Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Katika juhudi ya KUKUMBUSHA mtu kuwa matumizi ya KINYEO cha KUKU sio kutaga MAYAI tu ila ni mpaka kunya MAVI ya KUKU!:-(

>> Saturday, November 20, 2010

Binadamu huchagua,...
...na katika kuchagua KWAO  wanaweza kuangalia  HATA uzuri tu wa MSHAHARA wa MHESHIMIWA,...
...bila kustukia  MSHAHARA HUO UTOKEAKO  kingine kiwaumizacho ni NINI,...
...au labda kuna uwezekano  huo huo MSHAHARA MKUBWA ndio ufanyao MCHAGA kajitahidi ashindwe kuuza  viatu vyake VYA brandi ya  MCHAGA KAJITAHIDI  kwa kuwa WAHESHIMIWA na MISHAHARA yao jinsi inavyoendelea kuwa  mikubwa ,...
....ndivyo wazidivyo kuwasaidia zaidi  WACHAGA WALIOJITAHIDI Paris na CHINA  na wala sio wanakijiji wa MKULANGA ze-BONGO ambao kwa MSHAHARA  ukuavyo NDIVYO wazidivyoonekana waporipori na vyao si bomba kama cha KIITALI vitokavyo MILANO .:-(


Na kwa kuchagua,....
....eti kuna hata wachaguao kutokumbuka hata matumizi ZAIDI YA MOJA ya cha MTU kikojoleo ambacho tumizi lake kuu hudhaniwa ni  KUKOJOA  hasa kama vilivyo tawala mawazo ya WAHESHIMIWA kimwili ni MILANO.:-(

Swali:
  • Si unakumbuka pamoja na uzuri wote wa JUA   bado JUA  linaweza kukuletea  pia SARATANI?
  • Na siunajua pamoja na uzuri wote wa CHAKULA , chakula ndicho chaweza kukuletea  PIA madhara kama KITAMBI , utapiamlo au tu hadi VITA?

Ndio,...
.... labda hata MAISHA mazuri ya MHESHIMIWA,.....
..... kwa MTU kuyastukia HIVYO ndio kisa KUNA mtu maisha yake sio mazuri,....
....kwa kuwa inawezekana MOJA ulionalo  kama upande mmoja tu wa shilingi,...
... bado ni kweli SHILINGI ina pande mbili.:-(

Swali zaidi kiduchu:

  • Huwa ukiona ZURI hufikirii uwezekano kitoacho zuri  kinatoa na baya lake pia?
  • Si unakumbuka kama umeme uonekanao ni mzuri tu wa NYUKILIA utawalao NCHI ziitwazo zimeendelea huwa unakuja na  uchafu utokanao na nguvu hiyo ipendwayo ambao mpaka leo hakuna ajuaye jinsi  ya kuudhibiti ?

  • Na si unakumbuka pamoja na uzuri wote wa MAGARI bado magari ndio chanzo cha hewa MBAYA mijini na mazingira kuharibika mpaka katika kijiji cha Mkulanga?

Ndio,...
.....tumizi kuu la kinyeo cha KUKU taka usitake ni KUNYA mavi,...
...na wala hata sio kutaga mayai yafanyayo MPENDA Chipsi -MAYAI amfagilie sana KUKU.:-(

Swali nje kidogo ya tundu:
  • Si unakumbuka PIA  uharisho ni kinyesi cha kawaida tu chenye afya nzuri  kwa BATA na kitokeako hutokea pia YAI kubwa kuliko la KUKU?


NIMEACHA na ni wazo tu ambalo RUKSA kutolielewa MHESHIMIWA!


Moja kwa moja Mad COBRA aingie GHAFLA kubadili mshawasha kwa-SHOOT to KILL




Na labda atulize kidogo jazba huyu huyu MAD COBRA kwa -Too MUCH


Au tu MAD COBRA amalizie kwa kulainisha zaidi kabisa  kwa-FLEX

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP