Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Katika KUTAFUTA jinsi ya KABWELA kuitawala TANZANIA!

>> Friday, November 12, 2010

Binadamu ni wavivu kiasilia,....
..... na ukiwapa nafasi  kirahisi  NA KWA UVIVU WAKUBUNI KIPYA UPYA wanaweza kuamini yaaminiwayo kuwa  KUIGILIZIA mpaka staili ya KUONGOZA nchi ni jawabu,....

.... kisa  ni kwa kuwa STAILI YA UONGOZI  HUO  inafanyakazi MAREKANI aka USA , Japan na MBINGA ,...
....kwa hiyo BASI  staili HIYO  iigwe tu na itafaa pia DODOMA na TANZANIA kwa ujumla ambako labda kuanzia VIONGOZI WENYEWE mpaka wawapigiao kura,....
....hata KATIBA na HAKI ZAO  bado ki kuelimika ni shule ya vidudu na hapo sigusii  hata MENGINE  muhimu kama kujua MUELEKEO na KIMIKAKATI liwezekanalo kweli KIVITENDO.:-(


Swali:
  • Unabisha?

Nikikatizia denge HOJA,...
.... naweza hata kudai kuwa labda hata DEMOKRASIA,...
.... yaweza kuwa sio kitu sahihi katika kila NCHI,......
.... ukizingatia kuwa naamini inawezekana SI BUSARA  kudai unatafuta MAAMUZI ya BUSARA yahitajio UELEWA WA MAMBO,....

.... katika KUNDI LA WATU ambao hawajui  kwa undani SWALA LENYEWE  ZIMA ,....
....na kwa kuwa KIDEMOKRASIA  ni wengi  na WENGI WAPE kwa hiyo hata WASIOJUA wasiyoyajua  wayapigiayo kelele kwa wingi kwa kuwa wako wengi yachukuliwe kuwa ndio BUSARA na ndilo LAKUFANYA.:-(


Swali:

  • Unafikiri wingi wa kura za WATOTO wa CHEKECHEA kuhusiana na uchaguzi  wa staili bora za WEWE na LIMALAYA lako  unadhani zaweza kuwa zina busara nzuri yenye undani  wa kitu muhimu katika  kufurahiya staili zako za uasharerati ambacho labda ni UKATWAJI wa kiuno?

Ndio,....
.... kuna watakaodai pia labda kama KIPIMO ni maendeleo ya haraka sasa hivi,....
.... labda DEMOKRASIA wala sio  kitu KIHITAJIWACHO,.....
.... ikiwa NCHI  kama CHINA ijulikanayo kwa DEMOKRASIA YENYE UTAPIAMLO inafanikiwa katika  yale nchi zenye DEMOKRASIA  NONO kama U.S.A , UK au tu JAPAN zinashindwa sasa hivi.:-(

Swali:

  • Kwani wewe unaamini  kuwa kuna staili moja tu duniani ya kusaidia FAMILIA ZA WATU kulea mitoto yao ili ikikuwa iwe MIJINGA kama tu UKRISTO uaminishavyo waupao shavu UKRISTO  kuwa njia ya kwenda MBINGUNI ni  MOJA TU  na ni YESU TU  na kama unamzimia MOHAMMAD ibn ‘Abdullāh"peace be upon him" au hata tu N'GOMBE kikuabudu wewe unaweza usiende mbinguni kushuhudia kuwa huko kutakuwa na ngono au maswala ni kila siku ni Juisi , MAPARACHICHI na kuimbaimba tu HALELUYA?
  • Ni kweli unaamini ni KWELI  wamagharibi wasemavyo ni KWELI kikuongoza nchi huo ni ukweli pekee sahihi?


Na jinsi ya kutafuta jinsi KABWELA wawezavyo kurudia kutawala tena TANZANIA,....
...... kuna uwezekano kabisa kiigwacho hakifai ukizingatia TANZANIA wala sio KENYA,....
.... na labda KILIMANJARO kwa wale watani wangu WACHAGA WEZI na siye WAPARE MABAHILI  kunahitaji staili tofauti kiuongozi na ile ya DODOMA kwa WAHESHIMIWA WAGOGO au KAGERA kwa wataalamu wa KATERERO kama nia ni UFANISI na ubora wa UONGOZI katika maeneo HUSIKA.:-(

Na JINSI ya kutafuta jinsi KABWELA awezavyo kuwa tena kutawala TANZANIA bila kugeuka na kujisahau aliwahi kuwa KABWELA,....
...... BADO NAENDELEA KUWAZA.........:-(


Hebu  tumsikilize tena Jomo KENYATTA...

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP