Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

KULA BATA sasa hivi KAMA unauwezo wa KULA BATA sasa hivi,....

>> Tuesday, November 23, 2010

....kwa kuwa ukisubiria BAADAYE  inaweza kugundulika kula BATA ni dhambi hapo BAADAYE   wee shauri zako!:-(


Swali:
  • Unabisha?



Ndio,...
....LIWEZEKANALO sasa hivi lifanye SASA HIVI,...
... kumbuka kuna waliosubiria mpaka WAKASHINDWA KUPATA MIMBA,...
.....kwa kuwa kwa kudhani  watafanya baadaye WAKASUBIRI mpaka muda WAKUFANYA ukapita na mayai KIBONGE yakaisha au yakawa viza.:-(

Swali:
  • SI unakumbuka moja ya sifa ya BINADAMU ni ILE ya kutokujua ni nini kitamtokea BAADAYE?

Kwa hiyo kama sasa hivi ndio una MUDA na UWEZO;...

  • Malizia kujisomea sasa hivi.
  • Malizia kazi sasa hivi.
  • Tubu DHAMBI  sasa hivi.
  • Kama huogopi dhambi na unahamu na KUPOZA HAMU kwako ni muhimu , .......GETO LIPO na WAKUKUKUNA kipele yupo, PATA URODA sasa hivi a.k.a kwa KINDENGEREKO  -mpe sehemu zako za siri   mtu AZICHEZEE usikie TAMU uliyetaka kumgawia....  SASA HIVI , kwa kuwa baadaye huwezi kujua kama utakua bado na kiu ya utamu au kifaa chenye nguvu ya kuhimili  kuchochea utamu.
  • Osha kidude na nenda chooni kama umebanwa mkojo sasa hivi.
  • Msifie NDUGU YAKO, rafiki au LIMTU tu sasa hivi- usije kuwa miongoni mwa waliochelewa kumsifu mtu halafu akafa HALAFU ukaanza  tena stori za MAREHEMU alikuwa MTU MZURI na kupeleka zawadi ya maua kaburini wakati unajua kunauwezekano mkubwa MAREHEMU hawasikii sifa zako wakisha ondoka na labda sifa zako kwa hayati NYERERE ni bure kwa HAYATI NYERERE kwa kuwa wala hakusikii.:-(



  • Sikiliza MTU, miziki , mbayuwayu na KUNGURU sasa hivi kwa kuwa wajua tena siri ya afya ya masikio yako baadaye inawezekana ni kitendawili.:-(




Swali:
  • Na si unajua sasa hivi labda ndio unajibu UTAKALOLISAHAU baadaye?
Ndio,...
... kama unauwezo na muda KULA MBWA  sasa hivi,....
....na kama wewe ni MCHOYO kumbuka baadaye WAGENI wanaweza kukutembelea halafu unajua tena unaweza usifaidi MINOFU vyakutosha baadaye kutokana na tekinikalitizi za KAMBWA kenyewe kalikuwa kadogo :-(


Ndio,...
.....kama unanguvu za KUFANYA sasa hivi ,...
....LABDA fanya sasa hivi yaishe kwa kuwa kama BINADAMU hatujui ya BAADAYE,....
....ndio PAMOJA na UMUHIMU WA KUTAIMU MAMBO katika kufuata BUSARA za NGOJEA NISUBIRI MUDA MAALUMU kumbuka tu sisi kama BINADAMU  hatujui KWA UHAKIKA hata ya baadaye KIDOGO.:-(



Ni wazo tu hili BOSI na usikonde!:-(
Jumanne NJEMA Mheshimiwa!




Hebu OSIBISA wabadili mkao kwa -CHE CHE KULE



Osibisa waingizie pia ndude-Kelele



Osibisa watulize manyanga kwa-Woyaya




Au Osibisa watulize na kulainisha mshawasha zaidi kwa-Flyin' Bird

2 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Mija Shija Sayi 11:38 pm  

Nimekubali hoja.

Simon Kitururu 2:08 pm  

@Da Mija: Asante mtu wangu!

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP