Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Twanga Pepeta Wakamata Pipa

>> Friday, November 25, 2011

Bendi ya Twanga Pepeta wakijiandaa kuingia kwenye Pipa

Chalz baba akiwa tayari kuingia kwenye Pipa

Full Mzuka

kikosi cha Twanga kikijiaandaa kuingia Katika Uwanja wa Julius Nyerere

Kutoka Kulia Amigolous akiwapa Mikoba Jojoo, Jumanne, Baby Tall na Luiza

kutoka kushoto Shalapova, Charles Baba na Shakashia

Maria Soloma akiwaaga mashabiki wake Nyumbani

Victor Mkambi mpiga kinanda wa Twanga akiwa na Maria Soloma ambae ni dancer wa twanga




Salam,

Twanga Pepeta ''KISIMA CHA BURUDANI''  wameondoka leo asubuhi kutoka uwanja wa kimataifa wa Julius Nyerere kuelekea  kuvinjari katika Jiji la London ili kusugua kisigino na wapenzi wao walioko nchini Uingereza na nchi jirani ikiwa ni katika kusherehekea maadhimisho ya Miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania.  Kundi hilo lililokamilika katika safu zake za waimbaji, wapiga vyombo na wacheza show linatarajiwa kuwasha moto wa burudani yao siku ya Jumamosi, tarehe 26 Novemba 2011 katika Ukumbi wa Club 2000 Savoir Banqueting Suite, Popin Building Southway, Wembley HA9 0HB kuanzia saa Tatu Kamili Usiku mpaka alfajiri (9pm  til late).
Mheshimiwa Balozi Peter Kalaghe atakuwa mgeni rasmi. CD za album mpya na za zamani zitauzwa na vinywaji pamoja na vyakula vya kitanzania vitakuwepo vya kumwaga. Viingilio vitakuwa £20 (singles)  na £35 (couples) kabla ya saa sita (mid night) na £25 (singles) na £40 (couples) baada ya saa sita usiku.

Njoo tujumuike, njoo usugue kisigino, njoo usherehekee uhuru wa nchi yako, njoo ule na kunywa kitanzania. Burudani ni watu na watu ni pamoja na wewe. Tanzania itajengwa na watu wenye moyo kama wewe. Karibuni sana.

Shughuli hii imeandaliwa na Urban Pulse Creative wakishirikiana na Miss Jestina Blog, chini ya maelekezo thabiti ya Ubalozi wa Tanzania, London. 
Tumethubutu, Tumeweza na Tunaendelea Mbele


Nimetumiwa na :
Frank Eyembe

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP