Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Kama CHAKULA kingekuwa KINAONJWA tumboni na utumbo ndio wenye PUA,...

>> Wednesday, September 15, 2010

.... labda chakula hata kile kizuri vipi KINGEKUWA kama MATAPISHI na lile bomba la MSOSI  lingekuwa linanusiwa kwenye UTUMBO MKUBWA labda lingekuwa linanukia tu vizuri kama MAVI.:-(



Na kama CHAKULA kingekuwa KINAONJWA tumboni na utumbo ndio wenye PUA,...
.....labda MACHO ya binadamu yangekuwa VISIGINONI na wewe usingeitwa BINADAMU  hata kama usingefananishwa na TAIRI LA MICHELIN au tu mwenye maringo  KIWAVI.:-(

Swali:
  • Unauhakika NI UJINGA kwa BINADAMU kuukubali UBINADAMU WAKE pamoja na udhaifu wake wa KIBINADAMU?

  • Unauhakika  tabia ya BINADAMU ya kutaka hata kunukia vizuri wakati MCHAFU  kwa pafyumu katika kuficha harufu mbaya ya KIKWAPA na kimkojomkojo sio moja ya kuukataa uhalisia wa BINADAMU  ambaye ukimnusa kwa pua za MBWA utajua tu yuko kwenye siku zake mwezini hata kama kimkojomkojo pafyumu kali?


Ainisho la taralila:

Ukifikiria  mambo ya  SIKU HIZI  ya BINADAMU na baolojia/TEKINOLOJIA zake,....
..... waweza kuwa na wasiwasi kuwa labda ni KWELI wajanja KIBINADAMU ni wale wajitahidio kutokuwa na udhaifu uoanishwao na UBINADAMU.:-(


Ukifikiria mambo ya SIKU HIZI ya binadamu na MIKWARA yake,....
..... kwa kuwa hata kukimbia RIADHA TU watu mpaka watumie na MADAWA ya kuboresha UBINADAMU WAKE kwa fanya hata ushindi wa Usain St. Leo Bolt mshabiki wa mbio usiwe na uhakika nao kama tu ule wa Marion Jones  hata kama  USAIN BOLT asipodakwa sasa hivi kwa kujifunza kutoka katika mbio za baiskeli ya tetesi kuwa Lance Edward Armstrong kutodakwa katika DOPING katika TOUR de FRANCE ni kutokana na UDHAIFU wa bailojia za kuichunguza yake DAMU.:-(



Hitimisho la taralila:


Ndio ,...
.... labda kunasababu BINADAMU ameumbwa na udhaifu fulani na hatimaye atakufa na kitendo cha BINADAMU kujitahidi hata kukwepa kufa sio tabia nzuri ya KIBINADAMU.:-(


Ndio,...
.... labda kuna sababu BINADAMU HAOTI KITAMBI MGONGONI na katika KUJIFUNGUA halitapikii LITOTO MDOMONI kwa kuwa NI KAWAIDA  kulisukumiza LIMTOTO  kupitia sehemu  za siri ili UKAMILIKE ubinadamu.:-(



Si unamkumbuka Marion Jones huyu?




Alivyodakwa baada ya miaka ya kusifiwa kwa ushindi hakufanyi uwe na wasi wasi na ushindi wa USAIN BOLT huyu katika hata  MOJA ya haya mashindano ya BINADAMU ambalo ni KUJARIBU kumpita hata MBAYUWAYU kwa mbio kitu ambacho labda sio UBINADAMU?



SAMAHANI NI WAZO TU HILI MKURUGENZI na unaruhusiwa kulibishia!:-(

Hebu moja kwa moja katika kubadili mzubao URGE OVERKILL warudie-GIRL, you will be a WOMAN SOON

Tusikilize mazungumzo ya madhumuni ya MASSAGE



Au tu YOLANDA BE COOL wabadili kabisa shughuli kwa-WE NO SPEAK AMERICANO

1 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Yasinta Ngonyani 10:13 am  

Ninanukuu:- "Ndio ,...
.... labda kunasababu BINADAMU ameumbwa na udhaifu fulani na hatimaye atakufa na kitendo cha BINADAMU kujitahidi hata kukwepa kufa sio tabia nzuri ya KIBINADAMU.:-(" kufa hakukwepeki na huwezi kujua lini utakufa ingekuwa hivi ingekuwa bonge la kitu kwani tungeweza kuwaaga wapendwa wetu.....naacha

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP