Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

ISSA SEWE AJIFUA KUMKABILI RAMADHANI SHAULI

>> Friday, October 14, 2011

Mbunge wa Ilala Mussa Zungu atashughudia ZAIDI ya mabondia 42 wanatarajia kushiriki katika mashindano ya mchezo wa ngumi yanayotarajiwa kufanyika Oktoba16 mwaka huu Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari, Kocha wa Klabu ya Ashanti ya Ilala, Rajabu Mhamila, 'Super D' alisema kuwa mashindano hayo yanatarajiwa kushirikisha Klabu 12 kutoka katika maeneo mbalimbali.

Alisema kuwa mashindano hayo yanatarajia kufanyika katika ukumbi wa Panandi Panandi Ilala.

Super D alisema kuwa mashindano hayo yana lengo la kuhendeleza kuhamasisha mchezo wa ngumi nchini ikiwa ni pamoja na muendelezo wa mchezo huo unanaofanywa na Kinyogoli Foundation.

“Tumeandaa mashindano ya ngumi ambayo yatashirikisha vijana mbalimbali na lengo letu ni kuhamasisha mchezo huo ikiwa ni pamoja na kuuendeleza ili uweze kutuletea faida hapo baaye” alisema.

Kocha huyo alisema kuwa vijana watakaoshiriki watakuwa katika uzito mbalimbali kuanzia Unyoya mpaka uzito wa juu.

Alisema kuwa pia wanatarajia kushirikisha mabondia wa kike kutoka katika klabu hizo hizo Aliongeza kuwa katika mapambano hayo mgeni mwalikwa ni Mbunge wa Ilala Mussa Zungu ambaye kwa mara ya kwanza atangalia mchezo huo ukipigwa katika jimbo lake

Aliongeza kwa kusema kuwa wanaitaji wadau mbalimbali wajitokeze kuwasaidia mahitaji mbalimbali ya vijana ikiwemo maji kwa ajili ya mchezo huo kwa siku hiyo wenye nia ya kutaka kusaidia au kushiliki kwa kuchangia chochote wanaweza kuja katika ukumbi wa mazoezi uliopo Amana Ilala au kufika Ashanti Boxingi clabu kwa mawasiliano zaidi unaweza kuwa siliana na Kocha Mkongwe, Habibu Kinyogoli kwa simu 0655928298 au unaweza kuwasiliana na Super D Boxing Coach O713,0787-406938 Email.superdboxingcoach@gmail.com wadau mbalimbali mnakalibishwa



Kocha mkongwe wa mchezo wa ngumi , Habibu KInyogoli (kulia) akimwelekeza jinsi ya kutupa masubwi bondia Issa Sewe wakati wa mazoezi yanayoendelea katika kambi ya Ilala Dar es salaam jana Sewe anajiandaa na mpambano wake na Ramadhani Shauli litakalofanyika mwishoni mwa mwezi huu.(picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com)
Super D Boxing Coach
Photojournalist at Majira, Business Times
        +255774406938
        Po.Box. 15493
Dar es Salaam Tanzania


Nimetumiwa na:
Super D

2 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

tanzaniaKwetu 3:22 pm  

Hili pambano litakuwa nzuri sana! ni vizuri pia kuendeleza umoja atika michezo yetu hapa nchini!
Pia kupata link mbalimbali za michezo ya kitanzania tembelea http://www.tanzaniakwetu.com

Simon Kitururu 7:06 am  

@TanzaniaKwetu: Tuko Pamoja!

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP