Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

TISHA TISHA ina MIPAKA na LABDA ndio maana HATA utishie UKIMWI ,ngono hatuachi NG'OOO!:-(

>> Thursday, November 10, 2011

 Funzo kutoka kwenye TAHADHARI  za hatari  za UVUTAJI SIGARA ziwekwazo kwenye PAKETI  za SIGARA , sigara yenyewe au hata kwenye MATANGAZO ya SIGARA zaonyesha kuwa ,...

......WATAKAO KUVUTA SIGARA asilimia za kutosha TU,...
... watavuta tu SIGARA hata kama wanajua na WAMETAHADHARIWA kuwa uvutaji wao SIGARA utawapatia SARATANI ya MAPAFU.:-(

Swali:
  • Kwani unafikiri WAVUTA BANGI wangapi huacha kuvuta bangi kwa tahadhari wapewazo kuwa BANGI huleta KICHAA?
  • SI walevi wanajua POMBE si CHAI?
  • Na kwani unafikiri swala la NGONO PUMBAVU  kuwa chanzo cha uenezaji UKIMWI latisha wahusudu NGONO asilimia ngapi ambao wanafanya kazi katika N.G.O . za ``TISHATISHA UKIMWI UNAUA´´ ambao kazi yao  ni kinyume na NGONO pumbavu waendekezazo wakati wako katika ZIARA za kikazi ya KUELIMISHA watu watishike na UKIMWI?

Ndio,...
.... na labda  TISHATISHA inamipaka yake KIMAFANIKIO,...
... kwa kuwa kwanza WATU TWATISHIKA kwa vitu tofauti kitu kifanyacho  hata UCHOCHORO ukutishao  ule wenye GIZA kwa mwingine ndio mahali pazuri pakujibanza BILA WASIWASI kiofisi ya kazi maalumu kwake ya UPORAJI waogopao HUO uchochoro.:-(

Swali:
  • AU?


Ndio,...
... TISHATISHA  ina MIPAKA katika KUTISHIA kitu mtu,...
... kwa kuwa labda pia kwa baadhi kilengwacho kutumika kama TISHIO ilikusitishwa ,...
... hichohicho ndicho kifanyacho MAISHA ya MLENGWA kuleta MAANA.:-(

Swali zaidi:
  • Na si  wakati  mmoja anatishia mtu atakufa labda  kuna ambaye  ALENGWAYE NA KUTISHIWA KIFO ambaye kufa ndio kitu kiletacho maana KWAKE na ni poa kwa kuwa NAAMINI  ndio staili ya kwenda mbinguni kiaina?


Ndio,...
.... ukikosea WAKULENGA  na ulengacho kama TISHIO ,...
....... KITISHO CHAKO chaweza kuwa ni KICHEKESHO kwa kuwa UTISHACHO NACHO  kwake hukitambua kama Ze COMEDY.:-(

 NI wazo tu hili MHESHIMIWA!

Hebu DJ JESUS aanzishe kwa-Homem Casado



Tuga Agressiva na Titica waongezee dozi ya pambio kwa - MOTO



Halafu Gata Agressiva wazime kwa - Fula Mupepi

1 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Yasinta Ngonyani 1:23 pm  

mmmhhh!!

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP