Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

NDUGU wananchi, KUGOMBEA ubunge ghali kwa hiyo mkinichagua NITAKULA RUSHWA na KUWAFISADI ili kurudisha FEDHA ZANGU na FAIDA bwelele!:-(

>> Wednesday, September 08, 2010

[Tahadhari: Hii ni barua tu kwa WANANCHI kutoka kwa mgombea UBUNGE MKWELI!:-(]




Ndugu WANANCHI!

 Kama mnavyojua hali halisi ya UCHAGUZI siku hizi  hapa TANZANIA kuwa ni ghali na wenye pesa ndio wasikikao. Na mnajua kuwa hulka ya WATANZANIA NYIE na umasikini wenu ni UBAHIRI na michango ya kunichangia ili nishinde UBUNGE hamtaki kuchanga na mnategemea kwenye mikutano yangu ya hadhara nigawe VITENGE , kilaji , MDUNDIKO UWEPO na ubwabwa uwepo.

Kutokana na hilo nawataharifu kwa kuwa mimi ni MKWELI kuwa  mafungu yawezeshayo naweza kuhakikisha kuna UBWABWA , Ma T-SHETI, Sebene na kadhalika huwa nayatoa kwa mafisadi ambao  wao kwa nia zao binafsi  za kifisadi wanaamini wakiwa upande wangu  na kunisaidia kushinda watanufaika kwa mimi kuwafumbia macho wakifisadi.Na ndio, nitawafumbia macho kwa kuwa bila wao hata mafuta ya kuja kwenye mikutano KUWADANGANYA ingekuwa tabu kitu ambacho kingefanya msinipatie KULA.

Sasa kwa kifupi ni kwamba nataka kuwataarifu ukweli kuwa UCHAGUZI huu unanigharimu sana fedha kwa hiyo mkinichagua ntakula rushwa kisirisiri na  SIO KAMA WALAVYO WABUNGE  na VIONGOZI WENGINE WA SASA na ikibidi  kama nahisi hamstukii ntawafisadi mpaka kieleweke aka FWEZA niliyotumia irudi. Na kwa kuwa baadhi za siri zangu zitiazo aibu ZITATOKA KWENYE KINYANG'ANYIRO HIKI na kuniumiza  sana roho ,...
.... kwa kupoza hilo NTAFISADI zaidi kidogo zaidi ikiwa ni katika kupoza tu roho kwa hiyo MSIKONDE sana.Na naahidi sita komba kila kitu kama wafanyavyo VIONGOZI wa SASA bila aibu.

Ndugu wananchi kwani si mnajua swala hili la UCHAGUZI ni bonge la  DILI?

Kwahiyo karibuni kwenye MKUTANO wangu kesho , UBWABWA, kilaji  na POROJO NONO za jinsi ntakavyo igeuza TANZANIA kuwa kama MAREKANI kwa miezi miwili wa ubunge wangu ziko tayari. La muhimu nshawadokeza natoa wapi fedha ziniwezeshazo kuwakomalia KISAWASAWA kwa kuwaomba KURA kwa ufanisi ambao kimtongozo lazima mkae mkao wa kukubali.

Na msisahau kuja na miavuli kwa kuwa MVUA inaweza nyesha na pia kama inawezekana njooni na mifuko ya Rambo na kachumbari kabisa kwa kuwa Pilau lipo la kutosha, BIA, chipsi, ila samahani GONGO na BANGE safari hii hakuna mpaka nitakapofanya mihadhara kule kwa wasela.:-(

Wenu,
Mbunge MTARAJIWA  MSEMA KWELI kuwa kisa changu cha kutaka ubunge ni kutafuta ULAJI na wala Watoto wenu SIWAJALI kama niwajalivyo wangu na wa KIMADA wangu  pale Tegeta na yule wa kule KIJITONYAMA.


AKSANTENI!


Swali:
  • Si kuna uwezekano AKWAMBIAYE ukweli katika hata uchaguzi wa URAIS ndiye kirahisi atafikiriwa hafai URAIS?
  • Unauhakika hupendi kudanganywa MHESHIMIWA wakati kuna uwezekano unajua UKWELI unakatisha tamaa ?

NAWAZA tu MHESHIMIWA!

Hebu tuhame wazo kwa kumuacha  Mighty Sparrow adinye-Both of THEM




Naye Mighty SHADOW adunge-Whats wrong with me?




Au tu Mighty SHADOW amalizie kwa mkito-Yuh Lookin Fuh Horn

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP