Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Wakati WAMAREKANI WEUPE inaaminika wanajua ULAYA kwenye asili yao,.......

>> Thursday, August 12, 2010

.... HEBU tusikilize BAADHI ya WAMAREKANI  weusi MAARUFU ,...
....ambao INAAMINIKA wanaweza kujua AFRIKA  ni asili yao,....


....ISIKILIZWE WAKATI KISIKILIZWACHO KINAFIKIRIWA  kiaina KATIKA KUJIFUNZA wafikiriavyo KIAINA Afrika.


Kumbuka KUFIKIRIA kabla ya HUKUMU ni nini unachoangalia na KUELEWA!:-(



Tuanze na EDDIE MURPHY akiongelea WANAWAKE wa KIAFRIKA




Tubakie kwenye topiki ili baadhi ya miaka ya baadaye JAMIE FOXX aongelee kiania anavyofikiria  WANAWAKE WA KIAFRIKA


Au tu tumsikilize Eddie GRIFFIN ajaribu kuelezea kitu katika mkao huohuo katika  afikiriavyo WAAFRIKA kinamna  katika -BACK TO AFRICA



Au tu Tribe called QUEST walainishe kwa  kubadili mkuno kwa ndude -Hot SEX on a PLATTER





NI HILO TU   MHESHIMIWA  na linahitaji fikira kama umedeku kitu kabla HUJAFURUMUA mkao wa hitimisho la FIKIR!!:-(

Read more...

MTAZAMO kama SILAHA uwezavyo kumsaidia MALAYA kuvumilia maumivu ya biashara ya KUJIUZA!

>> Wednesday, August 11, 2010

MTAZAMO wa mtu juu ya KITU,....
..... ni bonge la SILAHA,....

..... ndio maana hata kuruka KICHURA CHURA kukitazamwa kwa mtazamo wa kuwa KICHURACHURA NI MAZOEZI  huwa ni MAZOEZI ,....

.... wakati ukirushwa KICHURA CHURA ukiwa na mtazamo ni ADHABU  hicho hicho KICHURA hugeuka kuwa ni ADHABU.:-(




Swali:
  • SI umewahi kuona watu katika mazoezi wanapigishwa PUSHAPU  na wanaitikia wito wa KOCHA WA ZOEZI  kwa FURAHA?


MTAZAMO ni kitu cha ajabu,.....
.... kwa kuwa unaweza kukufanya URIDHIKE hata na UMASIKINI kwa kuwa kwa mtazamom wako hicho ni kitu cha kawaida  kwa kuwa jamii yenyewe yote uishinayo ni MASIKINI na  kuona ombaomba ni KAWAIDA.




MTAZAMO ni kitu cha ajabu,....
.... kwa kuwa kwa MTAZAMO wako kama wewe unajihisi ni MBAYA hata uwe MZURI VIPI unaweza usijiamini KIUZURI kitu kiwezacho kukufanya upende kusifiwa mara kwa mara ni MZURI ili tu angalau ujiamini kuwa labda wewe sio MBAYA SANA kitu ambacho kinaweza kuhasiri hata ni NANI UNAFIKIRI NI MARAFIKI WA KWELI kwako kisa wanakusifia tako kitu ambacho kinafanya udhanie wasio kusifia kalio hao sio MARAFIKI WA KWELI na kwa kidhungu aka LUGHA YA KITAALAMU YA KIBISHOO  ukawaita MA- HATER  kama tu vile kutokusifiwa sio KAWAIDA.:-(


MTAZAMO ni kitu cha ajabu,....
.... unaweza ukakufanya usistukie MUHESHIMIWA ni MALAYA ingawa afanyacho ndicho ukiiitacho UMALAYA kwa kawaida.:-(


SAMAHANI NALIKATIZA WAZO HAPA kabla ya kuongelea kwa kina  ,....
....``MTAZAMO kama SILAHA uwezavyo kumsaidia MALAYA kuvumilia maumivu ya biashara ya KUJIUZA!´´




Swali:
  • Kwani kwa MTAZAMO wako hujanielewa naongelea nini katika kudai MTAZAMO wako unaweza kuwa ndio ukuponzao kusikia maumivu wakati ungegeuza mtazamo CHUNGU ingekuwa TAMU?





Hebu LOPANGO YA BANKA wadinye ndude kubwa KATIKA KUBADILISHA HALI YA HEWA KIJIWENI kwa kitu-MPO NA KONGO




Bisso Na Bisso nao wanyokolishe kwa kitu - Le Reve Africain






AU tu hebu tu BISSO na BISSO wamalizie na ndude-Bisso na BISSO


Read more...

Fafanuzi ya HOJA ya kwanini inasemekana Rais KIKWETE anamuigilizia Rais NYERERE kushindwa , KWA KUTUMIA kielelezo cha SEHEMU za SIRI!:-(

[Tahadhari: Wazo limepinda na linakonakona kimtiririko kwa hiyo shauri yako kama unanisoma halafu huelewi, Miye SIMO!:-(]


Kabla sijakupotezea muda; 
KWA KIFUPI nachokilenga mjeledi  KINUNDU katika TARALILA hii ni kuwa:

´´Rais yeyote yule atakayechaguliwa TANZANIA awe kutoka UPINZANI au CCM hataweza kutimiza malengo ya WAMPIGIAO KURA kwa kuwa MIUNDO ya TAASISI za BONGO na UKIRITIMBA WAKE haufanyi kazi ipasavyo......

Na kiongozi ambaye hataweza kulenga PAMOJA NA YOTE , miundo ya TAASISI ZA SERIKALI na ufanyakazi wa TAASISI kwa kuziboresha au kuzipamburua  ili kuondoa ukiritimba - na ambaye hata lenga kujenga Taasisi MPYA  ambazo zinalenga matatizo ya WATANZANIA na TANZANIA sasa, .....
.....hata weza kuondoa RUSHWA, umasikini, UJINGA, na kwa kifupi ataendelea kurudia yaliyomshinda NYERERE ambayo yanamshinda Rais KIKWETE.´´
- Mwisho wa KINUNDU.



HEBU tuliangalie swala aka KINUNDU  kwa kuangalia jinsi KUTOKA WAZO la kitu mpaka MAFANIKIO YA KITU yahitajivyo ufanisi wa MIUNDO ya TAASISI  kwa  kuangalia dondoo za miundo ya taasisi za SEHEMU ZA SIRI aka uchi  wa MNYAMA    ziwezavyo  KURAHISISHA uelewaji  hasa UKIZINGATIA;....

 ......mfano wa JINSI  mfikiria kupata mtoto awezavyo kufanikiwa kupata mtoto IKIWA TU  miundo mbinu  na miundo ya taasisi HUSIKA zinamuunganiko usababishao KIFIKIRIWACHO kizae mimba.ukikumbuka tu hapa KILENGWACHO KATIKA MFAN ULIOPINDA ni kuangalia jinsi  MKUU wa SERIKALI na WAFIKIRIAJI WENZAKE wahitajivyo miundo mbinu bora  na MIUNDO YA TAASISI  BORA ili WAZO lizae MATUNDA.:-(


Mwanzo wa  mtazamo:

MFIKIRIA kuzaa mtoto ili kiutekelezaji azae mtoto ,....
..... miundo mbinu ya taasisi za sehemu za siri hufanikisha tu anachofikiria- hapa na maanisha kumpa mimba au kupata mimba-   kwa kuwa miundo ya taasisi za sehemu za siri ipo na inafanyakazi bila ukiritimba ,....

  • ....kitu kifanyacho WEWE KAMA MWANAUME kinakuwezeshaKUFANYA UFIKIRIACHO kiamshe hisia , HISIA ZIAMISHIAZO MAJUKUMU katika MIUNDO YA  taasisi ZA CHINI YA KITOVU ambazo zina mfanyakazi mwenye support system aka miundo mbinu na shehena ambayo ingawa kuna ladha kama motisha kusaidia kazi ifanyike na kimiminika kisafirishwe mpaka katika mdomo wa KIFAA cha fani.

  • ....kitu kifanyacho wewe kama MWANAMKE kisaidie unachofikiria na kama muda ni sahihi KITAIMINGI miundo ya TAASISI zako za sehemu sehemu  itumie MIUNDO MBINU  BORA   ya taasisi za sehemu zako za siri  ILI ziwezeshe  malighafi YAI iliyotengenezwa katika moja ya TAASISI MWILINI  ifikishwe kwenye uchochoro  WA MAKUTANIO ya yai na mbegu hasa kama  miundo mbinu ya upelekwaji wa YAI lisilodariziwa na  LILILODARIZIWA TAYARI mahali maalumu yote ikiwa ni katika kuwezesha mchezo wa baba na mama uzae matunda.

..... kitu KITUKUMBUSHACHO PIA umuhimu wa mahusiano ya watu- IKIWA KATIKA MFANO ni mwanamme na mwanamke wajuao mchezo  - ingawa KISEREKALI ni WAFANYAKAZI BORA WAJUAO KAZI  hata kama kuna TAASISI BORA  KIMIUNDO ili matunda yatokee.

KWA KIFUPI,....
....inahitaji ushirikiano wa MWANAMKE na MWANAUME  hata kama TAASISI ZAO ZA SEHEMU ZA UZAZI ziko bomba ili kusababisha matunda ya dunia kujazwa yafanikiwe kama tu ihitajikavyo TAASISI bomba ki miundo kitu ambacho TANZANIA HATUNA  ili kufanikisha MAWAZO YA RAISI  kufikia utekelezwaji murua  hasa ukikumbuka umuhimu wa TAASISI HIZO ZENYE MIUNDO MZUKA ihitajivyo wafanyakazi BOMBA..:-(



SAMAHANI ngojea nilainishe lugha:


Sasaaa....






Tanzania kwa MIAKA NENDA RUDI imesifiwa hasa na WATANZANIA WENYEWE kuwa ni nchi ya amani. Cha kushangaza ni kwamba pamoja na amani yake maendeleo yake yanautapiamlo kiasi kwamba utakuta NCHI ZISEMEKANAZO kukosa amani huwa wala hazitishwi kimaendeleo na TANZANIA ambayo hata kwenye MPIRA wa miguu wenye washabiki wenye munkari au kwenye POMBE ambako kuna washabiki wenye motisha tumeshindwa kuwakilisha katika dunia kwenye fani.:-(

Na wakati huu wa uchaguzi TANZANIA ni rahisi kushabikia KIONGOZI MGOMBEA mmoja au MWINGINE bila kujiuliza ni kwanini viongozi lukuki waliotangulia kuanzia Rais NYERERE mpaka Rais KIKWETE ,....
.....siye na amani zetu bado hatuchezi mbali na UMASIKINI, ujinga, CHUPI ZA MTUMBA ,.. ...nk

Na tunajua kuwa WATANZANIA wanaweza wakiamua hasa ukifuatilia jinsi tuwezavyo kufanikisha KICHENI PATI , harusi za ajabu, kushangilia timu za mpira wa ULAYA, mazoezi ya kupata na kumpa mtu mimba, kupata kilaji ,nk

SWALI:
  • Umenielewa nalenga nini?
  • Umesikiliza ni hoja gani za MGOMBEA ambazo zinatekelezeka na umefikiria ni kwanini KILIMO kwanza haimfanyi BISHOO ajisikie kushika jembe KIUTEKELEZAJI?

Ndio,....
...... labda TATIZO SIO NANI NI RAIS Tanzania kwa kuwa LABDA hata UMRUDISHE Moringe SOKOINE hakuna atakachofanya kama MIUNDO ya TAASISI zenyewe ambazo ni muhimu katika utekelezaji WA LILILOKUWA WAZO mambo yake  ni kama tako la Mzee aliyejisaidia kaba ya kuchambwa.:-(

Ndio,...
....na LABDA hata kukiwa na TAASISI zenye MIUNDO bora, kama hazina WAFANYAKAZI wajuao kazi na wenye munkari wa kazi ni BURE kama tu Mbwa jike ALIYE KWENYE SIKU ZAKE mwenye taasisi zenye miundo bora ifanyayo kazi sawasawa lakini hajuikumgawia mbwa dume KISHUGHULI au tu Mbwa dume hapatii MSHUGHULIKO wawezavyo kusababisha TAASISI KUTOTIMIZA lengwa ya duninani kujae zaidi MBWA.:-(

Swali:
  • SI unakumbuka ni KWANINI Waziri MREMA alifanikiwa kusababisha UJAMBAZI upungue kwa kustukia TAASISI katika miundo unahitaji vituo vya polisi vidogo karibu zaidi na WANANCHI?

NIMEACHA!

USITISHIKE MHESHIMIWA hili ni wazo tu    NA SAMAHANI kiduchu  KWA KURAHISISHA hoja ngumu na NZITO kwa kuiingilia kimtindo wa taralila za UJINGAbusara   MKUU !:-(


Hebu Don Carlos arudie mkuno-Time


Au tu DON Carlos arudie ndude-Just a passing glance





Hebu nimuachie tu Tenor Saw enzi za 1985 arudie-Ring the Alarm na pia Fever




Au tu turudi Senegal DAARA J wadunge tena kitu- ALLAH

Read more...

ASILIMIA ya UKWELI kwa kitu mtu afikiriacho ni KWELI;......

... mara nyingi KINAWEZA KUELEZEWA kwa kutumia mfano WA JINSI  mtu afikiriavyo NI KWELI  hana hajakubwa wakati anatembea kwa maringo ,.....
..... kwa kuwa tu ETI hajabanwa hajakubwa.:-(

Swali:
  • SI unakumbuka labda kwa MTU labda mavi yapo hata kama ni kweli HAJABANWA choo?
  • Uongo si ni kweli ni UONGO kwa hiyo UONGO labda ni UKWELI?

Ukweli ,....
......labda ni UKWELI pale tu kabla hujastukia uongo wake na ndio MAANA MPAKA  hata imani ziko nyingi na zote ni za kweli kwa aaminiye kwa kuwa  kwa KUAMINI  KITU labda ni kukiri KWA MTU  kuwa bado hajastukia DANGANYATOTO kitu.:-(



Na  labda UONGO ni KWELI,....
..... kama ni kweli ni UONGO.:-(

NI WAZO TU HILI MKUU na RUKSA kulitemea koozi kama halipandi mukichwa!:-(

Hebu turudi HAITI  tena  ili Sweet Micky arudie ndude -Ou lala


Au tu tubaki tu hapahapa Haiti Michel Martelly aka Sweet Micky adunge na ndude -Cocorico



Na labda  tupitie tu tena Congo Tabu LEY alete ya kishtobe - Jolie Elie

Read more...

IJUMAA NJEMA wajameni!

>> Friday, August 06, 2010

Swali:

  • Unafikiri kuna UKWELI ukilitakia  LIJITU heri ni kweli LIJITU litapata heri?

NDIO,....
..... labda kumtakia mtu HERI  hakuna kibadilikacho zaidi ya kumuandaa MTU  kustukia ya HERI ZAIDI ya ya KIBANO.:-(

NI WAZO TU HILI MKUU!

AU tubadili tu haliya hewa kwa kudeku hii ngoma-Can animals think like humans?





SHOULD U let your man cheat?

Read more...

Labda USIMTISHE MTOTO wako!

>> Thursday, August 05, 2010


Kuna kitu WATU wengi hawajui kuhusu MIE Simon KITURURU,...
... ila ukweli ni kwamba mkono wangu wa kulia haufanyi kazi vizuri kama inavyotakiwa ,...
... kwa KIFUPI hata UKIWA  sio mbali sana siwezi nikakurushia jiwe  kama nataka kukubwenga JIWE kirahisi na MKONO WA KULIA.


Na tatizo lilianza kisa nilikuwa naficha siri eti kwa kumuogopa BABA.:-(

STORI fupi laini na YA KWELI :

Tulikuwa tunaishi SONGEA na moja ya vitu MDINGI alikuwa hapendi ikiwa pamoja na KUWA MCHAFU , kufeli mtihani enzi hizo nikisoma SHULE ya MSINGI MFARANYAKI (kitu ambacho nilikuwa sifeli) ,....
..... nilikatazwa kupanda juu ya MITI aka kuparamia miti kimichezo.

Siku moja mie na marafiki zangu tukaenda  kuiba maembe  aka KUTUNGUA MAEMBE yasiyo yetu shambani  kwa  WANAFUNZI WA SONGEA GIRLS. Enzi hizo shamba la songea GIRLS lilikuwa kubwa  na sisi tulikuwa tunaingilia upande wa UWANJA WA MEDICAL  karibu na nyumba za mwisho mwisho za walimu enzi hizo za miaka ya NAINTINI EITEZ( (Kumbuka ni miaka mingi sijafika Ruvuma sijui maeneo hayo yakoje siku hizi)


Basi BWANA katika kuwinda maembe bolibo na embe sindano  tukaupata mti ambao mbivu zilikuwa zimenona juu kabisa. Na mie ambaye hukatazwa kupanda miti nilikuwa kiongozi kuparamia juu kabisa kutikisa mti.

Kilichotokea ni kwamba,...
.... katika kutikisa tawi ili kudondosha maembe  tawi likakatika na kilichofuata nilijikuta chini nikijiuliza niko HAI au NIMEKUFA,.....

.....na chaajabu hata marafiki zangu wakinisemesha nilikuwa siamini kama niko hai kwa KUWASIKIA kwa kuwa nilikuwa nahisi kuwa labda hata MFU akisemeshwa huwa anasikia.:-)


Katika kufupisha stori hii ya kweli;...
 ....nilivyoanguka nilitegua mkono wa kulia na baadaye nikaja stukia labda na kitu kingine mkononi kiliharibika.:-(

KIKUBWA:
Kwa kuwa kwanza nilikatazwa kupanda miti na PILI miye na marafiki zangu tulikuwa tunaiba maembe ya wana SONGEA GIRLS nilifikiri sio busara kusimulia hicho kitu nyumbani. NILIFICHA maumivu na ugonjwa  kisa NAMUOGOPA BABA....
.....na kwa bahati nzuri ilikuwa ni kipindi cha baridi SONGEA na maswala ya SWETA na JACKETI pamoja na MAIGIZO kuwa NIKO BOMBA  yaliniwezesha kuficha nimeumia mpaka mkono ukapona kinamna.

TATIZO ni kwamba mkono ulivyopona mpaka leo hauwezi  kumlenga MBAJUWAYU  bila msaada wa mkono wa kushoto.


Kwa kifupi :
Nilijitia udhaifu wa mwili KWA KUFICHA UGONJWA kisa NAOGOPA KUCHAPWA. na BABA:-(
Unajua tena AKILI ZA KITOTO!:-(

NI moja tu ya stori ndogo ya KUJARIBU kukufanya MHESHIMIWA ufikirie kabla hujamfanya mwanao AKUOGOPE mpaka ashindwe kukutaarifu hana pesa za kutoa mimba kwa hiyo atajikorokochoa mwenyewe kisiri bafuni.:-(


Na ni HILO TU MKUU!

Hebu OCHESTRA MAKASSY wadunge ndude-MKE WANGU


Hebu NDALA KASHEBA arudishe ndude-MARASHI YA PEMBA




AU hebu tu DDC OCHESTRA Mlimani PARK wakite kwa -MTOTO AKILILIA WEMBE

Baadhi ya PICHA zaidi...

Photobucket




Photobucket




Photobucket




Photobucket



Photobucket




Photobucket




Photobucket





Photobucket




Photobucket




Photobucket





Photobucket




Photobucket



Photobucket




Photobucket



Photobucket



Photobucket




Photobucket




Photobucket





Photobucket





Photobucket




Photobucket




Photobucket



Photobucket




Photobucket




Photobucket



Photobucket




Photobucket

Read more...

MAISHA ya MBU ni magumu kama MBU BADO anaishi!

Na mbu JIKE ndiye aumaye watu kisa anatafuta VIRUTUBISHO vya wanawe.

Na jitihada za MBU JIKE aitwaye na wazungumzao ung'eng'e{  Anopheles}  za kutafuta PROTINI kwa kuwa ni mjamzito ndizo zimfanyazo apigwe vita na BINADAMU kwa kuambukiza watu MALARIA,....


Swali:

  • Unafikiri ni wangapi wanawahurumia MBU  NA KUACHA KUWA BWENGA kwa kuwa WANAJUA ni kweli MBU JIKE ambao ndio wanyonyao damu za watu WANANYONYA  tu katika kutaka angalau watoto wao wapate virutubisho vilivyopo kwa watu damu?
  • Si unajua nia ya MBU sio kuambukiza mtu MALARIA?
  • Unafikiri ni mangapi ukiruka mimba kuna mtu angepigwa BONGE LA MBATA kama kitendo  kingejulikana pamoja na tamu ni kile kimuambukizacho BINADAMU MWINGINE bonge la gonjwa kuliko malaria?

Ndio,...
.... labda MAISHA hata ya BINADAMU ni  lazima yawe magumu tu kama huyo BINADAMU anaishi.



Swali:
  • SI Binadamu tuna mchezo wa kuamini MAREHEMU ni mtu mzuri kwa hiyo akifanikisha umarehemu  kapumzika kama hakuwa mzinzi , mdokoa mboga au tu zile zambi mhusika adhaniazo ni bonge za dhambi zenye tako kubwa?

NAACHA wazo MKUU, na ni wazo tu hili BINGWA wala sio BIBLIA  !:-(


Hebu Mbaraka Mwishehe aulize - MATUSI YA NINI?



Kwa kubaraguza ngojea tudeku baadhi za MOVIE nilizo zirudia kwenye maktaba yangu ndogo ya nyumbani  kama:----
Samuel L Jackson katika diner  ndani ya movie - Pulp FIction



Samuel L Jackson katika Pulp Fiction - Ezekiel 25:17 ndani ya kazi ya Quentin Tarantino


Goodfellas JOE Pesci arudie kitu katika kazi ya Martin Scorsese




Nipo lakini...:-(



Photobucket



Photobucket




Photobucket




Photobucket

Read more...

NI kweli MBWA anajua kumnusa demu wa KIMBWA na kustukia demu huyo anafaa KUPANDWA ,....

... kuliko BINADAMU astukiavyo hata BINADAMU mwenzio mwenye kikohozi anaweza wakati wowowte KUBANJA.:-(


Swali:
  • AU?





Katika kunusa ,....
.... tunajua NGURUWE na MBWA wana pua kali kuliko BINADAMU.:-(


Ndio,...
... kuhusu kusikia ,...
... tunajua hata TEMBO na PWEZA wanasikia  kuliko awezavyo kusikia BINADAMU.:-(


Na sikubishii MHESHIMIWA ambaye unaweza kustukia mbwa kajamba kwakuwa unanusa,....

.....HASA KAMA  wakati unamuona BINADAMU ni kiboko kwa kuwa wewe ni BINADAMU unashindwa kustukia KUNGUNI na chawa wana janja zao hata katika kujificha katika MAVUZI ya MHESHIMIWA MCHAFU HATA SIO SANA ambaye ni binadamu.:-(

Swali:

  • UNauhakika BINADAMU ni mjanja KULIKO MINYOO kwa kuwa  kuna BINADAMU mwenye BENZI halafu aligundua tumizi la chupi?

  • Unauhakika MENDE wajuao JIKO lako MREMBO ni chafu hawana busara za utafutaji maisha kuliko WATANI zangu WACHAGA pale MOSHI stendi?

LAKINI BINADAMU huyohuyo ukimsikiliza ,...
.... kwa kudai yeye ni mtu apendaye amani kwa JINA hata la yesu anaweza kukubwenga kisawasawa ili uelewe AMANI ni nini hutu akimtukania mama yako.:-(

NI wazo tu hili MHESHIMIWA lililokaa KI-MAMA KISEBENGO!:-(
Usitishike BISHOOO MHESHIMIWA ni wazo tu hili!:-(




Hebu Tabou Combo adinye kitu - Pi Gro Pi Long





Au tu Jean Philippe Marthely adunge ndude - Bèl kréati




Au tu Patrick Saint Eloi akung'ute mkito -Chiré




Na labda tu  Jean Claude NAIMRO amalizie KWA ngoma - Ave'w Doudou








AU niache tu baadhi ya picha za juzi ya jana....:-(


Photobucket





Photobucket




Photobucket








Photobucket



Photobucket






Photobucket





Photobucket




Photobucket




Photobucket




Photobucket

Read more...

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP