Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Kwa kawaida NI WATU wauao WATU hata kama katika mauaji ni BUNDUKI na NCHALE wa NMAKONDE ndivyo katika UUAJI vinavyosingiziwa!.:-(

>> Thursday, November 18, 2010

Kuna VITU vingi ambavyo BINADAMU huvisingizia,...
....katika KUKWEPA lawama zisiwe ni za BINADAMU!:-(

Na ni kweli;...
... kuna mpaka LAWAMA binadamu awapazo mpaka  INZI,....
.....wakati mpaka uzao wa INZI wenye HARI MPYA na NGUVU MPYA ulosababisha majumbani kwa WAHESHIMIWA ni fulu KUHARISHA,...


...umesababishwa na BINADAMU haohao na TABIA ZAO MBAYA za kukionea kinyaa kinyesi na MAUCHAFU YAO MENGINE kitu kilichosababisha kutositiri vizuri mauchafu yao na kuyageuza kliniki za INZI na mende kidogo za KUJIFUNGULIA mitoto yao ya INZI na MENDE ambayo ndio chanzo cha waheshimiwa kuharisha na KUJIRUKA katika LAWAMA na kulalamikia inzi tu .:-(



Swali:
  • Si ni kweli INZI wanaweza kuwa wanasingiziwa tu mengi hata kama NI WATU WENYEWE ndio mchango wa hata kuwepo uzao wa hao  INZI ulioneemeka kama tu uzao wa mafisadi unavyoneemeka BONGO?




Ndio,...
... labda hata katika UKIMWI virusi vya hii NDUDE vinasingiziwa tu,...
.....ikiwa labda kuna baadhi ya ukweli AUAYE MTU hata kwa UKIMWI bado ni MTU ati.:-(

Ni ruksa kunibishia kwa kuwa hili ni WAZO TU MHESHIMIWA!:-(

Na moja kwa moja ngojea Tshala Muana atoneshe tena kidonda kwa kitu-DEZO DEZO



0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP