Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Tanzania Bwana! Kila kukicha kuna MKOA MPYA umeanzishwa!

>> Friday, March 09, 2012

Usije kushangaa kwenu sio kwenu KIJINA tena,...
... kwa spidi ya jinsi MIKOA inavyoongezeka TANZANIA!

SWALIZ za kizushi:
  • Hivi wingi wa MIKOA ni dawa ya suluhisho la maendeleo BONGO?
  • Wagawao MIKOA hawahisi labda Tugawe tu na NCHI  tuwe na SERIKALi ya visiwa vya MAFIA , yavisiwa vya ZANZIBAR , Visiwa vya UKEREWE na Serikali ya TANGANYIKA Bara?
  • Unauhakika unaweza kunitajia MIKOA YOTE ya TANZANIA sasa hivi bila KUJIUMAUMA?


    Ndio,...
    .... nahisi kuna WATANZANIA kibao,...
    ...... hawawezitena kunitajia TANZANIA ina mikoa MINGAPI na INAITWAJE.:-(

    Ni wazo tu hili MKUU baada ya kustukia ,...
    ...... MIKOA MINGINE ya Geita, Katavi, Njombe na Simiyu imeongezeka TANZANIA!

    4 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

    Yasinta Ngonyani 12:02 pm  

    Mimi ngoja niwe wa kwanza na nisema ukweli kwamba ni kweli mikoa inazaliwa kila asubuhi na wala siwezi kuitaja yote kama nilivyoweza miaka ileeeeeeeeeee

    sam mbogo 12:35 pm  

    Nafikiri,kunafaida yake,kimaendeleo ukienda mbali zaidi kutaka kujuwa. mimi kwa uhakika nimekuwa mmoja wa waliokumbwa na mabadiriko haya ya kuongeza mikoa. kwanza kabisa nilikuwa mzaliwa katika wilaya iliyo kuwa zamani chini ya mkoa wa Tabora, baada ya serikali kuongeza mikoa nikajikuta tena kwenye mkoa wa Rukwa,mpaka hivi leo kuna mabadiliko te ya wilaya nilio zaliwa ina tenganishwa na kuwa mkoa kamili utakao itwa KATAVI. nikweli unavyosema mtakatifu kama si mfuatiliaji unanaweza kujikuta hujuwi nimkoa upi unatoka. kwamaana hiyo wilaya ya mpanda kuwa mkoa (katavi) kuna faida yake kimaendeleo nimekuwa nafuatilia mchakato mzima,nina uhakika kimaendeleo mkoa huo mpya utasonga mbele sana. namabadiriko yaweza yasiwe natija kwamikoa mingine!. kwa kutaja majina naweza kwa asilimia 90%. kaka s

    o'Wambura Ng'wanambiti! 4:18 pm  

    Hatuwezi kujua nini kitatokea kesho hapa Tanzania...ha ha haiwezekani rais anashauriwa na Mkewe kitandani kesho asubuhi tunasikia jambo...JK Nyerere alipata kusema siku moja na watu wakacheeekaaa!

    Simon Kitururu 4:36 pm  

    @ Wote: DUH! Ila Kaka S asante kwa mnyambulisho wako hasa kutokana na migao hii ilivyokugusa moja kwa moja.

    Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


    Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

    Partner

    save mt. Kenya campaign
    In partnership with africapoint.com

    Taswira BANANGENGE

      © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

    Back to TOP