Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Wakati unafikiri UNAONGEA na MTU mmoja,.....

>> Wednesday, April 14, 2010

...ni vizuri kukumbuka UWEZEKANO uongeaye naye NAYA anaongea MUONGEACHO na mtu MWINGINE.



Na hicho ndio kitu kifanyacho KUWE NA UWEZEKANO siri umpayo mtu mmoja,....
....umewapa watu tisa na nusu  BILA wewe kujua.:-(



Swali:

  • Wakati unamtumia mtu mmoja text meseji umewahi kufikiria uwezekano  wa meseji hiyo ya siri kusomwa na kijiji kizima?

Ndio,....
... siri ya watu wawili na YA WATU MIA labda hazina tofauti  kinamna,.....
.... na ambacho sio wewe pekee ukijuacho KITU kuna uwezekano wote hicho kidude wanakijua.

NI WAZO TU HILI MHESHIMIWA!

Siku Njema!


Hebu Mahotella Queens wabadili kwa - Jabulani Mabungu



Au tu Mahlathini arudie tu ndude-Kazet

Read more...

ALIYE JUU akianguka CHINI KIDOGO,....

>> Monday, April 12, 2010

.... stori ZITAKUWEPO,....
....ingawa STORI NYINGI zaidi zitakazo kuwepo ni za kutungwa.:-(


NA ALIYEJUU akianguka CHINI KABISAA ambako ni chini zaidi ya ile CHINI KIDOGO,...

....kikubwa WALA SIO stori ZITAKUWEPO,...
.... bali  ni jinsi gani ALIYEANGUKA anakubali kwa haraka KAANGUKA ili ajifute mavumbi kwa haraka na KUANZA UPYA HARAKA kabla hajageuzwa kuwa wa KILE KITENDO CHA KUANGUKA mtumwa.:-(

Swali:
  • Si ukianguka umeshaanguka na hata ufanyenini hauwezi kubadili ukweli kuwa umeanguka?

  • Na ukianguka kifuatiacho ni kuinuka tu?
Ndio,....
.....UKIANGUAKA stori zitakuwepo mpaka kwa wasiohusika,....
......lakini KIKUBWA  kumbuka KUWA  hizo ni stori tu na labda ni mpaka uziruhusu zikuingie MUKICHWA ndio zinaweza kukufanya ujisikie MPAKA kama umevaa chupi chafu halafu watu WASAFI wanajua siri YAKO ujaribuyo kuitunza kwa makini HIYO.:-(


NI WAZO TU hili  MHESHIMIWA!
SIKU NJEMA!

Hebu The Blackstones warudie kitu - Sentimental Reasons



Au tu BLACKSTONES warudie tu tena na ndude - SWEET FEELINGS

Read more...

Nipo zaidi BONGO!

>> Wednesday, April 07, 2010

Nachezea vipengele zaidi MOROGORO, Dar ES salaam , ARUSHA na NAIROBI!

Na kwa kuwa niko njiani sana UNAWEZA kunikosa kwa muda HAPA kijiweni.:-(

Lakini kama unataka kuninong'oneza kitu,....
...waweza kufanikisha kwa kutungua namba:

    +255756295664

SIKU NJEMA MKUU!

Read more...

Umuhimu wa KUTOMUELEWA Maimuna katika kurahisisha FARAJA umuelewapo KHADIJA!

>> Monday, April 05, 2010

Labda ni tabia MBAYA kujisikia vibaya kwa kuwa tu humuelewi KHAMIS,...
....kwa kuwa kutomuelewa huko  kwaweza kuwa ndiko KUSAIDIAKO kufarijika kwako wakati unamuelewa KADALA kirahisi.:-(


Na labda PIA hata kutokuuelewa kwako UHANISI,...
...ndiko kusaidiako mpaka FARAJA za kudhani kwa kuwa  kuna viagra basi tatizo la bamia-nyama tepwetepwe si tatizo kwako kwa kuwa  bila maringo LINATIBIKA kirahisi.:-(



Swali:
  • Lakini hufikirii kutomuelewa kwako MUNGU husaidia kutomuelewa kwako SHETANI?

  • SI kuna uwezekano UNANIELEWA hapa?


Ndio ,...
.... hata KUTONIELEWA KWAKO kunaweza kuwa NDIKO kunakusaidia sana kufarijika wakati UNAMUELEWA paka au hata tu BLOGU YA MTU mwingine.:-(

NIMEACHA!
Kumbuka ni wazo tu hili MHESHIMIWA!
SIKU NJEMA MKUU!


Basi ngojea GREGORY ISAACS arudie -IF I don't HAVE U


Oliver Ngoma arudie ndude-Bane



Au tu Oliver Ngoma arudie tena mdinyo- Julie


Halafu sijui kwanini lakini ngojea tu na SEAL abandue kwa-Kiss From A Rose

Read more...

UNACHOKISIKILIZA,... nani anakisema?

>> Sunday, April 04, 2010

[Tahadhari: Taralila hii inawazo lililokaa uchi!:-(]


ASEMAYE,...
...anaweza kuwa ASEMACHO ni kwa MTAZAMO wa waliomsemesha!:-(


Na kwa kuamini wakusemeshao unaweza mpaka kuamini wavuta bangi WOTE wamechanganyikiwa hata kabla huja kutana na mvuta bangi kama Barack Obama au Bob Marley na kusikiliza wakati wamevuta bangi wanaongea nini.:-(






Swali:
  • Si KUNA MWENYE UHAKIKA KWA KUSIKILIZA TU MTU KUWA mvuta bangi na asiyevuta bangi wanaguna tofauti wakati wanazini ingawa hajachunguza wasiovuta bangi wawili wanaweza wakawa wanagunia shughuli kitofauti   wakati wanafanya shughuli  KAMA WEWE ile ya mtindo kavukavu?
Na wamseshao mtu  AKASIKILIZA kwa bahati mbaya ni wengi,...
..... na kwa kusikiliza tu watu unaweza mpaka KUSTUKIA NA  kufikia hitimisho asemaye mtazamo wake ni kwamba NYAMA YA BATA NI TAMU ANAPATIA  kuliko ya KUKU hata kabla hujamshikilia kiuno njiwa  au hata huyo binamu ya KUKU ambaye ni  njiwa.:-(



Swali:
  • Si wewe kama MUISLAMU hustukia mapungufu ya aongeaye KATIKA KUATHIRIWA ki MTAZAMO  aongeacho  kirahisi kinatoa siri umsikilizaye walio muathiri ni wakristo na KIMUATHIRICHO HATA KATIKA KUFIKIRIA kwa kutumia akili kuwa kwa nini kuingiza na kuchomoa BANANGENGE  anakuita ni uzinzi  kwakua  fikira yake ya mzalisho imekaa KIKRISTO kama aliyemsikiliza kuwa MKE WA NNE  DHAMBI ?



  • WEWE kama MSABATO si unastukia staili ya asemaye YESU kama huyo ni MROMANI KATOLIKI hata kabla hajamgusia BIKIRA MARIA aliye BIKIRA ambaye  AMUITAYE BIKIRA Maria anakiri  alimzaa kwa kugunia mzao kama kawaida YESU?

NDIO,....
....labda UNACHOSIKIA labda jaribu kumjua ANAYESEMA NI NANI kwa  kuwa kama unasikiliza tu NAKUFUATA  bila kujua asemaye,...

...unaweza kuchanganyikiwa bila sababu HATA  ukinunua CHUPI isiyoruhusu KIPENGELE CHAKO KIPUMUE WAKATI KIMEBANWA NA KIFICHA NYETI  kwa kuwa umsikilizaye katika stori za chupi anaweza kuwa ni yule ambaye HAJAWAHI KUVAA chupi mpya.:-(

 Swali:
  • Unachosikia huwa unachunguza nani anasema hata asemaye  AKISEMA  hakuna ajenda ya siri  katika hilo ASEMALO hata kama limeegemea  kukufanya upende KAROTI ZAIDI  wakati wewe ni mpenda MAPERA?

NIMEACHA

Usikonde lakini  hasa kama weye ni miongoni mwa wamsikilizao POPE  BENEDIKITI katika maswala ya husuyo ladha ya  KONDOMU kuliko MALAYA  aliye wahi kupata mpaka gono wakati anacheza na kivalishwacho kondomu!:-(



Tupate KWA KUBADILI USTAARABU angalau  tukunyema kidogo ya UKIMWI kutoka kwa FRANCO akinyambulisha kiua nyege katika ndude-ATTENTION na SIDA


Au tu VYBZ KARTEL na SPICE walainishe swala tena kwa mkito - RAMPING SHOP






Nilikuepo kabla sijaondoka ULAYA kama

Photobucket

Photobucket


Photobucket


Photobucket

Read more...

Kwanini WACHEKAO WAKITEKENYWA kwa kawaida hawakuambii wana HAMU YA KUTEKENYWA !

>> Saturday, April 03, 2010

Kumbuka  tu,...
...KUCHEKA KWINGINE  kwa wakuchekeao KWAO ni SHUGHULI tu kama tu ile ya kubinya jipu  kwa kuwa tu jipu limeiva.:-(



Ndio,...
.. UWATEKENYAO wakacheka,...
..... WAJICHEKESHAO bila kutekenywa,....
....... wachekao kwa kuwa UMETEREZA na kuanguka kitu ambacho ni cha kusikitisha,...

... na wachekao kwa kuwa KUNA  chakuchekesha,....

... LABDA vicheko VYAO vyote hivyo  havina undugu  ingawa vyote vimefanya  mtu akenue meno.:-(




Swali:
  • Unauhakika kikuchekeshacho ni kichekesho?
  • Unafikiri ni kwanini mwenye huzuni kwa kawaida hatekenywi katika kutibu huzuni kama KUCHEKA ni furaha na kitekenyeo SEHEMU SEHEMU anacho?
  • Unafikiri UWALIZAO hawakuwa na hamu ya kutosha ya kulia ndio maana wamelia?
  • Kwa kawaida  WEWE UKICHEKA huwa inakuwa umechekeshwa au unajichekesha ?


Ndio,...
.... apendaye kucheka labda si kweli anapenda kutekenywa kama tu apendaye kula MAGIMBI labda hapendi umlishe MAGIMBI.:-(



NIMEACHA!
NI WAZO TU na kutolielewa RUKSA!

Ngojea tena katika kubadili hali ya hewa baada ya wazo lililokaa vibaya  Safari Sound Band watoneshe kidonda kwa ndude - Mama lea mtoto wangu



Santana aturudishe WOODSTOCK kwa mkito-Soul Sacrifice



Au tu na Jimmi Hendrix  ajaribu kupoza kwa KUKITA KIUTU UZIMA  kwa banangenge-All along the watch tower



Sijui kwanini lakini SANTANA ngojea tu adungishe pia na -Evil ways

Read more...

Kwa waaminio....., NAWATAKIA WOTE PASAKA lakuchumpa!

>> Friday, April 02, 2010










Na,...
... kwa wale wenzangu na mimi;..
SIKU NJEMA hasa mkikumbuka IKIWEZEKANA msikojoe  pembeni ya choo NA CHAKULA kiliwe kistaarabu bila  kudondoshwa sakafuni!:-(





NI HILO TU kinamna WAHESHIMIWA!



Hebu lakini NINA SIMONE ambaye kanidaka leo KATIKA KUBADILI  aachie pia ndude- Black is the colour of my true love's hair



Au tu Kool & The Gang warudishe tu mkito- Let's Go Dancing

Read more...

Katika moja ya MTAZAMO WA JITIHADA za MWANADADA MZURI kubakia na MPENZI MMOJA!

[Tahadhari: Tararila ina wazo lililokaa vibaya!:-(]


Yasemekana PENZI halina mipaka,....
.... na ili penzi lako la MAANDAZI LIDUMU wakati  kila siku unaona vitumbua na keki  INADAIWA utumie juhudi za kushika breki  usije tu   kujikuta umerukia mpaka viazi vitamu  kwa muonekano tu na ukavuka MPAKA.

Swali:

  • Hivi una uhakika kuwa kama wewe ni MPENDA VIAZI VITAMU kwa CHAI huwa mapenzi yako ya VIAZI VITAMU kwa chai yanashushwa makali kisa  kwa adoado  asubuhi nyingine unagida CHAI kwa maandazi au UJI wa mihogo kwa VITUMBUA?



Ngoja turudi kwenye hoja kuhusu huyu MDUDE aitwaye MDADA;......




Kwa kuwindwa MWANAMKE anajulikana,...
... ingawa kwa KUWINDA  ni mahiri mpaka  adakwaye anaweza katika mawindo anaweza kwa kutostukia ni yeye aikuwa anawindwa na wala hakua mwindaji ndilo laweza kujulikana.

Kwa VISASI mwanamke ni risasi,...
... na kwa bahati mbaya kwa kulipiza VISASI anaweza akawa mpaka ni BUNDUKI na RISASI.



Na kwa huruma yasemekana MWANAMKE anaweza kuzaa mpaka na mwenye UKOMA,...
... na kama weye ni fundi wa kutia huruma kwa huruma kuna  MDADA anaweza  mpaka kukupa mbele na nyuma  wakati kwa huruma anakumegea UKOMA.



Swali:

  • Hivi kwa ujuavyo MDADA awindwavyo si unaweza kusahau MKAKA akipata mawindo kuwa katika mchezo huo  kufanikiwa ni MDADA ndiye mara karibu zote huwa MARADONA?
  • Unathamini JUHUDI za mpenzi wako adaiye ni wako tu  kubakia wako tu ?


NIMEACHA,... unajua ni PASAKA!
NA usitishike  kwa wazo ligusialo MDADA zaidi ya NJEMBA  hasa ukikumbuka hili ni WAZO TU MHESHIMIWA!:-(
AU?

Tubadilishwe wazo na NINA SIMONE katika -Young Gifted and Black




Nina Simone aingie ndani zaidi katika kuongelea ya roho katika-If U knew




Au tu NINA SIMONE alete pia ndude ambayo maneno yake hunitekenya sana tu katika- Ain't Got No...I've Got Life

Read more...

Leo tujikumbushe BIASHARA ya maiti UINGEREZA!

>> Thursday, April 01, 2010



DUNIANI kuna mengi ,...
....na hayo mengi kwa bahati MBAYA hutokea kona zote za DUNIA.

KWA Bahati mbaya MAMBO mengi ya AJABU kirahisi  husakiziwa WAAFRIKA au AFRIKA siku hizi  zidaiwazo zina mengi,...

.... lakini hali halisi  inaonyesha kuwa YA AJABU yako DUNIA NZIMA na cha ajabu kwako  chaweza kuwa ni kawaida mahali pengine SASA HIVI ingawa kuna kipindi LABDA yalikuwa ni kawaida HATA hapohapo ulipo katika upande huohuo wako wa  DUNIA.


Swali:
  • Unabisha?
Ukikuta STORI ya ajabu kutoka NCHI ZIITWAZO ZIMEENDELEA inakuwa kama  ni kitu cha ajabu  ,...
.....na chaajabu ZAIDI  ni kwamba  ni wale watokao NCHI ZIITWAZO HAZIJAENDELEA ndio wanakuwa wa kwanza KUSHANGAA na kuona ajabu kuwa   imekuwaje MFARANSA  mstaarabu ndiye anakula KONOKONO halafu ananiona miye wa ajabu kwa kuwa nagida KUMBIKUMBI na kwa kuwa  kwa mchoma mishikaki napenda kuagizia pumbu za mbuzi .[samahani katika  neno pumbu nilikuwa natakutumia neno LA KIHESHIMA ; ``makende´´:-(]

Stori kama ya juzijuzi ya JINSI YA KUMUANDAA PAKA MTAMU ya  mpishi maarufu wa KIITALIANO ilyosababisha sangambingo kwenye TV  katika kipindi cha La Prova del Cuoco  iliwakera WAITALIANO lakini katika wote nilioongea nao ,- watokeao KUNAKO BARA LA GIZA ndio nilishuhudia WAKITOA BONGE la mshangao zaidi  kuwa hawa jamaa wanavyopenda Paka na MBWA  kistaarabu sikutegemea kuwa walikuwa wanagida PAKA wala sio muda mrefu kwa kuwa bado kizazi cha wagida paka bado kipo- hasa kwa jinsi wajulikanavyo kwa kushangaa  wengine  wa pande nyingine za dunia wakati wanafaidi POPO wa kukaanga au tu  pale mitaa ya CHINA paka huyohuyo akibanikwa poa.:-(




OK!
Stori ya HISTORIA ya kula PAKA ITALI sio lengo muhimu la taralila hii ya leo ingawa KAMA UMEINGIWA MDADI WA STORI  ngojea niianzishie upya stori utamu ..

Basi  MUTU  MUKUBWA  ndani ya MAPISHI ITALY  kwa jina  Beppe Bigazzi alikasirisha WAITALIANO  kwa kutoa siri kuwa PAKA alikuwa KITOWEO MURUA TU  Italy. Watu walikasirika kwa kuwa wanaona hilo ni jambo ni shai kwa zaidi ya mtu kujamba makusudi mbele za WASTAARABU.:-(

AAAGH! endelea mwenyewe HAPA


...au pata tu  dondoo ya utamu wa NYAMA YA PAKA kwa maneno yake mwenyewe BEPPE BIGAZZI hasa kama umeshawahi kumdeku paka anakatiza halafu ukafikiria  kwa maringo yake inaweza kuwa KUMGIDA NI sumu.

 BEPPE anadai:
“I’ve eaten it myself and it’s a lot better than many other animals,” he told viewers. “Better than chicken, rabbit or pigeon.” He said that for optimum flavour the meat should be “soaked in spring water for three days” before being stewed.....


Ila kama nilivyosema LEO tujikumbushe BIASHARA ya MAITI UINGEREZA  katika enzi za ma-BODY SNATCHERS


STORI yenyewe ni   ...


Kuna kipindi  kufukua maiti na kuziuza Uingereza ilikuwa bonge la ujasiriamali ......

AAAAHG!  Hebu endelea mwenyewe HAPA na taralila ianzayo.....

``During the 17th and early 18th centuries, a grim profession emerged. A growing number of anatomists, keen to improve their medical knowledge, needed corpses on which to conduct dissections, which were often done in ‘theatres’, where members of the public could pay to watch............

Swali:
  • Si unakumbuka KUKUMBUKA idaiwapo AFRIKA hatuachi vita kuwa ULAYA  , Asia ,...na mpaka AMERICAS wana historia ndefu sana na ILIYOANDIKWA ya vita vya wao kwa wao ambayo imefanikiwa kuua vya kutosha tu labda hata zaidi ya AFRIKA ambayo hata jiografia yenyewe ilikuwa inafanya iwevigumu siye WAPARE kuwakong'ota vizuri WACHAGA mitaa ya Kilimanjaro?:-(

  • Kama unapenda kula nyama ovyo MTAANI unauhakika kweli hujawahi kula Kunguru wakuchoma? LIONE VILE!


NI MEACHA MKURUGENZI!
SIKU NJEMA!

Kumbuka...

Read more...

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP