Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

UMUHIMU wa nchi MASIKINI kwenye UMOJA wa MATAIFA aka UN,....

>> Wednesday, October 13, 2010

.... labda ni kama NAZI kwenye MAHARAGE,....
... kwa kuwa sio lazima  NAZI iwepo katika MAHARAGE ili  MAHARAGE yalike.:-(

Swali:

  • SI unakumbuka MATAIFA yenye nguvu kama USA  au hata CHINA  bila kuisahau ISRAEL maamuzi ya UMOJA wa MATAIFA  huyafuata tu kama wanayahitaji na yana manufaa kwao?
  • Si unakumbuka mara karibu zote ni maamuzi ya MATAIFA makubwa ndio hutekelezwa na  akina GADAFFI hata wasemenini ukicheki vyombo vya habari huonyeswa tu kama VICHEKESHO na wasemayo wanachemka?
  • Ushawahi kuona katika habari  hotuba ya raisi wa  BURUNDI ikinukuliwa ingawa anachakusema?
Ndio tunajua kuwa kama nia ni KULA ubwabwa wa nazi,....
.... NAZI ina umuhimu wake katika utamu wa WALI wa NAZI.


Lakini,.....
.....PAMOJA NA YOTE ,.....
... si ukweli bado upo palepale kuwa  WALI bila nazi walika?


NAENDELEA kuwaza.....


Hebu tu nibadili kwa kumsikiliza Nat KING COLE akishusha-Quizás, quizás, quizás





Au tu Buenavista Social CLUB warudie-Candela



Na labda hebu tu  Mayito Rivera akiwa na Los VAN VAN arudie-Tim POP

1 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

malkiory 9:01 pm  

Lazima tubadilike kwanza, jeuri ya kusimama kifua mbele itatoka wapi wakati viongozi wetu kutoka bara la Afrika kazi yao ni kuomba misaada ambayo sehemu kubwa itanatumika vibaya kwa kutokuwa na sera za kueleweka.

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP