Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

HAPA DUNIANI wakati huohuo unafikiri UNASHINDILIA KITU yasemekana ni wakati huohuo nawe UNASHINDILIWA KITU!:-(

>> Friday, November 05, 2010

Katika mambo mengi,...
.... ni MTAZAMO tu usababishao  anayefikiria anafanya hastukii   kuwa  labda ANAFANYWA.:-(

Na  katika  ung'eng'e kuna wengi,.....
.... wamdakao NEWTON swala hili  katika ile  ya NEWTON ya  ``To  every ACTION  there is always an equal and opposite REACTION ´´ au katika lugha ya kitaalamu ``Kutendea KIDUDE na majibu ya KITENDWACHO KIDUDE  katika KUJIBU MASHAMBULIZI au tu  kukabili nyomi ya kitendo cha kisukumizwacho  kitu na kisukumiwacho kitu huwa nguvu DROO,´´ ....
....kitu ambacho katika  swala zima kinamna hata  LA NIPE NIKUPE  kuna ambaye ataliangalia  kuwa KIFIKIRIWACHO KINA  FANYA   katika mtazamo fulani WA WATU WENGINE  kuna watakao kuwa na ushahidi KITENDO HICHO HICHO ndicho kinacho toa jibu kuwa  HICHO HICHO wakati huohuo NDICHO CHAFANYWA.:-(


Swali:
  • SI unajua wakati UNAMUUMIZA mtu  kunauwezekano wakati huo NDIO unajiumiza tu MWENYEWE angalau  KISAIKOLOJIA?
  • Kwani hujawahi kusikia kuna NJEMBA imempiga KIJEBA  bonge la NGUMI halafu nalo katika hicho kitendo ikastukiwa  imeumia mkono?





Katika kulainisha HOJA hebu swala zima tuliangalie  kwa  kulifikiria TUMBO la  aliyezamia  ubwabwa HARUSINI:

Nguvu ya chakula itumikayo KUTUTUMUA aka KUTUNISHA tumbo la mwenye jazba ya ubwabwa wa bure harusini katika  CHAKULA KUSHINDILIA tumbo kwa  UBWABWA ,.....
..... ni sawsawa na nguvu ya kuta za tumbo kukibana chakula kisije kikatanua tumbo mpaka likachanika KWA TUMBO KUSHINDILIA CHAKULA  hasa kama ubwabwa unaliwa kwa SPIDI KALI  kabla haujaisha kwenye sinia bila MLAJI KUKUMBUKA kufikiria  ni kilo ngapi tayari KIUPROFESA wa UZAMIAJI katika MISOSI kashabwia,...
....kitu ambacho kinaweza kustukiwa kwa kushuhudia  baadhi ya WAHESHIMIWA kuwahi kwenda msalani  kwa kuwa tu tumbo lilijaa sana na katika TUMBO kukabili shughuli umesakizia UTUMBO msosi  na  utumbo umekubali kuwa afadhali MHESHIMIWA akajisaidie tu  haja kubwa yaishe.:-(


Swali:
  • SI kuna uwezekano nilicho andika HAPO juu  ni UJINGA na eti umeusoma?


Lakini HATA kama ni UJINGA hebu  fikiria,....
.... kwa kuwa labda ni kweli ANAYE SHINDILIA  wakati huo anashindiliwa ,....
.... na kwahiyo kumbuka kuwa wakati UNAIBA labda unajiibia na ni mtazamo tu ambao haukustui hilo au lile la kuwa ROHO lako  linazidi kupwaya KWA UTUPU  kwa KILA  unavyozidi kujazia ya KILIMWENGU ambayo twajua mtu haendi nayo kaburini roho ikitoka baruti.:-(

Ni wazo tu HILI katika MTIRIRIKO wa MWENDO wa maringo Mheshimiwa  NA NI RUKSA KUTOELEWA!:-(

Hebu tuhame na kuendelea kupata  kitu FUNK na nani zaidi ya BOOTSY COLLINS awezaye kutekeleza hili kama katika  -Ahh The name is Bootsy ,baby/Disco to go



Au tu Bootsy Collins na Snoop dogg waendelee na FUNK katika -Undercova Funk


0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP