Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

LABDA ni rahisi kugeuza MANENO yageuke VITENDO kama hatuangalii KAMA hicho NI KITENDO sahihi wakati una PAKA a.k.a nyau MALAYA na utakacho mpaka katika TENDO ni watoto wa MBWA WAKO malaya!:-(

>> Monday, September 27, 2010

[Tahadhari: Wazo limepinda!:-(]


Wakati tunaangalia UWEZEKANO wa KILA MTU aongeaye kuwa anaweza KUTENDA,...


.... ni rahisi kugundua KUWA  kwa kuwa hata kuanguka ni KITENDO,...
... LABDA kila mtu  tukiomba aanguke sakafuni ,....
... kila mtu LABDA anaweza KUANGUKA  SAKAFUNI kama hatujaongezea  masharti AANGUKEJE kwa  maringo  na aangukie nini,...


....vitu viwezavyo kufanya KITENDO CHA KUANGUKA kiaminiwacho huwezwa na KILA MTU kiwe  na  watakaokosea kuanguka  kwa kuwa KATIKA kuanguka kwao MAJAJI watadai  KUNA USIO usahihi katika KUANGUKA hasa kama KATIKA KUANGUKA AANGUKAYE  hakuonyesha maringo yahitajiwayo KUTOKANA NA MASHART yakama WAGOMBEA U-Miss MBAGALA au tu katika kuanguka MUANGUKAJI aliangukia mavi ya kuku kitu ambacho kilitakiwa kukwepwa katika usahihi wa MUANGUKO.:-(



Katika hatua ya kwanza ya kulainisha  taralila na tukiwarudi PAKA na MBWA malaya wakati lengo ni kulenga tu swala hilo hilo la MANENO na VITENDO,...

Kuwa na PAKA JIKE malaya,...
.... wakati unania ya kuzalisha MBWA,....
....  kunauwezekano bado unasilaha ya mafanikio ya kupata ZE TOTOZ ZA MBWA kama unajua kutumia ulichonacho ambacho katika mfano huu  ni PAKA JIKE MALAYA kwa kuwa upo uwezekano kuwa kuna mwenye MBWA JIKE MALAYA ambaye naye shida yake ni PAKA JIKE malaya na katika kutatua TATIZO mkibadilishana tu  mlivyonavyo-  tatizo SOLVED ,....

...aka tatizo laweza tatuliwa kirahisi zaidi  kwako kisa tu una PAKA  kuliko kwa ambaye hana PAKA na anahitaji MBWA  katika ujazo wa matatizo yenu wahusika.:-(

Swali:
  •  Si unakuwa suluhisho la tatizo lako inaweza kuwa ndio tatizo la MWENZIO?
  • Si unakumbuka hata mababu katika kutatua matatizo yao walitumia mpaka BARTER TRADE kama suluhisho  kwa kuwa mwenye magimbi  asiye na MWIDU au MLENDA aliweza kubadilishana na mwenye MWIDU au MLENDA  ikiwa ni katika  kutatua uhaba wa ASICHONACHO  ingawa pia twajua  wenye ALMASI  enzi za MKOLONI waliopewa PIPI katika kubadilisha BIDHAA  kutokana na MAHITAJI?
  • Au?




Tatizo tu linaweza kujitokeza iwapo WEWE kwa kuwa unajua una PAKA malaya,...
... ukafikiri  basi unaweza kumlazimisha AJIFUNGUE watoto wa MBWA .:-(


Katika kuendelea kurahisisha taralila,.....
Swali:
  • Unafikiri unaweza KULAZIMISHA mfumo wa NCHI MBOVU uzalishe MAENDELEO hasa kama MAENDELEO huhitaji MFUMO MZURI  ufanyao kazi mpaka kwa mjumbe wa nyumba kumikumi hata kama RAIS MBOVU?

Kwahiyo labda,...
.... ILI maneno yageuke KITENDO sahihi  KIHITAJIWACHO,...
.... twahitaji zaidi ya MSEMAJI,....
.... ingawa bado labda MSEMAJI ni muhimu  vilevile katika uwezekano wa TENDO kufanyika KISAHIHI likiwa ni tendo SAHIHI kwa kuwa  ,....


... mara nyingi  ingawa tendo la kubinya JIPU ni tendo ,....
... waweza kukuta  bado UKWELI NI KWAMBA tendo sahihi  ni kutolibinya JIPU na kungojea liive vizuri ili lipasuliwe.:-(.


Na kuhusu lile swala la kuwa una PAKA na wahitaji MBWA,....
... huwezi kujua ,...

... LAKINI labda  ungeweza kusubiri PAKA azae watoto wa paka na baadaye uwauze paka na kununua MBWA malaya atakaye kutotoleshea watoto wa mbwa BAADAYE.:-(


Swali :
  •  Umenielewa?
  • Kwani  ni kwanini unafikiri WAKATI UNAHARAKA unafikiri unahitaji uwe na haraka sana hata katika kuelewa au tu katika ......nyingine?
NAWAZA TU MKUU na usikonde!

Tuendelee na Curtis Mayfield katika mdinyo-Freddy is DEAD





Curtis Mayfield arudie kudinya-Superfly





Na hatuwezi kuacha kipele bila kukunwa na hii kucha-Pusherman

3 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

malkiory 9:00 pm  

Mkuu nichotaka kusikia ni mabadiliko Tanzania. Miaka 49 ya ukoloni wa mtanzania kwa mtanzania imetosha.

Mimi siyo mshabiki wa Chama chochote cha siasa lakini namwangalia mtu mwenye vision na uchungu na nchi yake. Hakika ningukuwa Tanzania kura yangu ingeenda kwa Dr. Slaa.

Ahadi ni kawaida kwa mwanasiasa yeyote yule, lakini hata Obama ameshaanza kurudisha vikosi vyake toka Iraq. Hivyo kila kitu kinawezekana mkuu. Roma haikujengwa siku moja.

Simon Kitururu 9:09 pm  

@ Mkuu Malkiory Matya: Nakubaliana nawe 100%. Nachodokonyoa ni kukumbusha kuwa sio rahisi na ndio maana kuna wafuasi wa OBAMA wanafikiri kashindwa kazi wakati kuna mengi aliyoahidi katimiza. Nachojaribu kusema ni kwamba hii kitu tukizungumzia NCHI yoyote kuna watakao katishwa tamaa hasa ukizingatia hata Wanasiasa wafikiriwao ndio wema bado wao ni binadamu na sio MALAIKA.

Na Mkuu yote hii ni katika kuwaza tu hasa kutokana na wadau niliowapa sikio hivi karibuni waniwekavyo mkao wa kuwaza.:-(

Tuko Pamoja MKUU!

o'Wambura Ng'wanambiti! 4:51 pm  

...ati haraka? si katika vitu vyote kwa kuwa wawezakuta mlevi anaogopa kuwa na haraka ya kulewa....ili tu agide zaidi wake ulabu...lol!

Ndiyo...na labda ndo zake sababu mlala-puu kushadadia mafisadi ili tu apate kanga nk bila kuwa na haraka ya maendeleo :-(

ni mpaka hapo utakapostukia dili kuwa alileweshwa maneno ya kipuuzi akawa na haraka ya 'rambaramba' akiuza maendeleo ya ukweli :-(

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP