Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Kitu chanya kiduchu katika RIPOTI kuhusu TANZANIA kwenye HABARI ZA DUNIA !

>> Wednesday, September 22, 2010

MKUU nashea tu ripoti ya Global Campaign for Education;

'Back to School?' - the worst places to be a school child.

20 September 2010 The Global Campaign for Education today launched their report 'Back to School?' of the worst places to be a school child in 2010.......


Kigusacho TANZANIA ambacho kinauchanya ni  :
Progress is being made as in Tanzania three million extra children are now able to go to school.


AU  kwa lugha ya kitaalamu:

Ripoti inadai kuna ongezeko la watoto milioni tatu  wenyeuwezo wa kwenda  SHULE Tanzania. 


Na hicho MIMI BINAFSI naamini ni kitu kizuri .:-(



 Ukitaka kujua zaidi nenda kwenye ripoti kwa kubofya HAPA


KUMBUKA najaribu kuegemea kwenye UCHANYA kwa kuwa halihalisi si nzuri bado  .:-(

5 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

malkiory 3:51 pm  

Kitururu, haya mafanikio japo mimi bado nitayaita ni mafanikio ya kisiasa zaidi ya kitaalamu au kielimu.

Unajua hata wazo la Nyerere la elimu kwa wote lilikuwa chanya sana. Lakini hili la kukimbilia kiasi/quantity kuliko ubora/quality itatufanya vilema wa zao la mfumo wetu wa elimu.

Kama utakumbuka programu ya UPE (Universal Primary Education). Nyerere kama mwanasiasa alikuwa sahihi kutangaza sera ya elimu kwa wote, lakini je maandalizi yalikuwepo? jibu ni hapana.

Je walimu walikuwepo wa kutoa elimu hiyo kwa kila mtu? jibu ni hapana. Hapo sasa ni pale ambapo hata waliofeli darasa la saba walilazimika kuwa walimu. Tusichanganye siasa na elimu.

Simon Kitururu 4:11 pm  

@Mkuu Malkiory Matiya: Usemalo ni kweli kabisa.

Kazi ipo!

Ila katika ulimwengu wa habari ambao kila siku kisikikacho ni NEGATIVE nilijisikia ahueni angalau kwa kitu fulani ingawa undani wa kitu icho yaweza kuwa uozo.:-8

John Mwaipopo 5:18 pm  

TAWIRE mwalimu Matiya.

Pengine tujisifie kwa kujenga shule ambazo hadhi yake ni Day Care Centres. ni sehemu ya watoto kucheza mbali na nyumbani. kati ya hizo wanafunzi huingia gabbage in na wahitimu wake ni gabbage out. Gazeti la Mwananchi la jana lilitoa picha ya ubao wa mwalimu wa kingereza. sentensi zilizokuwepo moja ilisomeka "where are do you come from?"

Simon Kitururu 5:20 pm  

Chakujiuliza ni :
Je tusubiri tupate shule na walimu wa uhakika au tujikongoje na yale tuliyonayo ambayo ni uozo?

Kazi ipo!:-(

emu-three 8:23 am  

Yah, uzuri hutangazwa kwa mbwembwe, nasi hatuna budi kujipongeza!
Lakini baada ya kujipongeza, sasa twatakiwa kujiuliza `kwenda shule tu inatosha, ...mmmh, unafika shule unakuta majengo, mnacheza mwisho, mnaingia darasana, mnakaa chini sakafuni, vumbini nk,...mwalimu yuko wapi, hakuna ...mnacheza weee, mmmh, mwisho wa miaka saba, umemaliza shule...what is your name? mmmmh hivi mwalimu alitufundisha hilo kweli...mmmh, kwanza hatukuwa na mwalimu wa `maneno kama hayo' ....
Wenzenu watoto wa wakubwa wamepelekwa ulaya, au wapi sijui, wakirudi, mzungu kasingiziwa, `yes yes sana', na unajua tena makampuni mengi ni ya `wakuja' kama hujuii yes, bwana kalagabahwe, `hujasoma'!
Ni hayo tu mkuu!

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP