Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

SAMAHANI kwa kupotea! NIlikuwa naumwa na labda bado NAUMWA!

>> Thursday, April 30, 2009

Samahani ambao nilipoteza mawasiliano ghafla kwa simu , barua, au hata kukonyeza!
Wakiwemo PAPA MANENTO , YASINTA mtoto wa KIBAHA, na ........

Nipo na nitarudi zaidi hivi karibuni !
SAMAHANI kwa kupotea na kama bado ulikuwa unanitembelea na kunifikiria, ASANTE!

NIVUMILIENI kiduuuuchu!
:-(





Sijafa bado lakini !:-(















Nipo bado lakini!:-(



















Ngojea SOLOMON BURKE anisaidie kusema -Everybody Needs Somebody



Au ngojea tu nibadilishe hali ya hewa kwa kumuachia BILL HICKS atukanie katika-Your Children Aren't Special kama una WATOTO

Read more...

Katika KUMCHUNGULIA Mtanzania akijifunza KIINGEREZA!

>> Friday, April 24, 2009

Hii shughuli wee acha tu na kukariri imo!

Na hii shughuli bado BINGWA ni MTOTO.
Swali:

  • Ushawahi kumchungulia na sio kumuangalia MTANZANIA akijifunza Kingereza?
  • Wewe unashuka ung'eng'e?
  • Hivi Rais wa Ufaransa ni fala eeh kwa kuwa ung'eng'e haupandi?


Katika hii shughuli unaweza kujikuta unabana pua ikiwa yote ni katika miondoko yakujifunza UNG'ENG'E.


Na unaweza ukajikuta unaiga mapozi ya Padre Wakiitaliano asiyejua Kiingereza akiongea ,yote ikiwa katika kudhani ni miondoko ya lugha ya Ung'eng'e, hasa katika kudhani Wazungu wote wanashusha UNG'ENG'E.

Na kama ni mpenda miziki ya HIPHOP , hukawii kujikuta Dar-es-Salaam umevaa nguo za Winter , yote ni katika kudhani mapozi na azungumzavyo 50 Cent ni Kiingereza safi mpaka usikie eti ni akina OBAMA katika Wamarekani Weusi ndio waelewekao na kushusha lugha ipaswavyo na sio akina P. DIDDY.


Na wale wampendao Bob Marley , basi jasho litakutoka tukianza kuongea Kijamaika kwa lafudhi ya KIPARE au KIHAYA.

Hii shughuli wee acha tu!

Lakini kujifunza lugha yoyote mtiririko wa kujua ni uleule!

Na huwezi kupatia kabla hujakosea mara kenda zisizohesabika!

Swali:
  • Unakumbuka mapozi yako wakati unajifunza Kiswahili au kwa sababu umezaliwa Tanzania unadhani ulizaliwa unajua Kiswahili?
  • Kwani kujua lugha ni mpaka uwe na lafudhi ya lugha?


Na kumbuka kumcheki ajifunzaye lugha, kuna starehe zake na bado BINGWA ni MTOTO.

Kumbuka kama unajifunza kukosea imo ndani ya huu mchezo.
Na kama kuna akuchekaye, kumbuka inachekesha lakini maishani kuna ulivyomcheka mtu na hiyo sio siri ya kuacha kunoa NANIHII kama lengo ni kujua NANIHII hata kama unachekwa kwa kithembe.


Na kumbuka mwisho wa yote , lugha ni kwa ajili ya mawasiliano.

Na kama Wakatoliki wanamuelewa Papa, basi kama mtu akikuelewa ndani ya sentensi ''ze milk is standing'' huongelei maziwa ya kunywa bali titi lenye misuli ya nguvu na ncha kali iliyonuna , basi ujumbe umefika na matumizi ya lugha yameshamaliza kazi yake.

Swali :
  • AU?
  • Umestukia hata uongee kwa ufasaha gani kuna tutakaoshindwa kukuelewa unamaanisha nini?
  • Ni Watanzania wangapi unadhani wanajua Kiswahili fasaha ambacho ndicho Kiswahili?

Nimeacha!
Ni moja ya wazo tu na WIKIendi njeMA!

Narudi tena Nigeria kwa Majek Fashek aongee...


Au tu TMK Wanaume FAMILY wadai -DAR mpaka MORO


ASANTENI WADAU WOTE msionitenga!
Nakuacha na baadhi za Picha na Washikaji!
Photobucket

Photobucket

Photobucket


Photobucket

Photobucket


Photobucket







Photobucket


Photobucket

Photobucket


Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket


Photobucket

Photobucket

Read more...

SI BADO unajua HADITHI wasimuliwazo WATOTO na WAKUBWA, huwa ALIYETUNGA ni MKUBWA?

>> Thursday, April 23, 2009

Watoto ni wabunifu kuliko wakubwa wa HADITHI na kama unabisha wavizie wakicheza usikie wanavyosimuliana hadithi walizobuni wakati wanaendelea kuzibuni.

Kikubwa ni,...
... hata mtoto ukimuacha acheze mwenyewe, kama aliwahi kuona gari anaweza kugeuza ndala liwe gari na pia akajisimulia mwenyewe STORI kuhusu kuwa hilo gari aina ya NOLINOLI a.k.a ZIMAMOTO au ze AMBULANSI na jinsi lilivyookoa mtu na mende!

Swali:

  • Hivi hapa sijadanganya kweli kuwa watoto Wakibongo waliowengi wanajua kuna gari la wagonjwa na zimamoto a.k.a NOLINOLI?

Tuendelee.....

Ukikutana na MKUBWA anamsimulia mtoto hadithi iliyotungwa na MTOTO basi huyo mkubwa SPESHO!

Tatizo ni,...
.... stori a.k.a hadithi za wakubwa ndio zisakiziwazo watoto kwa kigezo cha kuwa zinamafunzo.

Na kama wakubwa wangekuwa wanajifunza na wanamafunzo , akina Yesu, Mohamedi, Gandhi, Babu Mrinde, na hata BULICHEKA na ABUNUWASI kuna mambo wangekuwa wamemaliza enzi hizo kufunza waliotutangulia wenye uume na uke, na siye wengine hata wasiwasi wa UKIMWI kama tu KASWENDE achilia mbali KUFA NA NJAA , tungekuwa hatuna kama jinsi tusivyokuwa na wasiwasi na matumizi ya choo cha shimo.


Na naamini HISTORIA haitufundishi kitu kutokana na STORI za wakubwa kufundishwa watoto , WATOTO wenye stori orijino.

Stori za wakubwa ukiziangalia vizuri , ni za Kiyesuyesu au za TISHA TOTO zisababishazo watoto HATA WAKIKUA wanakuwa WATOTO WAKUBWA halafu wengine ndio hawa tunawaita VIONGOZI WAHESHIMIWA WAKUBWA waendeleao kuongoza na KUTULEA kwa staili za TISHA TOTO!

Sikatai umuhimu wa uzoefu!
Sikatai ukisimulia uzoefu wako, na labda ndio maana wengine tumejifunza mpaka katerero kutokana na stori na sio kupiga chabo.

Lakini ukitazama , utastukia kuwa ni hadithi za wakubwa zinazopelekwa kwa watoto na kuendeleza sanaa za kutaka kutafsiri kwa watoto kuwa kwa kuwa wewe sio kama mimi kwa kuwa mimi na kifafa, basi unikwepe nikijamba usijepata kifafa , wakati kifafa inajulikana hakiambukizwi kwa ushuzi.

Na stori hizi a.k.a hadithi hizi ndio hizo zinasababisha toto likikuwa lifikirie sijui likubake au kukupiga konzi kama sio kukubagua kwa sababu wewe:
  • Zeruzeru
  • Muarabu,
  • Muhindi
  • Chotara
  • Jeusiiiii
  • Pua kama nundu
  • Sangara wamo
  • Titi ndimu na chuchu mwiba
  • Meno kama ngiri
  • Ustadh
  • Mlokole
  • BAYAAAA!
  • ZURIIII!
  • Muafrika
  • Muislamu
  • Mkristo
  • nakadhalika tatu na nusu.
Swali:
  • AU?
Na,...
...KUBWA ZIMA sikiliza watoto wakisimuliana hadithi orijino ugundue kitu au hata ugundue HADITHI NI NINI.

Na kama simulizi lako ni la yaliyotokea kweli, SIMULIA ingawa nayo inaweza kuwa ni HADITHI ila isiyotungwa. Na simulia kama unafikiri ni kweli ni lazima kila stori huwa inabidi isimuliwe.

Swali:
  • AU?
  • Si unakumbuka kuwa si kila hadithi hutungwa?
  • Unafikiri ni kwanini kuna unavyoacha kutusimulia na kwa vigezo gani kuna utusimuliavyo?

Nimeacha na ni moja ya wazo tu !
SAMAHANI!

Tulia na stori ya Sam na Esther (WARNING! Ni ya HUZUNI!)

Au mpate tu Innocent Galinoma asimulie kuhusu ya- RAIN

Read more...

Kama akina BUDHA , YESU , MTUME,... walishaongea na kufanya na HALIHALISI ndio HII!(simulizi za aliyekata tamaa)

Na kama akina....
..... Hitler, Mao , Mandela, Kenyatta, Nyerere na Kawawa walishaongea na kufanya na halihalisi ndio hii , akina Kikwete, Kibaki, Museveni na Zuma watakachofanikiwa kufanya ni kututafutia cha kuangalia pale watakapo ishia na labda pasipoeleweka wala kutosha!

Swali:

  • Na kama akina BUDDHA na .. walishahubiri na kufanya, watuhubirio leo wanajipya la kuongea na kufanya libadilishalo au kuongezea ONGEO au HUBIRI?

Na kumbuka,..
... kama hufanyi na tunaongea, hata ukifanya tutaongea.

Tatizo ni,....
...... kuna watu hawatajua ya Yesu, Mohamedi , Buddha au hata Mtikila kesho kama hutaongea.

Swali:
  • AU?
Nimeacha!

Ni wazo tu Kingunge!
USITISHIKE!

Namuachia Justin Kalikawe aseme ya -UGENINI



Au turudi kwa Mnijeria ASA azungumzie tena- Jailler....

Read more...

UKITAKA ndoto itimie , AMKA!

>> Wednesday, April 22, 2009

Ukiendelea kulala ndoto inawezaendelea kubaki NDOTO.

Na usipo AMKA ndoto hubakia NDOTO!


NA ukiamka ili ndoto itimie ,....
....kumbuka ufanyacho kwa kukitolea macho si NDOTO!


Na ukifikiri ulipata mimba au kumpa mtu mimba ndotoni, hiyo ni kubaka na haikuwa NDOTO.

Ndoto ni KISURA!

Ndoto ni JINAMIZI!


Na ukiamka waweza tengeneza JINAMIZI au KISURA na chachandu ya shughuli inakolea kwa kuwa UKIAMKA , wewe UKO MACHO!:-(

Na,...
... Amka ndoto itimie !
Ingawa tukikuona UMEAMKA na unalia tutajua nini KIMETIMIA!:-(

Na ukilia ni dawa ya majonzi na mwanzo wa utamu wa yasiyo NDOTO na unajua tayari kilichoKULIZA!

Swali:

  • Unauhakika uko macho?

DUH!
Wazo na linakomea hapa kwa leo!

Ngojea Richard Pryor abadili hali ya hewa kwa Kuongelea watoto wakidanganya katika- KIDS Lying

Au ngojea Beenie Man na Barbee warudishe kitu katika- GIVE IT UP

Read more...

WANAOANDIKA wanaandika nini kifanyacho TUSIOPENDA KUSOMA tusome AU tuone MAANDISHI yanaleta nyege ya MSHAWASHA?

Kusoma nishai, ...
.... ghafla unaweza ukasoma kitu halafu ukajua na kustukia kumbe unadalili za MIMBA!

Halafu,..
....kulalamika ni bomba la faraja kwetu wote NA karibu kila MTU ni PROFESA :-(



Wakati unalalamika kuwa vijana wa siku hizi hawapendi kusoma , KUNAUWEZEKANO unachangia KUSABABISHA tupende kuangalia TV na labda PICHA ZA UTUPU mtandaoni kwa kuwa unatuandikia maandishi yasiyonyegelesha watu kujifunza HESABU.


Lakini,...
... watu wasiposoma inasaidia !

Na kama unanibishia waulize MAPAPA wa KIROMA wakukumbushe enzi zile za waumini kutojisomea wenyewe BIBLIA jinsi ilivyokuwa starehe kuwasimulia watu biblia inasema nini halafu mtazamo wako na TAFSIRI ZAKO unakuwa ndio kweli tupu na hakuna wakukubishia.


Samahani LAKINI PAPA WAKIROMA!

Nilisahau kuwa watu hata siku hizi hawasomi biblia wala korani (ingawa vipo gesti pembeni ya kitanda tukienda kupona), kitabu cha JUMA na ROSA wala KAMASUTRA, na kwa kukubishia HUTEGEMEA ZAIDI ni kwa mtazamo wa nani MWINGINE wanafuata TAFSIRI ZAKE na mtazamo wake katika kuelewa njia ya kwenda mbinguni au tu ile ya LIMBWATA kidume aitulize nyumbani.

Na Lakini UNAYEANDIKA labda usitishike!
Bado tupo tunaosoma na kuandika hata ujinga kwa hiyo MHESHIMIWA ukiandika uandikayo YA MAANA na YAHESHIMA labda tupo tutakao soma hata kwa nia ya KUJARIBU KUKUELEWA TU au kujiweka katika mkao wa kutaka KUKUTUKANA , kwa hiyo usiache kuandika KINGUNGE.
Swali:

  • Au?
  • Hivi nilikuwa naandika kuhusu nini vile?

NA nimeacha KINGUNGE mheshimiwa!
Kumbuka ni wazo tu hapa MAWAZONI!
BAADAYE!
Ngojea Basi ERYKAH BADU alete -FUNKY NASSAU

Read more...

TATIZO la KUJIHESHIMU!

>> Tuesday, April 21, 2009

Kwa kujiheshimu,....
... unajiwekea MIPAKA!

Kwa kujiheshimu,...
... unajikaza ILI tusijue , ujitunzie HESHIMA.
Kwa kujiheshimu,....
.... unajitunzia yale ambayo unayo ila hutakituyaone ili TUKUHESHIMU.

Tatizo ni,....
.... waheshimuo wezi huheshimu wezi na kama wewe sio mwizi HUSTAHILI kwao HESHIMA.

LAKINI Jiheshimu tu huku ukijua kuwa,...
... wasiojiheshimu wanaheshimiwa pia hata kwa vigezo hivyohivyo vya kutojiheshimu.

Kizuri ni,...
... heshima ni kitu cha bure , hakitakukosti hata ngawira pesa mbili.

Tatizo la kutojisheshimu ni,...
......unaweza heshimiwa na wasiojiheshimu!


Swali:

  • Unapendelea kuheshimiwa na wanaojiheshimu au na wasio jiheshimu?
  • Ushastukia kama usingekuwa unajiheshimu , leo ungekuwa tajiri kidoooogo zaidi ya ulivyo sasa na labda ungekuwa umenuna zaidi?

NI wazo tu na NIMEACHA MHESHIMIWA!

Ngojea MZEE MZIMA gwiji la COMEDY a.k.a REDD FOXX aongee kwa heshima ya kujiheshimu katika-WASH YOUR ASS...( WARNING!Lugha chafu na mambo ya WATU WAZIMA)


Au ngojea James Brown aturudishe kanisani ...

Read more...

BINADAMU ni KITOWEO ukijisikia KUMLA au hata KUTOWEZA hata kama ni KWA NYUMA ya MBELE!

>> Saturday, April 18, 2009

ASHKI za kula MTU, si lazima iwe UNAKULA kwa KUTUMIA MDOMO!:-(

MAFISADI kwa KUMLA MTU , wanamuacha na NJAA.

CHEKIBOBU kwa KUMLA MTU , bado anabaki ashaliwa lakini bado ANAHAMU.

MSENGE kwa kula MTU , inasemekana huchagua nakuvutiwa KUMLA nyuma.

ASIYE MSENGE akila, anahisi anakula mbele ila LABDA ni analia mbele ya NYUMA.


MCHUNGAJI WA KANISA kwa KULA WATU , bado mpaka kwa wajinga huwadai SADAKA.

SHEKHE kwa kula ,anaweza asistukie umekaa mkao wakuliwa vizuri kwakua wengi HATA wainamao , wamkumbusha msikitini wakiinama ni katika mkao wa kuomba MUNGU.

WANAWAKE kwa KULA , wanaume waweza kuzidi kustukia utamu mpya wa CHAKULA.

WANAUME kwa UANAMME WAKILA, mama na mwana KAENICHONJO kama mwataka KULA.



WATOTO kwa KULA, mabaki ya wakubwa hayakawii kuwaacha na NJAA kwa ulafi WAKIKUBWA.

WEWE KWA KULA,....
....NYANI kasingiziwa.

Swali :
  • AU?

NI moja ya WAZO ndani ya kucheza na lugha ya KISWAHILI TU!
SAMAHANI usitishike Mheshimiwa!

Ngojea John LEE Hooker akiwa na Carlos Santana abadili wazo kwa kibao...-CHILL OUT



Au tu KUBB wadai - WICKED Soul

Read more...

KIBOXI Manyoya ni aina ya USHAHIDI!( simulizi zilizopinda)

>> Friday, April 17, 2009

MOja ya shughuli ya BINADAMU ni KUTAFUTA MAANA ya VITU!:-(
Na akisikia simulizi za KIBOXI MANYOYA ataoanisha nini kinamjia akilini katika mrengo wa KIBOXI MANYOYA.:-(

Na labda manyoya NI ushahidi kitu ni KUKU au NGURUWE!

KIBOXI MANYOYA labda maana yake UMEKUA!:-(

KIBOXI manyoya LABDA maana yake wewe ni NYOYA na nikipuliza UTAPEPERUKA!:-(


KIBOXI MANYOYA labda ni KIBOKSI cha MANYOYA chini kidogo ya KITOVU pamoja na ukweli kwamba ni NYWELENYWELE na wewe UNAJUA NI MTU na huna MANYOYA.

Kiboxi MANYOYA ni ushahidi binadamu anavisivyo na mpango wala matumizi MWILINI na AKILINI.

KIBOKSI MANYOYA ni ukubwa hata kama bado MJINGA.!

KIBOXI Manyoya labda ni kiboksi chenye MANYOYA na maana yake ni tafsiri za ubongo wako na kama ni mfikiraji wa matusi labda KIBOXI Manyoya ni MATUSI!:-(

Swali:
  • Unauhakika kuna kitu ninamaanisha?
  • Kwani ni lazima kila kitu uelewe mwaniwane?
LIONE VILE!

NIMEACHA na kumbuka nikatika kupitia moja ya wazo katika MAWAZO na ,WIkienDI Njema KINGUNGE!

Ngojea basi kidogo MACY GRAY achokonoe kwa kibao-I TRY


Au tu John LEE Hooker akiwa na SANTANA adai-HEALER

Read more...

Kuna MAMBO huhitaji KUYAELEWA!:-(

Ndani ya mambo MILIONI ndani ya siku,....
.... KUBALI kushindwa yote KUELEWA ili uishi kwa furaha.

KUELEWA sana ni siri ya KUTOELEWA SANA,...
....hasa katika pande na SURA MIA za KITU KIMOJA wakati mmoja.


LAKINI elewa KIELEWEKACHO,...
... kwa kuwa ukijifanya HUELEWI UELEWACHO,...

KUNA JAMBO UNAELEWA!:-(


Swali

  • AU?
NAWAZA tu USITISHIKE!
Ngojea Kool and THE Gang waseme -Hi De Hi Hi De Ho

Au tu YellowMAN adai -AFRICAN CHRISTMASS

Read more...

DUNIA YA MATANGAZO ya TV na MAGAZETI itanifanya mpaka NICHAGUE nani MCHUMBA MZURI kwa kuangalia TAKO!:-(

>> Thursday, April 16, 2009

GHAFLA maoni ya wazazi hayatoshi....
... Wazazi katika uchaguzi wa kigoli hawalipi umuhimu kama magazeti yalipavyo kipaumbele TAKO.

GHAFLA tabia nzuri iliyozoeleka haitoshi,...
.... Nikitazama TV nastukia ni ya kishamba na naogopa nitachekwa kijiweni tukikaa KITAKO.

GHAFLA titi ni dogo na mnuno wa chuchu isiyomumunyika haitoshi,...
... hasa katika staili za siku hizi za hata wasiopata kwa kukuna kichwa wawezapata kwa kukuna TAKO.


GHAFLA hata wastaarabu wavaavyo haitoshi,...
... baada ya kuangalia tangazo sijali roho wala moyo mkubwa, kama nguo itaonyesha japo udogo wa TAKO.

GHAFLA aitwaye modo asiye na tako ingawa alikuwa hatoshi,...
....baada ya tangazo kwenye luninga nimejifunza jinsi ya kuligundua lake TAKO.


Labda na GHAFLA mke nitakayepata atakuwahatoshi,...
... Lakini TV na Magazeti yatakuwa na tangazo nitakaloletewa lenye dawa ya tiba ya huzuni nikikaa KITAKO.


Si hata nitakao wasikiliza wakinishauri haitoshi,...
... na si busara zao zatoka kwenye matangazo na wanapenda kubwa au dogo TAKO?

Matangazo mwanaharamu weye na tuombee iwe hautoshi,...
.... la sivyo kwa waitwao wajanja ubongo utatoka kichwani na kuhamia kwenye TAKO.:-(

NIMEACHA!
Swali:

  • Unafikiri matangazo hata ya pipi hayajakuathiri au kukufunza ununue pipi gani?

NI moja ya wazo tu USITISHIKE!

siKU NJema!

Au tu St Germain waje tena na kibao nikihusuducho kiitwacho- SURE THING...

Read more...

Dhana a.k.a Konsepti ya MUDA na MAISHA katika jicho la MTOTO!

Asubuhi,...
....... jioni ni mbali.

Ikifika Jioni,....
.... asubuhi ni mbali.

Mtoto akifunga macho,...
.... viliombele yake hakuna au viko mbali.

Pembeni ya baba,...
.... mama hayuko mbali.

Na swali ukiuliza,...
.... jibu hata la uongo kutoka kwa wazazi au wakubwa ni kweli tupu na haliko mbali.

Na latosheleza udadisi,...
...... kama na pipi haiko mbali.

Pembeni ya kufokewa,...
.... woga na machozi haviko mbali.

Kwa kugombezwa,...
.... kukua na uwoga hakuko mbali.

Kwa kuchapwa na kutukanwa,....
.... kutojiamini hakuko mbali.

Kwa kupendwa,...
... amani , upendo na furaha havina umbali.



Dunia haitishi kama amani iko nyumbani.

Na dunia yote ni wazazi, ndugu, jamaa na marafiki hata wale buriani.

Labda mpaka mtoto aambiwe na kutishwa , asiyemjua ampitie mbali.




Na kama wewe ni Mzee,....
.... wakumbuka bado kuna mtoto ndani yako kwa ndani?


Kama ni mtoto yatima,....
.... labda ni vigumu kujua wapi na nini nyumbani.

Na yatima utajifunza ya utu uzima,...
... wakati kuwa mzima ni shughuli ya kuotea mbali.


Na ukimgundua mtoto ndani yako, ...
.... kesho haitishi hata kama haiko mbali.

Ingawa kama mtoto ndani yako katishiwa kuhusu ya mende,...
... bado kutishika na mende hakutakuwa mbali.

Na katika maisha yategemea ni mtoto gani wamkuza,...
.... katika maisha haya ujue unaishi maisha gani na ufike mbali.

Swali:
  • Lakini si bado siku yako utotoni ilikuwa ina masaa ishirini na nne kama siku yako ukubwani?


NIMEACHA na ni moja tu ya WAZO mkuu, usitishike!

Tutulie tena kwa kwenda Haiti kukutana na Wyclef Jean ft T Vice + Buju wadai- Party by the sea


Au tu ST Germain wajazzfai tena katika - Rose Rouge

Read more...

Tangazo- "Saturday Night Live!" Pata Muziki na JHIKOMAN!

>> Wednesday, April 15, 2009

Event: Saturday Night Live!
Tukio: Performance
Sehemu: Sweet Eazy Restaurant and lounge
Muda wa shoo: Saturday, April 18 at 9:00pm
Muda wakumalizika shoo: Sunday, April 19 at 1:00am
Mahali: Oysterbay, Dar-es-Salaam

Read more...

Unachotumia nguvu sana kujihami KUKIKANA labda ndicho kinacho KUTAFSIRI, ndicho WEWE!

Nikawaida kukana wengine wakikuhusisha na usichohusika kitu!

Ingawa unaweza kuchelewa kukana kama kitu uhusishwacho nacho kinalipa kitu!:-(

Ukijihami na kukana , ....
......ni wewe umejihusisha na kitu!

Ukikanacho sana, .....
......LABDA ndio kinacho kuwakilisha na KUKUTAFSIRI.

Upendacho kikutambulishe sana , ....
.......LABDA hicho sio chako kitambulisho bali ni chako KIFICHA SIRI.


Na malaya sana, ...
....labda ndiye amshindaye PADRE na ajulikanaye MTAKATIFU kwa kujua staili za kwenda mbinguni zilizo SIRI.

Na padre wa kikatoliki asiyefanya sana,..
......labda ndio amshindaye malaya kwa staili za matumizi ya sehemu za siri!

Na shekhe na mlokole sana,..
.... labda kwa shetani wataenda kwa yao tusiyoyajua ya SIRI!

Swali:
  • Ukitaka ujulikane msomi sana , hakuna uwezekano unajaribu kufanya Ile -BADO HUJAELIMIKA iwe au kubakia siri?
  • Kwa kuhakikishia watu una roho nzuri sana, sio tu udhaifu na mapungufu ya roho ya kibinadamu wataka kuyafanya siri?

Ni moja ya wazo tu usitishike!

Ngojea nimuache Fally Ipupa alete kibao- Bakandja kama alivyokipiga Dar-es-Salaam


Au tupitie Haiti nimuachie tena Misty Jean azungumzie - Maladie D'amour

Read more...

Kama sio lazima KUJIBU, unaweza usijute kwa KUKAA KIMYA!

>> Tuesday, April 14, 2009

Ongea unukuliwe!

Ongea silika yako tusiyoijua umati iuhakikishie!


........AU!.......

Kaa kimya ilitukuaminio tusiyojua tukushabikie !


Kaa kimya na binadamu wako bize ,...
.....yasiyo lazima kwao huyaacha yajifilie!


Kama sio lazima kunena , kaa kimya UKIMYA ukujibie!


Swali:
  • Au?
Ni moja ya wazo tu MKUU!
Ngojea Keith Sweat abadili hali ya hewa katika wimbo -Nobody



Au tu TUPAC aulize - I wonder if heaven's got a Ghetto

Read more...

Uwezekano wa MJINGA KIJANA kuzeeka MJINGA!

Hakuna fomwula za kuacha au kujifunza ,....
......kwa kuwa tu jambo UMELIPITIA!:-(

Unaweza kuzeeka na UJINGA ingawa tokea ujanani ....
.....Ujinga UMEPITIA.

Kwa kupitia kitu unaweza ukachanganyikiwa na kuchanganyishwa zaidi na ...
......usijifunze wala kujua ingawa yote UMEPITIA.

Na kwa kuuzoea ujinga , ...
.... unaweza kukomaa kwa ujinga usiuone tena ujinga na yote ni kwa sababu UMEUPITIA.


Kwa kuzeekea shughuli ,...
... unaweza kuzeeka na shughuli tu, na usijue shughuli UNAYOIPITIA.

Swali:
  • Unafikiri ndoa ihusishayo mabikira wawili ambao shughuli bado hawajapitia sio bora kuliko ya wale waliokomazwa na shughuli na advencha za hughuli wameacha kupitia?

  • Kwani hujawahi kukutana na Mzee MJINGA?



NA bado ni kweli,...
..... kila mtu anachakukufundisha kwa kuwa karibu kila mtu kuna kitu sio MJINGA!
Na,...
.... mjinga anaweza kukufunza jinsi ya kuwa mjinga madhubuti!
Swali:
  • AU?

Ni moja ya wazo tu katika UjingaBUSARA na USITISHIKE!

Siku njema!

Ngojea Sanchez aseme -Baby can I hold U tonight


Au tu Buju Banton na Wayne Wonder wadai-I dont know why

Read more...

Halelujah! Rais Obama kapata MBWA!

>> Monday, April 13, 2009

Binadamu kiboko katika kuamua nini ni muhimu!

Karibu DUNIA NZIMA iitwayo ya kwanza, moja ya habari kubwa ni kuwa Rais Obama kawapatia Mbwa watoto wake!

Na inasemekana ugeni wa mbwa katika WHITE HOUSE ni miongoni mwa ugeni mkubwa hapo Waiti Hausi tokea Obama awe RAIS!

Swali:

  • Wewe kwako nini ni muhimu?

Ngojea tumuone mbwa

Au tumsikilize tena Rais Kibaki akitukumbusha anamke mmoja tu....katika -I have only one wife

Read more...

Kumpenda MPENZI tu labda HAITOSHI ndio maana sio wote kwa kitendo cha kupewa PENZI wanapata MAPENZI!

Inasemekana wanawake hawasikii kama wanaume na wanaume wenye sikio zuri la wanakike , ni wasenge!:-(

Na labda ni kweli kama wewe unamtunza MPENZI au una penzi basi wewe ni bingwa wa michezo ya akili.

Na,...
...hata ukilivutia punzi penzi unaweza kuambulia mwili na sio penzi ndani ya michezo ya akili ya apendaye na apendwaye yenye mwili.


Na usipoangalia huu ndio wakati unaweza kufikiri unapatapenzi, kumbe mtu kafikia hatua ya kuwa anachokupa ni kikojoleo na kiungo cha kutemea mate na sio tena kiungo cha penzi na busu katika penzi.

Na huhitaji kuvutia punzi au kututumua misuli kujua umeachana na mpenzi, kwani kitendo chakumuacha mtu hakihitaji nguvu wala akili:

Siku ya kumuacha mpenzi kimapenzi utajua tu umemuacha hata kama hutamuambia na utaendelea kuendelea kuishi naye katika hii michezo ya AKILI ya PENZI na kutobadili uliyokuwa unafanya wakati unapenzi! Na kikwapa chake utakistukia.


Na katika michezo ya akili, anayechunwa buzi anaweza akawa anajua anachunwa buzi na hiyo ndio kete yake katika michezo ya akili ya PENZI na anajisikia vizuri angalau unaona anafaa angalau kwa kuchunwa buzi, na ni PENZI!

Na pamoja na yote bado nivigumu kuwa na uhakika umepata mpenzi hasa katika dunia hii ambayo mwanamke na mwanaume wanatokea sayari tofauti na swali moja linaweza likawa linataka jibu tofauti na swali hasa kama ni mwanamke anauliza na sio katika PENZI.

Na bado,..
..... katika MICHEZO YA AKILI hata kulia IMO , ingawa wakati unalia ili mpenzi AKUONEE HURUMA, unaweza ukawa unalia kirahisi kwa kufikiria lile shamba la mihogo ambalo mkiachana ndio nalo limetoka hivyo:-(


NIMEACHA!
Nawaza tu kumbuka hilo MKUBWA!

Swali:

  • Unauhakika gani kuwa wapenzi uwaonao wanapendana na sio mmoja ndio ampendaye mwingine?

Namuacha Erykah Badu adai - Didnt cha know


Au tu Arrested Development waseme- Mr Wendal

Read more...

ASIYEAMINI zaidi ya YA UBINADAMU kapungukiwa, na AAMINIYE MUNGU au hata ya SHETANI anaishi maisha ya kujifunza IMANI na kutafuta UKWELI mpaka AFE!

YAKIBINADAMU tu hayatoshi,...

.... YA MUNGU yanachanganya.....
.... na ya SHETANI hayakawii kuisha UTAMU.



Binadamu katika kujazia mapungufu, .....
..... hujaribu kuongezea ya MUNGU, Miungu au hata ya SHETANI
na ukweli katika imani kirahisi tu unaweza kujikuta unapitia

  • Kutokuwa na IMANI,
  • Kujifunza Imani,
  • KUAMINI ,
  • kupungua imani,
  • kuacha kuendekeza imani na hata mwisho kuanza KUAMINI TENA!
Yote huwezekana ndani ya maisha ya binadamu!

Na ukifa wakati tunaamini unaamini tunachoamini kama vile MUNGU, katika mazishi yako tutadai umeenda MBINGUNI!

Na tukiwa na wasiwasi na imani yako wakati unatutoka, BADO tunaweza tusikiri hadharani kwa kusema tunauhakika unakwenda kwa SHETANI ingawa kwa kimoyo wazo hilo lipo.

Swali:
  • AU?


Kuna sababu karibu kila jamii DUNIANI kuna kitu inaamini ambacho kinaoanishwa na kuwa na uwezo kuliko binadamu hata kama hicho kitu ni binadamu kama walivyokuwa MAFARAO Misri.

Na atafutaye jawabu na faraja KATIKA IMANI ashawahi kukwama kibinadamu!

Na kama ushawahi kukwama kibinadamu labda ushaanza kuwa na BUSARA.

Swali:
  • AU?
  • Bado hushangazwi kwa wasiojua vizuri hata dini zao walivyonauhakika na kasoro za dini za wenzao?


NAWAZA TU MKUU hapa MAWAZONI usitishike!
Tutulie na Black Uhuru waulize- What is life

Read more...

MTOTO mzuri NAKUTAKA!-(simulizi za asiyenacho!)

>> Saturday, April 11, 2009

Unatamanisha kwa kuwa SIJAKUPATA!:-(

Na labda hunogi AKIKUPATA:-(

Ingawa katika maisha hakuna anayepata,....
..... bado waitwawo wajanja wanafagilia ambao tunahisi kunakitu wanacho ambacho HATUJAPATA.

Na katika maharage bado UPO ndio maana hata katika mboga kuna MBATATA!:-(

Na kabla hujanipa MATATA,.....-
....kumbuka kama uko hai hata kama huna TITI LA KUTOSHA, labda wewe MATATA.:-(

Na JIAMINI tu katika huo UTATA!:-(

Swali:
  • AU?

DUH!

NIMEACHA na ninawaza tu MHESHIMIWA!


Ngojea SHABA RANKS aonee wasenge katika kibao - WICKED IN BED


AU tu tuendelee na LAGBAJA katika -SKENTELE Skontolo

Read more...

Lione vile LIMEJINYEA! Hadharani MENGI hatufanyi yanogayo FARAGHA usipotakakutia AIBU MTU mwanawane, INGAWA INANOGA!:-(

>> Friday, April 10, 2009

FARAGHA bomba ya kitu labda ndio maana ndio kutengenezewako watoto!


Hadharani nishai ndio maana MPAKA wapenda ngono wanaweza kukupiga MKONG'OTO ukionja hadharani kama vile hawajui kwanini unaonja , kama Padre wakikatoliki asiye MBONGO!:-(

Na labda padre asiyeonja anatubu faraghani kwa kumfikiria tu hata muumini mwanana akaaye kiti cha mbele kanisani ambaye anahisi faraghani au hadharani akibinuka kunatatizo la dhambi hata ambayo haijatendeka inatendeka.

Swali:

  • Umestukia ni hadharani tu unawatia aibu WATU?
  • Umewahi kujiuliza kama MUNGU anakuona mpaka chooni wakati unafikiri hujamtia aibu hata kwa staili yako ya kuchamba?

Kumbuka hata ukijinyea faraghani tusipojua ni poa tu !

Na labda,..
..... waheshimiwa wanaheshimiwa kwa yasiyo faraghani na ndio maana labda WANAHESHIMIWA!
Swali:
  • AU?
NIMEACHA
Na kumbuka ni moja ya wazo tu hili na labda ni lakijinga kwako MHESHIMIWA!


Narudi tena NIGERIA kwa the best Afro Beat artist ever in my opinion kwa jina LAGBAJA aseme -FEYINE

Au alete -Gragra

Read more...

Heri ya KUFIWA na YESU!

Lakini,...
...HERI ya PASAKA labda pia PAMOJA na YOTE , ni HERI ya kuokolewa kwa waumini HASA waaminio walitakatishwa kwa YESU KUFA, hasa kwa waaminio kwa IMANI!
:-(


Swali:

  • AU?
Labda ni kitu kizuri kama wewe ni miongoni mwawaokolewao na damu ya YESU!:-(

Tatizo ni...
.... katika vigezo, VIGEZO vinaweza kusisitizia tarehe , au tu leo, au TU wewe, na sio kutokana na nguvu ya imani.:-(


Swali:
  • Unauhakika hii ndio ile tarehe?

  • Unauhakika kama HII sio tarehe huhitaji kutubu kwa kusherehekea siku ya kufa MAREHEMU wakati sio siku yenyewe marehemu alikufa?

  • Kama wewe ni Mkristo unasikiliziaje CHANSI zako za paradiso leo hii ya PASAKA?
  • HIVI ni kweli wewe MUUNGWANA huwa unafurahia KUFIWA na ALIYEKUPENDA ?

Heri ya PASAKA!
Na labda kama unaamini kwa hilo, HILO ni kweli na LEO NI PASAKA!:-)

Na NIMEACHA!
KUMBUKA nawaza tu na niombee au tubu kama unakwazika!


Labda tupate BISO na BISO...


Au Ali KIBA amuongelee -MAC MUGA...

Read more...

KATIKA kutostukia nyege za UPUUZI mpaka baadaye kidogo baada ya kumalizia KUFANYA UPUUZI!

>> Thursday, April 09, 2009

Wapuuzi wengi hawana nia ya kufanya UPUUZI, nikatika kumalizia kitendo wanastukia au kustuliwa kilikuwa ni kitendo cha kipuuzi!:-(

Na,...
... upuuzi NISHAI!
Upuuzi wa LEO unaweza usiustukie mpaka MWAKA KESHO,

....Na...
Isingekuwa hivyo waheshimiwa wengi wasingeumia roho baada ya kufumaniwa baadaye kidogo baada ya kuwa WAHESHIMIWA kuwa yaliyowapa sifa JANA labda hata uheshimiwa, karibu yote LEO ni UPUUZI.

Na labda,...
.... wengi wasiofanya UPUUZI hawafanyi upuuzi kwa kuwa hawajitahidi kutofanya upuuzi bali wamebobea TU kujaribu kuishi tu LEO maisha yao kama kawaida , kama ilivyokuwa JUZI.

Na ,....
... wale wajitahidio kutoonyesha upuuzi wanasifa labda hata za kujisifia,...
.... ingawa....
ukiwaangalia wengi wao wamenunia shughuli nzima leo usijekushuhudia wakifanya upuuzi leo ingawa kama kawaida ya ubinadamu wapo WATAZAMAJI na WASIKILIZAO wasubirio mpaka kesho kutafsiri ya leo.
Swali:
  • Unauhakika mheshimiwa ahitajiye kuheshimiwa sio mpuuzi kwa hilo?
  • Unauhakika hujawahi kubadili mawazo kuhusu ulichodhani ni upuuzi na leo unadhani ni njia ya kwenda mbinguni?

Ni kweli kabisa,...
... wengi wakati wanahangaikia kukwepa upuuzi hufanya UPUUZI kwa kuwa vigezo vyao vya kwanini sio upuuzi ndio KIINI, MISINGI na tako la UPUUZI!

Sikubishii lakini ukinibishia!
Naacha UPUUZI kama unauhakika nilichoandika ni upuuzi!:-(
Swali:
  • Unauhakika wakati unataka kumbishia ambaye haelewi utakachokufanya sio UPUUZI kama hujajaribu kumelimisha?


Kumbuka HATUKUONI na USIJIHAMI!:-(

siKU Njema!

Hebu tumsikilize AL PACINO katika sinema SCARFACE....atoe -BAD GUY SPEECH (jihadhari lugha chafu!)



Au tena Les Wanyika wamuongelee -Paulina

Au tu twende Ivory Coast tukutane na Joelle C - MAN DINKA

Read more...

Hivi hamu ya kuwa kama WAZAZI WAKO hufifia?

Wakati unataka kuwa kama WAZAZI wako LABDA ni kweli wazazi wako hawataki uwe kama wao!

Kunauwezekano kabisa wazazi wako wanataka uwe kama WAZAZI WAKO walivyotaka kuwa na ikashindikana .

Na ni kweli,...
.....ukizaliwa tu wazazi wako ndio wanakuwa kioo chako na kama wanaongea Kichina kunauwezekano utaongea KICHINA.

Swali:

  • Unauhakika kuwa wewe hujawahi kama bado sio Mkristo , Muislamu au Mpagani kutokana na wazaziwako kutoamini kuwa ubinadamu ni dini?

Lakini ,...
..... wewe sio WAZAZI wako!:-(

Wazazi wako wanaweza wakawa wamefanikiwa mpaka unaweza ukataka kuwa kama WAZAZI WAKO,.....

....Lakini...
.... wewe ni WEWE!:-(

Na unaweza ukawa ni miongoni mwa ambao hawakulelewa na wazazi wao wakibaolojia lakini kuna waliokuwa kiioo chako cha maisha hata kama ni cha jinsi ya kuwa ombaomba au jambazi,...
...na....
....hao ni wazazi kinamna kama katika kundi, ni hao unaweza kukiri walikuwa kama wazazi wako wakati unawaelezea WATU kuhusu hao ila unataka tujue hawakukuzaa.

Labda hamu ya kuwa kama wazazi wako ikififia ndio mwanzo wa KUWAKOSEA HESHIMA wazazi.

Kabla hujaacha kuheshimu wazazi kwa KUSHINDWA KUFIKIA KUSTAHILI , jaribu kupata jibu la kiswali KWANINI....
  • Kwa nini wameshindwa
  • Kwa nini wangefanikiwa
  • Kwa nini
  • Na kwanini unafikiri jibu la yote ni kutoWAHESHIMU.

Na bado binadamu pamoja na kuwa tofauti, jinsi wengine walivyo kunasaidia kutengeneza sisi tulivyo.

Mwingine akivaa JINSI anaweza akawa ndio sababu tunavaa KODRAI .

Mwingine akivaa KODRAI labda ndio sababu tunavaa KODRAI.

Hamu ya KUTOKUWA inaundugu na HAMU YA KUWA, na kwa hivyo anayetaka KUWA kama wazazi wake na ASIYETAKA wote wanafanya jambo moja ukizingatia kuwa hakuna mtoto aishiye katika umri na wakati sawa na WAZAZI wake . Nikiwa namaana wakati mtoto ana miaka mitano mwaka 2000 labda Mzazi alikuwa ana miaka hiyo mitano mwaka 1960 na hauwezi kulingana na wazazi wako ingawa mnaishi pamoja.


NAWEZA kusema,...
.....ukitaka kuwa kama wazazi au usipotaka kuwa kama wazazi vyote ni vitendo vya kujaribu tu lisilowezekana.
Swali:

  • Unauhakika kuwa unamjua hata mtu mmoja aliyefanikiwa kuwa kama wazazi wake?
NI MOJA ya wazo tu na sio kweli tupu!

Baadaye!

Ngojea Bozi Boziana anisaidie kubadili hali ya hewa kwa kibao-Demayo

Au Peter Tosh arudie kuongelea msiba katika -Burial

Read more...

Kama ungekuwa na ukubwa wa SISIMIZI na unajaribu kuelewa ukubwa wa MTU!

Inawezekana kwa SISIMIZI mtu haonekani na maisha ya mtu kwa sisimizi ni MILELE.

Na ukipiga teke jiwe alilopo sisimizi lika vuka mfereji na sisimizi , kwa SISIMIZI ataona MUUJIZA umetokea kama tu ukidondosha kibonge cha sukari na kumletea SISIMIZI kitoweo pale asipotarajia.



Swali:

  • Ushawahi kujiuliza kuwa labda MUNGU wa BINADAMU hasa yule wamuaminiye wawamuaminio MUNGU ASIYEONEKANA , haonekani kwa binadamu kutokana na UKUBWA TU kama SISIMIZI asivyomuona MTU?
  • Ushawahi kustukia kuwa hata utumbo wako ni ulimwengu wa baadhi ya bacteria ambao wanaumbwa na kufa kabla yako MUMO KWA MUMO wakiishi kwa manufaa yako ya kulainisha chakula na kukusaidia kukutengenezea kinyesi bomba?
Na ukimkanyaga sisimizi ni kiama kwa sisimizi!:-(

Nimeacha!
Na ni moja ya wazo tu kumbuka!

Badili Mudi kwa kusikiliza En Vogue wadai -Dont let GO...


Au tu Michael Jackson aseme -WORKING DAY and NIGHT

Read more...

Katika kuendelea kuchunguza USHUJAA wa SHUJAA!

>> Tuesday, April 07, 2009

Shujaa ni shujaa kwa sababu anafanya usichofanya ukitumia AKILI.


Na kumbuka,...
... mashujaa karibu wote HUKUMBUKWA kwa JAMBO MOJA TU la kishujaa LILILOSHUHUDIWA katika maisha haya ya binadamu yenye mambo mengi YASIYOSHUHUDIWA.

Na ni kweli,....
.... unahitaji jambo moja tu ili ukumbukwe kama SHUJAA au MJINGA.

Na tendo la kishujaa karibu mara zote hukaribiana na tendo la KIJINGA zaidi kuliko tendo la BUSARA ndio maana ukikosea kidogo tu, jitihada zako za kutaka kuleta ushujaa zinaweza kutafsiriwa kuwa ni UJINGA.

Swali

  • Unauhakika wewe sio shujaa na hatujashuhudia tu TENDO MOJA lako ambalo litakuoanisha wewe na neno SHUJAA?


Kumbuka tu ,....
... mjinga umjuaye kwa ujinga kwa kuwa umeshuhudia ujinga , kuna wamtambuaye kwa jina shujaa kwa kuwa WALISHUHUDIA wake USHUJAA!


NIMEACHA!
Tupumzike kwa kubadili hali ya hewa na kusikiliza ni kitabu gani hakiuziki Kenya wakati tukifikiria ya Tanzania...

Ngojea JAMES DANDU aongelee- MPENZI


Au tu REMMY ONGALA aulize- MIZIKI ASILI YAKE WAPI?

Read more...

HUZUNI!

Moyo leo unauma na wataka KULIA,....
... ingawa YAKUHUZUNISHA kila siku yako maishani mwako kushoto na KULIA.

Wakati unacheka, yahuzuni kicheko hayajakitangulia,.....
.... lakini yapo na ukihuzunika si lazima UTALIA.

Na labda dawa ya HUZUNI bado ni KULIA!:-(


Swali:
  • AU?

Nawaza tu mkuu USITISHIKE!


Pata WORDS of WISDOM kutoka kwa -Muhammad s.a.w!!


Au ngojea MUNISHI adai -MSIABUDU MAREKANI....

Read more...

FURAHA!

Ni mchanganyiko wa kemikali UBONGONI ukuambiao UNAFURAHA na kikufurahishacho ni katalisti tu a.k.a kichocheo, kisaidiacho ubongo kukushawishi kuwa UNAFURAHA.

Na kwa kawaida Homoni , Nevu,....- mwilini , husahaulika katika mchango wake katika kufanya kikufurahishacho kikufanye UNAFURAHA.:-(

Na kwa kuwa tunafurahia FURAHA bila kutafakari ni nini HASA kiko kwenye kitufurahishacho kwenye FURAHA,...
... daima kitaadimika hiki kitu FURAHA!



NAWAZA tu usistuke!
Swali:
  • AU?
  • Unafuraha?

Au pata WORD OF WISDOM ya kinamna kama unamoyo....


ASANTENI Ndugu, jamaa , marafiki pamoja na MAADUI!

Asanteni sana wadau wote ambao wengine ni hawa kwenye picha nilizodakwa na kudaka juzi ya jana ya juzi.......


Photobucket

Photobucket

Photobucket



Photobucket

Photobucket




Photobucket





Photobucket


Photobucket



Photobucket



Photobucket


Photobucket






Photobucket


Photobucket



Photobucket


Photobucket


Photobucket


Photobucket



Photobucket


Photobucket



Photobucket


Photobucket



Photobucket






Photobucket

Photobucket

Read more...

Kunauwezekano UKAKATISHWA TAMAA kwa kumjua unaye M-ADIMAYA!

>> Monday, April 06, 2009

Labda ,..
... umzimiaye KWA HILI hana kasoro katika hili kwa sababu HUMJUI!

Ukianza kumjua umzimikiaye na kama hujapofuliwa na UKIZIMIACHO, labda UMZIMIAYE ndiye bingwa wa USIYOYAZIMIA.


Lakini ku -ADI-MAYA mtu bado ni bomba kama kuna kusaidia kupata nguvu mpya ya kufanya tendo badala ya kulifikiria tu TENDO.

Na labda unaye M-ADIMAYA kwa sura na umbo zuri ndiye mwenye tabia MBAYA.
Na labda unaye M-ADIMAYA kwa kumsikia tu, ukikutananaye ndio itakuwa mwanzo wa chuki yako kwake.

Na labda kuna unayemnunia kwa hili lakini ungejua lake lile sasa hivi ungekuwa unajishughulisha akuone ili UMCHEKEE.
Swali :

  • Bado unauhakika unataka kujua zaidi kikufurahishacho wakati unajua kunauwezekano kwa kujua sana hata maziwa, ni kweli maziwa ya mtindi ni maziwa yaliyoharibika na unayanywa kwa sababu za kutoyafikiria kuwa yameoza?

NAWAZA TU usitishike!
SIKU NJEMA!

Tulia na THE POWER OF ONE...

AU ngojea Peter Tosh adai- Wanted Dread and ALIVE

Au tu aseme tena katika -WHY MUST I CRY!

Read more...

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP