Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

KUHUSU nini kwa Mrembo KHADIJA kinaleta MAANA wakati kwako ni MKOROGO TU!

>> Tuesday, June 14, 2011

Kiletacho MAANA kwako labda ni matokeo yako KIVYAKO,...
.... katika kujifunza nini ni cha MAANA.

Swali:
  • SI umestukia CHAA MAANA  hakina maana kama hakuna kitu kikujengeacho misingi ya kufanya ufanyacho ni cha MAANA kiwe cha MAANA?

  • SI unajua labda KAMASUTRA kwa Padre wa kiromani KATOLIKI  yule ambaye kweli hafanyi ngono hata za kuibia na baadhi ya waumini wake kisiri inaweza kuwa haina MAANA kwa kuwa iongeleacho ni kuwa kuna staili zaidi ya kimishenari na KICHUMA mboga vitu ambavyo kwakuwa yuko kwenye selibasi kirahisi kwake vinaweza kuwa havina MAANA?

Ndio,...
... kama kitu hakileti MAANA kwako ingawa kuna wakidandiao kama GAZETI la UDAKU ambalo kwako liongeleacho kutokana na ulichojifunza ni UJINGA,...
...kumbuka tu si kila mtu alijifunza kujenga misingi ya kuelewa mambo ya maana kwa staili yako hata kama kutokana na ulivyojifunza unaamini mtazamo wako ni sahihi na ufikiriavyo mambo ndivyo itakiwavyo KITU kimambo   kuleta MAANA!:-(

Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!

Hebu Lyle Lovett na Al Green warudie - Funny How Time Slips Away



Au tu GLADYS KNIGHT na VINCE GILL wabadili kwa-AIN'T NOTHING LIKE THE REAL THING


5 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

malkiory matiya 5:17 pm  

Hata Bhoke na Ernest japo ni vajana wamaliza dk tano kwa missionary!!!!!!!!!!!

Rachel Siwa 7:30 pm  

haahahhaa @kaka malkiory nao walikuwa na maana yao,kiu,kutaka waongelwe sana au kijimtindo chao au...

@Kaka wa mimi Simon, hapo nimekuita kama ilivyo kwa kiswahili, Umenena!!!!

Simon Kitururu 3:33 am  

@MkuuMalkiory: Labda ni kwa kuwa ilikuwa ni shughuli ya kupukuchua mahindi anda presha!Najaribu tu kumtetea Mwananume !:-(

@Rachel Mmmmmmh!

Goodman Manyanya Phiri 4:47 am  

Hapana, thamani katika mambo ya maisha, jinsia, au biolojia, HAMNA.


Ugali kila mtu lazima ale tu, au anaweza kuumwa kimwili au kiakili. THAMANI YA UGALI NI NJAA!


Ndio maana hata simba au mbwa, wanachuma mboga tu. Hata hao wanaojidai ni watakatifu mimi nasema waongo tu! Jamaa bondeni huko akitaka ugali wake lazima utampatia tu! Mbona tunazidi kudanganyika bure!?

Simon Kitururu 5:18 am  

@Mkuu Goodman: Hilo nalo ni neno!

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP