Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

KATIKA yahusuyo UCHI mzuri!

>> Friday, May 18, 2012

Na kuna YAVALISHWAYO nguo MAISHANI,...
.... ingawa bado yasemekana MAISHANI yale ya KIKWELI ni yale  yaliyoko UCHI,...
.... hata kwa ALIYEVAAA!:-(

Swali:
  • AU?
  • Na  si YALE mazuri hata yakikaa UCHI huwa yana mchezo wa KUPENDEZA?


Ndio,...
... labda ni kweli UCHI mbaya hufichwa na mwenye UCHI,...
.... hata FARAGHANI!:-(


Na ni  wazo tu hili MHESHIMIWA!:-(

Hebu J. Martins aingilie kati tena kwa -OYOYO





Halafu Fally IPUPA aingilie ya J. Martins halafu kwa pamoja wazime kwa -JUPKA

12 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Yasinta Ngonyani 2:09 pm  

Ila kumbuka mficha uchi hazi!!! Simon/Kadoda Duh!

Simon Kitururu 2:11 pm  

Ndio hapooo!:-( @Kadala Yasinta

sam mbogo 4:26 pm  

Kwani uchi ni kiungo? kama ndiyo kwa nini kisisemwe/tamkwa wazi.kama siyo kwanini kinapewa nafasi ya kiungo kimojawapo katika jinsia ya kike na ya kiume.mfano, jamaa kakaa uchi......ina maana sehemu yake iko katika hali ya kuonekana,bila kusahau kuwa kile ukionacho hakiko vile au hakikusudiwa kuachwa vile kionekane au hata wakati mwingine yawezakuwa ni makusudi ya mkaa uchi ili kiungo chake kionekane natuweze kuliita tendohilo ni la kukaa uchi. kwa maana hiyo uchi nisiri utaratibu uliobuniwa na binaadamu kuficha udhaifu wake wa baadhi ya viungo hadharani,au bila kukusudia",uchi ni siri"na ina maana sana katika jamii zetu kimaisha hivyo tujitahidi tusikae uchi tutunze siri tuwe wepesi kusema samahani sikukusudia kukaa uchi. asante mtakatifu nimeipenda fasihi hii ya uchi. kaka s

Simon Kitururu 4:31 pm  

Ndio Hapoo!Pamoja sana na kuna mrengo mpya nimeupata baada ya kukusoma.@Kaka S

Yasinta Ngonyani 4:40 pm  

Simon na Sam Duh! kazi kwelikweli. Hivi kweli uchi ni siri? najiuliza kwa sauti tu...

sam mbogo 5:07 pm  

Yasinta ,uchi ni siri.usiri wake unakuja tu pale unapo jifungia ndani nakuvaa nguo zako na wala hutoki kuzivalia nje. uchi kama kiungo nisiri , hatakama mkijifungia ndani na mpenzi wako usiri wa uchi bado uko palepale ninyinyi wawili ndo mnajuwa kadamnasi zenu zime kaaje,hivyo bado nisiri(uchi) wanawake wanapo jifungua siyo kila mtu ana ruhusiwa kuona tendo hilo,muhusika ni uchi kama kiungo.kimawazo unajuwa uchi upo na ushawahi kuuona lakini una taratibu zake katika kuonekana hadharani.ukiona mtu anaonyesha viungo vyake vya kike/kume hadharani huyo lazima ni punguwani.kwa hiyo naongezea tena uchi nisiri inayo fuata utaratibu kwa mtu/binaadamu aliye kamili.kaka s

ray njau 5:48 pm  

Hapa Simon anawaumiza watu vichwa kupitia kipaji chake cha kuumba lugha ndani ya lugha.
Angalizo hapa ni jamii iendeleze utamaduni wa kuficha mambo na hata kufikia kuficha mambo yasiyostahili kufichwa.

ray njau 5:49 pm  

"JAMII ISIENDELEZE UTAMADUNI WA KUFICHA MAMBO HATA KUFIKIA NGAZI YA KUFICHA MAMBO YASIYOFICHIKA"

Simon Kitururu 10:32 pm  

Kaka yangu RAY NJAU- hapa UMEMALIZA!

ray njau 11:22 am  

@Simon;
Kaka nimeliza kwa kheri au shari?

ray njau 11:23 am  

"NIMEMALIZA KWA KHERI KWA SHARI?"

Simon Kitururu 11:47 am  

Kwa kheri kabisa Mkuu!@Ray Njau

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP