Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Kama ampendeaye mtu TABIA bado naye atahitaji SEHEMU ZA SIRI ZA MTU ili penzi litimie!:-(

>> Sunday, January 31, 2010

[Tahadhari: Wazo limepinda na LINAWEZA kukukwaza kama mtoto au tu kama weye ni Mzee wa kukwazika!:-(]





Kuna wagundulikao kuwa pamoja na kudai wamempendea mtu SURA au tu nyonyo,...
....bado walengacho na wahitajicho kutoka kwa mwenye HIYO sura nzuri wala sio HIYO sura na labda ni zake tu SEHEMU zenye NYETI.:-(


Na kwahiyo mara nyingine kumbuka kama hutachukulia hili kama ONYO,...
....kuwa pamoja na kwamba wako WASIFIAO HARUFU YA CHAKULA ambao hudai wamevutiwa na harufu ya chakula katika PENZI LAO LA HICHO CHAKULA,....

... lakini KUNA UWEZEKANO MKUBWA mapenzi YA harufu ya chakula kwa apendaye kula au MWENYE NJAA ni danganya toto kwa kuwa kwa yoyote mwenye njaa anajua kiliwacho katika chakula si HARUFU na afuataye harufu hata ya ubwabwa wa msibani ni KUGIDA MSOSI na sio KUSIKILIZIA HARUFU ndio SWALA NYETI.


Swali:
  • AU?

  • Unauhakika kikufanyacho umpende mtu sio CHAMBO tu chakukurahisishia kukabiliana na vipengele vyake huyo mtu ambavyo labda vinanuka na vinasura mbaya ambavyo ndio unavihitaji katika huyo MTU?

  • Unafikiri harufu ya wali sio tu msaada KWAKO wakukuwezesha ule wali ingawa mahitaji yako yangetimizwa na MATOKE au ugali wa mhogo?


Ndio....
.... labda kuvutiwa kwako na SURA au tu shepu ya matako ya mtu,...
.... ambavyo UKIFIKIRIA labda katika huyo mtu hivyo ndivyo vipengele vyake ambavyo hutavitumia na huna mahitaji navyo,...

... NI DALILI ya udhaifu wa UZURI wa uvihitajivyo katika huyo mtu vikiwemo TABIA YAKE au tu sehemu zake uzihitajizo katika shughuli nzima ya KUUJAZA ULIMWENGU a.k.a kuzalishana hasa kama SEHEMU HIZO huzitumii kimaridhawa kama VYOMBO vya burudani.:-(


Swali:

  • Unauhakika ni nini hasa umpendeacho wako MPENZI?

  • Unafikiri katika kila PENZI hakuna lako hitaji ambalo unalipata kwa huyo mpenzi ambalo halina uhusiano na kifanyacho MPENZI kwako anavutia?

  • Unafikiri mapenzi hayana UBINAFSI na ni kweli unampenda tu MTU kwa roho yote bila ubinafsi kwa kuwa tu ANA ROHO NZURI na hakuna chochote binafsi upatacho KIFARAJA ?

Ndio,...
... kuna MAPENZI ya aina nyingi,....
.... kwa mfano yale ya NDUGU kwa NDUGU au tu MTU na MBUZI.


Ndio,....
..... UKIFIKIRIA waweza kustukia hata MAPENZI ya mtu na MBUZI au KUKU aliyenona,....
... yawezekana ni DANGANYA TOTO hasa kama ASIFIWAVYO MBUZI na KUKU ni kimvutio WA MUONEKANO kama nia ya kuwafuga MBUZI au KUKU hao inalenga sana cha binadamu KITOWEO kuliko kupamba ya binadamu DUNIA.:-(


Swali:
  • Unauhakika MAPENZI yako kwa NDUGU yako nayo kiyakupavyo faraja , KWAKO hayana UBINAFSI ?
  • Wakati kuna adaie amempendea MTU mwanya AU MATEGE,-kama sio tako,- unafikiri MWANYA au MATEGE ya apendwaye unateleza kitu gani muhimu katika PENZI la hao wapendanao?
..
NAKATIZIA HAPA katika hili WAZO Mheshimiwa nikiamini unaelewa hili ni wazo tu na kulibishia RUKSA!:-(






Hebu twende tu tena Ivory Coast Meiway aendelee na -Voila String



Au tu MEIWAY aweke tu na-DJ Tassouman

Read more...

Kuendekeza ANASA,...

... labda ni hata kunywa UJI wakati huna HITAJI la UJI.:-(


Na kwahiyo,...
....wakati KUMBIKUMBI wanakidhi mahitaji yaleyale ya SENENE ghali,...
.... LABDA kula SENENE ni ANASA pia.:-(


Swali:
  • Au?

Ndio,...
... anasa hutofautiana kutoka MTU na MTU,....
.... na anasa kwa wengine LABDA ndio maisha ya kawaida kwako.:-(



Swali:

  • Si kuna uwezekano kuwa na chupi zaidi ya mbili ni anasa pia, au unafikiri IKIBIDI chupi tatu hazikutoshi?
  • Unafikiri kama UNA AKILI kufanya ujinga bila kutumia akili sio ANASA?


Ni wazo tu HILI Mheshimiwa na kumbuka blogu hii wala sio BIBLIA au Korani kibusara!:-(

Na moja kwa moja ngojea twende Nigeria Nkem Owoh aonye madhara ya kwenda shule katika - School Na Good Thing




Au tu twende Ivory Coast Meiway abadili hali ya hewa kwa kitu- Koundoum Beat

Read more...

Jamani jamani SHIKAMOO MPENZI![Sentensi HII imebaniwa pua na demu mwenye mafua.:-(]

>> Saturday, January 30, 2010

Na kuna watoao SHIKAMOO mpenzi ,....
... kama mkakati wa KISIRI wakumuambia MTU kiumri amezidi sana na KWA HILO kukwazwa asiombe PENZI.


LAKINI kwa kuwa HATA kama kwa UMRI ni mkubwa MPENZI,...
.... kumbuka lake laweza kuwa ni CHANGA na ndio kwanza limezaliwa tu PENZI.




Swali:
  • AU?



SHIKAMOO KIPENZI,..
... yaweza toka kwa AHESHIMUYE lako PENZI.

Na kwa kuwa anakua KIPENZI,...
...umri wako na wake waweza kuwa UNAANZA kufanana kama kipimo ni PENZI.

Kwa kuwa KIPENZI,....
.... wakati wengine PENZI LAO linakua, wapo ambao WANAPIGA MAKITAIMU kipenzi.:-(

Kwa kuwa KIPENZI,...
... wakati wengine PENZI LAO LINABALEHE, wapo ambao PENZI LAO linakufa MPENZI.


Na SHIKAMOO MPENZI,....
....inaweza kufikia kumaanisha tu``SHIKAMOO MPENZI bila PENZI´´ kwa kuwa labda ni kweli kwa kuwa PENZI HUZALIWA, ....
... basi labda pia HUKUA, hudumaa, hunywea, na KUFA tu kama vingine vizaliwavyo MPENZI.





Swali:

  • AU?

  • Hivi SHIKAMOO maana yake ni nini vile?

  • Sasa hivi ni MPENZI au PENZI lake listahililo SHIKAMOO?

  • Tukiachana na PENZI na kuingia kwenye SALAMU TU,- NI mara ngapi weye MTZ utumiaye SHIKAMOO kama salamu huwa unamaanisha hiyo SHIKAMOO KISALAMU kwa umsabahiye?




NI wazo tu hili MKUU na NIMELIACHA ingawa kwako ni RUKSA kulifikiria kivyovyote vile UPENDAVYO Mheshimiwa!

SHIKAMOO basi!
Umefurahi eeh!
Jumamosi NJEMA!





Au hebu Frankie Paul abadili hali ya hewa Kijiweni kwa kumuongelea - SARA



Frankie Paul alete tena -SHUB eeN








Au tu Delinquent HABITS na Hurricane G wabadili zaidi tena kwa -Underground Connection [Tahadhari: lugha watumiayo haijaoshwa mdomo!:-(]


Read more...

Kabla ya MUDA WAKO wa kueleweka KUFIKA, labda AKILI ZAKO na UFIKIRIACHO ni ukichaa kwa WENGINE!:-(

Kuna watu mawazo yao yako mbele ya MUDA,....
..... na sasa hivi hawaeleweki ni nini WAZUNGUMZIACHO.



Swali:
  • Au?

  • Unauhakika MAWAZO YA NYERERE ya siasa ya ujamaa na kujitegemea hayatakuwa ni MAWAZO na siasa inayotekelezeka mwaka 3000?

Na walio KIMAWAZO mbele ya MUDA,....
.......jamii inaweza kuwahukumu sasa hivi KAMA wafikiriacho wakikigeuza kuwa ndio WAKIZUNGUMZIACHO.

Swali:
  • AU?

Na ni mambo mengi katika huu muda,....
...... hayaeleweki ukiyachagua kuwa ndio UFIKIRIACHO,.....

.....na LABDA nikuanzia;

  • DINI,
  • NDOA,
  • SIASA,
  • WOGA WAKO,
  • ni nini LAANA,

.... au TU ni mpaka NI NINI ni aina ya gwaguro au chupi za wajanja,...

.... NA unayaona YANALETA MAANA kwa kuwa TU UNAFUATA MKUMBO WA watu wengi UWAHESHIMUO, utakao kuwa kama wao,NDUGU, au tu WALE TU udhaniao wameukata au tu wanaelimu kwa kuwa unajua waliposomea .:-(

Swali:
  • Au?
  • Unakumbuka UKWELI wa jambo hauathiriwi na IDADI ya watu na labda ni kweli KWELI ya kitu mara kedekede waijuao ni wachache?

  • Unauhakika na sababu za ujanja au tu mambo tu ya kileo kuleta maana kwa BINADAMU leo?

  • Unauhakika mambo ya kileo ya mpaka ya JUHUDI ZA WAJANJA kumvalisha mpenzi pete wakioa YANALETA MAANA wakati inajulikana pete haizuii mpenzi kuonjwa au kuonja LAWALAWA NYAMA MTAANI ingawa anakitumbua nyumbani?


  • Unauhakika wakati wa TANZANIA kupata uhuru haukuwa ni muda wa KAMBONA kuwa RAIS halafu wakati wa Rais MKAPA ndio ungekuwa wakati wa NYERERE?


Tukiachana na hilo,....
... naamini hata kisanaa TANZANIA ,...
... itafikia muda FULANI ndio ITAKUWA UJANJA kwa watu kustukia ni kwanini MORIS NYUNYUSA na ngoma ZAKE au tu Dr ZAWOSE ni mahiri kwa kuwa sasa hivi hawaeleweki kwa kuwa wafanyacho sio BONGO FLEVA.:


Tukiachana na hilo,....
Swali:
  • Si unakumbuka wengi wape kama tu zilivyokuwa demokrasia tuzisifiazo moja ya matunda YAKE ni kupotea kwa wengi hasa kwa kuwa NI KWELI lifuatwalo na wengi haina maana ndio usahihi wa hilo jambo?

  • Unauhakika IKIWA kura za wengi TANZANIA ni za wasio elewa hata ni nini wanakipigia kura maana yake hao wengi ndio wapatiao jibu la matatizo ya TANZANIA?

  • Hivi wewe MKUU unaeleweka?

  • Hivi Mheshimiwa wewe HUMJUI HATA MTU MMOJA ambaye ni wale wafuatao mkumbo wa jambo kwa kuwa ndilo lielewekalo AU TU LIFUATWALO na wengi?

  • Si unajua moja ya siri la urahisi wa kitu kuwa na wafuasi wengi ni MDHANIO wa urahisi wake kueleweka wakati tunajua MATATUZI ya mengi si rahisi?
  • Si unajua wazo lako lisilo wezekana leo labda tu muda wake haujafika?
  • Si wazo lihangaikiwalo NA MAARUFU leo linaweza kuwa ni wazo lililopitwa na wakati?




Naacha na ni wazo tu hili MHESHIMIWA !:-(


HEBU tu Fela andelee kwa kuleta another underground SPIRITUAL GAME kwa kitu - Beasts of no Nation.



Au tu FELA KUTI aendeleze SPIRITUAL GAME kwa hiyo hiyo- Beasts of no NATION



Au tu Phil Collins atulize kwa NENO kueleweka kirahisi kwa - Another day in Paradise

Read more...

Kwa kuwa hata SAMAKI aringe vipi BADO ukweli uko palepale kuwa ana SHOMBO!:-(

>> Friday, January 29, 2010

Samaki weye kisura, na kwa ladha ni mtamu
Napenda yako sura, na kukugida mtamu
Kwa protini kinara, kukukaanga na hamu

Ila samaki kipenzi, we una harufu mbaya!:-(


Samaki we unanuka, vundo lako sina hamu
Harufu yako kunuka, shombo lako sina hamu
Na samaki unanuka, kwenye ya wali karamu

Hivi samaki kwanini, wanuka ila mtamu?:-(


Na siri yako nyingine, weye una miba ndani
Nje wapendeza vingine, kwa miba kuficha ndani
Wanikumbusha wengine, roho zao watu ndani

Kweli kipenzi samaki, wanuka bila kuvunda.:-(






Swali:
  • Hivi unapenda kunukia harufu ya samaki?
  • Hakuna mtu KIROHO akukumbushaye samaki, kwa nje tamu ukimjua undani roho miba?
  • Unafikiri samaki angenoga zaidi kama angenukia kama manukato?

  • Unafikiri ni kwa nini samaki hunuka kama samaki?
  • Unauhakika Mtu ananukaje ikiwa watu hutofautiana hata harufu ya ushuzi?
P.S
Ndugu Samaki;...
Kwa kunuka mwanawane ,....
..... wewe wanipagawisha. :-(


NIMEACHA na ni wazo tu dhaifu HILI Mheshimiwa NA halikuhusu kama wewe ni MPENDA SHOMBO YA SAMAKI na kwahiyo USIKONDE!

Nakutakia IJUMAA na WIKIENDI njema MKUU!


Hebu Keith Sweat abadili kwa kurudia -Twisted



Au tu Peter Tosh apoze mchecheto na kukumbusha- The poor man Feels it



Au tu Peter Tosh akumbushe tu kuwa tupo watu kama mie Simon Kitururu tunaugua- Reggae Mylitis

Read more...

Udhaifu wa KUONA kabla ya KUPAPASA,....

>> Wednesday, January 27, 2010

.....kwa mwenye macho hapa DUNIANI ,....
..... ni bonge la udhaifu uponzao WENGI na ambao umesababisha mengi ikiwa pamoja na ya ;....
  • Ubaguzi wa rangi
  • Baadhi ya embe dodo zisitomaswetomaswe
  • Watu kuogopa giza na kuchagua kuwa nguvu za giza ni za shetani na za Mwanga niza MUNGU
......au tu hata Maimuna kupendewa kwa ujazo wa TITI badala ya roho yake nzuri.:-(




Na unaweza kubisha, lakini KUONA pamoja na mazuri yake yote hapa DUNIANI,...
.... huleta udhaifu wa KUSIKILIZA na KUJISIKILIZA, kitu kisababishacho waonao wengi kusahau mapungufu ya wakionacho hasa kimtazamo wa muda mrefu KISA WAMEKIONA , na wamejiaminisha HICHO kitu kwa sasa NI kidude kizuri.:-(

Swali:

  • AU?

Na udhaifu wa `` KUONA KABLA´´ uathirivyo ,....
... usipoangalia waweza kukufanya ujiaminishe mwenyewe kuwa EMBE DODO ni TAMU kisa MUONEKANO WAKE na kusahau kuwa KUONA EMBE DODO na hata KULITOMASATOMASA embe dodo bado sio kipimo kizuri cha utamu WA EMBE DODO kwa kuwa ni LADHA ambayo huhitaji embedodo LIONJWE kwanza ndio kithibitisho cha UTAMU kipatikane,.....
..... na hapo ni kama hatufikirii MANUFAA YA EMBE DODO ni virutubisho vyake na wala sio muonekano WAKE , ..
....na wala sio hata ule wake UTAMU.:-(

Swali:

  • AU?


Na kuna UDHAIFU WA KUSIKIA kabla ya KUONA.

Udhaifu HUO wa kusikia kwanza pamoja na mazuri yake yote DUNIANI,...
... huweza kuathiri kwa ;...

  • Kudhoofisha makali ya kushuhudia kwako
  • Kukuandaa woga
  • Kukufanya udhani unajua ukweli kuwa Rais Mkapa Fisadi
  • kukuandaa kuamini Maimuna havai chupi

....au tu kunaweza kukusababisha upende MTU au tu SIASA YA UJAMAA NA KUJITEGEMEA kabla ya KUTHIBITISHA MTU HUYO au TARALILA HIYO ana/ina mbivu zipendekazo KWA VITENDO kwako.:-(


Ndio ,...
...sikatai kuwa ``UKISIKIA kabla ´´ unaweza kustukia ni nani KIRUKA NJIA au tu KIBAKA,....
..... au tu KUJIANDAA tu na UCHOCHORO kisa umesikia kuna majangili hapo,..
... au tu kuna MBUYU wenye majini kwa hiyo usipige teke vifuu,....

... na kwa hilo nasikia kuna wapatao faraja.



Na ,....
.. sikatai kuwa nasikia kuna wapatao faraja za ``KUSIKIA KABLA ´´ wengi ambao wanasaidia sana dunia hii iwe kama ilivyo KWA BAADHI YA MAZURI YAKE kwa kuwa tu WAMESIKIA BILA KUONA na sasa hivi WANAJIANDAA tu na;...
  • kwenda MBINGUNI walikokusikia tu
  • kutofanya UASHERATI kwa kuwa wamesikia ya UKIMWI
  • kuwa wafuasi wa siasa za CCM na kufanya TANZANIA tulivu
  • kuwafanya waogope GIZA na kufanya usiku uwe mtulivu

....ila tusisahau tu kuwa moja ya UDHAIFU wa ``KUSIKIA kabla´´ ya kushuhudia ni kwamba faraja yake iko tu katika UWAZO(imagination) UBONGONI mwa mwenye kusikia tu bila kushuhudia kitu ambacho kirahisi husababisha;...
  • WATU kuhukumu watu kwa kusikia tu
  • Watu kuhukumu vitu kwa kusikia tu
... na WAKATI hali halisi ni kwamba wala VITU, Simon Kitururu, au tu Kadala binti ya Kadoda haviko/hawako hivyo.:-(



Swali:
  • Si inasemekana kuna waliosikia tu na kudhani ULAYA bomba kweli na mambo yake ni mswano sana tu?

  • SI kunawasikiao tu na kung'ang'ania ni kweli fulani Malaya?
  • Hivi unafikiri VIPOFU wa macho HAWAONI?


Ndio,...
...pamoja na yote mazuri,...
...KUNA UDHAIFU utokanao na ``KUONA kabla ya KUPAPASA´´ na ``KUSIKIA kabla ya KUONA na KUPAPASA´´,....

  • ... kwa hiyo UKIONA, - kumbuka KITU kina zaidi ya UONACHO na kwahiyo hata kama ni lako LIMCHUMBA lionekanalo NONO kimuonekano, ukiingia kichwakichwa labda lina UKIMWI na kwa hiyo ni vizuri ujue kabisa unalipenda LIMCHUMBA na umelipenda na MDUDU WAKE ili penzi lako lililo sababishwa na KUONA tu MBIVU inaelea, linoge na kusaidiwa kudumu kwa vitendo pia KWA KUWA unalijua LIMCHUMBA kwa zaidi ya lionekanavyo LIMCHUMBA.

  • ...kwa hiyo UKISIKIA kabla ya KUONA kumbuka KITU kama tu GIZA liogopwalo, si lazima ni kweli GIZA linatisha hivyo ukikumbuka hasa isemekanavyo na ISHUHUDIWAVYO na mpaka NA watoto wengi wazuri uwaonao MTAANI ambao WENGI WAO walitengenezwa na wazazi wao vizuri GIZANI kwa kitendo kilichoenda shwari tu gizani na kwahiyo tu kumbuka aliyeoanisha GIZA na vitu vibaya si lazima aaminike kwa kumsikia tu kwa kuwa MABAYA mengi hufanyika kwenye MWANGA na kwahiyo labda nguvu za shetani ni NGUVU za MWANGA na wala sio NGUVU za GIZA.




Swali:


  • Au?
NI WAZO TU HILI MKUU na NIMEACHA!

Tubadili kwa kwenda MALAWI kwa Lucius Banda alete - Tina


Au twende tu na MOZAMBIQUE ninmuache mwanamuziki mwingine aliye uawa Afrika Kusini na waliotaka kumuibia gari miaka michache iliyopita kwa jina GITO

Read more...

Kwa kuwa kuna WAONGEAJI watumiao sauti ili KUKAA KIMYA!

Wengi waongeao haki ya nani hawasemi KITU,...
....ndio maana usitishike na stori ndefu kwa kuwa kisemwacho chaweza kuwa kinajaa tu MSTARI.

Na ni kipaji kuwa KIMYA huku unaongea,...
..... na ajuliaye hicho kipaji NI mpaka baada ya kuagana naye ndio utastukia na kuanza kujiuliza:

  • Hivi jamaa lilikuwa linasema nini vile?
  • Hivi Mheshimiwa kunachochote kweli alichokuwa anajaribu kutuambia?

... kwa kuwa watumiao SAUTI kukaa kimya na wenye kipaji KWA HILO wakati unawasikiliza unaweza ukajiaminisha mwenyewe kuwa kuna kitu unapata katika waongealo.:-(



Na KWA MTAZAMO MWINGINE labda ukweli ni kwamba,...
.... ukichunguza utastukia kuwa tunaishi katika JAMII ambazo hufunza watu kuongea kwa SAUTI wakati huo huo katika baadhi ya mambo kukaa KIMYA.


Na labda ni kweli ukiniuliza miye ,....
.... KWA ASIYELAZIMIKA KUONGEA NAWE AKIFIKIA kuongea nawe ,....
huyo kashapitia UCHAGUZI wa afikiriacho kinafaa kukuongelesha, MANENO atakayotumia asije akakukwaza weye MSWAHILINA kwa maneno ya KILOKOLE au tu hata jinsi ya KUKUONGELESHA ustukie mahaba wakati neno mahaba limekaliwa KIMYA.


Swali:
  • Si unajikumbuka tu WEWE MWENYEWE wakati unaongea na MTU ukwepavyo baadhi ya MANENO, MAMBO au tu vitu fulani kimsisitizo, KIKUVIDOKEZEA au hata tu ugusiavyo baadhi ya mambo ili tu kufanikisha kukalia kimya baadhi ya mambo?

  • Si unajua stori yako ya kufeli mtihani iliyoko kichwani mwako itofautianavyo na umsimuliayo Mzazi?

  • Ukikutana na mtu si unastukia ni mambo mangapi ya kupitiayo kichwani kuhusu huyo mtu na wawezakung'amua ni asilimia ngapi ya mambo yamuhusuyo huyo mtu ambayo huyaongelei?
  • Kwani unafikiri kila unavyoongea kuna kitu hasa unachosema?


NI wazo tu HILI MKUU!


Samahani Caiphus Semenya yuko mawazoni tena na kitu - Angelina





Pat Shange naye arudie- Sweet Mama

Read more...

UPROFESA wa nukuu za mstari mmoja MMOJA!

>> Tuesday, January 26, 2010

Napenda kunukuu hasa nikitaka kulazimisha hoja nayoshindwa kuijengea HOJA.:-(

Na nawajua wapendao kunukuu kwa kuwa hoja yao ili iaminike kama ni hoja kuna WAWASIKILIZAO wapendao kusikia angalau jina maarufu ambalo kimtazamo lakubaliana na ya mdau mpya HOJA.


Na haki ya nani kama hoja yako ni ya magimbi,...
... na ukaingizia`; ``NA Yesu alisema ......,´´
...... halafu ukamalizia na hoja zako za magimbi ni matamu kuliko Mihogo kuna watakaosita kukubishia KUHUSU UTAMU WA MAGIMBI ingawa WANAPENDA MIHOGO kisa umemnukuu tu Yesu katika ya kutetea magimbi HOJA.


Na kama ni siasa za Tanzania za kujisifia unakula tu magimbi ...
... na ukaingizia na`` Nyerere alisema.....,´´
.... halafu ukamalizia na kula UBWABWA PEKEE MBELE YAO wakati kwenye SINIA KUNA MAGIMBI PIA kuna ambao hawatasita kukuunga mkono na HOJA YAKO kuhusu magimbi NDIO CHAKULA PEKEE kifaacho kuliwa wakati wanashuhudia wewe unalenga na unaonyesha kwa vitendo ni mtu wa UBWABWA kisa umemnukuu Nyerere na umeingizia magimbi katika HOJA.

Ndio ,...
...kunauwezekano kuwa nimepitiliza kudhaifisha kiunyambulisho hoja ya magimbi hapo juu !:-(

Swali:
  • Si unakumbuka lakini nukuu za mstari mmoja miwili katika STORI ya Bata Mjamzito inaweza ikafiti vizuri kuzungumzia au tu kujenga madhari kuwa stori ni ya mbuzi /BEBERU lisilo basha?

  • Kama wewe ni Mkristo kwani hujawahi kufanikiwa kusikiliza mahubiri yaliyojengewa hoja na baadhi ya vifungu vya BIBLIA halafu baadaye ukaendelea kusoma vile vifungu na kugundua wala haviendani na hoja viliyoisaidia wakati mchungaji anashuka mahubiri Kanisani?


Ndio,....
... tuna nukuu na baadhi ya nukuu haki ya nani lazima umtishe mtu kuwa wewe MSOMI SANA kama ukipatia kunukuu,.....
....na si utani kuna mpaka MAPROFESA wa nukuu za mstari mmoja mmoja na katika kuipamba hoja utakuta mtu anaweza kukusimulia stori hata ya MBWA kiruka njia halafu akanukuliwa kuanzia Plato, Socrates, Nyerere, Rais Mkapa , Askofu Mkoba, mpaka MIMI katika kukuelezea kwa nini mbwa yule hajapata bado gono na mbwa wenzake wanafikiri ni mchoyo wa MIFUPA katika jamii ya MBWA katika tu kujenga HOJA.


NAACHIA HAPA nikiamini unajua hili ni wazo tu na labda halina hata UKWELI!

Na katika nukuu za tishatoto za ghafla hapa nami nanukuu bila sababu maalumu;
~Andre Gide akidai ´´Believe those who are seeking the truth. Doubt those who find it.´´

Na ~Alfred Lord Tennyson adai :``I am a part of all that I have met. ´´


Na ~Baba Ram Dass adai ``Only that in you which is me can hear what I'm saying. ´´

Swali:
  • Umestukia ni hoja mamilioni mangapi nukuu hizo zaweza kuingizwa bila mtu kujua wakati wanaziongea NILIOWANUKUU walikuwa wanaongelea nini?


Hebu tuamishwe kimawazo na RZA arudishe ya dunia katika -La Rumba




Au tu Zain Bhikha arudishe busara za Mungu katika- Allah knows

Read more...

ASILI ya MIIKO kwangu na UASISI /MWASISI wa ni nini MWIKO kwako!:-(

Asili ya vingi ambavyo ni mwiko kwangu ni KUTISHWA ,...

... na vingi ambavyo bado kwangu ni MWIKO na ambavyo sijatafuta sababu zake ni kwanini ni MWIKO, sababu za hiyo miiko bado SIJAPATA.

LAKINI pamoja na sababu ya MWIKO yaweza kuwa ni kutishwa BADO ni MWIKO !:-(




Na MWIKO kwako labda sio MWIKO kwa wengine hata kama hukutishwa,...
... na kwa hilo ukitafuta sababu ni kwanini , sababu UTAPATA.:-(

LAKINI pamoja na sababu ya MWIKO KWA WENGINE yaweza kuwa sio kutishwa BADO ni MWIKO !:-(



Na kwa wengine ni MWIKO kula KITIMOTO, au KUTAHIRIWA ,..

... wakati wengine MWIKO ni POMBE kama Uarabuni , au wengine ilivyokuwa sio mwiko katika mila baadhi kucheza ngoma matiti nje kama TANZANIA, au tu RUKSA bangi kidogo kama Uhindini,...

....ingawa NA kwa wengine Msichana mkubwa kuoga uchi na baba yake ni RUKSA na sio MWIKO kama Ufini, au tu Mwanamume kumuoa Mwanamume mwenzako ilivyo RUKSA na sio MWIKO Sweden ,....


... na ukitafuta sababu , UTAPATA.


Swali:

  • Unafikiri asili ya MIIKO ambayo kwako ni MWIKO ni nini?

  • Unafikiri kushika MAKAA YA MOTO wakati wewe na kila MTU wanajua MOTO UNAUNGUZA ni mwiko?
  • Unauhakika MIIKO ya wengine kwako inaleta MAANA?

  • Unafikiri MIIKO yako kwa wengine INALETA maana?


Ndio KILA MWIKO unaasili zake,....
..... na labda kama kuna asiyevunja MIIKO basi kila MWIKO itafikia hakuna ajuaye kwa uhakika sababu ZA UZALIWA wake kitu ambacho kitasababisha KUNA KIZAZI CHA UMMA NA KIJIKO kitahitaji kuwe na PROFESA afanyaye utafiti wa KUVUMBUA ni kwanini baadhi ya JAMII ziliamua ni mkono wakushoto ndio wa kuchambia mavi na kufanya baadhi ya jamii kufanya ni MWIKO kuutumia MKONO HUO wa KUSHOTO kumsalimia mgeni au kuutumia kuchovyea tonge la UGALI WA YANGA kwenye bakuli moja la maharage swafi ya nazi,- na yote hayo IKIWA TU ni katika juhudi za kujaribu kuelewa MWIKO.:-(


Na ni kweli MWIKO unaasili yake,...
... na baadhi ya miiko ya hapo baadaye labda MWASISI ni wewe na tabia zako!:-(


Ni wazo tu hili Mheshimiwa USIKONDE!

Na hebu R. Kelly abadili kwa-Bump & Grind



Au tu Wu Tang Clan warudie- The heart gently Weeps

Read more...

STAREHE ya kutumia MUDA BINAFSI kuhukumu WENGINE na maisha yao BINAFSI!

>> Monday, January 25, 2010

Ni kweli,...
... kunyoshewa vidole hainogi kama KUNYOSHEA wengine vidole hasa kama kilengwacho ni KASORO.


Na kunyoshea wengine vidole KUHUSU MAMBO YAO BINAFSI inasaidia sana kupunguza muda WA mtu kujichunguza mwenyewe BINAFSi hasa kama lengo ni kukwepa kujistukia zako KASORO.


Na mtu asipokuwa muangalifu anaweza akafikiri kutambua kasoro ni kitu rahisi mpaka itakapotokea AKAFIKIRIA na kustukia ukiwadadisi watu utagundua karibu kila kitu ukionacho hakina kasoro kuna AMBAO wanakikosoa kwa KASORO.:-(

Na haki ya nani uonacho kina kasoro kama tu MATEGE,...
.... kuna apendaye MTU kisa matege mpaka KWENYE ndoto zake za kikubwa za MCHANA ofisini WAKATI YUKO MACHO, ndoto zile za uasherati za kuombea siku moja afanikiwe kupata nafasi ya kufanya dhambi ya uzinzi na MTU mwenye bomba la matege ambaye atamsalimisha kutoka kwa wanaomfuatafuata KATIKA MAISHA HALISIA wenye miguuu imenyoka kama fito za kujengea kigenge cha kuuzia nyanya na vitunguu MIKESE,- na ni miguu iliyonyoka NDIO kitu ambacho kwake ndio KASORO.:-(

Swali:

  • Unafikiri kama mtu ana BONGE la pua kubwa kiuwiano na SURA YAKE imsaidiayo kupumua vizuri na kudaka harufu bwelele NZURI au tu za chooni, huyo anakasoro ya pua au ni yule mwenye pua UJAZO wa kawaida AMBAYO HAINUSI VIZURI na inazingua upumuaji , na ambayo inasababisha astukiwe ZAIDI kwa masikio kama Rais Obama ndio mwenye KASORO ya PUA?
  • Hufikiri KASORO kwa asilimia kubwa ambazo SI UGONJWA zilalamikiwazo ni za KUBUNI kwa aliyenacho ndio maana mwenye aibu kwa midomo minene hushangaa watu wakilipia kujazwa midomo ili LIPS zijazie tako?

Ndio,....
.... kuna watumiao nyenzo ya KUHUKUMU WENGINE katika kuepusha wengine kuwachunguza yao yaliyojaa KASORO.

Na kwa bahati mbaya au NZURI, kwa ung'eng'e wanadai `` IT WORKS!´´,...
... kuhukumu wengine KWA KIPINDI KIFUPI inasaidia sana kukwepa KUJIHUKUMU wewe MWENYEWE.
Swali:
  • Wakati unahukumu wengine si unakumbuka kama kuna lako lihitajilo hukumu wala haliondoki na liko tu lakusubiri?
  • Je, umefanikiwa kuhukumu mtu leo na kusahau kujichunguza yako yenye KASORO kwa muda leo?
Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!

Hebu Aaliyah abadili hali ya hewa kwa kurudia- One in a Million

Au tu Aaliyah adai -Age ain't nothing but number

Read more...

UMEKIFIKIRIA unachokifikiria LEO?

>> Sunday, January 24, 2010

Jinsi unavyofikiria ,....
.....HUWEZA athiri UNACHOKIFIKIRIA lakini.:-(


Swali:
  • Ni mangapi uliyoyafikiria jana AMBAYO HULAZIMIKI KUYAFIKIRIA LEO ambayo unakumbuka kuyafikiria tena leo?


NI HILO TU!:-(

Read more...

MANUFAA ya MAUMIVU!

NDIO,....
...KUUMIA INASEMEKANA hatupendi.:-(


Swali:
  • Unafikiri bila kusikia maumivu unauhakika usinge haribu hata kikojoleo chako kwa kukiingiza vijiti au ANGALAU kuchoma TU tako lako kwa kukalia jiko la mkaa?
  • Unafikiri bila maumivu maisha au hata vitisho vya JEHANAMU vingeleta maana katika kukudaka hofu?
  • Hivi unajua adaiye roho inauma huwa anamaanisha anasikilizia maumivu wapi vile?
  • Unauhakika hupendi kuumia?

BADO nafikiria hili swala MHESHIMIWA ingawa kunihukumu RUKSA!.:-(

BAADAYE Mkuu!




Au tu ngojea katika kubadili hali ya hewa KIJIWENI hapa Tabu Ley Rochereau alete - Mokolo Nakokufa




FRANCO & le T.P. O.K. JAZZ warudie - C'est Dur la Vie d'une Femme Célibataire


Au tu Too Short abadili kwa -The Ghetto


Na Skee Loo arudie- I wish

Read more...

Jinsi watu watofautianavyo katika kusikia TUSI!

Kunauwezekano kabisa UKIFIKIRIA,....
... utagundua UBUNIFU wa jinsi ya kustukia ni nini hasa ni TUSI haupo katika JAMII .:-(





Swali:
  • Huwa unafikiria ni nini hasa siri ya misingi ya fikira zako za UTAMBUZI WAKO WA ni nini hasa ni TUSI?
  • UKIFIKIRIA unafikiri binadamu wenye busara na akili UWAJUAO HUWA wanapatia tusi la kulikasirikia?


Kuna uwezekano kabisa UKIFIKIRIA,....
..... utagundua labda tafsiri ya tusi katika mawazo ya wengi ni potofu ndio maana hawastukii TUSI HASA ila wanasikia WALILOFUNZWA KUTAFSIRI TU kuwa ndio tusi katika jamii NA JAMII ,....

..... ambalo laweza kuwa kwa mfikiriaji wala SIO TUSI na ni jinsi tu ya lipakuliwavyo na kuwekwa mbele za mtu kumfanyako mtu kuacha kufikiria na kukasirika kisa kaambiwa ana meno kama uchi wa kuku na haki yanani kapandisha mori kuwa alicho ambiwa ni TUSI.


Swali:

  • Ukifikiria kama BINADAMU AKIFIKIRIA unafikiri wengi wadhaniayo ni MATUSI yata faulu mtihani wa kuitwa ni MATUSI duniani ?
Na labda kimfano ,...

.. tusi la kweli ,....
.....KISIASA- ni lile la kubwa zima kufanywa mjinga kwa kuahidiwa AHADI ZA uongo na MWANASIASA KILA WAKATI WA UCHAGUZI MPYA ili umpigie kura KITU AMBACHO kirahisi kikiwekwa katika sentensi chaweza kuwa: ``Haya majinga kweli yani nikitunga TU stori kila wakati wa uchaguzi na kuahidi nisiyoweza hayaachi kunipigia KURA.Yaone vile kama vile haya stukii vile KUWA nalia ofisini na wala siwazi TATUZI la matatizo yao!´´

Na matusi KAMA hayo hutukanwa watu KIJAMII, KIDINI, KIUCHUMI au hata KIUTU tu WAO hata bila kustukiwa kwa kuwa kwa kiswahili watu wamefikia MPAKA kufikiria TUSI KUBWA ni mpaka tu jina la sehemu za siri za mtu.

Swali:
  • Si ushastukia moja ya tusi maarufu kwa kiswahili ni kutajiwa JINA LA SEHEMU ZA SIRI ZAKO halafu mbele ya jina la NYETI ZAKO ikaongezewa neno ``YAKO´´?
  • Hujastukia watu wengi hukasirishwa na wayatambuayo kama MATUSI ambayo hayana kabisa UBUNIFU?
  • Unauhakika ulishawahi kutukanwa au ni tafsiri yako tu ndio itafsiriyo na kulijenga tusi?
  • Unauhakika hatuhitaji kuwa na somo mashuleni ya jinsi ya kustukia tusi halisi ni nini ili tuache kukasirikia tafsiri za tusi ambazo zina fanya watu wakosee kustukia tusi halisi ni lipi?

Kwa bahati mbaya,...

... NA WASIWASI kuna uwezekano mkubwa,...

...wengi wadhaniao wamewahi KUTUKANWA na kufanikiwa kulikasirikia TUSI,...

...walichofanya ni kukasirikia TAFSIRI tu zao ZA KILE walichojifunza kukitambua kama TUSI,....

....na wote twajua tafsiri ni mwanaharamu ndio maana hata sentensi ``BAISKELI WEE!´´- ikilengwa kwa mtu mwenye udhaifu na baiskeli anaweza akakurukia kichwa, kabla ya kukukaba kabali halafu akakukata ngwala huku yuko bize akikukutajia jina la kikojoleo cha mwanamke halafu akaongezea neno ``WE´´mbele yake kwa kuwa anaamini kwa kufanya hivyo ana KUTUSI .:-(



Swali:

  • Si unakumbuka kusikia au kutambua tusi ni kitendo cha kujifunza KUTAFSIRI TU ndio maana IRAKI kumrushia Rais George Bush KIATU ni tusi wakati kwa Mmarekani kumrushia mtu kiatu MAANA YAKE ni KUMRUSHIA MTU KIATU?
  • Unauhakika jina la sehemu zako Nyeti chini kidogo ya kitovu ni MATUSI au ni kitendo tu cha kuzitumia hizo sehemu kabla ya kuhalalishiwa na Kanisa au Msikiti au VIBABU FULANI ndio matusi?


NI WAZO tu hili BINGWA na usikonde!:-(

Hebu FELA KUTI arudie-Mr Grammarticologylisationalism is the Boss



Au tu FELA KUTI aachie lawama kuhusu AFRIKA katika -Upside Down

Read more...

KWELI si kila MTU anapenda KACHUMBARI,....

>> Saturday, January 23, 2010

...na kwa bahati mbaya,...
... huwezi KUMLAZIMISHA mtu upendacho AKIPENDE,...

....ingawa unaweza kumshikia KIBOKO asiyependa UJI KIFUNIKO akanywa UJI BILAURI na kukuchekea wakati ANAGUGUMIA huo uji wa muhogo ingawa UKWELI UKO PALEPALE KUWA kwa uji hana PENDO.:-(


Na kwa kuwa si kila mtu anapenda KACHUMBARI,...
....kwa hiyo mpenda kachumbari kama unajali watu wengine kumbuka kuangalia wenzio kama wananogewa KWELI NA KACHUMBARI YAKO KWELI kama wewe hasa ukikumbuka labda kachumbari yenyewe unogewayo nayo labda imezidi nyanya HATA KWAKO ila wanogewa zaidi na si kachumbairi hiyo , ila tu wanogewa na lako la KACHUMBARI pendo.:-(


Swali ndugu katika hoja kwa afikiriaye:
  • KACHUMBARI kama ni SHEREHE YA BIRTHDAY ambayo KWA kawaida hausherehekei kwa misimamo YAKO, unafikiri unaweza kulazimisha watu wasisherehekee birthday yako kwa kuwa wewe husherehekei?



Kwa kifupi,...
.....SI KILA mtu alaye kachumbari anapenda KACHUMBARI na ,...

... kama ASIYEPENDA KACHUMBARI alaye kachumbari bila kudhurika kwa kuwa kwa kitendo hicho wamuandaliao KACHUMBARI wanafarijika na kitendo zaidi ya utamu wa kachumbari ,..

.....UKINIULIZA naweza kudai LABDA hiyo ni moja ya VIITWAVYO kutokuwa MBINAFSI KWA AJILAZIMISHAYE KACHUMBARI ajuaye hadhuriki na kachumbari KWA kuwa anaheshimu WAPENDAO KACHUMBARI, ingawa asiyedhurika hapendi kachumbari NA anashiriki KACHUMBARI.:-(



Swali:
  • Unafikiri kunaapotezacho Mgogo akijiunga na sherehe ya Wamasai KATIKA kusherehekea kupoteza Umasai wao kwa kuwa ni Krismasi ambayo haihusiani na UGOGO na anaamini Wamasai hao hawadhuriki na shamrashamra zao za Krismasi ingawa KIMILA Krismasi haina uhusiano na Umasai?
  • Tukirudi palepale kwenye kipele cha hoja, SI unakumbuka kuwa hata kama unapenda VIPI KACHUMBARI lakini BADO UKWELI UKO PALEPALE kuwa sio kila MTU anapenda KACHUMBARI?

NAACHA WAZO na ni RUKSA kutolielewa HASA KAMA wewe ni MVIVU KUFIKIRIA kwa kuwa haki ya nani HILI ni wazo tu MKUU!

Hebu tupooze kwa kwenda tena CUBA Ray Baretto na MONGO Santamaria warudishe- Congo Bongo




Au tu Santana Ft Rob Thomas warudie- Smooth

Read more...

Umpendaye SANA HASA kwa uzuri wa TAKO, kwa bahati mbaya TAKO likidondoka au KUSINYAA!:-(

[Tahadhari: Wazo limepinda!:-(]




Kwa bahati MBAYA,...
... UKIFIKIRIA ,...
....chochote kikufanyacho umpende mtu kimuonekano HAKIDUMU!:-(



Kwa bahati MBAYA,...
.... UKIFIKIRIA,...
...chochote KISABABISHACHO unampenda mtu NA kisichoonekana kwa MACHO pia hubadilika hata kama utadai kama tu pendo , KIMEDUMU.:-(




Swali kabla hujatafakari hoja :


  • Kwani unafikiri wewe wa jana ni wewe wa leo?
  • SI unakumbuka kabla hujafa hujaumbika?
  • SI unakumbuka KUNAUWEZEKANO MKUBWA kila umtamaniye kwakuwa KAUMBIKA hata kama ni kwa tamaa ya kutaka kumuonja tu KIDUDE, kama unajua alishaonjwa BASI si unajua kunauwezekano MKUBWA kuna aliyemchoka ingawa kwako bado MZURIII?





NDIO,...
....tunapenda kwa sababu LUKUKI!:-(



Lakini,....

....Upendacho cha MPENZI mpendwa,...
... kama hukuinacho kama akuavyonacho MPENZI basi KUNAUWEZEKANO MKUBWA kesho kishazeeka HICHO kwako.:-(


Na fikiria tu kuwa,....
...... umpendaye kwa kuwa CHUCHU saa sita,.....
.... kumbuka kuna saa ISHIRINI NA NNE katika siku,...


... na kama mapenzi yenu yananyegeleshwa na MUGONGOMUGONGO au tu BONGO FLEVA,...

... kumbuka kulikuwa na JAZZ BENDI kibao BONGO na KWASSAKWASSA pia sio muda murefu uliopita kimtindo ambo sasa hivi kuna watakao apia ni ZILIPENDWA.



Kwa kifupi,...
... KUMBUKA upendavyo KIKUPATISHACHO NYEGE kikupandishavyo nyege cha UMPENDAYE ,....


.... kuingiliana nacho kila siku KATIKA kutibu nyege ni tofauti na kuishi nacho jumlajumla kila siku MAISHANI kwa kuwa tu UKWELI NI KWAMBA katika MAISHA,...
......JUMLA YA MAISHANI na MTU ni zaidi ya tibabu la nyege.:-(


Swali:
  • Si unakumbuka KAMA UMESHAWAHI KUSIKILIZA WAHENGA , umpendaye kwa kuwa ANAKUVUTIA kwa mwanya , mkiingia MAISHANI unaweza kutokumbuka kumuangalia MWANYA kwa kuwa tu unajua ni wako na UNAMPENDA?

  • Si unakumbuka sista DU mpenda mpiga CHUMA kwa kuwa ana SIXPACK unafikiri akipata mimba ni rahisi kumuacha ALIYEKUWA NA SIXPACK kwa kuwa kaota kitambi?

  • Unakumbuka asilimia kubwa ya vilema hawakuzaliwa vilema?
  • Ushawaza wewe bila tako ukoje na akupendaye siku ukiwa hauna tako utu wako unatosha kutunza pendo?
  • SI unakumbuka mwenye mwanya aking'oka jino moja tu mvuto wa mwanya hufanana na mvuto wa kibogoyo?


NI WAZO TU hili MKUU na wala usikonde!



Hebu tubadili kwa Third World ft Bounty Killer & Shaggy wakileta - Reggae Party


Au tu VYBZ KARTEL Ft SPICE warudie -RAMPING SHOP




Nipo,...
.... na baadhi ya siku ni kama pichani ,

......na asanteni WADAU ambao hamkunitenga hizi siku za karibuni ambao baadhi mko PICHANI...:-(

Photobucket



Photobucket





Photobucket








Photobucket


Photobucket



Photobucket




Photobucket




Photobucket




Photobucket




Photobucket



Photobucket




Photobucket




Photobucket

























Photobucket





Photobucket





Photobucket




Photobucket




Photobucket




Photobucket




Photobucket





Photobucket




Photobucket




Photobucket




Photobucket


Photobucket





Photobucket



Photobucket




Photobucket




Photobucket

Read more...

Wakati na wasiwasi na ukweli wa msemo ``RASILIMALI YA MNYONGE NI UMOJA!´´.:-(

NDIO,..
...UMOJA ni kitu cha ajabu,...
.... ndio maana umoja wa KUKU na jeshi lake la VIFARANGA vyao ni BONGE la sherehe ya ulaji laini kwa MWEWE.:-(



NDIO,...
.. kuna wanyonge afadhali hata wasiwe na UMOJA kitu ambacho sio ajabu ,...

... kwa kuwa matokeo ya umoja wao ni kuongeza UNYONGE tu kama wingi wa vifaranga vya kuku kwa MWEWE.



Kabla sijaendelea....
Swali:
  • Unafikiri Tanzania, CCM ni umoja wa vifaranga vya kuku au ni umoja wa MWEWE?
  • Kwani hujastukia TANZANIA hata kama unyonge wa RAIS KIKWETE ni MZURI, unafikiri kundi lake lisipokuwa na aina kadhaa zenye nguvu tofauti na za unyonge wa RAIS KIKWETE , Rais Kikwete anaweza KUKIKWETELISHA?
  • Si ulicheki HASA kama uliwahikucheki TANZANIA wakati wa RAIS NYERERE jinsi umoja wa WANYONGE alivyokuwa anapata tabu nao KUNYERERESHA nao?


Umoja ni NGUVU,...


.....si pingi hilo NG'O.:-(




Lakini umoja tu kwa kuwa wote chama chenu cha kuvizia UBWABWA MISIBANI ni kimoja na wote NYIE ni vifaranga,....
..... haki ya nani kwa mwewe -UMOJA HUO WAKATI HUO ni kitoweo ,..

....na KWA BINADAMU- labda WANADAMU wengine wanawasubiri TU vifaranga mkuwe wawachinjie WAGENI kuku MZIMA.:-(


Swali:
  • SI ushawahi kushuhudia baadhi ya ukarimu WA WATU WENGINE ni kukaa na njaa wakati mgeni akija atachinjiwa jogoo?

NIMEACHA WAZO na SI lazima uelewe naongelea nini MHESHIMIWA na ni WAZO TU HILI Mkuu!:-(



Hebu TUBADILI HALI YA HEWA KIJIWENI kwa kumpata General Larry Platt katika- Pants on the Ground




Au tu tumpate General Larry Platt katika -Pants On The Ground (TFG Remix)

Read more...

Sura MIA za MTU MWENYE sura moja!

>> Thursday, January 21, 2010

.....kuna WASAHAUO kuwa sura ,...

... waliyozaliwanayo SIO sura,....
.... watakayokufa NAYO hasa kama walizaliwa HAI.:-(




Na kwa mkao MWINGINE WA MAWAZO naweza sema ALILIACHO MTU wakati analilia KIWEMBE,...
....kwa kawaida sio KILEKILE aliacho MTU baada ya KUJIKATA na KIWEMBE.:-(




Swali:
  • AU?
  • Unafikiri uifurahiavyo CHUPI dukani ni vilevile uifurahiavyo baada ya kuivaa?




Kumbuka Binadamu huyohuyo mmoja,....
..UKIMTAZAMA SURA,.....
... ndiye mwenye SURA ya:

  • HOFU
  • UJASIRI
  • KUJIDAI
  • KUSHINDWA
  • KUKATA TAMAA
  • KUTONGOZA
  • uijuayo ni ya KUKUKATAA USIMUONJE
  • KUKUDHARAU
  • KUTUBU dhambi ya mwaka jana
  • KUJIDAI
  • KISENGE
  • KIJEBA mchovu tu
  • UZURI kama kalamba limao
  • UBAYA kama kunyanzi la tako la Kima mzee
  • .....YENYE CHUNUSI

  • ......NZURI KAMA MALAIKA
  • KUHITAJI KUKUBALIKA
  • KUKUBALI KAKOSEA
  • HUZUNI
  • FURAHA
  • .....NK,...
.....na labda BINADAMU HUYOHUYO umfikiriaye mwenye sura zote hizo ukimpa muda AU UKIMUULIZA MUANGALIAJI ASIYE....
..... WEWE ,...

....labda huyo MTU mmoja MWENYE SURA mia ni WEWE,....
.... kama sio MIMI.:-(







NAACHA WAZO HILI NYOKO MHESHIMIWA lakini kumbuka MHESHIMIWA hili ni wazo tu !:-(



Hebu tuangalie sura mbili za PAPA SAN Moja akilia.. katika -MADDY MADDY CRY




Au tu akiongelea enzi hizo -hippity hippity Hop

NA sasa msikilize sura yake nyingine akiwa KANISANI katika-Step Pon Di Enemy


Au tu endelea tu kumsikiliza akimsifu Yesu kanisani katika-God is for me

Read more...

Hasira kama HISIA ni CHACHANDU ya maisha na kama hukasiriki , labda nenda KAMUONE daktari!:-(

>> Friday, January 15, 2010

Kuna mambo kama HASIRA utakuta kuna BINADAMU hujaribu sana kuyakimbia,....
.... labda kwa kuwa huo ni UBINADAMU.

Kuna mambo kama HASIRA ili binadamu awe BINADAMU hawezi kuyakimbia,...
....na hiyo ndio hali halisi ya UBINADAMU.:-(



Swali:
  • Si unakumbuka STAILI YA KUONYESHA HASIRA inaweza mpaka kutumika kama ushahidi kwa uliyewahi KUMSIKIA AKIDAI au mpaka hata uakaamini kuna mtu hana hasira?
  • KIHISIA ZA BINADAMU SI umestukia kama KIFO kingekuwa kinapigiwa kura na BINADAMU au tu kinaweza kukimbiwa labda kufa kusingekuwepo duniani na kwa BINADAMU kujaribu kufa kwa uzee ingekuwa ni kitendo cha kuvunja sheria?


Lakini,...
....kama wewe ni BINADAMU ,ukifikiria HATA SIO SANA waweza kugundua kuwa HISIA zako zote kama binadamu zina umuhimu wake KWA BINADAMU na kwahiyo si kitu cha kipuuzi HATA KAMA HISIA ZENYEWE katika muda husika ni JIPU LINAUMA , na labda zinakupa tu shughuli ili maisha yako yalete maana KIBINADAMU yaletavyo sasa MAISHANI MWAKO.



Ndio ,...

......hisia zako ni MUHIMU.

Kwa mfano ,....
... hisia zako kama za:


  • Njaa- labda bila kusikia njaa wewe labda usingestukia ujivuniacho kuwa unaakili kwa kuwa tunajua tu kuwa unaakili kwa sababu ya ufanyayo kazi na labda kisa unafanya kazi hiyo ya utafiti wa mende NI kwa kuwa tu unalipwa mshahara ambao UNAUHITAJI ILI UNUNULIE CHAKULA,- na wala huzimii kiasi hicho mende , panya, au hata sehemu za siri za ng'ombe ambavyo vimekupa PHD kama mtafiti tukuzimiaye kwa MIAKILI.:-(

  • Huzuni- hasa kama unastukia mchango wa kuwa na huzuni katika FURAHA yako.

  • Kukasirika- hata kama hapa nikigusia kukasirika kwa wazazi WAKO kama umestukia mchango wake katika kukufunza abadu usiwe toto tukutu.

  • Kuchoka- katika kukusaidia kupumzika ili baadaye ufikirie upya kwa akili iliyotulia.

  • Au tu HISIA zikufanyazo uhisi UNANUKA KIKWAPA au tu sehemu za siri - zikusaidiavyo kukufanya utafute maji uoge , AU TU uwe msafi na mwenye AFYA zaidi kwa kuwa msafi.

Swali:
  • AU?




Tukirudi katika hoja ya kukasirika a.k.a HASIRA,....

.....kujinyima kukasirika mara kwa mara, kama tu matatizo ya kutunza sana nyege mshindo kwa wenye ukame ,- kwaweza kusababisha siku moja kikukeracho kidogo kikasababisha UKASIRIKE sana KUBWA KULIKO na kutuonyesha vioja bure MHESHIMIWA !



Kwa kifupi,...
labda jitahidi kukasirika mara kwa mara angalau ufanye mazoezi ya kujulia jinsi ya kuporomosha hasira kistaarabu au tu kuepuka KUKASIRIKA SANA ghafla kisa tu umejilundikia hasira kibao za vitu vingi na hapa siongelei umkasirikiacho Rais Kikwete au tu JIRANI.:-(





Swali:
  • Kutunza hisia KAMA WEWE ni MUUDHURIAJI MISIBANI si unakustukia KILIONI hasa ukistukia kuna waliao sana kupita kiasi KWA WASIYEMJUA na majina wayaliliayo hayana uhusiano na Marehemu aliyesababisha msibani hapo kuna mnuso?



Lakini,..

...JARIBU kumkasirikia akukasirishaye basi,...
... kwa kuwa ni uonevu kukuudhi akuudhi BOSI wako halafu HASIRA ZOTE unaziamishia nyumbani na kukasirikia watoto , BILA KUSAHAU na pia kumnyima unyumba MZAZI MWENZAKO.:-(

Jaribu kumkasirikia akukasirishaye basi ,...
.....sio iwe LIMZAZI lenzio limekuudhi nyumbani KWA KUKATAA KUFAFANUA, halafu unaleta fujo BAA - samahani- kwa watu wengine OFISINI ambao wala hata hawajui unawasiwasi MZAZI mwenzio ni mgawaji wa tendo la ndoa kwa wengine na labda MDUDU unao.:-(



Swali:
  • Unadhani ni kila wakati unauhakika ni nini kinachokukasirisha?
  • Kwani utanibishia nikidai hasira zina utamu wake wewe?
  • Unafikiri kwa TANZANIA haiwezi kuwa ni fasheni tu kuikasirikia CCM ikiwa bado inasemekana WATANZANIA wengi wasikikao wakiilalamikia CCM, ndio waipigiayo kura kwa siri?
  • Au ni kweli fasheni ya hasira siku hizi TANZANIA ni kuwakasirikia MAFISADI kabla mkasirikaji naye hajawa FISADI?





NIMEACHA wazo MKUU, na kumbuka hili ni wazo tu MHESHIMIWA!
Ijumaa na WIKIENDI njema MHESHIMIWA!


Hebu BB KING na Tracy Chapman warudie- The thrill is gone



Au tu ngojea Sade azungumzie tu - King of Sorrow

Read more...

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP