Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Unafikiri MWALIMU NYERERE angekuwa hai na kaanzisha BLOGU angekuwa na wamfuatiliao WANGAPI?

>> Tuesday, March 22, 2011

Ndio,...

..... kuna BAADHI ya MASWALI labda hayana jibu  la UHAKIKA KIBINADAMU  hata kama kuna watakao jibu  na majibu yao kuchukuliwa kama ndio jibu lakusadikika,....
... ndio maana hata kama SASA HIVI kuna wajaribuo kufikiria  kuwa wana JIBU la  labda YESU angekuwepo KARNE hii angekuwa na BLOGU na angekuwa anafuatiliwa na MTUZ kadhaa wa kadhaa ambao  kwenye KIBOXI cha MAONI aka COMMENT wangekuwa wanatoa maoni BWELELE hata ya kumtusi na WAKAAMINIKA kwa kuwa wamedai wameoteshwa kama BABU wa LOLIONDO,...
..... bado wafanyacho sasa hivi KWA MAJIBU YAO  HAYO kirahisi LABDA  itakuwa ni KUBUNIA TU .:-(

Swali:
  • SI unajua kuna MAMBO labda yana JIBU ila JIBU lake  sio lazima awe nalo MTU?
  • Si unajuwa jibu la tatizo la  KUBUNIA na KUOTESHWA  kama la BABU wa LOLIONDO linaweza kuwa ni sawa kama HUNA IMANI na maswala ya KUOTESHWA?

Ndio,...
... labda bado ni kweli kila kitu hata kisichomuhusu MWALIMU NYERERE kina JIBU,...
... ila  haki ya nani  HAKUNA  mtu  ajuaye   kwa usahihi NA UHAKIKA  hilo JIBU .:-(

Swali:
  • AU?
  • Na kukosa jibu na kukiri ``HAKUNA JIBU´´- si labda ndio  aina moja wapo ya JIBU aka ndio jibu LENYEWE?
Na najua ,...
.... ni silika ya BINADAMU kutafuta MAJIBU,....
..... lakini labda kuna mambo KUTOYAJUA ndio  chanzo cha FURAHA maishani ,...
.... kwa kuwa labda KUJUA kila kitu sio UBINADAMU na  wala hakuboreshi  UBINADAMU,...
.... ukizingatia kuwa hata tukijua kama NYERERE angeanzisha BLOGU angekuwa anafuatiliwa na watu wangapi isingesaidia kuweka tonge mezani  mwetu na wala isingetusaidia sana kupata hata kificha nyeti kwa wengi wetu!:-(

NI wazo tu hili MHESHIMIWA!

Hebu tumfuate tena hko Kameruni mdada SANDRA NKAKÉ arudie -I miss my LAND



Sandra amwage kitu kiushauri kuwa -Stay True




Au anikune tu tena kwa sindimba-Higher

2 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Masangu Matondo Nzuzullima (MMN) 3:23 pm  

..... lakini labda kuna mambo KUTOYAJUA ndio chanzo cha FURAHA maishani ,..

Na mimi nadhani hapa ndipo binadamu tulipoenda kombo. Tunajitahidi kujua kila kitu na badala yake tunaishia kuishi kwa wasiwasi na hata kugonjweka.

Ni kweli ninahitaji kujua kwamba moyo wangu unapiga sijui mara elfu ngapi kwa siku, unasukuma sijui galoni ngapi za damu kwa siku, na kwamba ukisimama hata kwa sekunde chache tu basi mimi marehemu?

Umegonga pointi mkuu!

Rachel Siwa 6:38 pm  

Tusichoke kuuliza,kujifunza na kudadisi! japo si kila jibu ni sahihi.
@kaka Matondo nakuunga mkono!
@kaka Kitururu asante kwa maneno machache yenye maana na kujifunza.

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP