Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Hata uangalieje naweza kusema NCHI za MAGHARIBI sasa hivi KIUCHUMI na KIDEMOKRASIA ni DHAIFU!

>> Thursday, November 10, 2011

Na wakati  AFRIKA twaendelea KUIGA nchi za MAGHARIBI,....

.... tuigacho ni MFUMO  unaokufa na ushahidi ni jinsi  WAO wenyewe unavyowahenyesha KIUCHUMI wao  mpaka hata KIDEMOKRASIA ZAO tuigazo.

Swali:
  • Kama yao ni BORA SANA - hujastukia  mapungufu  ya DEMOKRASIA na UCHUMI wao viwazinguavyo wao wenyewe?
  • Na kuna ajifunzaye kutokana na  wafanyavyo CHINA?

Ndio,...
.... pamoja na UMUHIMU  wakujifunza yaliyowafanikishia MAENDELEO  waliyonayo,....
... tukumbuke kuwa  labda KIHALALI wasingekuwa WALIPO na kwahiyo  tusiruke kujifunza kustukia UDHAIFU wa ya kwao.

Na  pamoja na kuwa KUIGA si lazima ni kitu KIBAYA,...
...lakini tukumbuke KUIGA kila wasemalo na wafanyalo ni UPOFU  MBAYA na labda ni kosa KUBWA.


Pia tusisahau,...
... yawezekanayo CHINA labda  ni kwakuwa hiyo ni CHINA,...
.... kitu kifanyacho  kama weye sio CHINA,...
.... ya CHINA sio ya KUIGA kila KITU!:-(

Ni angalizo tu hili kimtazamo wangu MHESHIMIWA!:-(


Hebu  tupate kamanyola bila JASHO  tena kutoka MALAWI kwa msaada wa WAMBALI katika kibao - Kujipheleka



McCoy Mrubata aingilie kati kwa - Wanna Talk About It



Au tu McCoy Mrubata na Ringo Madlingozi waingizie - Abukho



Halafu tu Ringo Madlingozi amalizie tena kwa - Into Yam

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP