Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Labda ni JAMII NA MAZINGIRA YAKO tu ndiyo SIRI YA urefu wa UONYESHAVYO MASIKITIKO YAKO.:-(

>> Thursday, March 04, 2010

[Tahadhari: Wazo limenuna!:-(]


Katika juhudi za MAISHANI kufupisha HUZUNI,....
....uonekanavyo UNAHUZUNI  yaweza kuwa ndio moja ya yatafriwayo kuhusu wewe ni MTU wa namna gani.:-(


Lakini kwa BAHATI MBAYA yaweza pia kuwa kuna walazimikao KUCHEKELEA ya huzuni HADHARANI ,....
......kwa kuwa tu JAMII inafikiri  kikutiacho huzuni hakifai kuonewa HUZUNI.:-(

Swali:
  • Unafikiri wakati  MTU kamalizia KUWA NA HUZUNI waweza kuwa ni MIONGONI  MWA WAMFANYAO  inabidi aongezee MAPOZI TU  ya HUZUNI ili asijeonekana MTU mbaya na MAJIRANI?

KUHUSU kuhangaikia urefu wa KUONEKANA una- MASIKITIKO na katika  juhudi za kufupisha za mtu  HUZUNI,....


.....waweza kusababisha MTU achanganyikiwe hata MSIBANI kwa kuwa tu mategemeo ya JAMII  yanataka alie wakati labda STAILI YAKE  yakukabili mambo  na HUZUNI haihitaji MTU ALIE MUDA HUO na yahitaji awe pekee ili kisahihi AHUZUNIKE na wala sio HADHARANI hata kama marehemu na ya marehemu HAYAJUI  yanamgusaje NA kutokana na ukweli pia kuwa MAREHEMU  alivyokuwa hai kutokuwa chochote muhimu kwa MTU MHUSIKA  kwa hiyo ni vigumu kuitafutia mkao wa masikitiko na kujua  AHUZUNIKE WAPI  kinamna gani.:-(


KUHUZUNIKA hasa sehemu ambazo utahitaji michango ya watu ya MSIBA ni SANAA pia. :-(

 Swali:

  • AU?
Ndio narudia,...
....MOJA ya kitu ambacho JAMII hujijengea,.....
.... ni pamoja na muda AMBAO  wakujuao wanajisikia faraja kukuona una HUZUNI.:-(



Na kwa bahati mbaya,...
.... kuna WAHITAJIO KUKUONEA HURUMA ambao huweza kulazimisha asiye na MASIKITIKO  kuonekana mnyonge na mwenye MASIKITIKO  kwa kuwa HURUMA YAO inatokana na wao kujijengea,....

...  MAZINGIRA ambayo  yanahitaji kama unahitaji HURUMA  na huduma ZAO  sharti tu uonekane  katika MUDA FULANI una HUZUNI.:-(

Ndio ,..
.... wapo watu ambao JAMII IMEWAFUNDA kuonisha utiavyo HURUMA KIMUONEKANO ndio sawa na jinsi UNAVYOHUZUNIKA na kwa kurefusha muonekano KUWA UNAMASIKITIKO basi  wewe ndio kweli MTU MZURI na umepata pigo kweli kitu ambacho huwapa faraja ya KUKUHUZUNIKIA KWA KUTO KUSUASUA kisawasawa  katika hata yasiyowahusu sana wao KIHUZUNI.:-(

Swali:
  • Si unakumbuka kwa aliyefiwa  KUCHEKELEA Msibani  sio kithibitisho aliyefiwa hana HUZUNI?
  • Unafikiri kwa mwenye FURAHA ni lazima ahakikishiye wengine kuwa ni mwenye FURAHA?

Ndio,...
....LABDA.....
....ni MAZINGIRA tu na jamii ikuzungukayo AMBAVYO ni SIRI ya uonyeshavyo FURAHA YAKO,....
... INGAWA wajua akenuaye meno kwa kicheko,....

.... BADO sio  ushahidi kuwa ACHEKAYE na kusababisha wengine nao WACHEKE  PIA kuwa ni kweli ni MWENYE  FURAHA.:-(


NI WAZO TU HILI MHESHIMIWA!

Hebu Mbongeni Ngema abadili hali ya hewa hapa KIJIWENi  kwa - Woza my fohloza


Au tu Mahlathini arudie- Kazet



Au tu tudie ya matumaini tu kutoka kwa SARAFINA kuwa pamoja na yote -FREEDOM is COMING

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP