Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

CHANZO cha wazo lilelile BAYA ikiwa ni RAIS NYERERE na sio MCHUNGAJI MTIKILA,....

>> Friday, February 24, 2012

....LABDA kuna watakao LIHESHIMU  ,...
.... kwa kuwa TU wanaheshimu na wana IMANI  na CHANZO cha WAZO!

Swali:
  • Si unajua CHANZO cha WAZO kina nguvu zake pia kwa wafuatiliao WAZO hata hasa katika kuaminisha watu kirahisi hata UJINGA?
  • Kwa wakristo si CHANZO kikiitwa ni BIBLIA kama kwa WAISLAMU wakisikia chanzo ni KORANI si kirahisi wanaweza amini jambo hata ambalo kitafsiri labda kimekosewa ila CHANZO cha fanya jambo lipewe TU shavu kiaina?

Ndio,...
.... labda hata MIMI na WEWE,...
.... kuna tuaminiyo KIRAHISI kwa kuwa tu tunaamini CHANZO cha WAZO,...
.... ingawa WAZO lenyewe ukweli wenyewe ni POTOFU.:-(

NI wazo tu hili MHESHIMIWA!
Ijumaa NJEMA MKUU!

Hebu KY-MANI  Marley na PRAS warudie- Avenues




Inner Circle wazime kwa -Discipline Child


6 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Yasinta Ngonyani 11:13 am  

Hivi kuna wazo potovu?...najiuliza kwa sauti. Ijumaa njema nawe pia Mtakatifu wa watakatifu:-)

Simon Kitururu 11:29 am  

Kimsingi hakuna wazo potofu. Ila kwa kuwa jamii na watu waejijengea maadili fulani-wazo lifanyalo mtu au jamii ivuke/ipinde kimaadili iliojiwekea huweza kutafsiriwa kama POTOFU.

Na kwa kuwa kuna wapotezwao na WAZO la wengine - basi wazo hilo huweza kuwa ni POTOFU ingawa itabidi na kupotea kwenyewe kunyambulishwe kuwa ndio nini.

Yasinta Ngonyani 11:37 am  

Ahsante kwa ufafanuzi. Kwa hiyo wazo/fikra likisha yambulishwa kila kitu kinaweza kuwa swari tena?

Simon Kitururu 11:39 am  

Si lazima kwa kuwa saa nyingine ukichokonoa kidonda ndio unapokutana na usaha@Yasinta

Yasinta Ngonyani 11:49 am  

Mmmmhh! kwa hiyo ndio inakuwa MWISHO?

sam mbogo 2:35 pm  

Kwa hoja hii,la muhimu ni jinsigani unavyo lipokea wazo hilo, na kulitafsiri katika ulimwengu/jamii unayoishi. siku zote jamii au wnajamii ndiyo wafikishao wazo la mtu fulani katika uwanja wa kuoneka kiupotoshaji au laa!. kwa mfano nikiuliza swali kati yako mtakatifu na yasinta nikitugani kinawavutia nyinyi binafsi kusoma blog zenu? je matokeo yakuzisoma ni kama chanzo kimawazo ?na je kunaupotoshwaji ndaniyake au laa!jeni kwasababu mnafahamiana kama wana blog? na sisi wasomaji wenutunaamini lipi katika hoja hii, wazo ukilisimamia nakuliamini,kwa nguvu zako zote laweza kugeuka bibilia au msahafu kwa walifuatalo. hoja nzuri kwa kutafakali,napia kubadirisha mitazamo yetu ya kuangalia mambo kiju juu. kaka s

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP