Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

LABDA hakuna MTOTO awazaye akikuwa atakuwa mfanyakazi wa MOCHWARI kuosha MAITI!

>> Wednesday, November 23, 2011

Swali:

  • Au unafikiri kuna MTOTO atamaniye akikuwa ofisini kwake kuwe kunalazwa WAHESHIMIWA MAREHEMU?

Ndio kuna ya UTOTO,...
.... na ya UTOTO ya mpenda UDEREVA ,....
..... mara nyingi sio  yale ya UKUBWANI ambayo huweza geuza MTOTO aliyependa kuendesha apende KUENDESHWA!:-(
Swali:
  • SI umestukia UKUBWA nuksi  hasa pale  kama MTU ni mwenzangu na mimi asiye na MIURITHI ya KITAJIRI astukiapo inabidi afanyie kazi MSHAHARA na ofisi labda ni popote?
  • Na kazi si  ni KAZI tu  ingawa bado ukweli uko palepale  kuwa kazi nyingine MUHIMU   ni zile za kupima wingi wa minyoo kwenye kinyesi cha Mheshimiwa MAABARA ili kuhakikisha kama kweli MHESHIMIWA ana MINYOO?

NDIO,....
... na MAITI wanahitaji WATAALAMU husika ambao ni muhimu tu,...
.... ndio maana MOCHWARI ni ofisi tu za kawaida za WATU  tena labda wale waliokuwa wanaogopa stori za vifo UTOTONI.:-(

NI WAZO TU HILI MKUU!




Hebu AKON aanzishe upya kwa-Mama Africa



Halafu Céu azime  kwa - Roda


2 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Goodman Manyanya Phiri 1:28 pm  

Yule Céu vipi uvutaji bangi? Naona video yake imejaa mimea vile?! Pia nashindwa kumtofautisha (kama ni tofauti) na muziki wa reggae.


Kifupi, "Roda" yake Céu ni pambo kabisa kwa sikio! ASANTE, MKUU!


Kuhusu suali lako. Mtoto anamaliza ndoto zake za ukubwani kabla ya umri wa miaka 7.


Kwa hiyo mazingira yamtoto kwa wakati huo ni muhimo pita maelezo ili aamue mwenyewe kwamba atakuwa daktari wa sehemu za siri au yeye mwenyewe atakuwa msiri wa kuchunga siri za serikali au hata kufagilia siri za nzi kuwekea mayai kwenye pipa la takataka Kariakoo.

Simon Kitururu 8:36 am  

@Mkuu Goodman: Kwa bahati mbaya mie ndoto za utotoni mpaka leo nazo!:-( Tatizo kuna ndoto kiulazima wa maisha niishiyo nashindwa kuzifanyia kazi!:-(

Na natamani kweli ndoto zangu za utotoni zingeishia miaka 7 hasa sasa hivi uliponistua kuwa kwa kawaida mtoto akifikia miaka saba anazima ndoto fulanifulani. Yani mkuu mpaka titi nimehama tu kuwa sinyonyi litoalo maziwa ila nikigewa na wadada huwa bado hupenda kunyonya hasa kama chuchu inamshiko.

Mkuu kuhusu Ceu na bangi zake mie huko siko. Mie napenda tu kazi zake Mbrazil huyu tokea nimuone live maeneo fulani ambapo akafanya niwe mshabiki.

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP