Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Katika kutetea haki ya watu KUJISAIDIA HADHARANI!:-(

>> Tuesday, September 21, 2010

 [Tahadhari: Wazo limepinda!:-(]


Kuna MAMBO huhitaji uwe na kidhaniwacho ni TABIA MBAYA hadharani,...
..... laasivyo unaweza KUJINYEA BURE HADHARANI  wakati ni kweli ulipo hakuna vyoo hadharani na labda katika kibano hicho BUSARA ni kunya HADHARANI!:-(

Swali:
  • Unadhani kati ya KUJIKOJOLEA au kwenda msalani pembeni ya gari la MBUNGE hadharani  kama umebanwa ni nini  busara?
  • Unauhakika ni rahisi hivyo kujisaidia HADHARANI wakati unalaumu wajisaidiao HADHARANI wakati vyoo vya uma haviko hapo HADHARANI?


Na wakati niko katika HOJA nawezakusema  pia  UDHAIFU wa wenye tabia nzuri HADHARANI,....

... ni moja ya kichangiacho TABIA MBAYA HADHARANI!

Swali:
  • Kwani unafikiri kwa kuwa unaTABIA NZURI zikufanyazo umekaa kimya HADHARANI wakati adhaniwaye KIBAKA  anabwengwa  bila uhakika kama kweli KAIBA, wananafunzi wananyanyaswa kwenye DALADALAZ mbele yako, watoto wanatukanana ,........ hakuna uwezekano TABIA YAKO NZURI YA KUKAA KIMYA hadharani  inachangia TABIA MBAYA uzichukiazo HADHARANI?


Ndio,...
.... kuna hata MABLOGA wajulikanao kwa tabia nzuri MTANDAONI,...
....INGAWA wanatabia NZURI wakijulikana majina tu ,...
...na ukiwastukia kumbe ni haohao  wenye tabia mbaya chumbani/WAKIWA ANONYMOUS unaweza  hata kuanza KUHISI  kuwa mmoja wa waliowahi kukutukana mtandaoni ni  yule MCHUNGAJI / SHEKHE wako  ambaye anatabia nzuri sana na unadhani hana matusi ya nguoni  kwa jinsi umjuavyo HADHARANI kisa umestukia KITU kwa KUSTUKIA kumbe Simon KITURURU umdhaniaye hana adabu HADHARANI ni yule mwenye tabia nzuri kweli  chobisi asikoonekana.:-(

Ni wazo tu hili MKUU na nakutakia KAMANYOLA bila JASHO Mkuu!
Au ngojea nikuage kwa ung'eng' e -BADAYEZ!


Kwa kubadili hali ya hewa hapa KIJIWENI  tumrudie Lil VICIOUS wakati bado kinda ingawa msiniulize BUSARA za kumuachia mtoto aongee aongeayo  LIL VICIOUS ni nini tukianza na -FREAKS


Au tu Lil VICIOUS arudie- NIKA



Lil VIcious amalizie  na-The GLOCK


Au tu tubadili kwa kumuachia mtoto wa Will Smith kwa jina Willow alainishe kwa-Whip my HAIR

1 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

MARKUS MPANGALA 2:05 pm  

siku moja inawatu wengi .... cha ajabu ni walewale wenye jinsia ya kike na kiume...

siku moja ni ileile yenye mawio na machweo... sasa kuna uhakika kuwa mwenye jicho chongo hawezi kuona machweo?.... Duh nawaza tu hapa nimejaa kibwanyenye

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP