Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

UONGO ni aina ya NDOANO na hunasa uwavutiao!

>> Tuesday, June 07, 2011

UONGO unamvuto wake,...
.... ndio maana labda UONGO kuna wauaminio sana tu KIRAHISI hata kuliko UKWELI.:-(

Swali:
  • Kwani hujui kuna waaminio kirahisi UONGO kwa kuwa labda tu UONGO kuurembesha ni rahisi kuliko UKWELI kwa kuwa UKWELI ukirembeshwa maana yake asilimia za UKWELI zimepunguzwa kwenye UKWELI huo?

  • Na si inajulikana kama UKWELI ni mavi hata ujaribu vipi kuurembesha kama unataka ibakie ni kweli mavi ni mavi tu?

Labda ndio maana,...
... ni muhimu kustukia ni NINI cha KUKIAMINI,....
.... na hasa kustukia UNAAMINI kitu kwa kuwa ni kitamu MASIKIONI a u kwa kuwa ni kweli hicho ni KWELI,...
.... kwa kuwa KIAMINIKACHO kinaweza kuwa KINAAMINIKA kwa kuwa tu kina UTAMU wa UONGO!:-(

Swali:
  • Unabisha?


Ndio,...
.... UONGO ni bonge la CHACHANDU pia,...
..... na kama huamini jaribu kuwaulizia waliotongozwa wakakubali kwa kuwa MANENO ya UONGO MATAMU au wenye mpaka bonge la MKE kwa kuwa walifanikiwa kudanganya MTOTO mzuri !:-(

Ni wazo tu hili MHESHIMIWA ,...
....na wala usikonde kama unahamu kwa mara nyingine  ya kudanganya mtu leo!:-(




Hebu Mathey aingilie kati wazo kwa- Ama



MATHEY arudie-Aameyatchi




Au tu Mathey arudie tu na  - Maloune

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP