Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Kuhusu ule UHAKIKA wa HATA kumpa MIMBA mtu KESHO!

>> Tuesday, May 26, 2009

Uhakika wa ya vitendo vya binadamu LABDA ni kama wa mbegu za kiume mamilioni zipiganiazo yai moja la kike wakati mmoja na kwenye shahawa zenye mbegu mabilioni ,mbegu mshindi kwa kawaida ni moja.


Chakutia moyo ni kwamba,...
..... katika mbegu mamilioni moja ikifanyakazi yake binadamu tutasahau uzembe na bahati mbaya za mamilioni ya mbegu kwa sababu mbegu moja imehakikishia uhakika!


Chakutisha ni kwamba,...
..... mamilioni husahaulika kwa sababu tu ya vurugu ya moja na kama hilo moja lina pua kubwa kuliko sura ndio imetoka hiyo kwa UHAKIKA.

CHA KUTISHA ni kwamba,...
.... hata sasa hivi unavyonisoma , kunashughuli mamilioni lakini kuwa kwenye internet ndio iliowini na shughuli ya kwenda kumvizia SISTA wa KIKATOLIKI umgeuze awe mke wako kwa sasa hivi labda ndio imetoka hiyo kama hayuko mtandaoni , e-mail hana na gia za kumuingilia bado hazijaandikwa mtandaoni.:-(

DUH hivi nilikuwa natakakuongelea nini vile?

Ok turudi kwenye swala la UHAKIKA KESHO!

Na KUHUSU KESHO,..
...sina UHAKIKA!:-(

Uhakika wakumalizia leo yenyewe SINA UHAKIKA, ingawa ni mwepesi kudhania mipango ya kesho nimeimaliza.

Na KUHUSU MIPANGO YAKESHO,...
...sina UHAKIKA,...
.....Ingawa nasifiwa kwa hata mipango ya kesho kutwa kwa jinsi nilivyoipangia ratiba na kuisimulia kwa UHAKIKA!:-(

CHA ajabu NAANZA kuwa na wasiwasi na hili neno UHAKIKA kuwa labda lina kasoro kama likitumiwa na BIN-ADAMU kudai anauhakika!:-(

Swali:

  • Inawezekanaje Mtu akawa ni binadamu halafu anauhakika?
Sikubishii!

Labda,...
... unauhakika na hata wakwenda Mbinguni ingawa hupajui mbinguni ingawa hata kwa kulia utashuhudia kwetu siye walokole kuwa UNAUHAKIKA!

Na labda ni kweli ,....
.... ninauhakika sitakupa MIMBA, kwanza sikujui halafu labda weye TASA kama tu WEYE ulivyokuwa na uhakika kuwa sasa hivi hujabanwa mkojo!

Halafu HAPA labda wote tutabishania ni nini unauhakika na kipi unadhani kila mtu inahitajika awe anauhakika na lazima kuna uhakika , lakini MUHIMU KULIKO VYOTE;....
  • Unauhakika wewe ni kweli ni wewe na sio akili zako zinakuchezea akili na ukweli labda wewe ni yule?

Narudia;..
  • Unauhakika wewe ni wewe ?
  • Unauhakika wewe ni nini?
NIMEACHA wazo Kingunge na kumbuka ni moja ya wazo tu USIZINGUKE!
Nakutakia siku KIBONGE Mkurugenzi ndani ya lako LIBENEKE!

Ngojea Sade abadili hali ya hewa...-King of Sorrow..




AU tu Sade arudishe tena -Smooth Operator..

2 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Yasinta Ngonyani 6:28 pm  

kazi kwelikweli na nakusifu kwa kuwaza!!:-(

Simon Kitururu 5:50 am  

:-)

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP