Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Matatizo ya KUSHIBA yakifanya mtu ARIDHIKE na kujisikia mvivu kutafuta tena MLO kama kupata kwake MUME kulivyomuondoa MREMBO juhudi za kuendelea kupata HAMU kwa ajili ya MUMEWE!:-(

>> Saturday, March 19, 2011

 Inasemekana aliyeshiba ,...
 ......ni rahisi KURIDHIKA hata bila kula  ,...

... kama tu ilivyo kwa ajuaye anacho kama tu MUME au MKE awezavyo kuingia uvivu kukihudumia kwa kuwa ANAAMINI TU  anacho na kiko  BWELELE na akitaka tu,....
...ni maji mara moja kama MAHARAGE ya MBEYA !:-(

Swali:

  • Si inasemekana  juhudi nyingi za hata WASOMI   huishia wakisha pata vyeti kwa kuwa ushahidi upo kwa JAMII walifaulu na kuwa waliwahi kwenda shule na kiendeleacho baada ya hapo ni  ujinga tu ulindwao na  kuwa wana VYETI vikumbushao JAMII  kuwa hapo mwanzo walikuwa na juhudi ya kujua kitu kifanyacho watu wadanganyike kuwa LABDA WASOMI HAO WALIOSOMA ZAMANI bado wanajua?
  • SI unajua unaweza ukaridhika UNAJUA kitabu kwa kuwa uliwahi kukisoma miaka fulani iliyopita ingawa ukweli ni kwamba UKIPIGWA maswali  ukumbukacho kuhusu hicho kitabu  ni hiyo tu KUMBUKUMBU kuwa uliwahi KUKISOMA?

Ndio,...
... kuna wengi ubunifu wa hata kutibu nyege huisha tu pale wajuapo tu matibabu ya nyege wanayo,...
... ingawa wanasahau kuwa  kwa  kuua juhudi BADO HAKUBADILI KUWA wenza wao bado wanahitaji TIBA kama ileile yenye juhudi za  MWANZO,...
...kitu kiwezacho kusababisha KWA APUNGUZAYE JUHUDI  kutostukia MWENZIE inabidi ahudumiwe na wengine MTAANI!:-(


Ndio,..
... inasemekana kuridhika ni chanzo cha uzembe,...
.....na UZEMBE  pamoja na kwamba nao una FARAJA ZAKE,...
... lakini kabla HUJARIDHIKA na kuwa MZEMBE labda pima kama unafarijika zaidi na FARAJA ZA UZEMBE wakuridhika au LA!:-(


Ni wazo tu hili MHESHIMIWA na ni ruksa kulitemea koozi!:-(


General levy aanzishe mshawasha tofauti upya  kwa -Incredible




Achezecheze nayo  kwa -Shake





General Levy adodose zaidi mbirimbi kwa-Champagne Body



Generali LIVI aendelee kumwaga njugu kwenye bata wengi kwa -Heat



General arudishe dalili za kueleweka kwa -The Wig




Au tu General Levy alainishe zaidi tu NDUDE kivyake kwa nyundo-Right Thing



Sijui kwanini ngojea Apache Indian aanzishe upya kwa-Original Nuttah

2 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Koero Mkundi 7:40 am  

Ama kweli wazo hili limepinda

Simon Kitururu 9:27 am  

@Dada Koero: Kweli kabisa yani inatia hata aibu yani!:-(

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP