Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Ni rahisi kuongelea uwezekano wa kuwa RAIS NYERERE hakuwa na VIMADA wengi kama RAIS JACOB ZUMA,...

>> Friday, September 10, 2010

.... kuliko  kuongelea ni jinsi gani RAIS Mikail SERGEYEVICH Gorbachev alikosea KUENDESHA NCHI ya URUSI  kama tu RAIS Kambarage NYERERE alivyokosea  kuiendesha TANZANIA
kwa kinagaunaga kama  siri za uendeshaji nchi huzijui ,HUNA UZOEFU, na pia vyanzo vyako vya data za nini kiutekelezaji VINATAKIWA VIFANYIKE na KWA STAILI ya MKAO GANI hutoka tu  kwa ambao KAMA Mheshimiwa AJUZA   hawajawahi kutekeleza kitu.
:-(


Swali:
  • Kwani ni kweli kuna la kushangaza ikiwa WATU wanajadili kirahisi tetesi za labda Dr Slaa ana demu kama Rais KIKWETE ukizingatia ugumu wa kuongelea TEKNIKALITIZI za KISIASA na mikakati yake ya  jinsi gani ya kutekeleza kikweli  na KITEKELEZEKE na  kufanya HIGHWAYS  za Dar-es SALAAM zisiwe na msongamano wa magari kama zile za TUKUYU?
  • Ushachunguza elimu za WALALAMIKIAO udaku halafu ukaoanisha na kwanini kama wewe ni mfanya biashara mwenye nia ya kuuza biashara yenye wateja wengi sharti uuze UDAKU?

Ndio,...
... maswala ya kuongelea jinsi NYERERE alivyokosea ni magumu kwa mtu wa kawaida ambaye hajawahi kuwa RAIS au hata angalau  AMIRI JESHI MKUU wa JESHI LA MGAMBO,...

...na ni rahisi kumuongelea Rais MKAPA kama mtu wa kawaida MWANAUME  na si o kama RAIS  mwenye URAIS USIOUFAHAMU kwa kuwa KIRAHISI ukimuongelea kama BINADAMU wakawaida ambaye akila sana ANAWEZA KUVIMBIWA,...

....unaweza kuunganisha KIRAHISI  kuwa kwakuwa RAIS MKAPA ni MWANAUME  kama wanaume wengine wowote basi;...

..... tatizo la suruali kuharibika zipu analo,JAZBA ya njaa humgusa, WIVU anao ukimmendea demu wake,CHOONI anakwenda, HAMU za KIUTU UZIMA zinamuhusu -  kitu ambacho kinaweza kufanya ajadiliwe tu kirahisi kama Mheshimiwa MAUMBA fundi cherehani  kabla hajadakwa kwa kubaka watoto au tu MIMI Simon KITURURU katika udaku wa kuwa kunauwezekano akichekewa na dogodogo roho inapata ile KITU mwanana ambayo ROHO inapenda kuliko maswala ya kuratibu BAJETI  za nyumba za mpaka MAKOKONEO , bila kusahau pia kuzingatia KUWA michango ya HARUSI siku hizi bongo IMEPANDA BEI na   inakula sehemu kubwa tu  ya MSHAHARA kama wewe kama mimi sio MWIZI.:-(




Kabla sijaendelea:
  •  SI MHESHIMIWA unakumbuka kucheza kwa tahadhari na wazo langu katika  TARALILA hii na STAILI yake YAKUSHUSHWA  ili kunielewa naongelea nini ingawa SI LAZIMA unielewe?

Au niulize tu kinamna:
  • Unafikiri kuanza  kwa mbeya  apendaye udaku  KUONGELEA MAMBO BINAFSI ya WATU na MKAKATI wa  PASHKUNA aliye choshwa na udaku  kuacha kuongelea mambo ya watu NANI ana kazi ngumu?


PIA,...
...labda ni BUSARA za KIBINADAMU PIA ,  kuchagua kuongelea mambo RAHISI ya watu,....
.... ukizingatia MAISHA YENYEWE MAGUMU tayari  KITU KIFANYACHO  labda ni matumizi mabaya ya muda baada ya kukomaliwa na maumivu ya MAISHA NDANI YA SIKU  halafu tena uendelee tena na kujiumiza kichwa kwa kujadili  mambo usiyoyajua kama ya ni jinsi gani KAWAWA alifanikisha VIJIJI vya UJAMAA KIUTEKELEZAJI viwepo wakati   MADIWANI mpaka WAKUU WA WILAYA na ----,----,-----wanashindwa kufanikisha  mtaani KWAO   watu wafyeke majani au angalau wazibue mitaro ya kupitisha maji machafu hata kwa KIPOROJO tu.:-(
 



NIMEACHA WAZO HILI MHESHIMIWA kwa KULIKATIZA  na usikonde kama HUNIELEWI  ukizingatia kutoelewa ni moja ya sifa BOMBA ya ubinadamu wa BIN-adamu!:-(


Hebu twende Zimbabwe mwaka 1978  ili  - Thomas Mapfumo na  The Blacks Unlimited walete ndude-KUYAURA





Tubakie Zimbabwe Thomas Mapfumo amwage mdinyo-Moyo WANGU




Au tu baki tu na Oliver Mtukudzi na Ringo Madlingozi wakite TENA kitu mwanana -Into Yami


Basi bwana Oliver Mtukudzi ngojea tu atubakize hapa hapa Zimbabwe kwa shughuli nzito iitwayo-Todii

1 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Yasinta Ngonyani 1:32 pm  

Kuyaura... unipeleka mpaka ungonini nilikuwa na bibi yake baba alikuwa anaitwa kuyaura ikiwa na maana kuachama au kupika mwaya.. ahsante

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP