Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Wakati MATATIZO hayaishi na bado na HAMU ya kuyatukana SHENZI kitusi la nguoni MATATIZO yani!:-(

>> Monday, February 28, 2011

Lakini,....

....kama kuna KITU KIZURI kiwezacho kutoka katika MATATIZO ni ukweli kuwa ,...
.... MATATIZO ndio chanzo cha karibu yote YAITWAYO KAZI au vilivyozalisha KAZI  zipendwazo au zifanyazo kuna baadhi  wanaringa MPAKA utafikiri kama hawaendi haja kubwa vile kwa kuwa ni VIBOSILE  tu MAOFISINI au  pengine tu kwenye WAFANYAKAZI,..
..... kwa kuwa ni kweli ,...

... kama unakwenda KAZINI kunauwezekano KAZI YAKO ni matunda tu ya MATATUZI ya MATATIZO yaliyowahikumsumbua tu MTU FULANI  katika  ya KITU FULANI na katika utatuzi wa hilo  ndio ikazaliwa KAZI YAKO ambayo mpaka leo lengo lake ni kutatua tu TATIZO  fulani  ambalo  kama unafanya kazi kwenye kiwanda cha TISHU ,...
...basi TATIZO la mtu aliyegundua TISHU a.k.a MAKOKONEO wote twajua ilikuwa ni kutatua tatizo la kuchamba bila mheshimiwa kushika mavi.:-(




Kwa hiyo MATATIZO ni siri  ya UTAJIRI kama MTU  atatumia akili kugundua DAWA YA MATATIZO yamsibuyo kwa kuwa,...
.....MATATIZO  yamsibuyo mtu MMOJA yanamchezo wa kuwa ni matatizo ya WENGI  kwa hiyo tatuzi hilo MOJA  linaweza kuwagusa watu wengi sana HATA WASIO NA NYEGE  kitu kiwezacho kuligeuza kuwa bonge la DILI hasa ukiwa na spiriti ya KIJASIRIAMALI kama ya WACHAGA na WAKINGA ya kujiajiri MWENYEWE - kwa kuwa unaweza kujikuta umeanzisha kitu ambacho mwisho wake kimezua bonge la kazi kwa watu wengi huku wewe ndiye KIBOSILE kitu ambacho kitakuwa BOMBA SANA hasa kama unamchezo wakupenda  kuitwa KIBOSILE au angalau kuchekewachekewa BILA SABABU na wajigongao kwa VIBOSILE  ambavyo inasemekana ni baadhi ya vitu VIBOSILE hupata bahati ya kuvigida HASA KWA KUWA KUNA WAJIGONGAO KWA MABOSI - na kwa kuwa kuna VIBOSILE ndude hizo zinawafanya wajisikie wao ni BORA mpaka wengine hujisahau kuwa  chooni hunya tu kama kawaida na wakati wakunya KABLA ya KUJISAIDIA HAJA KUBWA  hujamba vizuri tu mashyuzi  YANAYONUKA TU kama kawaida ya MASHUZI  au  tu kwa kifupi kama matimba a.k.a mavi .:-(






Swali:

  • Si huwa unakumbuka TATIZO lako labda  kuna watu wengi tu  LINAWASUMBUA pia  -kwa hiyo UKIGUNDUA jinsi ya KULITATUA labda maana yake umegundua TATUZI la wengi kitu kiwezacho kugeuza TATUZI LAKO a.k.a SULUHISHO lako kuwa ni bonge la DILI?




  • SI unajua hata waliotatua  TATIZO lao kwa kugundua mafuta ya TRANSFOMA za UMEME yanafaa kupikia CHIPSI MTAANI suluhisho lao HILO limesaidia wakaanga CHIPSI wengi kweli  TANZANIA kutonunua mafuta ya kupikia na kubana matumizi hasa baada ya kustukia UMEME wenyewe wa TANESCO hauwahusu sana huko kwao kwenye vibanda vya MAKOROBOI na pili TRANSFORMER zenyewe za TANESCO   kupitisha kwake kwenyewe UMEME  ni kwa kubahatishabahatisha hasa kwa kuwa UMEME WENYEWE wa TANESCO hata kwa msaada wa shirika mashuhuri la umeme la DOWANS ni vyakubahatishabahatisha kama tu sera za Mchungaji MTIKILA, Mheshimiwa Waziri wa mambo ya ndani MREMA, Papa BENEDICT na Rais Kikwete  kwa ujumla?




DUH nimeacha!:-(
Jumatatu  na KAZI njema MHESHIMIWA -hata kama safari hii bado LABDA HIYO ni  kazi  ya kuosha chupi za KIBOSILE katika kutatua TATIZO la bosi la kuwa chupi yake  sasa hivi ni chafu MHESHIMIWA!:-(





Hebu John Legend & The Roots wakatizie denge shughuli nakurudisha ustaarabu hapa kijiweni kwa - Wake Up Everybody





Erykah Badu aingilie shughuli ghafla kwa - Honey




Au tu Erykah Badu arudie tu tena - Window Seat




Kabla hajazima tu tena manyanga kwa-Didn't Cha Know




Ndio,...
....michezo mingine bado nachezea KANISANI bado!:-(






0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP