Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Katika JITIHADA tena za MTU za KUHAKIKISHA anaheshimiwa HADHARANI,....

>> Thursday, April 28, 2011

.....si kuna UWEZEKANO imefikia mpaka  kuna WENYE busara na HEKIMA wanakaa kimya HADHARANI,...


....na labda ni mpaka UKUTANE NAO pembeni wakati mnaongea wakati WATU wengine hawasikii ndio waweza kujikuta unastukia HEKIMA busara na majibu ya maswala ya maisha yasumbuayo ULIMWENGO jinsi walivyo nayo?

Ndio,...
....kuna jamaa ni mpaka ukutanenao PEMBENI,....
... ambao HADHARANI hukaaga KIMYA kwa kuwa wamefikia KUAMINI hadharani,...
.... ni mahali  ambapo MHESHIMIWA asipochagua cha KUONGEA atajiharibia HESHIMA!



Ni wazo tu hili baada ya kukutana na MHESHIMIWA ambaye hukaa kimya HADHARANI hata kama tunaongelea CHIPSI na MISHIKAKI ili asije julikana anahusudu  vitu hivyo na UMATI!:-(

Hebu King Yellowman aongee anavyofikiria hadharani kuwa-FOOLS GO TO CHURCH on SUNDAY



Au tu Mister Yellowman  aombe tu na kidude kitu ambacho sidhani wengi wanaweza kuomba aombavyo hadharani katika ngoma-Gimme KIDUDE/gimme vagina





Kabla ya kutuliza kitu kwa kustukia- Wrong Girl To Play With

4 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Goodman Manyanya Phiri 12:38 am  

Asante, Mkuu!

Vilevile watu wengi wanaotoa maoni hadharani, hasa hao waheshimiwa, sio maoni yao, bali wanaambiwa waseme nini kivipi. Wengine ukiongea nao kando hawaamini kabisa kile waliekuwa wanakisema hadharani!


Katika mambo haya ya INTERNET, nimeshangaa kujifunza hapo majuzi hata blogu zetu hizi, sio wote wenye blogu ndio waandishi wablogu, posti au mandhari zao!

PESA, SABUNI YA ROHO, BWANA! Na siku moja tutashangaa kusikia kwamba "Mtakatifu Simon Kitururu yule wa Mawazoni sio mwandishi wa blogu yake, BALI ANAWALIPA WATU WENGINE KUJENGA ILE status YAKE TU!!!!"

Au...

"Mtu kama Manyanya Phiri hayupo kabisa duniani ya Mungu na mnayemuona ni ACTOR tu na yule mwenye mawazo katika blogu ya Manyanya ni Mzungu fulani kutoka Wapiwapi"

BELIEVE NOTHING OF WHAT YOU SEE PARTICULARLY ONLINE!

Simon Kitururu 12:59 am  

@Mkuu Goodman: Umenitisha unajua na hoja yako!

Unajua nimesikia mpaka kwa MABLOGA MAARUFU TANZANIA KARIBU WOTE UWAJUAO hasa wenye matangazo ya BIASHARA wanachaguliwa cha KUANDIKA na wawapao MATANGAZO.


Nimetishika kwa kuwa ni baada tu ya kutumiwa ujumbe huo nikasoma maoni yako haya!

Ila ikifikia na mimi naandikiwa nafikiri utastukia Mkuu!


Ila ndio hivyo kuna watu hadharani ni fulu kujifanya ni watu wengine wakati kama unawajua hasa wale ambao...... sio hao!:-(

Unazidi kuniwazisha Mkuu!

Halafu hii:

``BELIEVE NOTHING OF WHAT YOU SEE PARTICULARLY ONLINE!´´

imetisha mpaka mdau ambaye alikuwa anadeku nachoandika!

Goodman Manyanya Phiri 6:19 am  

Naam, Mkuu!!!! Tunajifunza kila siku aisee!!!

Unknown 12:56 pm  

Aiseee...ni kama kweli vile!!

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP