Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Wakati tunafikiria MTU wa kwanza aliye angalia KIDUDE na katika fikira akawa WA KWANZA kuona ni BUSARA kutahiri MTU.:-(

>> Friday, November 05, 2010

Katika KUNDI LA WATU,.....

.... ukichunguza karibu  katika kila kitu hata kama kile cha kubanwa mkojo ,....
...kuna wa KWANZA.:-(


Inasemekana pia katika swala la  WA KWANZA,....
....MTOTO WA KIKE na wa KIUME wenye umri sawa ,...
.... hata wakikua WENYEWE TU bila BINADAMU wengine,....
.... kuna siku tu  WENYEWE watastukia kuwa kuna tumizi jingine LA ZIADA la kikojoleo,...
... na wa kwanza kugundua hilo yasemekana ni mtoto wa kike.:-(

Swali nje kidogo ya tundu:
  • SI unajua hata VIFARANGA vya KUKU ukivikuza bila MAMA na BABA YAO huwa havihitaji SHULE vikibalehe na kuvunja ungo kustukia shughuli ya KUKU utofauti wake na ile ya JOGOO ni upi katika swala zima la kutaga mayayi yaliyorutubishwa?


Ndio,...
.... UKIFIKIRIA,...
.... unaweza KUKUZA HESHIMA ya WATU WA KWANZA kufikiria KITU hata kama ni cha kijinga.:-(

Na ukizidi kufikiria,...
.... unaweza kugundua PIA  kuwa pamoja na MAZINGIRA kuwa na MCHANGO WAKE katika kuchokoza aina ya FIKIRA ZA MTU,...

... ila bado  labda kuna watu wenye sifa MAALUMU katika KUSTUKIA mambo kwanza hata kama jambo lenyewe ni KUMKEKETA BINTI ,...
... kwa kuwa hata  ukimfikiria JAMAA wa kwanza kugundua swala kama  la KULA DENDA aka BUSU BICHIBICHI lenye MATE    kuwa ni busara katika kulionyesha LIMTU unalipenda,...
... bado  yawezekana alikuwa mtu makini sana kwa kuwa MIBINADAMU KIBAO mpaka leo inamuigilizia kulambana na katika hilo huyo anastahili sifa kwa kuwa katika ubunifu wa KULA DENA yeye alikuwa WA KWANZA.:-(

Swali:
  • Si unajua UKIFIKIRIA mazingira ya MTU WA KWANZA kuvumbua CHOO CHA SHIMO unaweza kukuta hayakufanana na aliyegundua kwa mara ya kwanza kuchambia MAJI  kwa kuwa labda aliyegundua kuchambia maji alikuwa hana haja ya kuchimba sehemu  kwa kuwa alikuwa anamchezo wa kunya MTONI?

  • SI unajua labda kuna kitu wewe ni wa kwanza kukistukia hapa DUNIANI ingawa hata wewe mwenyewe hujastukia kuwa UMEKISTUKIA??
Ndio,....
..... pamoja na YOTE,....
..... kuwa WAKWANZA labda  inapewa sifa mpaka zisizostaili,.....
...... kwa kuwa KWA KUWA wakwanza kufikiria kitu hata mpaka JAMII nayo kama tujuavyo ipendavyo kufuata MKUMBO,....
.... ya wezekana fikira yenyewe nzima KWANZA ni batili.:-(

Swali:
  • SI una jua WA KWANZA haina mpango kama hakuna WA MWISHO kitu kioneshacho kuwa WA MWISHO hata kwa KIKUFIKIRI labda anaumuhimu wake sana tu kama wa yule WA KWANZA?
  • SI unajua  wakati mnakimbia yule wa kwanza anaweza geuka wa MWISHO kama bonge la MBWA likitokea kwa mbele na kufanya wote mgeuke na kutoka baruti kurudi mlikotekea?

Ndio,...
....kuna mtu alikuwa WA KWANZA  baada ya kucheza sana na kidude halafu akili ikamuingia kuwa,....

... nafikiri hiki kidude  itakuwa bomba KIKITAHIRIWA.:-(

SAMAHANI  ni WAZO TU HILI na SAMAHANI TENA kwa FIKIRA zilizopinda MHESHIMIWA mwenye HESHIMA !:-(


Hebu tubadili kwa kuwaachia The DRAMATICS , The DOGG Pound na Snoop DOGG warudie- Doggy Dogg World

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP