Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Mambo MENGI ni RAHISI mpaka uyatafute undani KIDOOOGO!:-(

>> Friday, November 05, 2010



Ndio,...
... kuanzia SHULE, Imani mpaka MAHUSIANO YA MTU na MTU,...
....kwa juujuuu HAYAKUNISHI SANA KICHWA,....
.... ila ukianza tu kuingia ndani zaidi na kuanza kutafakari ,KUYACHIMBUA  na kujiuliza mpaka katika UKRISTO  ya MUNGU BABA, Mungu mwana na ROHO MTAKATIFU ni MUNGU MMOJA,....

.... kama tu uanzapo kustukia MPENZI WAKO si kila siku anajisikia KUKUCHEKEA kama ilivyokuwa wakati MAHUSIANO YENU ni YA JUUJUU tu  na yenye lengo KUU MOJA nalo ni kusikilizia  tu UTAMU  au
kama tu jinsi uendeleavyo kustukia  MPENZI alivyo na ngozi mbaya ASIPOJIPODOA baada  ya kuliingia ndani zaidi penzi kwa YA MPENZI mliyekuwa hamuishi pamoja  na sasa hamkutanii migombani kwa kuwa penzi limepamba moto na kwa kuliingia undani zaidi sasa  MNAISHI PAMOJA,....


....HAPO NDIPO utastukia jinsi URAHISI huwa na tabia ya kugeuka na kuwa  UGUMU  na unaochanganya  kisa UMEINGIA tu kichwakichwa  kitu  wake UNDANI:-(

Swali:
  • SI unajua  kwa undani labda ADUI yako ni rafiki yako na ukimchunguza kwa undani ufikiriaye ni RAFIKI YAKO unaweza kuta kuwa kumbe huyo ndiye BOMBA YA ADUI yako?:-(
  • SI unakumbuka kwa kumfikiria BINADAMU kwa undani  ni kweli karibu kila BINADAMU ukutananaye anatembe na kinyesi mwilini hata kabla  bado hajabanwa haja kubwa?
Ndio,...
.... kuna watu na BUSARA zao  watakuambia,....
.... hata MKE au MME wako achilia mbali LIMPENZI TU lako kama mnataka muishi bila kukwazika ,...
... LABDA usichunguze sana wake UNDANI  kwa kuwa unaweza  kustukia mpaka kitu  ambacho ndio hasaa  hukipendi MAISHANI mwako ,...
.... na hapa siongelei kuwa  utastukia moja ya undani wa ni kwanini LIMTU lako likiwa na mafua huchukuwa muda kutoka BAFUNI ni kwa kuwa huwa linatumia muda wa bafuni kulamba kwa uhuru MAKAMASI ambacho ndicho uchukiacho sana zaidi kuliko  mtoto mkubwa mgonjwa umuhudumiaye AJINYEAVYO.:-(

Swali kidogo zaidi:
  • SI inasemekana ukichunguza sana CHAKULA cha HOTELINI kiundani unaweza kuugua tu  kwa kuwa waweza mpaka kustukia anayekatakata KACHUMBARI huwa hanawi vizuri mikono baada ya kujisaidia NAMBA MBILI?
NI wazo tu hili Mheshimiwa!:-(

Hebu SAM COOKE arudishe busara na USTAARABU hapa kijiweni kwa kuachia ngoma-You send me




Sam Cooke aendelee na-Only Sixteen



Au tu Otis Redding aingilie kati tu na -Sitting on the dock of the bay


Au tu Otis Redding amalizie tu na-Pain in my heart na I can't turn you loose.

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP