Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Kama UNATAKA!

>> Monday, February 20, 2012


Kwa kawaida kama UNATAKA,....
.....yasemekana UTAKACHO huwa unapata KIUTAKACHO,...
.... ila UPATACHO huwa  huja na KUONDOKA kwa  makali ya ULICHONACHO!:-(


Swali:
  • Si unajua ULICHONACHO chaweza kupotea kwa wewe KUPATA kipya ambacho labda wala hata sio MUHIMU kwako kama ulichonacho sasa hivi?

Ndio,....
....UTAKACHO na UKAKIPATA,...
..... kwa hilo la kukipata tu kitu kipya LABDA huondoa BIKIRA ya ambayo ulikuwa nayo manono kwa kufanya uustukie zaidi ubaya wa uliyonayo kuliko MAZURI ambayo kwa kawaida hutunza ULIYONAYO yaliyo MUHIMU sana hata kuliko USIYONAYO sasa HIVI.:-(

Ni wazo tu hili MKUU!


Hebu Junior Reid aanzishe tena kwa- One Blood





Eric B. na Rakim wafanye tena matusi ya - Don't Sweat The Technique




Halafu Dr Dre azime kwa- Let me RIDE




Halafu sijui kwanini ila hebu tu COCOA TEA azime kabisaaa kwa-Hurry up and COME

3 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Yasinta Ngonyani 10:41 am  

kama unataka! na je nikisema nataka inakuwaje? Jumatatu njema nawe pia

Simon Kitururu 12:38 pm  

@Kapulya: Watakao yaeleweka zaidi kivitendo. AU? Juma tatu njema sana Yasinta!

Yasinta Ngonyani 2:04 pm  

nimekupata Simon...Ila nina .....mmmhh naacha

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP