Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Tukifikiria umuhimu wa INZI hata wakati tunaendelea angalia makalio ya BONGE la TOTOZ yaliyotepweta!

>> Saturday, February 19, 2011

Hapa DUNIANI kila kitu kina umuhimu wake,...
.... kama tutaangalia MAPANA na MAREFU ya kila kitu,...
.... na wakati unaua hata  INZI au tu MBU,...
....kumbuka LABDA hata kama kuna kitu kwa harakaharaka HATUSTUKII umuhimu wake,...
....bado  umuhimu wa  UWEPO wao  UPO:-(


Swali:
  • Si inasemekana moja ya kiondoacho uozo wa MIZOGA  hapa DUNIANI ili igeuke kuwa udongo tena ni INZI ambao kwa kutaga mayai kwenye MIZOGA husababisha mafinyofinyo yalao MZOGA  na kuugeuza udongo wenye rutuba ili ulime BAMIA kabla mafinyofinyo hayajabalehe kwa kukua na kugeuka INZI?

  • Si umewahi kufuatilia mzunguko mzima wa maisha ya inzi kutoka yai mpaka INZI kigoli adoeaye chakula mezani kwako ukashuhudia jinsi hatua mbalimbali za maisha ya inzi zichangiavyo kwenye mazingira yako?


  • Na kama wewe unaamini MUNGU aliumba viumbe vyote hapa DUNIANI- je unafikiri aliumba mpaka INZI bila INZI kuwa na mchango wake katika afya ya MAZINGIRA ya DUNIA hii?

Ndio,...
....ukiuliza  wana MAZINGIRA watakuambia,...
.... karibu kila kitu mpaka MINYOO inamchango wake hapa DUNIANI  hata kama hustukii kuwa labda ni MINYOO kwenye udongo  ndio irutubishayo udongo wa  kwenye shamba lako la MIHOGO ikusaidiayo kutengenezea CHIPSI DUME utumiazo kuhongea watoto wa shule!:-(




NIMEACHA wazo ,...
.... na sasa tunaweza kuendelea kuliangalia bila bughudha BONGE la TOTOZ!:-(
KUMBUKA TU nawaza  tu hapa MHESHIMIWA!:-(

Hebu Dub Mafia warudie -Danger

4 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

EDNA 1:03 pm  

Duuuh umenifanya nikune kichwa kwa falsafa yako na utaalamu wa kucheza na maneno.Ni kweli kuna vitu/viumbe vingine huwa tunavizalau kwa kutojua umuhimu wa uwepo wake.....lol kuanzia sasa nitaanza kumuheshimu hata INZI.
Much respect SIMON.

Simon Kitururu 6:04 pm  

@Edna: :-)

Goodman Manyanya Phiri 8:33 pm  

Inzi ni nzuri sana inapofanya shughuli zake aliyekusudia Muumba.

Lakini ikianza kutembea usoni wamtoto wangu mchanga, kunywa vinywaji vyake kabla yeye kunywa...


HAKIKA NITAWUA TU!

Simon Kitururu 7:30 am  

@Mkuu Goodman: Nahisi wewe huamini mafundisho ya BUDDHA!:-)

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP