Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

INASEMEKANA ukizoea sana mahubiri ya JEHANAMU kanisani, kama tu MSIKITINI yanaweza kuwa hayakutishi kama tu usivyotishwa na KUTONGOZWA baada ya KUZOEA!:-(

>> Thursday, November 18, 2010

Mazoea yanatabu zake,.....

..... kwa kuwa MAZOEA yanaweza mpaka kuchuja  heshima ya aliyekuwa anakupa SHIKAMOO kisa kakuzoea na wala sio kwa kuwa siku hizi kaota MATITI,....

...ndio maana yasemekana kuna mpaka WANAFUNZI waliomzoea sana MWALIMU,....
.... huanza kusahau kuwa MWALIMU sio MWANAFUNZI mwenzao ,....
....na kuanza kushindana naye hata katika somo awafundishalo ALILOLITUNGA MWENYEWE  na alifundishalo kwa kutumia KITABU CHAKE  MWENYEWE kama tu washindanavyo na wanafunzi WENZAO wengine.:-(

Swali:
  • Si unajua ukizoea sana MAHUBIRI , aongeacho PADRE ,askofu au tu SHEKHE KANISANI au MSIKITINI hata vile vya vitishio vya  JEHANAMU vyaweza kugeuka mazoea na wala hata havikutishitishi na HAVIKUBABAISHI  hata angalau KITISHA TOTO?
  • Unafikiri kama YESU huyohuyo aitwaye MWANA wa MUNGU angekuwepo sasa hivi mtaani hakuna waliomzoea ambao wangetaka kumgawia mpaka  URODA kisa wamemzoea tu swaga lake?


Ndio,,....
....yasemekana staili ya KUIZOEA hata KORANI,....
.... inaweza kusababisha MSWAHILINA kuzoea tu YATOKAYO kwenye KORANI  na kuyalainisha kiupokeaji kama tu alainishavyo stori za udaku ambazo ni zakuingia sikio hili na KUTOKEA jingine hata bila kuhitaji kujifunza kitu chochote.:-(

Ndio,...
.... yasemekana hata kwa wakristo  kwa kulizoea sana KANISA,...
....wayafikiriayo KANISANI hugeuka sawasawa tu na WAYAFIKIRIAYO BAA,...
... kitu kifanyacho baadhi  nia na MADHUMUNI ya kwenda KANISANI ,...
....ni kuangalia tu uwezekano wakutongoza WATOTO wa GETI KALI ambao  ni makanisani ambako wanazagaa kwa uhuru HASA  kabla ya kuondoka kwa WAZAZI WAO  na kwenda VYUONI kuonja uhuru kwa mara ya kwanza ambao unaweza hata kuwafanya wawe  angalau MALAYA KIDOOGO kwa mbaali katika staili ya kuonjaonja waliyowahi kusikia na kwa kukosa uhuru hawakuwahi kuyajaribu migombani.:-(




Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!

Na hebu DMX na Aaliyah washushe tena-Back In One Piece



Au tu Aaliyah na Timbaland warudie-Try Again

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP