Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Weka AKIBA ya MAUMIVU NDANI YA ROHO kwa KULIA kwa MADOIDO!:-(

>> Friday, January 23, 2009

NI BUSARA kwa ajisikiaye kulia , KULIA.

KULIA ni muhimu ingawa kwenye FASHENI ni KUCHEKA NA TABASAMU ambavyo viko kwenye chati.

Na,...
...KICHEKO na TABASAMU vyaweza kusifiwa zaidi MPAKA kwa kusaidia kuamsha MSHAWASHA wa liMTU kukustukia UPO,mwenye tabia fulani kufikiria kama UNAFAA kulawiti au KUKUPENDA tu kwa mvuto wako wa DIMPOZI zako kwenye SHAVU la kumimina wakati unakenua meno kwa kufurahia zaidi KIDOGO ya wakati UNALIA ingawa unavutia UKILIA.

KULIA ni bomba la shoo!
Unaweza kupata UMAARUFU kwa jinsi uliliavyo pipi au uliavyo msibani.

Ila,...
....KULIA PEKE YAKO ni muhimu zaidi ya kucheka peke yako.

AJALIYE jinsi AONEKANAVYO akilia, atafanikisha kuchelewesha kupunguza maumivu ya roho YALIZAYO.

Katika fasheni za kulia,...
... ..kuna vikorombwezo na MAZAGAZAGA kama vile ya...
............kuongezea MSISITIZO wakulia kwa kutoa kamasi, kujamba kidogo au kuongezea na chachandu ya KWIKWI kwa mbaaaaali, viwezavyo kukusaidia KUPAMBA jinsi ya MUONEKANO WAKO UKILIA.

Lakini.....
...... wakuonao ukilia pamoja na kujisikia vibaya au vizuri kwakua BINGWA unalia, LABDA MISINGI YA MAUMIVU bado iko ndani yako uliyeanzisha KULIA.

KUNA wajaribuo PIA kuchanganya kulia na kucheka katika jitihada za KUTUNZA MUONEKANO, kitu ambacho MARA ZOTE hufanikisha utengenezaji wa sura ya TISHA TOTO.

Labda....
.....LIA kama unajisikia KULIA hata kama ni mbele ya WATOTO ambao labda watalia wakikuona unalia.

Kuwaliza watoto kwa kuwa unalia , inaweza kuwasaidia KUKUA wakijua kuwa kulia ni kitu cha kawaida na labda watakua bila kufanikiwa kutunza maumivu ya moyo kwa kukwepa KULIA.

Kulia ni bomba la KAULI isemayo na kufikisha ujumbe kwa NGUVU zaidi ya MLIO.
Swali:

  • AU?
  • Katika UTANI , ukimtania mtu ni lazima uwe na wasikilizaji?
NAACHA!

AU ngojea tupumzike kwa kumuangalia Bill Clinton akiwa inspired KULALA na Martin Luther King Jr......


Basi Mkuu, ngojea tu Mr Nice aseme katika - RAFIKI
WIkienDI NjeMA!

3 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Anonymous 9:49 am  

Mkuu Simon mzima?
kaka nipo ndugu yangu.
namba yangu mpya
0753 339 449

amani kaka.
rasta hapa.

Anonymous 9:54 am  

mkuu napatikana hapa kwa sasa,najaribu kutumia wordpress.
http://www.ringojr.wordpress.com/

rasta hapa.

Simon Kitururu 12:43 pm  

@Rasta luihamu:Nimeshafika kijiwe chako kipya.Tuko Pamoja!

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP