nimetumia Blinds katika Filmloop, kwa hiyo subiria pazia lipite upate picha inayofuata.....


Powered by www.myfabrik.com

Uncle/Allen konekshen
Powered by www.myfabrik.com

Aliko/Abdul konekshen
Powered by www.myfabrik.com

T.I/Chacha/David konekshen. Byamungu siunaona mpaka T.I hakunitenga, wewe tu ndio unaendeleza kunitenga:-)
Powered by www.myfabrik.com

Simon Kitururu konekishe...
DUH! najua nawazingua watu fulani ....!Ngojea nnichanganye basi washikaji zaidi waliokuwepo.Usisikitike usipotekea lakini.Tuko Pamoja
Powered by www.myfabrik.com

Washikaji zangu kisawasawa. Deo na Said sijui mlipotelea wapi lakini:-)!
SIKU NJEMA!
Basi wadau zangu , ngojea ni waache na Jack Radics akiwa na Chaka Demus na Pliers

Read more...

MWANAMKE HUWEZA KUKOJOA KASIMAMA!

>> Thursday, August 23, 2007

Wanaume huweza kukojoa wamechuchumaa.
Tatizo ni binadamu waliofanya liwe tatizo hili swala la staili ya kukojoa!
Duh!
Inasemekana wanawake wakikojoa wamesimama ni rahisi kujikojolea.

Lakini.....

  • Ukifuatilia swala , utagundua kuwa staili ya kukojoa si muhimu kama uwezo mzima wa kukojoa
Ukishindwa kukojoa ni kasheshe.
Na ni jamii tu imeamua kuwa kujikojolea ni nishai!
Nahisi kama mikojo ingekuwa inanukia pafyumu, marashi yanukiayo kama harufu ya mikojo tuijuayo hivi sasa, yangekuwa ndio ujanja kununua.

Sasaa....moja ya nachomaanisha katika insha hii ya mikojo.....

Enzi zile za mababu, uwe mwanamume usiye na misuli fulani yakuwindia,kulima, ku... staili yako ya kuleta chakula nyumbani isingefanana na ya mwenye misuli na kufua kama simba.

Karne hii , huwezi ukamdharau asiye na misuli , kwani anaweza kuwa anafikisha msosi nyumbani kuliko weye mwenye misuli kama simba.
Mwanamke na mwanamume, hawatofautiani sana katika kufikisha matakwa ya kimaisha chobisi.
Mwanamume na Mwanamke wote hukojoa , hata kama ni kwa staili tofauti.

Wewe kama unachuchumaa, unakaa, au unasimama katika kukojoa haina maaana sana.
Cha muhimu unakojoa!
  • Fanya kwa staili yako yoyote , ili mradi unapata upatacho kihalali.
AU?
Namuachia Jack Radics

Read more...

MAANDAZI YAPO, UNAHAMU YA KUONJA VITUMBUA?

Kila kitu hukinaisha!
Ukitamanicho jua kunamtu kimemkinai!
Si unajua kinaa cha:

  • Kula vitumbua kila siku!
  • Kwenda kanisani kila mara!
  • Ugali kwa maharage kila siku!
  • Kula kuku kila siku!
  • Kwenda chooni kila siku!
  • Kunywa tule tubia kila siku!
  • Kupigia chabo kale kakitu !
  • Ku...........nk.
Swali:
Si unajua kwenda haja, pamoja na kuwa ni lazima kama umekula, kuna kastarehe kake?

K
wa binadamu ni rahisi kuona kautamu ni kakijani zaidi katika kisamvu kilichopo sufuria jingine. Maswala ya kutaka kujua , kuelewa uzuri wa vyetu kwa kuona au kuonja vya wenzetu, pamoja na kashule tupatako, yanatuponza mara nyingi.

Lakini....

  • Wewe ungejuaje kuwa Zubeda au Abdallah wako ni mzuri , ikiwa hakuna Anna au Wilson wa kufananisha kakitu?

  • Ungejuaje utamu wa chai yenye sukari kama hakuna chai isiyo na sukari?
Mimi sipendi sana maandazi kama vitumbua .

Sasaaaa.....
UKWELI, na si ni kaBUSARA fulani, kama sio ujanja, kuvumilia na maandazi hata kama vitumbua hupatikana?

AU wewe unataka vyote?
Ukipata vyote ni nishai?

DUH!
Siku njema!


Tulia na Tshala Mwana Akikupa kibao MBOMBO

Read more...

Blogu ina BUGS!

>> Monday, August 20, 2007


Nina shughulikia kutatua tatizo hili. Naona computer yangu na blogu zote zilivamiwa. Computer imepona.Nimeweza kupata data zote zilizo kuwa zimevamiwa na zimesafishwa.Yale maswala ya JUMUWATA yamepona sasa , tutaendelea zaidi.
NAOMBA KWA YEYOTE ANAYEJUA NIFANYEJE KUONDOA HII BUG IFANYAYO WATU WATEMBELEAO BLOGU YANGU WAPATE MATANGAZO YA AJABU AJABU, ANISAIDIE INFO BASI!

SAMAHANI KAMA ULIZINGUKA NA HAYO MATANGAZO YA AJABU AJABU!
Kumbuka kuyafunga tu yakijitokeza wakati uko kijiweni kwako mpaka nitakapo jua dawa yake!Usiache kunitembelea lakini kwa sababu ya tatizo hilo!
DUH!
Burudika na Jocelyne Beroard wa kassav


Read more...

Kwa Hawala Bunduki AK 47, POKEA Busu!

Bunduki ni kitu cha ajabu ingawa ni kitu tulichozoea!
Bunduki , ni ka kitu kaliko saidia sana sisi Waafrika kutawaliwa.
Lakini bunduki zinatutesa sana sisi binadamu sasa hivi.
PAMOJA na kumu-adimaya huyu Mikhail Kalashnikov ,bado najiuliza sana anajisikiaje kuwa bunduki yake ndio maarufu kwa uuaji sehemu kibao, hasa sehemu sehemu fulani ambazo bado tunajifunza kuwa na uhuru ingawa mpaka sasa tumefanikiwa kutawaliwa kifikira na ki.....
Mpenzi AK 47.....DuH!
Sikiliza kahistoria ka mpenzi hapa kidogo....


Nisikutie majaribuni!
Ngojea nikuache na picha za Washikaji nilizozidaka wiki mwisho hii, kabla hazijapoa...

Powered by www.myfabrik.com

Washikaji walio nitenga!
Wax
najua unakaa mbali !Lakini unanitenga!:-)Kevin ,nimefurahi kukudaka , maana unanitenga na picha hutaki:-)Deo, duh, unanitenga lakini siku hizi:-). Dj Ezza, mbona unanitenga?:-) Kuna wadau wangu kama T.I , Byamungu ambao ndio kabisaaaa sijui mko wapi?:-)
Powered by www.myfabrik.com

Washikaji, picha mchanganyiko.
Powered by www.myfabrik.com

Rasta Koneksheni
Powered by www.myfabrik.com

Kenyan Koneksheni
Powered by www.myfabrik.com

Mkuu wa Kikao
Powered by www.myfabrik.com

Dj Ezza!
Powered by www.myfabrik.com

Bonanza The Great
Powered by www.myfabrik.com

Abdulkarim

Powered by www.myfabrik.com

Big Ben!Asante Mkuu ,siku haikuharibika!
Powered by www.myfabrik.com

Pichani ni Allen na Mjomba.Allen hongera kwa kuachana na ukapera! Nimepoteza e-mail yako!Nistue basi!
Powered by www.myfabrik.com

Burudani!

Huduma na burudani

Usitishike!Burudani nyingine zilikuwa hivi...

DUH! Ngojea niache!
Pumzika na Jacob na kundi zima la KASSAV

Read more...

KATIKA KUPIGANIA UHURU WA KUJAMBA!

>> Sunday, August 19, 2007

Kujamba hadharani nishai!
Nakubali , kijambo kinanuka.

Swali:
Si ni kila mtu hujamba ?
Lakini kwanini tunaona aibu kujamba sehemu fulani?

Turudi kwenye hoja......
Nia ya kuwa na uhuru ni kutaka kuwa na uhuru.
Nia ya kuwa na uhuru wa kufanya tu, tuyapendayo , ndio moja ya njia itufanyayo kukosa uhuru.

JAMII NI JELA.
Inatujengea misingi ya uhuru ambayo inatufunga.
Inatufanya...

  • Lile panki ulilokata nishai!
  • Ule msuko uliosuka nishai!
  • Zile rasta ulizonazo nishai!
  • Zile nguo ulizovaa nishai!
  • Zile tamaa zako nishai!
  • Lile kabila nishai!
  • Yale matako nishai!
  • Yule hausigeli/hausiboi umpendaye nishai!
  • Ile rangi nishai!
  • Na.....Nishai!

DUH!

Unajua.......

  • Tokea tupate uhuru kama nchi, tumekosa uhuru wa kutokuoanishwa na nchi fulani!
  • Tokea uoe/uolewe, umekosa uhuru wa kula sambusa fulani ambazo huzidi kujitokeza baada tu ya ulipochukua kitumbua!
  • Tokea ujulikane kama mwenye busara, mkubwa,... umekosa uhuru wa kufanya ujinga!

Swali:

Ujinga kama we ni binadamu, ni nini?

DUH!

Tulia na STEVIE WONDER!


Read more...

UNAJUA UNA SEHEMU ZA SIRI?

Kuna watu hupenda kujua zaidi na zaidi kuhusu watu wengine.
Kuna watu hatusemi mengi kuhusu sisi .
Kuna watu tunasema lakini hatusemi.
Swali:
Unajua ni asilimia fulani tu , kwa mtu anayesema anajijua, ni kweli anajijua?
Wewe unajijua?

DUH!
Mpate Mzee Doudou wa Guadeloupe....akifanya vitu katika kile kiwanja cha FUCKLY wakati ukijiunga katika mawazo.USINITUKANE LAKINI!:-)

Read more...

WEWE ni MLEVI eeh?

>> Saturday, August 18, 2007

Hadithi ! Hadithi!

H
apo zamani za kale alitokea kiumbe fulani , kipindi hicho alikuwa hana jina. Huyo kiumbe akagundua utamu, uchungu na katabia kabaya.............

Tabia yoyote ni tabia mbaya kama haioani na kipimo jamii ikichukuliacho kama ni sahihi.
Lakini ........

Ngoja niseme..........

Katika akili ya binadamu ya kuunganisha maneno na tabia , imefanikiwa kuonisha maswala mengi tu yasiyo husiana na kitu chenyewe, ila yakatafutiwa sababu za kibinadamu kuoanisha hayo maneno na jambo hilo, kitendo hiko na hata hisia hizo.

Swali:
Unafikiri utamu neno na utamu uhisio ,vina uhusiano?
Wewe una uhusiano na jina lako?

Duh!

Turudi kwenye hoja......

Pombe si chai!
Pombe nishai!
Lakini pombe yako yaweza kuwa ni kahawa!

DUH!
Tatizo la kilevi ni pale lilivyoweza kujiweka katika sura ya aina yoyote.

Kilevi chako waweza kuwa unakiita jina tofauti Lakini!
Usistuke!

Kwa mfano kilevi huweza kuwa:

  • Mke wako.- ambaye bila yeye akili yako haitulii
  • Kazi yako.- bila hiyo , kila kukicha unakumbuka kujishusha kibinafsi pale uonapo wenzako wanaenda kazini.
  • Mpira wa miguu.-ukufanyao usipate muda wakufuatilia kama watoto wako walimaliza kazi za shule walizo ambiwa wazifanye nyumbani.-ikufanyao ughairi kuangalia taarifa ya habari na kumalizia ile shughuli.
  • Chakula.- ambacho kikinukia tu hukawii kushindwa kuwaza jambo jingine lisilohusiana na mlo.
Swali:
Ushawahi kuwa na kile kitabia cha kulamba sukari watu wasipo kuangalia?

Ndio sipingi kuwa matatizo ya kilevi yanazidiana kutokana na aina ya kilevi na pia yule aathiriwacho na kilevi chenyewe.

Si siri , tatizo la ulevi, ni kwasababu ulevi umegeuka kuwa ulevi.Unalewesha!

Lakini kumbuka.....
  • Wengi hulewa kwa sababu zihusianazo na furaha na kuishi
  • Wengi hulewa kwa sababu zihusianazo na matatizo na maisha
Utamu wa kaulevi, kila mtu ana kipimo chake.
Usishangae kuona :
Wengi wakipigania kautamu ka ulevi au kutoelewana tu kutokana na kaulevi hako!

LAKINI WENGI WATAPIGANA NA KUTOELEWANA KUTOKANA NA UKWELI KUWA WAME LEWA.

ULEVI Katika MIZANI ya SIMON leo HII:
  1. DINI
  2. Sehemu za siri
  3. Pombe
  4. Chakula
  5. Nguvu(Ubwana mkubwa wa kijinga)
  6. Na......
  7. Nk
Duh!
Burudika na Miriam Makeba

Read more...

UBINADAMU WAKO SHILINGI NGAPI?

>> Friday, August 17, 2007

Kabla sijasema, ngojea DATAZ na Joan wakukumbushe maswala ya MUME wa MTU!

Binadamu huthamanisha maisha ya binadamu bila hata kufikiria wanafanya kamchezo hako.

Ukiongelea ughali wa maisha mara nyingi watu huupima kwa kipimo cha pesa , mali na....


Uthamani wa maisha ya mtu, wengine huupima kutokana na ukaribu wao na huyo mtu.

KWA Mfano , uthamani wa mtu utokanao na:

  • Undugu wako naye
  • Huyo mtu akuathirivyo kifikira, kimaisha...
  • Umpendavyo au kumchukia huyo mtu
  • Umuoneavyo wivu
  • Maamuzi na tabia zake zikuathirivyo kibinafsi , kimaisha, kiimani na....nk
Duh!

Uzuri na ubaya wa maisha tafsiri zake ni binafsi. Maisha ya mtu mwingine waweza kuyatolea macho kwa kufikiri ni baabu kubwa kumbe hakuna kitu. Na kunayule unayempita chobisi hata bila kumuangalia mara mbili kutokana na jicho lako lilivyojaa kasumba ya nini baabu kubwa, na likakuambia yeye nishai , kumbe ndio mwenye siri ya nini muhimu katika maisha na ndio alaye maisha.
Jicho la mtu mwingine limtazamapo mtu mwingine na kufikia hitimisho kuwa jamaa maisha yake :
  • Mabaya
  • Mazuri
  • Anakula raha
  • kaharibikiwa
  • anajiua
  • anaaafya
  • ana....
Inawezekana kuwa hicho kipimo kinampima Athumani kwa mizani iliyo na sifa za kumpima Hassani , William au hata!
DUH!
Ngojea tupewe Vidonge na Malika (Asha Abdow Suleiman)


SWALI:
  • Ukiona maiti za watu usio wajua au unyanyasaji uendeleao duniani;kina kuuma zaidi wahusika wakifanana nawe(kirangi,kidini,maadili nk)au kwa kuwa ni binadamu?

  • Ukishabikia michezo , hasa timu usizozijua , unavutiwa na mchezo wachezao katika kuamua unashangilia timu gani, au kwa sababu kunajamaa unafanana nao?
Turudi katika somo la Uchumi.....
  • Nimeanza kufikiria ni mizani gani jamaa waliofanya biashara za utumwa waliyotumia kujua bei ya binadamu(mtumwa)!

  • Hivi bei ya kunanihii inapatikanaje pale kona ukitaka kunanihii kwa kulipia?

  • Bei ya nazi je?

Duh!
Ijumaa njema!
Nakuacha na kakumbukumbu kafupi kaenzi hizooo!Donna Summer..

Read more...

Wadogo/Wanyonge wakipata nguvu!


Kabla sijasema, Musical Youth wako mawazoni...Wasikilize kidogo...

Wadogo wengi hukosa sauti kutokana na udogo wao.
Wanyonge wengi hukosa sauti kutokana na unyonge wao.

Lakini.......
Duh!
Simon akiwa mdogo wa miaka mitano hapo chini....

Powered by www.myfabrik.com


Tatizo ni moja tu!
  • Wadogo walionyimwa sauti na kujiamini haina maana wakikua watakuwa na sauti na watajiamini.
  • Mnyonge si kweli ukimpa muda atafuta unyonge.
Saikoloji ya anyimwaye sauti au mnyonge inategemea na mtu mwenyewe. Kuna mnyonge anakubali unyonge kutokana na unyonge ulivyomuathiri .Kuna aliyekosa sauti na ataendelea kutotumia sauti yake kutokana na kutojiamini hata apatapo nafasi ya kutumia sauti.Ingawa kuna mnyonge ambaye kutokana na kunyanyasika , moja ya maana ya kuishi kwake, itakuwa ni kuweza kujitoa katika unyonge na kupaza sauti wote wasikie.

Samahani kidogo....
Kasikilize kawimbo kengine kahawa watoto(Musical Youth) enzi hizo zetu......

Kinachofariji ni :
  • Mdogo ananafasi kubwa ya kuwa na sauti na mamlaka akuapo. Ukiwa unamnyanyasa kwa udogo wake, jiandae kwa kukabiliana naye akuzidipo ukubwa.
  • Mnyonge kama Mjusi, ukimsakama , hugeuka nyoka.
LEO katika MIZANI YA SIMON:
  • Mtanzania kama mnyonge, bado ni mjusi.Sasa hivi anazidi kusakamwa na hali mbaya ya maisha , uongozi mbovu nk..Kumbuka sisemi viongozi wote wa TZ ni wabovu. Naamini kisa cha mjusi kuchelewa kugeuka nyoka Tanzania ni kutokana pia na kuwepo Viongozi ambao wanajitahidi kivyao na kwa uwezo wao kikwelikweli.Bado sijui ni lini huyu mjusi atageuka nyoka Tanzania!Wewe unahisi lini kama mambo hayabadiliki?
  • Wadogo wakikua , watakuwa na sauti, ingawa sijui watasema nini. Sina imani na wajengwavyo kifikira, kikuona mbele, hasa katika maswala ya kuona majibu katika matatizo.
DONDOO:
Mwenye sauti si lazima ajue kuimba!
Mwenye sauti si lazima anachakusema!
Lakini mwenye sauti anaweza kukohoa!

Swali:
Weye mwenye sauti na unacho chakusema ,unasema nini?

DUH!
Ngojea nikupige dozi ya mwisho ya Musical Youth baada ya kukua, wakiimba ule wimbo wao uliowapatia umaarufu wakiwa wadogo.

Je unafikiri walipokua wakubwa , wakiwa na sauti kubwa wame.....

Read more...

Che , Aliko na...... Mwakanjuki!POLENI!

>> Wednesday, August 15, 2007


Pichani ni Waziri Mkuu akimtembelea Mzee Mwakanjuki aliye hospitali, ambaye ni Baba ya marafiki zangu.
Picha kwa hisani ya ISSA MICHUZI!

Powered by www.myfabrik.com

Pichani ni Aliko ambaye ni Rafiki, Mshikaji , Ndugu na .....Pole sana!...Che, vipi London? Naona umenitenga.Pole sana!
Nawaacha na wimbo fulani wa SUPERCAT ambao sitaki kuuhusisha na hauhusiani na tukio la Mzee ambalo ni la kuhuzunisha!

Read more...

Zawadi ni kitu kizuri! Unapenda Embe Ng'ong'o EEH?

Kabla sijasema !Unamkumbuka Ndala Kasheba?

Unatakiwa kutochagua zawadi upewayo. Tatizo la zawadi ni kwamba , tunajitahidi kuioanisha na kitu kizuri.
Kitu kizuri kina tatizo, Kwa sababu , kitu kizuri kwako kinaweza kuwa kina nijazia tu , sio kabati tu , bali hata chini ya kitanda.
Nisikufiche, huwa na nunua maua kwa wapendao maua.
Zawadi ni kitu cha ajabu sana. Ukisikitikia zawadi, ukiwania zawadi, au ukichagua zawadi , hiyo si zawadi.Zawadi kwa Athumani na kwa Zubeda zina tabia tofauti.Lakini...

Swali:
Hivi zawadi ni nini? Si ni embe ng'ong'o tu?Si lile shati, chupi, kondomu na.....?
Au vitu vya bure ukipewa ndio zawadi?

DUH !
Kuna wadau zangu hupenda viatu!
(Ngojea Kelly aseme ingawa naomba kama wewe mdogo usimsikilize)....


Akili ya binadamu nishai! Zawadi anazijali kutokana na kakitu ambako binadamu mwingine anaweza kukajua ingawa binadamu wengi uchagua kutojua hako ka kitu ambako wengi wao hujiumiza kichwa kutokana na ukweli hawajui Zawadi ni nini.
Swali:
Zawadi kwako ni nini?

Nashukuru kupata zawadi fulani kutoka kwa watu walio jua zawadi kwangu ni nini.
Asante kwa Kitabu. Unajijua uliye nizawadia hicho kitu!
Asante kwa Ukarabati wa Blogu hii!Unajijua uliye nizawadia hicho kitu!
Samahani kwa wote niliyo wa zawadia kitu walicho fikiria kumpa yule jamaa chobisi kutokana na kutopata nguvu ya kuniambia ile haikuwa Zawadi!
Duh!
Kawimbo fulani ka zamani ka Wayne Wonder na Buju Banton Kako akilini. Kasikilize basi...

Ngoja niache!
Baadhi ya picha za Jana kwa KANYE WEST

Powered by www.myfabrik.com

Duh!
Hebu subiri kidogo.....

Duh!Kumbe walikuwa wanakataza kurekodi na hata kupiga picha eeh!
Ngojea basi niziache picha nyingine za siku ya Kanye.....Ben , Aliko na ....eeh, Asanteni!
Powered by www.myfabrik.com

Nakuacha na Kanye ...

Siku njema!

Read more...

MSAFIRI KAFIRI!Haja Ikibana, Breki ya Choo Hupungua Nguvu Ufikapo Chooni!

>> Tuesday, August 14, 2007


Kabla sijasema ngojea ST Germain waturudishe kwenye mudi.......na Sure Thing.

Kuna mambo mengi ukiyakaribia kakitu fulani hupungua.
DONDOO:

  • Enzi za kukariri kabla ya mtihani , unaweza kujikuta fomula fulani unazotaka kuziingiza akilini baada ya mlango wa chumba cha mtihani kufunguliwa , huwa akili inajaribu kuzikataa wakati wewe unajaribu kuzing'ang'aniza zikae akilini.
  • Ushawahi kubanwa na haja zile mbili maarufu(Kubwa na ndogo)kisawasawa , halafu ukaanza kustukia breki ya kuzibana inaanza kupungua nguvu mara tu ufikapo msalani nakuanza kuangaika na zipu?

Ngoja nikupe vistori VINNE, basi vya safari zangu nisizozisahau......

Kila safari inasura yake. Na mara nyingi ni kawaida kutokwenda utarajiavyo. Lakini safari ni shule fulani, kwani hukawii kujifunza mawili matatu kuhusu wewe mwenyewe bila kusahau kujifunza pia kutoka katika mazingira unayokutananayo.

  1. Sisahau safari moja ya kwanza iliyoganda akilini, iliyonifunza matumizi ya choo na unishai wa kulakula.Nilikuwa nasafiri kutoka Mbeya kwenda Kilimanjaro na famili.Kipindi hiki nilikuwa na miaka mitano. Kinamna nilifanikiwa kushika mfuko uliokuwa na kilo kadhaa za karanga.Basi kwa kutumia ujanja nikafanikiwa kuzila zile karanga sana tu.Matatizo ya kula kila mtu anayajua, ni lazima choo ndio hitimisho.Enzi hizo za mabasi ya KAMATA , inabidi umsitue kondakta kuhusu maswala ya kuchimba mzizi. Mimi na utoto wangu enzi hizo nilichanganyikiwa. Kwa kuogopa kustukiwa nimekula asilimia kubwa za karanga za wote, nikawanaogopa kusema kuwa tumbo lishachafuka.Kilicho niokoa nisiachie kinyesi chepesi ndani ya nyeti, ni jinsi nilivyodhoofika na sura ilivyobadilika kwa kujitahidi kuzuia kinyesi chepesi kwa nguvu zote.Shangazi yangu aliyekaa karibu yangu alipostukia maswala nakuomba basi lisimamishwe nikachimbe mzizi , nilikuwa katika hali ya hatari. Nilipofika nje ya basi wala sikuhangaika kwenda mbali kwani breki zilianza kukataa. Kitendo hiki kilinisababishia kutupa chupi porini na kusafiri safari nzima bila chupi na kutaniwa kwa miaka kadhaa na ndugu na jamaa. Kitu hiki kikanifundisha matumizi ya choo kabla ya safari na pia umuhimu wa kuwa na kiasi katika vile vitu uvipendavyo.Unajua tena mimi pamoja na kuwa mvivu wa kula , karanga na vinywaji fulani huwa vinapanda.DUH!
  2. Safari ya pili nisiyo isahau, ni ile iliyotokea mwaka 1980 wakati famili nzima tunahama Mbeya kwenda Songea. Hii safari ndio ilinifunza ni nini kinaweza kutokea katika barabara . Barabara yakwenda Songea kipindi hicho ilikuwa mbaya sana. Nafikiri katika Landrover niliyokuwepo, ni mimi tu na dereva walikuwa hawatapiki. Safari ilijaa harufu ya petroli na matapishi kitu ambacho mpaka leo hakinitoki akilini.Ukiachana na watu kutapika mpaka matapishi hayatoki, barabara ilikuwa inapita katika sehemu inayo itwa Lukumburu, ambako ni kwenye udongo wa mfinyanzi. Katika milima hiyo kila bonde unaloangalia kulikuwa na mabaki ya magari. Kutokana na kusafiri wakati wa mvua ndio ilikuwa mara yangu ya kwanza kuona magari yamefunga breki lakini yanakwenda kutokana na udongo kuteleza. Basi kwa mara ya kwanza nikaingizwa katika matembezi ya hiari katika matope na msitu usemekanao una Simba.Watu waliamua kumuacha dereva aendeshe mwenyewe na kutungoja baada ya mlima kuliko kuwemo ndani ya gari lisilo funga breki kutokana na utelezi.Safari hii ilinifunza mengi, mojawapo ilikuwa; mtu huhofia sana akionacho kuliko asicho kiona katika mazingira fulani.Tulikubali kutembea ingawa kunauwezekano kuwa tutembeapo tutaliwa na Simba kuliko kuwepo ndani ya gari ambalo ninaonyesha dalili zote za kutuua. Kabla ya hapo nilikuwa nafikiri mtu huogopa tu kile asichokiona kama giza. Si unakumbuka zile stori za kutisha, za majini nk. ambazo nilikuwa napenda kuzisikiliza wakubwa wakiongea halafu naogopa kuzima taa wakati wa kulala?DUH!Kakitu haka kamenikumbusha jinsi gani baadhi ya binadamu tunamuogopa yule tu anayeonekana ana UKIMWI.Akiwa ana UKIMWI lakini hauonyeshi ,basi twende kazini. AU?
  3. Baada ya kufika Songea , kila mtu akaapa kutotumia magari kwenda sehemu nyingine. Kipindi hiko uliweza kutumia likizo yako yote njiani kwa kutumia mabasi au magari kutokana na ubovu wa barabara za kwenda Songea.Njia iliyojitokeza ikawa ni ndege. Watu walikuwa wanasafiri na ndege za jeshi za mizigo kama kawaida. Kitu ambacho siku hizi ukisisitiziwa ufunge mkanda kwenye ndege kama ulipitia kusafiri na ndege za mizigo zisizo na viti unakuwa na jeuri kidogo.Ndege nyingine za abiria za Air Tanzania zilikuwa ni zile ndogo ndogo za Focker (watu 42 kama nakumbuka vizuri). Kipindi hiki nakikumbuka kutokana na mvuto uliokuwa unatokea ukiwa katika ruti ya kwenda Dar , wakati wa kukatiza maeneo ya Mto Rufiji.Hapa ndege ilikuwa inarudishwa chini kwa sekunde fulani unajisikia unaelea.Halafu unarudishwa tena kitini ndege ikienda juu.Kitu nisicho kisahau ni jinsi katika safari yangu ya kwanza na hizi ndege za aina ya Foka zenye injini mbili, ilipotokea kuwa katika kasheshe za mvutano injini moja ikazima. Tulisafiri chini chini mpaka Dar-es Salaam Airpoti kwa injini moja.Yale maswla yakuona mawingu juu yalisahaulika. Nachokumbuka ni kuwa kila mmoja alikuwa anaomba sala fula .Ila kulikuwa na Mhindi mmoja mweusi ambaye ndiye alikuwa mhindi wa kwanza mweusi kumuona ambaye yeye safari nzima alikuwa anapiga picha wakati wengine wanalia na kutubu dhambi zao. Kitu kikubwa nilichojifunza kuhusu mimi katika safari hii ni , nauwezo wa kutulia katika mazingira ambayo kila mtu amepaniki.
  4. Safari ya nne ambayo niliifurahia ilikuwa ya kwenda Nairobi. Niliifanya na Kaka yangu Davie Kitururu. Tuliamua kutembea kwa miguu kwenda kenya. Safari hii ilianza kama utani tulipokuwa Arusha na kutaka kuchukua taxi mpaka Nairobi.Si unayakumbuka yale mataxi ya kushea? Duh!Ngoja niache basi......!
Nachojaribu kusema ni kuwa , safari inaweza kuwa shule lakini inaweza kukufundisha tabia mbaya vilevile!Si unajua tena Masafiri Kafiri?
Bado sija kaa sawa kutoka na maswala ya safari....Lakini ngojea nikuache na baadhi ya picha za safarini.
Kabla ya hapo ngojea tudake baadhi ya safari za mzigo....

Kamzigo kupakiwa kwenye kadege fulani....

Kamzigo kaingiapo chobisi fulani.....
Powered by www.myfabrik.com

Ombaomba walikuwepo hata sehemu usizotarajia...
Powered by www.myfabrik.com

Msafiri kafiri
Powered by www.myfabrik.com

UL(l)EVI
Powered by www.myfabrik.com

Baadhi ya Marafiki njiani!Kuna wngine nimestukia hampendi kupigwa picha:-)
Powered by www.myfabrik.com

Safarini baadhi ya picha zaidi..
Duh!
Ngojea niache....!
Bado sijarudi kisawasawa katika kublogu.
Swali:
Ushastukia kila siku stendi/Stesheni /kituoni kuna watu wanasubiri usafiri?
Dondoo:
Maisha ni safari!Safari usizofanya kwa kutumia baiskeli, miguuu na ....unazifanya kimawazo!
SAFARI NJEMA!


Lakini ...TUKO PAMOJA!
Namuacha COCOA TEA na DENNIS BROWN wakikumbusha maswala ..... Getting Myself Together..

Read more...

Blogu Iko Gereji!

>> Thursday, August 09, 2007

Samahani Wadau wa Blogu hii!

Powered by www.myfabrik.com


Blogu inafanyiwa ukarabati kwa muda!
Pia niko safarini kwa muda,kwa hiyo sitatokea hapa kijiweni kama kawaida yangu kwa masiku kadhaaa!

Wakati unanisubiri pumzika,cheka au burudika na wimbo huu wa Michael Jackson wa India siunakumbuka Thriller?

Read more...

Ukiwauliza Watoto Wakikua Wangependa Kufanya nini!

>> Wednesday, August 08, 2007

Kabla sijasema ngojea nimuache Chris Isaak aseme baadhi ya jambo ambalo baadhi yetu huombea tukikua tufanye...lakini....


Ukimuuliza mtoto akikua angependa afanye nini, unaweza kupata majibu kama ningependa kuwa:

  • Dereva wa magari!(Eti nasikia nchi nyingine huwa wanachagua kuwa madereva wa magari ya Zimamoto.Duh!Naombea magari haya yawe mengi na kwetu bongo)
  • Polisi
  • Daktari
  • Mwalimu
  • Muuza duka
  • Na.............
Lakini baada ya kuingia katika mfumo na kuanza kunyoshwa na hali halisi ya maisha kuna mambo mengi ambayo unajikuta yanakubadilisha muelekeo wa kutoka kutaka kuwa Polisi na kujikuta mlinzi nyumbani kwa mtu au kujikuta......
Badala ya kuwa muuza duka , unastukia ni muuziwa gongo
Badala ya.....

Cha kawaida ukishakuwa mkubwa ni kujaribu kufikiria kamaungelijua ungefanya hivi na vile ulipokuwa mdogo ili maswala yako yawepoa zaidi sasa.

Maswala mengi kama watoto tuyafikiriayo kuwa tungependa kuyafanya tukikua, yanaongozwa na kutojua hali halisi ya shughuli hizo ukubwani. Na maswala mengi ambayo tunafikiria sasa hivi kuwa kama muda ungerudishwa nyuma tungefanya vingine, hutokana na ukweli kuwa hata ukweli halisi wa hali halisi tuliyonayo hivi sasa , hatuujui kwa asilimia mia.Kwa hiyo siwezi kushangaa kuwa , hata ukirudisha muda nyuma na kuanza upya kuelekea upande ambao sasa hivi unafikiri ndio bora, unaweza kufika huko uelekeako na kufikia hatima ileile uliyoifikia sasa hivi kuwa; ukipewa nafasi nyingine ya kurudisha muda nyuma ungefanya mambo vingine mwaka uleeeeee.........

Dondoo:
Ukweli ni kwamba , tulipo sasa hivi ndio hali halisi ya maswala. Mengine ni alinacha.Piga ua lakini hakuna ujanja zaidi ya kudhibiti hali halisi ituzungukayo sasa hivi.
Duh!

Ngojea nimuachie Sorab Wadia Akiigiza kama Hussein Al Mansour aelezee atakavyo kuwa kama Osama Bin Laden

Sasaaa....
Da! Ngoja niache...
Siku njema!
Tulia basi na Safari Sound Band wakikupa Chakacha

Read more...

Hivi ni nani masikini kuliko wote Duniani?


Powered by www.myfabrik.com
Wakati waoshavinywa wakilumbana kati ya Bill Gates na Carlos Slim nani anapesa zaidi.....kuna sura mamilioni hazinakitu

DUH!
Swali:
Hivi Utajiri ni nini?
Umaskini je?
Hivi ukiwa huna kitu maana yake wewe maskini?

Nilijikuka katikati ya ubishani wa kuwa nani nitajiri kuliko wote duniani. Katika gumzo hilo walio wengi wanauhakika kuwa tajiri kuliko wote ni Carlos Slim Mexicano/Mlebanoni, bepari mmoja. Wengine wakawa bado wanadai kuwa ni Bill Gates.
Mimi bado niko mawazoni , nikiwaza;

  • Hivi kwanini wenye pesa ambazo hata matumizi ya pesa hizo hawana wanakuwa ndio waonekanao kuwa wanaumuhimu kuliko wengine katika jamii yetu?
  • Hivi ushawahi kujiuliza kwanini kazi fulani za muhimu, mishahara yake ni mibovu ukilinganisha na umuhimu wake katika jamii yetu? Hivi hata malipo mengine kama heshima kwa wafanyao kazi fulani muhimu ni jambo kubwa sana katika jicho la jamii hii tuishio?
Duh!
Hivi manesi/ walimu na akina David Beckamu/Tiger Woods ni nani muhimu zaidi katika jamii?
Usitake kufananisha mishahara yao lakini, kwa sababu ..............

Umaskini nishai!Ila umaskini si kukosa pesa tu, tukumbuke hilo. Kwa sababu pesa ni kamchezo fulani binadamu amejitungia na masharti yake yamekaa kibinadamu. Leo unazo ukiwa nazo nyingi, kesho hata ukiwa nazo nyingi, hazina mpango.

Swali:
Unakumbuka Zimbabwe na pesa zao?

Naacha hii ....!
Cheki tu madansa hawa Lacey and Danny wakikuchezea Samba katika kulainisha siku na kukuapa nguvu ya kuendeleza libeneke....DUh!sina uhakika lakini kama utapata nguvu:-(


Photos kutoka:
Queenzy
India Ink
Wikipedia:
Bill Gates
Carlos Slim

Read more...

Katika Majaribio!

>> Tuesday, August 07, 2007

Usitishike!
Najaribu tu Filmloop kama alivyonishauri Maricha hapo chini kwenye komenti.
Sema basi kama poa au la!Ni picha tu mchanganyiko, zangu na marafiki.

Powered by www.myfabrik.com

Read more...

Udongo Uukanyagao Yawezekana ni Mabaki ya Maiti Fulani!

Kabla sijasema!
Mpate John Lee Hooker akisikitikia mji wake ulipokumbwa na mafuriko.

Kuna watu wanadai kuwa dalili za siku ya mwisho ni haya majanga kama mafuriko, tetemeko la ardhi, volcano kulipuka nk.

Lakini ukifuatilia historia ya dunia utakuta kuwa milima na mabonde pamoja na maafa kibao ni moja yayaliofanya dunia iwe kama ilivyo.

Sehemu kubwa ya tabia ya binadamu imejengwa kutokana na binadamu kushuhudia watu wakifa njaa, kuumwa na nyoka,kupigana vita nk.

Lakini cha ajabu ni kwamba hitoria mpaka leo imeshindwa kuwa ni kitu cha uhakika kumfanya binadamu asirudie kosa.

  • Sehemu nyingi zikumbwazo na mafuriko na kuua miaka iliyopita usishangae zikaua tena siku nyingine kutokana na wakazi kutokuhama au kuyaendeleza maskani ili yasidhuru.
Sehemu kibao zinazokumbwa na majanga ya aina fulani ni mara chache watu kujifunza na kuepusha majanga ya baadaye.

Sisi binadamu ni kiboko kwa kusahau kirahisi. Nahisi maswala ya Oldoinyo Lengai kutokana na kwamba mlima haukulipuka mambo yashasahaulika.

Swali:
Ukisikia mtu kafa na UKIMWI unatishika siku ngapi?

Sisi binadamu huwa pia na kamchezo kakuuana halafu tunadai tunaogopa maiti. Kwa jinsi tunavyokufa na tulivyokufa nahisi karibu udongo mwingi tuukanyagao ni kaburi la kitu fulani. Maiti ya panya ,ndedere mwanakaka au mwanadada inaweza kuwa ni moja ya mbolea irutubishayo kaudongo fulani usikokaogopa wakati una ogopa kupita makaburini na unaogopa maiti.

Duh!
Ngoja niache !
Mpate tena John Lee Hooker aponyeshe na wimbo The Healer akiwa na Santana


Mwandani, unakumbuka tulikuwa tunamsikiliza huyu John pamoja?

Read more...

Chifu Fundikira Afariki(1921-2007)!

Naona kizazi cha viongozi fulani wakongwe wa TZ kinaendelea kututoka. Akina Chifu Fundikira walijaribu ingawa wanaweza kukosolewa kwa mapungufu, lakini kizazi kipya cha viongozi wa TZ bado hakijatuonye maajabu yake:-(

(Picha na IPPMEDIA)
Chifu R.I.P!

Read more...

Elimu za Kufundisha Kukariri na Kuigizia

>> Sunday, August 05, 2007

Kabla sijasema...
Samahani nimemkumbuka mama , ngojea Banana Zoro anisaidie kusema....



Ingawa binadamu hujifunza kwa kuigiza,bado nazani hakuna sababu ya kuendekeza elimu itufundishayo kukariri na kuigiza bila kutujenga kufanya yale ambayo tuyawezayo na yajengayo .Naamini karibu kila mtu anauwezo wakufanya kitu kizuri kivyake kama hajakaririshwa.
Duh!
Kuigiza hata yale tusiojua au kuelewa ni sanaa fulani lakini!
Swali:
Unakumbuka kukariri maswala fulani ambayo hata hayana umuhimu kwako kabla ya mtihani?


Duh!
Pumzika kidogo na Apache Indian

Picha kidogo za jana ambazo nahisi nilikuwa pale mama aliponikataza kuwa...
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
MadIce akitutumbuiza
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Allen
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Abdulkarim
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Edo akishangaa kitu...:-)
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Tompura aka BassMan.Nilisahau kuwa ilikuwa birthday yako
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Magonella
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Ben
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Erick kazini
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Raymond aka Mkuu wa kikao, David, na ...
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Najua ushachoka kuangalia picha ngojea niseme....



Nakuacha na Vince Black...

Read more...

Fest AFRIKA

>> Saturday, August 04, 2007

Kabla sija sema.....

Nahisi unakumbuka Bembeya Jazz ,,.....
Lakini.....

Kumbuka Hii festivo ambayo Watanzania wanaiandaa na kuifanya babu kubwa!

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket




Read more...

Stela Wangu.....!Saikoloji ya kumdaka Mwanadada Apendaye Mbwa!

Katika neti, washikaji wangu wamekumbwa na kipupwe cha kuongelea siri nane wafichazo na sasa Maswala ya Stela ambaye nimeshindwa kuchagua mmoja wa kubobea kujulisha ku.....
Stela halafu stela
Duh!
Stela...

Kabla sijasema ....Bilal aongee...

Nilimpenda mwana dada fulani ambaye na chagua jina Zubeda, ingawa wadau wangu(Ndesanjo, Rasta , Mwenyemacho, na..... hapa wanapenda jina la Stela.
Nilikuwa na miaka kumi tu, mtoto mdogo, na nataniwa lakini napenda....
Huyu mwanadada alinifanya nizidishe kucheza nguti .Si unajua mchezo wa gololi?
Huyu mwana dada alini sabababisha niwe na cheza mitaa ya mbali na nako ishi.
Kipindi hiki pia nilimpenda sana Anna Gama. Ndio... Ni Gama ambaye ni........wa CCCCCCM. Kipindi hicho alikuwa Mkuu wa mkoa wa Ruvuma.Lakini Anna hakujua hicho kitu.
Duh!
Kuna Salome pia alinizingua....
Duh!
Hivi Raulensi Gama ambaye alikuwa mshikaji kipindi hicho tulivyokuwa watoto yuko wapi?

Ngojea ni wapumzishe kwa picha za juzijuzi,leoleo ......

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Zubeda !
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Zubeda eeh!
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Duh!

Samahani kidogo kwa kutoandika kwa muda. Llakini .. kabla sija hata andika ....Mpate Dave ambaye ananichekesha sasa hivi...

Tuendeleee....
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Teddy

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Teddy bear!
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Duh!

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Mr Dj
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Ze Zubeda
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Ze Zubedas
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Kenya , Tanzania ,Kenya
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Hivi si binamu ni ndugu?
Mpate binamu yake ambaye ni Binamu wa Buju Banton..

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Stesheni ya treni Copenihageni,Deni Maki
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Maswala ya boti la kitalii..
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Huwezi kufika deni bila kumuona huyu sanamu

Duh!
Turudi chobisi...

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Aliko eeeh!
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Duh!
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Al-U na Mimi

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Janet
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Erick
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Simon ..Mzungu aliyejiingiza...Leonardo(Columbia)
duh!


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Prince Badara

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Prince eeh!
Nisitake kuficha kuwa Stela wangu alinizingua , na nitamsimulia zaid baadayei. Natamani ningemzingua kama Diana anavyo sema hapa akisaidiwa na Michael.

DUH!

Nili pata kumzubalia Stela wangu pale Songea aliyeitwa Fatuma, ambaye alinisaidia katika utoto nichapwe mara ya mwisho na mara ya kwanza na mama yangu. Nilitembea bila viatu, dada yangu(Joyce ) aka ni semelea nyumbani ,kitu ambacho mpaka leo sielewi kwanini mama yangu aka chagua kunichapa kwa hilo.
Duh!
Ilikua mwaka 1985 na ilikuwa mara ya mwisho kuchapwa maishani mwangu.
Duh
Kabla ya picha Mpate Nguza...


Stela wa mwisho ambaye nafikiri ni yule aliye fanikiwa kuniumiza roho.....
alitokea Morogoro. Huyu nilimpenda na alifanikisha mambo kibao ambayo tulikuwa tunaibia. Lakini alikuwa anapenda waaarabu na wahindi .Niligundua pale alipokua anaiba mbele ya macho yangu na kukana.

Duh!
Lakini washikaji wangu na pamoja na ujanja wangu , akafanikiwa kuniambia kuwa mimi nishai. Alifanikiwa kupata futari ya ngono na jamaa wengine. Nisikufiche nilifurahi kidogo nilipo sikia awapendao mambo yao ovyo..Lakini yale maswala ya kufanya.....matusi na mambo mengine sijui alijifunzia wapi, kwa sababu .....
Duh!
Picha baadhi za juma ileeeeeeeeeeeeeee nazo ziangalia sasa..Zinikumbushazo siku niliyofurahi kinamna....
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Vibe
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Katika kuwepo...
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Dereva..
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Usafiri..

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Malizia na Beenie Man

Ndesanjo ! Duh!
Kweli na Stela wengi katika fikira:-) NaNitajaribu kumnukuu mmoja mmoja kirefu siku nyingine....au baadaye...

Read more...

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP