Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Unafikiri wakati unananihii huwa ni kweli UNANANIHII, au UNANANILIWA?

>> Monday, August 31, 2009

Kuna WANANILIWA ukiongea nao ,...
......utagundua wanafikiri WANANANIHII!:-(
Swali:
  • Unafikiri wakati Rais wa Tanzania anaomba UGENINI huwa anakumbuka kuwa awaombao wali KOMBA na kwa kuomba anawahakikishia watazidi kukomba?
  • Unakumbuka KWA KAWAIDA umuombaye akakupa hahitaji kukuomba kabla hujafikiria kumpanulia hata kabla hajalilia?

NI hilo tu na ni WAZO TU Papaa MUZEE au tu wewe SHUGA DADA!
JUMATATU NJEMA lakini Mheshimiwa!


Twende tena Trinidad kupata CHUTNEY MUSIC kutoka kwa Chris Garcia katika kitu- Chutney Bacchanal


Au tubakie tu Trinidad tupate SOCA MUSIC kutoka kwa David Rudder katika kitu- Trini Tuh D' Bone

Read more...

Katika KUOMBA umeshastukia kuna wasahauo wakiomba kikojoleo, WAOMBACHO kweli ni KIKOJOLEO?

[Tahadhari: Sina uhakika na maudhui ya taralila hii!:-(]

Wakati kiombwacho hutumika kukojolea,...
.......labda ukikiomba kwa kutaka kufaidisha MADHARA mengine kama ya kujaza chupi, bado ulichoomba kuna uwezekano mkubwa BADO ni KIKOJOLEO!

NDIO!
Tunaweza tukabishana hapa kuhusu kitu cha mende kwa kuwa hujaona wake mkojo kwahiyo sio kikojoleo,...
... lakini LABDA bado inawezekana atakaye kiti AJARIBUCHO KUSEMA ni anataka kipumzikio cha tako ingawa labda KILICHO CHOKA si tako na wala si KIKOJOLEO.:-(

Ndio!


Na inadaiwa kuna apataye ujauzito akikojolewa kwenye kikojoleo,...
...ingawa kuna mimba au hata UKIMWI uzawadishwao na vikojoleo, ingawa mara nyingi kwenye sentesi zihusuzo hayo ziwakilizwasho na WAHESHIMIA huwa zinakwepa kugusia HILO au TU ni kweli mpaka na gono na kaswende huzawadiwa NA hata urembesheje hoja, BADO msingi wa yako hoja wakati unapongeza hata waliopata mtotot U, huwa unachopongeza ni UJEMEDARI wa vyao VIKIKOJOLEO.


Na hata woga wa kwenda JEHANAMU labda ni kama tu kikojoleo,...
... kwa kuwa unawafanya watu KATIKA KUJIPENDEKEZA KWA MUNGU wadai wanapenda dini na utakatifu wakati wanacho maanisha wala sio kupenda dini bali NI woga wa kufa na kwenda jehanamu kifanyacho waogope kutangazia umati kuwa WANAJIPENDEKEZA TU KWA MUNGU HATA WASIYEMUONA NA KUMUELEWA kwa KUWA waogopacho ni kuonekana hawafai katika jamii IAMINIYO ukifa utaenda SEHEMU FULANI ingawa hujui NI WAPI ndio maa na unajiita tu MWANA DINI na wafikiri Mungu ni bomba au ili tufikiri unafikiri MUNGU NI BOMBA ingawa labda wakati huo una tamaa KEDEKEDE za matumizi ya KITOBO na unaogopa kutumia TOBO kwa kuwa dini na ya MUNGU yanamasharti hasa katika swala zima la kutumia tundu mbalo hutumika kukojolea pia kwa hiyo bila aibu nitaliita KIKOJOLEO

KUMBUKA tu kuna watu kwa kukuambia WANAKUPENDA kuna uwezekano wanajaribu kukuambia wanataka kukitumia chako KIKOJOLEO!:-(
Swali:
  • Unauhakika hapa sija tukana kweli?:-(
  • Unauhakika tusi huwa halimaanishi tu usichotaka au jamii isichotaka kusikia?

NALIKATIZIA WAZO hapa ila kumbuka HILI NI WAZO TU Mkubwa!

Ngojea Third World waongelee kuhusu ya -Now that we found love


Au tu Aswad warudie-54-46 was my number

Read more...

Sababu za hamu ya mtu KUMCHUNGULIA mtu!

>> Saturday, August 29, 2009

Kunakitu unataka jua,....
Wadhani utafananisha ukijua,....

au wataka ujue ili ufananishe na usicho na uhakika unajua,...
Lakini labda hata KUKU umeshawachungulia FARAGHA bila kujua,...
....ndio maana bata wakiwa katika shughuli za FARAGHA huhitaji kupiga chabo mara mbili kwa kuwa wafanyacho TAYARI unajua.


Tatizo ni kwamba binadamu wote kuna kitu hujifanya wanajua,..
....ingawa wote hufa wakati kuna kitu hawajui ingawa labda ya mbinguni ni moja wapo ya waliotaka kujua.:-(

Na chakuchekesha kuna akuchekaye kwa kutokujua KWAKO hili wakati KIRAHISI ATATAKA KUKUCHUNGULIA kwa kuwa kisiri tayari kwa UBINADAMU ANAJUA kuna kibao kumzidi unajua.

Kwahiyo naweza kusema hamu ya KUCHUNGULIA ni moja ya jinsi ya KUKIRI HUJUI au huna UHAKIKA kama ni kweli UNAJUA.

Kumbuka tu pamoja na wengi kusifia wanao jua , KUNA MAMBO WENYE AFADHALI ni WASIOJUA.


Lakini:

  • Unauhakika unajua?
  • Na unauhakika wajifanyao wajuzi ni kweli WANAJUA?
  • UNafikiri usingejua kuna sukari na chumvi usingenogewa tu na AISHIKIRIMU YA UKWAJU isiyo na sukari au tu MLENDA usio na chumvi?


NI HILO TU na ni wazo tu MHESHIMIWA!


Au tumtembelee tena mwanadada aongelee YA MBWA anayojua chini ya kichwa cha habari[Tahadhari: Usiangalie kama mtoto au ni Mkuu wa kukwazika au tu unakwazika kirahisi!:-(] -Bestiality Woman



Ngojea tusikilize tena maswali aulizwayo mchungaji na watoto kuhusu NABII ISSA au tu kama kwa wengine ajulikanavyo kama YESU katika-Awkward Questions about Jesus

Read more...

Wakati mtu ANAJISHUKU!

Kuna kasoro MTU alisha istukia au kuihisi,....
.... kama hata kwa sisi kuangalia upande aliko tu kunatosha kumfanya mtu AJISHUKU!:-(


Na bado kuna kitu anajua au kukihisi,....
.... tayari, kama WATU waongeayo hata ASIYOYASIKIA au hata ayasikiayo YASIYOMUHUSU cha kwanza anahisi ni YEYE anaongelewa hata tu kwa KUJISHUKU!:-(


Kujishuku au tu kasoro za kujihisi,...
... kwaweza KUCHANGIA na sio KUBOMOA kama tu utasawazisha UNAYOJISHUKU.


KUJISHUKU hakuna la zaidi ya kuhisi,...
.....au kusababisha tu ujipotezee muda kwa unalojishuku TUNAHISI hasa kama cha zaidi linakuacha bila PEMBEJEO au MORI WA KUSAWAZISHA na ukweli labda UNAJISHUKU tu na wala kimaisha chupi haijakuingia mnato na unajisumbua bure kubadili mwendo kwa KUJISHUKU kwa kuwa hakuna mwingine zaidi yako limjialo kichwani AHISI na au tu ASHUKU!:-(

Swali:

  • Au?
  • Unafikiri hata watu wahisi bila wewe kujishuku kuna kikuathirishacho?


NI HILO TU!


Hebu Werrason alete za -Sous Sol


Au tu Awilo Longomba amzungumzie-Carolina
















Asanteni wadau wote Wakiwemo Claudius na Cliff asante kwa baadhi ya picha hizi hapa....
Photobucket




Photobucket



Photobucket




Photobucket





Photobucket



Photobucket



Photobucket




Photobucket




Photobucket




Photobucket



Photobucket




Photobucket



Photobucket

Read more...

MTU muhimu!

>> Friday, August 28, 2009

Kuna uwezekano unahitaji kujisikia MUHIMU na mtu MUHIMU kwako ni yule akupaye nafasi au sababu za kujisikia wewe MUHIMU.


Na labda kuna kitu unahitaji na UMUHIMU WA MTU kwako sio huyo MTU bali ni KILE KITU mtu akupacho ambacho ndio kwako kina U- MUHIMU!


KWA HIYO labda huna MTU MUHIMU KWAKO na UMUHIMU WA MTU kwako ni yako tu MAHITAJI mtu akupatiayo udhaniayo ni MUHIMU!

Ndio !
Labda umuhimu wa ndugu, WAZAZI, limchumba, poozeo, SHEKHE, mchungaji, PADRE, malaya,......
...... umuhimu wake ni kama tu ASPRINI au KWININI kama kutibu swala NI MUHIMU ingawa hapa swala lenyewe sio ugonjwa ila katika kusikilizia UTU WAKO kama MTU lina UMUHIMU!

Kumbuka tu hata jambo lisilo muhimu laweza geuka kwako kuwa muhimu UKILIPA UMUHIMU!


Swali:

  • AU?

Ni wazo tu MHESHIMIWA na nakutakia SIKU NJEMA!


Ngojea Jean Knight amzungumzie-Mr Big Stuff


Au tu Kaysha adai kastukia-Somethin' is going on

Read more...

Baadhi ya sababu zimfanyazo BINADAMU atake KUHESHIMIWA!

UDHAIFU ndio sababu kubwa ya binadamu kufarijika AKIHESHIMIWA!


Unaruhusiwa kunibishia lakini!


Na katika BINADAMU kuhangaikia KUHESHIMIWA asilimia kubwa za awaheshimuo ni kwa vigezo vyao vya KINAFIKI vionyeshavyo UPANDE MMOJA WA YAO ili kuficha upande mwingine wa YAO au tu ili kulenga UDHANIE ni WAHESHIMIWA!

Ndio!

INASEMEKANA kila mtu anastahili HESHIMA kwa hiyo usiemjua LABDA sharti UMUHESHIMU kama hujui yake yaliyovulia nguo HESHIMA .


Ukifikiria zaidi labda ni busara kutowachunguza sana uwaheshimuo kama unataka KUWATUNZIA heshima!


Swali tena:

  • Hivi kwa kuwa heshima ni kitu cha bure hudhani inachangia HESHIMA kuheshimiwa kama vitu uvijuavyo vya BURE?
  • Hivi huwa unakumbuka kuheshimu vya bure?

  • Hivi si kuna uwezekano kama wewe si MDHAIFU basi huhitaji na hakikusumbui kujua ni nani AKUHESHIMUYE?



NALIKATIZIA HAPA HILI SWALA la heshima na labda ni la kijinga KIHESHIMA!

Twende tu BURUNDI kwa Khadija Nin alete kitu -Wale WAtu



Au tu ngojea tena Khadija Nin amzungumzie-Mama

Read more...

Uhusiano wa WAHESHIMIWA na USIVYOVIHESHIMU!

Mara nyingi BINADAMU huheshimu mtu bila sababu MAALUMU.


Na BINADAMU anaweza akajikuta mpaka anaongozwa na AWAHESHIMUO bila kuchunguza wampelekapo WAHESHIMIWA ambao labda sio waheshimiwa kwa kuwa hawastahili HESHIMA.

Hili ndilo sababu kubwa isababishayo MTU kujikuta anaongozwa hata katika yale ambayo angetakiwa AONGOZE!

Na heshima labda ni kitu tokea UZALIWE huwa UNAKUWA na hamu nacho kitu ambacho kinaweza kukuponza ukajikuta wasio stahili heshima ndio wana chati katika HESHIMA YAKO kwa kuwa ndio wenye KAULI na MAPOZI uyazimiayo au jamii iliyokufunza kujali na kwa hilo WAMESHAKUTONGOZA na kwa hilo unasifiwa UNAHESHIMA.

Swali:

  • Unauhakika hufuati viongozi wakuongozao wakati labda huna sababu maalumu zikufanyazo uamini HAO wanajua waendako wakati WANAKUONGOZA?

NI WAZO TU MHESHIMIWA!


Twende kidogo ZAMBIA tukutane na Kachanana alete za -Mbululuka

Read more...

KAMA UNAJULIKANA KWA HESHIMA NA SIO kwa ya KIPUMBAVU na UJINGA!

>> Thursday, August 27, 2009

Swali:

  • Unakumbuka kama unafanya yenye heshima maana yake unajua tofauti ya YAKIPUMBAVU na YA HESHIMA?
  • Au wewe ni yule aaminiye ya KUBAHATISHA kiheshima?

NI HILO TU!

Read more...

KUHUSU Kijambio!:-(

>> Wednesday, August 26, 2009

Swali:

  • Hivi unakumbuka NI KWELI kijambio hutumika zaidi KUJAMBA zaidi ya tumizi lake LIJULIKANALO KWA UMAARUFU au liitwalo KUNYA?
  • Hivi unakumbuka ingawa wewe ni MSTAARABU itakuwa BOMBA LA shida kwetu kama tu KWAKO ukishindwa kujamba wakati unahitaji kujamba na HASA ukishindwa kuachia ushuzi MPAKA KWENYE ILE KONA AMBAYO KWA KAWAIDA ndio kona ujisikiayo huru sana AU tu TUIITE jina BAFUNI ambako ULIKOZOEA KUJICHUNGULIA MAENEO au TU ulikojaribia mara kwanza kuonja KAMASI ?
DUH!
NI hilo tu na ni WAZO TU Mheshimiwa!:-(

Ngojea basi tumuachie Mjamaika Usain Bolt aonyeshe jinsi ya kukimbilia choo ukibanwa..



Au tu tumuachie Mjamaika mwingine kwa jina Burro Banton alalamike tena katika kitu--Sekkle Yourself

Read more...

DADA MIRIAM na : www.TasteofTanzania.com

Hi friends!

Sorry for being silent for a while now. I have been dealing with a few issues. Now it is time to come back and continue what I started year 2004.

With Masters of Information Technology and a demanding job as a web designer and developer, I can say I can never run away from my kitchen. Even though I took a leave from blogging for personal reasons, i have been busy cooking, and lets pray that the best is yet to come.

In Short:
In 2004 I started miriammalaquias.com: I was the first Tanzania to have recipes posted in the website. I used my skills as a web developer to share my recipes with friends.

In 2006, I changed to www.mirecipe.com to make it easy for my visitors to remember. I also started to blog.

Now August 2009, I am happy to start a new domain www.TasteofTanzania.com:
This domain will be different from the last two. I now believe I have the right name for the site. And also more surprises will follow.

HABARI NDIO HIYO!

Unaweza kubadili hali ya hewa kwa kwenda GHANA kumtembelea MUZEE WA MAVAZI na si MAVUZI kwa jina Ozwald Boateng













Au tu INI KAMOZE alainishe kwa kitu-General

Au NGOJEA twende studio..

Read more...

HISTORIA fupi ya KIRUKA NJIA!

>> Sunday, August 23, 2009

Hapo zamani kulikuwa na NJIA na LIMTU ambalo halijaruka njia.

Ikatokea siku moja HILI LIMTU likarushwa njia na mtu mmoja ajulikanaye kama BOYFRIEND/Poozeo!:-(

Na baada ya watu kadhaa WASIOJULIKANA KAMA NI VIRUKA NJIA kuendelea KULIPA MSAADA wa kulirusha njia hili LIMTU au TUSEME kwa msaada wa WAZEE wa kuchovya pamoja na WAKATASHINGO waka sababisha ghafla BINTI Johnson/Khalufani akaanza kujulikana kama ni KIRUKA NJIA kwa kuwa kuna waliochovya waongeao na WAKATASHINGO wasio na siri za kutunza siri kuwa Binti Johnson/Khalufani anahuruma na KWA MGAO hawezekani!:-(
NAWEZA KUSEMA kwa KIFUPI HISTORIA nzima ndio HIYO!
Tatizo ni:
  • Unafikiri ni kwanini ni Binti na si Kidume hujulikana ni KIRUKA njia wakati KIGOLI akiruka huwa anaruka na KIDUME?

  • Si unakumbuka kidole kimoja hakishikilii titi?[Samahani nilitaka kusema;'' Kidole kimoja hakiui chawa! '':-(]

  • Kwa hiyo si UNAKUMBUKA haiwezekani kukawa na MALAYA a.k.a KIRUKA NJIA bila msaada wa wale hasa WASIOITWA MALAYA wamtongozao na kumuonja kidude MALAYA?


NIMEACHA na kumbuka HILI NI WAZO TU MHESHIMIWA na wala sie hatujui hata kama NI kweli NA WEWE ni MALAYA/Kiruka NJIA!:-(


Ngojea hali ya hewa ibadilike basi KIBONGE kwa msaada wa Harry Enfield atukumbushe zaidi tena miaka ya elfu moja mia tisa hamsini huko UINGEREZA katika unyago uitwao- Women Keep Your Virtue



AU tu twende miaka hiyo hiyo ya Hamsini Marekani tukakutane na Duke Ellington aturudishe miaka hiyo kwa kitu -Satin Doll

Au tu Miles Davis alete tena kitu -Tutu

Read more...

Kwa MPENZI SERIKALI Vinduna a.k.a SERIKALI YA WAJANJA!

Vinduna MPENZI wangu,....

.... wataka niua MOYO?


Kama WEWE ni wangu,....
....kwangu usiwe mchoyo

Tunza KIHARAGE changu,...
... usiniumize MOYO.

Nikiogopa na changu,...
....ni shinikizo la moyo.

Wengine usionjeshe, kwanza hudumia YANGU.



Wasahau ya WADOGO,...
... katika mwili husika.
Huridhisha ya VIGOGO,...
....yale yote wanataka.
Kujazia ya KIGOGO,...
.....kwa PANYA waweka PAKA.

Nyumba yetu ilo NDOGO,...
... wataka ijae TAKA?
Vinduna mpenzi WAMO, kilicho kidogo TUMO?


Lione tu kubwa hivyo,...
...mpenzi mwendo KA bata.
Nikikasirika hivyo,....
... na hamu LIKATAKATA.

Naongea hata hovyo,...
...ya uchungu penzi TATA.

Ningenogewa vilivyo,...
... wafikiri ninge BWATA?
Tako kubwa lina kubwa, na wadogo hatupati?


VINDUNA kipenzi changu,...
...mwenzio MI nina HAMU.
Ya kukiri we ni wangu,...
... na umeshika HATAMU.

Kutetea hamu yangu,...
...lete tibabu la HAMU.

Ondoa naya KIWINGU,....
... kwenye yale ya MUHIMU.

Sasa kama WE mpenzi, basi lete hilo penzi!


DUH!

Nakatizia wazo hapa!

Swali:
  • Hivi unaipenda au unaiogopa serikali yako ya KIBONGO NYOSO?
  • Hivi kama wewe si mfanyakazi wa serikali yako ya BONGO NYOSO unaamini serikali ni ya watu wake na SERIKALI YA NCHI YAKO ni yako?

NIMEACHA!

Ngojea COMMON asibadili kwa kitu-A letter to the LAW




Au tu Eddy Grant arudie kitu-Living on the frontline

Read more...

KUHUSU MWAKA jana!

Swali:

  • Unakumbuka MWAKA jana kama saa hizi ulikuwa unafanya nini?
  • Hivi mwaka juzi kama saa hizi unauhakika haukuwa umebanwa haja kubwa?
  • Au unafikiri si muhimu kukumbuka yaliopita hata kama sio ya mwaka jana kwa kuwa eti tuna ganga yajayo?

Hili ni WAZO tu MHESHIMIWA a.k.a WEE Waziri wa MAMBO YA GHAFLA na Starehe NDOGONDOGO!


AU ngojea The ROOTS wabadili hali ya hewa kwa kitu -The Seed/Melting Pot



AU tu Prince atekenye kwa kitu-Somewhere here on earth

Read more...

KATIKA staili ya kuvutiwa na mtu KWA SABABU TU TAYARI unajua yeye ni NANI!

>> Saturday, August 22, 2009

Unaweza kubisha LAKINI kuna watu unawasikiliza kwa kuwa unajua TU wao ni akina NANI!

Kuna USOMAO mpaka waandikayo kwa kuwa tu unadhani unajua wao ni akina NANI.

Labda pia kuna mpaka UWATAMANIO na kudhani ni wazuri KUBWA KULIKO kwa kuwa unajua tu wao ni akina NANI.


Na mpaka katika ya UJINGA WAO hao akina nani, utawatafutia sababu za nini ni busara ZA WAFANYAYO na kwa nini umati hauelewi yao wasemayo , waandikayo au tu yaliyo kwenye picha zao hata za uchi KWA KUWA TU unadhani unajua wao ni AKINA NANI.


Na LABDA usingejua ni akina nani WAO,...
.... yao ni UPUMBAVU na wala hayapandishi mdaDI.

Na kuhusu huo mwanya WAO,...
... kwako ungekuwa ni MAPENGO au UKIBOGOYO na wala haupandishi mdaDI.:-(

Hata ule mwendo wa maringo wa kudunda WAO,...
...wewe ungehakikishia watu kuwa ni kuchechemea kwa sababu mguu wao mmoja mfupi na wala si mwendo maridaDI.

Na wangecheka hata kuhusu yao WAO,...
...ungekunja uso kwa kufikiri wanakuchekea WEWE na ungedhani unatakwa au kwako wanajipendekeza kwa kuwa unadhani wewe BABU KUBWA na maridaDI.




DUH!

Swali:
  • Unadhani hakuna angalau hata BLOGU uzitembeleazo hata za kipuuzi kama HII YANGU si kwa liandikwalo au picha za uchi ila ni kwa kuwa unajua mwenye blogu ni nani?

  • Unadhani hakuna watu unawaheshimu au kuwadharau kwa kuwa unadhani unajua wao ni AKINA nani?

  • CHA KUSIKITISHA NI KWAMBA ,si kuna watu hata huwasikilizi hekima na busara zao kwa kuwa tu hujui wao ni AKINA nani?
Samahani NALIKATIZIA WAZO HAPA Mheshimiwa, Msela au tu wewe Kiruka njia!

Jumamosi njema MKUU wa MASWALA!


Hebu basi tubadili hali ya hewa kwa kujifunza tena jinsi wanawake wabadilishavyo nguo katika-NANIHIII


Au tu twende South Africa kukutana tena na Soul Brothers walete kitu -Usemncane


Au tu turudi tu tena Tanzania MATONYA aongelee tena ya -TAXI BUBU

Read more...

KUHUSU anayekunyima!

Labda hata SASA HIVI unastukia ANAVYOKUNYIMA,....
.....kama wengine UNAOWANYIMA wastukiavyo sasa hivi UNAVYOWANYIMA!:-(


Swali:
  • AU?

NI HILO TU na ni wazo tu BISHOO au weye BINTI MARINGO!:-(


Hebu tubadili tena hali ya hewa kwa msaada wa HARRY ENFIELD akitukumbusha kitu katika-SEXIST



Au tu MC HAMMER atukumbushe kitu -Have U seen HER?

AU tu twende MIAMI kumsikiliza PITBULL akiongelea tako au tu kwa wengine akitukana katika kitu -CULO

Read more...

Mbuzi hulia MEEEEE!Jogoo huwika KOKORIKOOOO! Na labda kimiminika MSALANI kuna watakaodai husikika CHWILILILILI!:-(

>> Friday, August 21, 2009

Na mwana hulia NG'AAAAAAAA

.... kuku HUTETEA kwekwekwekwe...
Ng'ombe huleta zake za MOOOO!
...bila kumsahau NYAU na zake za Nyauuuuu nyauuuuUUUU!...

Na kama ushawahi kujaribu kuiga hata mlio wa bundi KUJAMBA , kumbuka labda WEWE UNABAHATI UNASIKIA au ULIWAHI kubahatisha KUSIKIA.....!

Swali:
  • Unafikiri aliyezaliwa kiziwi hafikiri wakati UNAFIKIRI unacheka HA HA HA au KWI KWI KWI KWI sauti ya kicheko chako kwake sio NG'AAAAAAA au PruuuuhH?
  • Hufikiri kuna uwezekano kwa wanaosikia wamezidisha umuhimu wa KUSIAKIA mpaka wengine zimeua zao HISIA?


Nalikatizia wazo hapa na KUMBUKA NI WAZO tu NA nakutakia IJUMAA na WIKIENDI MSWANO wewe SISTERI wa shoka AU tu wewe MUZEE wa kuleta kibezi PUUH a.k.a PruuuH!:-(

Ngojea kidogo Harry Enfield aturudishe miaka ya hamsini UINGEREZA tufundishwe ya unyumba katika tena- The Conjugal Rights Guide


Au tu Papa Wemba na Koffi Olomide wakumbushe-Wake Up

Read more...

Nyuma na MBELE, usiposahau dunia ni MDUARA!

Nyuma ya MBELE labda haiko NYUMA,...

.... ingawa labda utapata mpaka mashahidi kuwa iko NYUMA.


Na mbele ya NYUMA,...
....kwa mtazamo au tu ukichukulia NYUMA kama vile uso wa tako,...
.... basi si utani ; Mbele ni NYUMA.

Lakini NYUMA ,...
..... hata ya MBELE YAKO kwa kuwa dunia ni mduara labda BADO iko mbele yako na si NYUMA.


Na kwa kuwa dunia ni mduara hata tukiwa tunatafakari ya NYUMA,...
....hata kwa AFIKIRIWAYE yuko MBELE kuna uwezekano katika MDUARA mara kibao ukweli ni kwamba kwa wenzie huwa anakuwa yuko NYUMA.

Swali:

  • Au?

  • Ushawahi kuangalia wanariadha wanakimbia uwanjani halafu ukachanganya wa mwisho ni yupi na wa kwanaza ni nani?

  • Kama uko mbele unafikiri tukigeuka sio wewe utakaye kuwa nyuma?
  • Unakumbuka aliyekukutangulia hata katika MDUARA HUU wa kuzaliwa na kuvalishwa nepi kwa utoto ndiye atakaye kuwa anajikojolea na kufungwa nepi hata kama tunamuita ni mzee lakini kuna mambo AFANYAYO hata UKIBISHA yata kukumbusha mtoto?

NI wazo tu na wala huhitaji kunielewa Mheshimiwa!


Ngojea Prince alainishe kwa kitu- Crimson and Clover


Au tu Osibisa warudie kitu -WOYAYA

Read more...

Kama wewe ni MTANZANIA na hustukii NYERERE, Mkapa, KIKWETE bila kumsahau Mtukufu mwingine kwa jina Rais Ali Hassan Mwinyi kuwa ni SARE SARE MAUA!:-(

>> Thursday, August 20, 2009

Ngojea niseme kihivi....


Labda Rais Nyerere alieliMISHA,...
.... na ulipoaanza kujifanya mjuaji akakukata ULIMI!

Labda Rais Mwinyi akaruhusu ikawa RUKSA ingawa katika swala la kujiRUSHA,...
.... ukastukia viko dukani NA kuvikodolea MACHO ruksa lakini wawezao kuvinunua VIWARUSHE hawakuwa wewe wala MIMI.:-(


Na labda Rais Mtukufu Mkapa kama ulijaribu chake KIBIRITI kutiNGISHA,...
....alijitahidi kukusaidia kukuelimisha ujue nguvu ya DOLA au tu serikali NI NINI ingawa wakati huohuo pia UKIENDELEA kushuhudia jamii ikiendelea kufunzwa UPROFESA wa ya KIBINAFSI na sio tena YA KIJAMII KWA UJUMLA na hapa ni katika tu kujaribu kutoliita swala zima UMIMI!:-(



Na labda Rais KIKWETE yupo na unaruhusiwa fikra zake kuduMISHA,...
....ingawa kumbuka wakati unamlaumu kwa kutofanikisha isije ikawa wewe mwenyewe unaongea zaidi kuliko kutenda ukasababisha naye Rais Kikwete ukimbana kona akakuzidi hoja kwa kukuambia ulitegemea msosi AKUWEKEE kinywani na akakusuta ''Koma babu wewe mengine usinilalamikie MIMI!'':-(

Na kumbuka Rais ingawa huwa TUKIONGELEA YA RAIS huwa tunamuongelea MMOJA mtu, RAIS ni OFISI ingawa tukiichukulia kuwa kama gari , ajulikanaye ni RAIS ndio anaeNDESHA,....

..... ingawa kama gari ni bovu Rais AMBAYE NI DEREVA mwenye MENO akikuchekea WAWEZA KUONA tu MAPENGO na kwa hilo unaweza usistukie TU la maana afanyalo kama tu USIVYOSTUKIA MCHANGO WA MAENDELEO YA NCHI wa yule mwenzangu na MIMI!:-(

Na ya ZANZIBAR ya RAIS kama ni pombe basi HIYO POMBE yaleWESHA,...
... na katika YA ZANZIBAR mara nyingi hata ADAIYE ajua tofauti ya Rais Karume, Salmin , Karume na ... na kutaka tuamini majibu yake na pamoja na MASWAHUBU , mie kwa hilo sina MAJIBU ukiniuliza MIMI!:-(


NIMEACHA!
Na, kumbuka MIE NAWAZA tu hapa KIBONGE au tu wewe ZEE la FACTS!

Swali:
  • Hivi unauhakika Rais HUWA anafanya nini ofisini?
  • Unafikiri Ofisi ya Rais ikiwa vile vile nini kinabadilika hata ukibadili aitwaye RAIS?
  • Hivi unajua hata kazi ya Balozi wa Nyumba kumikumi ni nini hata kama akitokea unamchunga hausigeli wako?

DUH!

Ngojea twende NIGERIA kidogo tukakague hali ya UKIMWI tena katika ...-HIV couples WEDS



Au tubakie tu hapa hapa Nigeria LAGBAJA alainishe tena kwa kitu- Nothing for U





Au tu LAGBAJA alete tena kitu-Feyine




AU tu nimuache tena katika kitu LAGBAJA live

Read more...

Wakati siri ya kwanini hufanyi ni kuogopa tutastukia ukikosea au KUCHEMKA!

LAKINI!.......


Wakati husemI,....
.... afadhali.....

..... iwe HUSEMI tu kwa kuwa katika tafsiri yako, kukaa kimya ni BUSARA na sio hofu ya ukisema utachemka na TUTAKUCHEKA!


Wakati hufanyI,...
....afadhali ....
....iwe ni kwa kuamua hufanyi kwa kuwa ukweli ni kwamba binadamu hakosi CHAKUFANYA kwa kuwa kwa yeyote mwenye ubongo vya kufanya VINABUNIKA na usipojazia muda na chakufanya unaweza UKACHEMKA kwa kutumia muda wako kusubiri siye WENGINE tukosee na kwa kufikiria ni ujanja eti utafurahia ukidhania tumekosea KUTUCHEKA!:-(




Na kama wakati KIKIFANYIKA huangaliI,.....
....afadhali....
....uwe mwangalifu na uwachekeao au kuwashabikia wanaoshabikiwa usiojua walifanikiwaje.
Kwa kuwa kunauwezekano majibu ya matatizo yako au tu maswali yako LABDA yanajibiwa zaidi na wajulikanao kushindwa na labda HUJIBIKA PIA kirahisi ukishuhudia wanavyoshindwa ingawa umuhimu wao na yao waliyoshindwa jamiii inaruka na JAMII pamoja na wewe kirahisi tu mnaweza mkawa KWENU ni kawaida KUWACHEKA!:-(


Ni hilo tu na ni WAZO tu KIBONGE!


Hebu basi OSIBISA wanisaidie tena kulainisha swala kwa kitu-CHECHE KULE



Au tu tena OSIBISA waifanye iwe siriasi katika kitu -Why

Read more...

Hadithi hii NIMESIMULIWA na MTOTO![stori ya kweli!]

Hadithi hadithi!


Hapo zamani za kale kulikuwa na SUNGURA!

Asubuhi moja Sungura aliamka na njaa akaamua kwenda kutafuta uyoga ale.

Basi akaenda weeeee AKAENDA weeeeeeeee AKAENDA weeeeee halafu akakata kona.

AKakata kona halafu akaenda weeeeeee AKAENDA weeeeeeeee mpaka msituni.

Hapo msituni akakutana na FISI, fisi akataka kumla Sungura.

Sungura akagundua hawezi kupigana na FISI kwahiyo akaamua kukimbia.

Akakimbia weeeeeeeeeee AKAKIMBIA weeeeeeeeeeeee AKAKIMBIA weeee mpaka akakuta shimo ambalo akaingia kujificha kusubiri Fisi akate tamaa aende zake .


Basi akajificha weeeeeeee Akajificha weeeeeeeeee Akajificha weeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee!

Ingawa aliumwa njaa shimoni akasubiri weeee akasubiri wee mpaka Fisi akaondoka kwa vile alijua akiumwa njaa si lazima atakufa lakini akipambana na Fisi atakufa.

Anko Simon Mwisho wa HADITHI!
------------------------------------_______________-------------------

Mazungumzo yetu baada ya Hadithi!

Mie Mtakatifu Simon: Hadithi nzuri sana!
Mtoto: Anko unajua hii hadithi inatufundisha nini?

Mie Mtakatifu Simon: Niambie basi Anko inatufundisha nini?
Mtoto: Inatufundisha kuwa akitokea mtoto mtukutu anayekuzidi nguvu au kitu cha hatari kimbia si lazima upigane nacho halafu ukiumwa na njaa vumilia kumbuka sio lazima utakufa!

Mie Mtakatifu Simon kwa mara nyingine nikawa nimekatwa kauli na kwa sababu fulani mpaka sasa hivi hiii stori niliyosimuliwa na mtoto wa miaka sita INANIFIKIRISHA!



Basi ngojea tubadili hali ya hewa kwa kwenda NEW ZEALAND kuangalia tena hii kesi ya jamaa kula MBWA katika kitu -Man COoks a family Dog



AU tu turudi KAMERUNI kwa Manu Dibango aseme tena ya-Woa

Read more...

MATATIZO ya kuwa huru wakati umeshazoea kuishi JELA!

>> Wednesday, August 19, 2009

Kuna wazoeao kuishi kijelajela na uhuru kwao ni ....

.....PRESHA!

Na kuwa huru kuna presha za kufikirishwa ufanye nini na uhuru ambao labda hata ukitaka kula WAWEZASTUKIA ghafla mpishi ni wewe na utajikuta tu unalazimika mpaka....

.....KUJIPIKILISHA!:-(



Na unaweza MPAKA kututangazia MAMBO kwa kuwa uko huru , ila kasheshe ni katika kutekeleza LA sivyo yatakushinda kama yalivyowashinda WATANZANIA hata baada yakututangazia wanuiayo kwenye lao .....

...... AZIMIO LA ARUSHA!:-(


Uhuru kitu cha ajabu kwa maana usipoangalia eti kwa kuwa tu uko huru waweza kujikuta kwa uhuru umeamua hata kidonda chako mwenyewe kwa kukosa vyakufanya kujazia uhuru....

....UMEKITONESHA!:-(

DUH!
Ni wazo tu MHESHIMIWA ingawa labda kuna ukweli kwenye hii HOJA!:-(
Swali:
  • Uko huru?
  • Unauhakika kuna aliye huru?

Hebu twende Gabon kidogo tupate Patience Dabany


Au tubaki tu Gabon tukutane na VIBRATION walete kitu -Mone Bone

Read more...

WAkati binadamu wanaendelea kumsingizia shetani VITU!

Kuna mambo binadamu anaharibu mwenyewe kibinadamu na LABDA wala shetani hausiki!

Na kuna mambo binadamu hahitaji baraka za Mungu kufanikisha, na LABDA ndio maana kuna wafanikishao mpaka umalaya , wizi, mauaji na ...... na kwa hayo labda MUNGU wala hausiki!


Swali:

  • Au?
  • Unauhakika kwa nini bado unaweza kukosea wakati unaamini Mungu na MUNGU yupo?

Ni wazo tu KINGUNGE na nakutakia siku KIBONGE!




Hebu TUENDELEE KUFIKIRISHWA kwa kumuangalia tena Saddam Hussein kabla HAJAUAWA NA WAHESHIMIWA , ambaye ni baadhi ya binadamu wachache waliofanikiwa KABLA YA KUFA kujua ni muda gani watakufa



AU ngojea JAGGED EDGE walainishe katika- Walk out of Heaven


Au tu tena JAGGED EDGE warudie wimbo huuhuuu- Walk out of Heaven katika hiii remix

Read more...

SHENZI mwanawane SHENZI![sentensi hii imebaniwa pua na msichana mwenye mafua:-(]

>> Tuesday, August 18, 2009

[Tahadhari: sina uhakika na maudhui ya taralira hii!:-(]
SHENZI mwaniwani SHENZI!!

LABDA kwa furaha umefurahishwa ,...
.... na kabla huja- NISONYA kama bado unaamini katika furaha wakati sifurahi unaweza tu mpaka kunitukana hata kwa zaidi ya SHENZI!:-(

SHENZI mwanawane SHENZI!

.... Halafu mtoto mzuri kama MALAIKA na kama unajua nakufananisha na MALAIKA unafikiri wakati UNANICHEKEA nitasikia au kujali yako ya KISHENZI?


SHENZI totoz SHENZI!

.....Na labda hata wakati tunachekeana yote ni UNAFIKI kama hatulengi nia na ingawa unajua wote sie katika tafsiri ni WASTAARABU bado nia yetu inaweza kuwa ni tufanye yatafsiriwayo kuwa ni USHENZI.:-(


SHENZI sista du SHENZI!
....sasa NTAFANYAJE wakati unajua chakukifanya labda ni kweli kimekunasia na tukileta jeuri ya kukitungua na kukifanya inaweza ikawa ni DHAMBI hata tukifanya kiustaarabu nafasi ikijitokeza na sio kwa kutaka kuhakikishia WATU ukweli KUWA kitendo chenyewe kama kilishafanikisha kuzalisha mtu labda si cha KISHENZI.:-(


SHENZI binti mrembo SHENZI!
... tukana tu KWA KUWA hata kama hupendi kubinuka au hata kutoa ukilala chali , hata ukiipigia magoti kwa afikiriaye kifanyikacho ni USHENZI hata umsomee ALBADILI atafanya akifikiria kuna uwezekano kifanyikacho hata kama kimebarikiwa na MZEE WA KANISA a.k.a SHEHE, bado HATA KAMA SIO WEWE bado kuna watakao kihusianisha na USHENZI!:-(

NALIKATIZIA WAZO HAPA na labda kama umenisoma mpaka sentensi hii kuna uwezekano ulichosoma ni USHENZI!:-(

DUH!




Hebu twende Angola KIDUCHU tukakutane na ya -BONGA

Au tu tubakie mpakani mwa KONGO na ANGOLA Ricardo Lemvo asemetena ya -MAMBO YOYO

Read more...

kama hata si kawaida unaamini MUNGU!

Swali:

  • Unauhakika wewe ni mjanja kuliko wasio amini MUNGU?

NI HILO tu na WALASIENDELEZI KUREMBESHA hoja!:-(


Hebu Sam Mangwana alainishe kwa kumsifia- KABIBI


AU tu twende tena Trinidad nimuachie CRAZY aongelee tena ya - CRUMBS

Read more...

MUNGU kama huwa kweli kunacho UNACHO BARIKI,kama inawezekana endelea KUBARIKI tena angalau hata KITOVU!:-(

Unajua imefikia mpaka kuna mambo tudhaniayo ni MAKUBWA,....


.... na inawezekana ikawa ni mpaka KWAKO KIKUBWA NI KULA na sie wengine WATU tumefikia KUFIKIRIA ingawa HATA katika kufikiria TUNASAHAU chakula cha kwanza hakikujua mdomo katika fikira na KATIKA kufikiria hasa KAMA sie kweli SI watoto wa chupa , tumboni kwa mzazi kumbuka HATA KAMA UNA domo kubwa SIKU HIZI kwa kula KOVU LA KITOVU ndio ulipo pata rutuba hata ya maharage na kwa kuwa hukumbuki ndio maana unasahau kwanini una KITOVU!:-(


Na labda siku hizi kuna wajifanyao wajanja na ukileta za kuleta wanaweza kukutisha eti yao ni MAKUBWA,....

...labda ndio maana KITOVU kimegeuka mpaka kudhaniwa ni KOVU na mengi hata YA wenye KITOVU wamesahau kwanini KWELI hata kama siku hizi una meno kama ngiri UMUHIMU au tu KWA NINI tuna KITOVU.:-(

Na katika KUBWA,...

... labda BADO wengine hawakumbuki hata KIDONDA ingawa tayari wana KOVU na labda bado wanafikiri kuwa wao ni SPESHO ingawa labda hakuna mtu spesho kama katika yote aliyonayo AJULIKANAYE KUWA NI MJANJA hata chini ya kitovu ukweli unabakia palepale kuwa HATUZIDI KITU KAMA YEYE kama sisi naye ana KITOVU.:-(


Swali :
  • AU

NI WAZO TU MHESHIMIWA usitishike na NIMEACHA!:-(

Hebu OASIS wabadili hali ya hewa kwa kitu - Wonderwalll



Au tu Tooots & Maytals wadai tena ya -54-46 was my NUMBER




ASANTENI WADAU WOTE wakiwemo hawa katika picha zangu za juzi ya jana....

Photobucket









Photobucket





Photobucket













Photobucket



Photobucket




Photobucket




Photobucket




Photobucket








Photobucket



Photobucket








Photobucket



Photobucket




Photobucket




Photobucket




Photobucket




Photobucket









Photobucket




Photobucket




Photobucket




Photobucket





Photobucket




Photobucket



Photobucket

















Photobucket




Photobucket



Photobucket

Read more...

Hivi NA HAMU kweli ya MWANAMKE au NA HAMU tu ya CHAKE kipengele hata kama sio UKE?

>> Sunday, August 16, 2009

Labda KATIKA hamu,...

..mara nyingi LABDA ukiwa na hamu ya MAGIMBI kunauwezekano huo ni msimu wa VIAZI!:-(


Na KATIKA hamu,...
....unaweza kula MAGIMBI kwa kuwa ni kweli unayapenda MAGIMBI , lakini LABDA ni ugali wa MHOGO unaoumisi mpaka KATIKA NDOTO na katika shughuli NI kweli ni UJI WA ULEZI UMEPEWA ambao NA bado upo INGAWA ni KWELI kuwa katika MAISHA YAKO na si katika NDOTO ZAKO huwa hupendi UJI achilia mbali UJI WA ULEZI, na kwa HILO hata usipotuuliza bado SISI twaweza JUA NINI KINAENDELEA na ukweli ni kwamba katika nyege zako za ugali wa sembe ukipata uji wa ulezi BASI katika hilo HIYO kama ni ndoto yako BASI hiyo ndoto ni JINAMIZI!:-(


Na KATIKA hamu,...
... hamu nyingine ni MATUSI ukizizungumzia INGAWA ukionja hata kiitwacho MATUSI unaweza kuguna kwa kunogewa na wakati umenogewa ukijaribu kuongea nasi hata kwa simu wakati unaendelea KUNOGEWA , .....SISI wengine tunaweza kudhani siku hizi WEWE una KIGUGUMIZI.:-(

DUH!
Mie Mtakatifu Simon KITURURU naachia hapa wazo na UKIENDELEZA WAZO SHAURI YAKO mie sikushiki KIBINDO!:-(



Swali:
  • Hivi ukiwa na HAMU YA MWANAMKE au MWANAMME huwa unafikiri unahamu yake MTU WOTE au unakuwa na hamu ya CHAKE tu KIPENGELE?

  • Hivi wewe kama MTU unauhakika kuwa MTU MWENYE HAMU YA MTU akimpata mtu anaukumbuka bado mwili wake wote na sio kama MIE MTAKATIFU SIMON KITURURU huwa anakumbuka baadhi ya vipengele vyake fulani kama vile roho na VIGANJA?[Kwani wewe ulifikiria mie MTAKATIFU ntapenda kipengele gani zaidi ya viganja? LIONE VILE!]

Hebu Mr Blue abadili hali ya hewa tena kwa kuongelea- MAPOZI


Au tu MANU CHAO aongelee tena- Me gustas tu

Read more...

WAKATI unaendelea KUJAZIA SIKU shughuli!

Ndani ya siku,...

.... ufanyayo ya muhimu ukifikiria sana ni machache na YANAHESABIKA!

Na uchache wa ya YA MUHIMU kwa siku,...
.... mengineyo siku ikiendelea ingawa uliyaanza vizuri labda nayo YAMESHAHARIBIKA!


Lakini hatuwezi kusikitikia tu ya siku,....
... ya mwezi na mwaka yanamkusanyiko wake wa usaha au asali hata kama kwa yaliyonyoka baada ya muda mrefu kuna siku yalikuwa YAMEPINDIKA.

Na labda uko kwenye zako siku,...
....lakini kumbuka kwa wenye mahitaji ya leo hata kama utachelewesha nanihii UTASAMEHEWA SIKU UKITIBU lakini kumbuka bado leo UNAHITAJIKA!:-(


Na shughuli ni nyingi ndani ya siku,...
... lakini bado ukweli ni uleule kuwa labda vya leo ulivyofanya katika yote cha muhimu ulichofanikisha ni KULA, KUNYA na kama ni mlalamishi angalau umefikiria cha muhimu kama hata sio HIKI NIANDIKACHO basi KINGINE katika YOTE ya katika kuchambua NI nini ukilenge hata baadaye wakati UKILALAMIKA!


DUH!
Naacha na NI WAZO TU kumbuka MHESHIMIWA !

JuMApili njEMA KInguNGE!

Swali:
  • Hivi ushawahi kufikiria kuwa labda udhaniacho ni cha muhimu labda ndio sio cha MUHIMU?
  • Unafikiri kuna BINADAMU ALIYEWEZA kujaza SIKU?

Ngojea tumtembelee dada Speech DEBELLE atutonye ya-The KEY


AU tu KRS1 aongelee tena ya URAFIKI katika kitu-A FRIEND


AU tu Lil Wayne adharaulishe watu katika- Lollipop

Read more...

WAKATI UNACHUNGULIWA!

>> Saturday, August 15, 2009

Kumbuka,...
... kama unachakuonyesha ,...
na unauhakika na upendavyo kilivyonuna unaweza mpaka ukakibenjua makusudi katika staili ya kukionyesha kama unajua UNACHUNGULIWA!

Kumbuka,...
...NDIO!Labda kuna kitu hutaki kukionyesha,...
...lakini moja ya sababu ya kutotaka kuonyesha ni jinsi utafsirivyo tu MUKICHWA maana yake nini ukituonyesha KITU CHAKO ambacho labda ni KIZURI KULIKO CHETU ndio isababishayo ukasirike au kuona aibu ukistukia UMECHUNGULIWA!


Kumbuka,...
... ukipewa sababu za kuonyesha,...
...kuna kitu utatubenjulia tukiangalie vizuri wakati kabla ya kupewa sentensi kadhaa ungeona aibu wakati unakikagua ukastukia UMECHUNGULIWA!


Kumbuka,...
...vingi ufikiriavyo unavionyesha,...
....kumbuka wengi watazamao hata bila kuchungulia huwa hawavioni na hata kama nia ni kuonyesha CHUCHU kuna uwezekano hata TITI halistukiwi INGAWA KIFUA KIKO WAZI wakati huo na hapa siongelei wakati UNACHUNGULIWA!:-(


Swali:

  • Unafikiri hata barabarani ni mangapi yaliyo wazi huwa unayastukia na kuyaona?

  • Unajua ni kweli asilimia kubwa ya wachunguliao hawaoni kitu na wakiona hawajakiona vizuri kidude?

  • Unajua wengi hata unao ongea nao uso kwa uso huwa hawakuangalii?


NI wazo tu na UNARUHUSIWA KUNIBISHIA KINGUNGE!

Hebu tupumzike kwa kwenda CANADA kumuangalia BINTI mheshimiwa wa KiMAREKANI kwa jina AMY G aonyeshe kipaji katika-The special and sexy talent of Amy G(TAHADHARI: Usiangalie kama mtoto au ni MZEE WA KUKWAZIKA kwa kuwa ni ujinga afanyacho kwa tafsiri fulani)



AU tu PAM HALL alete ustaarabu tena katika kitu-Late at NIGHT



Au tu MIRIAM MAKEBA alete kitu kiitwacho-POLE MZEE



Read more...

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP