Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

CHAMA CHA NGUMI DUNIA (AIBA) KUWAPIGA MSASA MAKOCHA WA TANZANIA

>> Monday, November 07, 2011

                    BOXING FEDERATION OF TANZANIA (BFT)

                                                                                  SLP 15558
                                                                                   DAR ES SALAAM
                                                                                       6/11/2011
                                                               Email; bft.tanzania2009@gmail.com
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI;
         YAH;KUFANYIKA KWA MAFUNZO YA KIMATAIFA KWA
                 WALIMU WA MCHEZO WA NGUMI ZA RIDHAA
                  TANZANIA 12-20 Nov 2011 KIBAHA PWANI.
Shirikisho la ngumi Tanzania (BFT) kwa kushirikiana na Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) wameandaa mafunzo kwa walimu wa mchezo wa ngumi Tanzania.
Kozi hiyo itafanyika kuanzia tarehe 12-20 Nov 2011 Kibaha, Pwani katika shule ya Filbert Bayi.
Mkufunzi katika kozi hiyo ni kutoka Algeria,aliyeteuliwa na Chama cha ngumi cha Dunia (AIBA)
Jumla ya washiriki ni 30 wamechaguliwa kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania bara kuja kuhudhuria mafunzo hayo, kwa kuzingatia mchango wao katika ushiriki wa matukio mbali mbali ya BFT hasa mashindano kwa kuleta timu au mikoa yao kama makocha na kujihusisha kikamilifu katika shughuri mbalimbali zinazohusu kuendeleza mchezo wa ngumi Tanzania
Zaidi makocha hao tayari walishapata mafunzo ya awali yaliyoandaliwa na BFT.
Baada ya kumalizika kwa mafunzo hayo washiriki watakaofuzu watatambuliwa na kuingizwa katika data base za Chama cha ngumi cha Dunia [AIBA]
Pia wataweza kufundisha mchezo wa ngumi popote Duniani na kuruhusiwa kushiriki mashindano yote ya kimataifa kama makocha kwa mashindano yote yatakayo andaliwa kwa kufata sheria za AIBA.
Kwa uzoefu sisi kama BFT tunategemea mara baada ya kumalizika kwa mafunzo hayo,tunategemea kupata ushindani wa uhakika kutoka katika mikoa iliyopata nafasi ya ushiriki,na tunategemea kupata timu ya Taifa ya ngumi yenye sura ya kitaifa tofauti na awali ambapo wachezaji wengi walitokea DAR ES SALAAM na hasa katika vyombo vya ULINZI NA USALAMA.
Kwa msingi huo sasa tutategemea kupata ushiriki wenye tija katika mashindano mbalimbali ya kimataifa hasa kufuzu katika ushiriki wa timu yetu ya Tanzania katika mashindano ya Olimpiki 2012 London Uingereza.Na mashindano mengine ya kimatafa.
Makore Mashaga.
KATIBU MKUU BFT.
 Mob; 0713588818.
 Email;mashagam@yahoo.com                                                                              







--
Super D Boxing Coach
Photojournalist at Majira, Business Times
        +255774406938
        Po.Box. 15493
Dar es Salaam Tanzania

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP