Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Wakati na wasiwasi na ukweli wa msemo ``RASILIMALI YA MNYONGE NI UMOJA!´´.:-(

>> Saturday, January 23, 2010

NDIO,..
...UMOJA ni kitu cha ajabu,...
.... ndio maana umoja wa KUKU na jeshi lake la VIFARANGA vyao ni BONGE la sherehe ya ulaji laini kwa MWEWE.:-(



NDIO,...
.. kuna wanyonge afadhali hata wasiwe na UMOJA kitu ambacho sio ajabu ,...

... kwa kuwa matokeo ya umoja wao ni kuongeza UNYONGE tu kama wingi wa vifaranga vya kuku kwa MWEWE.



Kabla sijaendelea....
Swali:
  • Unafikiri Tanzania, CCM ni umoja wa vifaranga vya kuku au ni umoja wa MWEWE?
  • Kwani hujastukia TANZANIA hata kama unyonge wa RAIS KIKWETE ni MZURI, unafikiri kundi lake lisipokuwa na aina kadhaa zenye nguvu tofauti na za unyonge wa RAIS KIKWETE , Rais Kikwete anaweza KUKIKWETELISHA?
  • Si ulicheki HASA kama uliwahikucheki TANZANIA wakati wa RAIS NYERERE jinsi umoja wa WANYONGE alivyokuwa anapata tabu nao KUNYERERESHA nao?


Umoja ni NGUVU,...


.....si pingi hilo NG'O.:-(




Lakini umoja tu kwa kuwa wote chama chenu cha kuvizia UBWABWA MISIBANI ni kimoja na wote NYIE ni vifaranga,....
..... haki ya nani kwa mwewe -UMOJA HUO WAKATI HUO ni kitoweo ,..

....na KWA BINADAMU- labda WANADAMU wengine wanawasubiri TU vifaranga mkuwe wawachinjie WAGENI kuku MZIMA.:-(


Swali:
  • SI ushawahi kushuhudia baadhi ya ukarimu WA WATU WENGINE ni kukaa na njaa wakati mgeni akija atachinjiwa jogoo?

NIMEACHA WAZO na SI lazima uelewe naongelea nini MHESHIMIWA na ni WAZO TU HILI Mkuu!:-(



Hebu TUBADILI HALI YA HEWA KIJIWENI kwa kumpata General Larry Platt katika- Pants on the Ground




Au tu tumpate General Larry Platt katika -Pants On The Ground (TFG Remix)

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP