Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Kwa kuwa BAHATI MBAYA huchelewa kustukiwa na MHUSIKA kuwa ilikuwa ni BAHATI nzuri!

>> Thursday, December 02, 2010

Kwa BAHATI MBAYA,....

.... ukiachwa na BASI,.....
....unaweza tu kustukia kuwa hiyo ilikuwa ni BAHATI NZURI,....
....mara tu ukisikia BASI lililokuacha limepiga BONGE la mzinga a.k.a LIMEBIMBILIKA a.k.a  kwa lugha ya kihuni- LIMEPATA AJALI.:-(


Na kwa kuwa MTUZ huchelewa kustukia mambo hata ya kuwa siku ileile ya kitendo alipata MIMBA,...
.....hata BAHATI NZURI huchelewa hata na wajanja KUSTUKIWA hasa wakati MUKICHWA wanang'ang'ania kuangalia swala kimkao wa kuwa  HATA kwa kuwa tu SASA HIVI swala halipendezi MACHONI wala masikioni kwa kulisikia tu basi SI ZURI na  lina uhusiano na BAHATI MBAYA.:-(

Swali:
  • Lakini si unajua MAISHANI hata kufeli mtihani kwa aliyetaka kufaulu MBELENI kunaweza kugundulika kuwa ndiko kulikuwa ni BAHATI NZURI kwa MHESHIMIWA ambaye baada ya kufeli  akastukia kitu ambacho angefaulu asingejifunza na sasa hivi AKIHITAJIPO katika wakati husika ili kitumike asingejua kitu?

  • Na kwa iliyodhaniwa ni BAHATI MBAYA kwa kuwa uliyemtaka alikutolea nje si waweza kujagundua BAADAYE kuwa ilikuwa ni BAHATI NZURI kwa kuwa TOTO lenyewe wakati linakukatalia lilishakuwa nimerithishwa kiroba cha uchawi cha UKOO ambacho moja ya sharti ni kumgeuza mtoto wako wa kwanza kisusio halafu UKIMWI lilikuwa nao tayari ingawa bado ulikuwa haujalikolea - ambavyo ni vitu viwili uviogopavyo sana hata ukiwa bafuni peke yako umejimwagia tu maji hata kabla ya kujiosha kipengele?


Ndio,....
....kwa idhaniwayo ni  bahati MBAYA ,.....
.....yaweza kuwa ndio misingi ya yote ya MTU katika bahati zake nzuri,.....
....na hapa wala siongelei zidhaniwazo ni bahati MBAYA za BINTI mwenye sura mbaya ambazo zikawa ni BAHATI NZURI kwa kumfanya asome kisawasawa na KUSTUKIA anamiakili KEDEKEDE  kitu kimfanyacho sikuhizi NI KIBOSILE WAKO hata kama hata  siku hizi BADO  analisura na tako baya kama tu enzi za ZILIPENDWA.:-(


Ni wazo tu hili MHESHIMIWA na usikonde!


Hebu Toots and The Maytals na Shaggy washushe - Bam Bam



Au tu kwa kuwa tamu Toots and the Maytals waendelee tu na jiwe- 54-46 was my number

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP