Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Salamu Kutoka Tallin!

>> Wednesday, February 28, 2007


Kuna washikaji wamestukia kuwa nimepotea na hawanipati katika baadhi ya namba za simu.
Tatizo ni hii mitaa ya Tallin, Estonia, isababishayo hilo.Tutakuwa pamoja hivi karibuni.

Kama mitaa hii ya huku Tallin huifahamu, naweza kusema huu ni miongoni mwa miji ambayo inabadilika haraka sana ,kutoka katika hali ya umashariki ya Ulaya kuwa magharibi ya Ulaya. Na uhakika baada ya miaka si mingi, bei za vitu hapa zitakuwa sawa tu na miji mingine ya Ulaya magharibi.

Ila hapa bado hakuna watu weusi wengi. Ni kawaida tu mara nyingine kupitisha siku bila kumuona mtu mweusi. Ila kuna kitu kingine kinifanyacho ni waheshimu hawa watu. Hawa wa Estonia na Wafini , wanahistoria yakutawaliwa kwa miaka mamia na wenzao.Nawapa heshima kwa kutosahau wao ni akina nani. Mpaka leo Waestonia wanaongea kiestonia. Kwa Wafini mpaka leo wanaongea Kifini ingawa Waswedi walishawahi kuwabadilisha wote mpaka majina yao .
Sasa hapa Tallin , kinachotokea ni kwamba kuna mvutano kati ya Waestonia wenye asili ya Kirusi na Waestonia kamili. Ukiniuliza nitakwambia Waestonia halisi hawawapendi Waestonia wenye asili ya Urusi. Sasa inapotokea mtu kama mimi ambaye sina uhusiano na wote , huwa unaweza ukajikuta unavutwa pandezote mbili. Warusi wanataka uwaonepoa na Waestonia kamili wanataka uone kuwa wao ndio poa. Halafu hapo wakati bado uko katikati yao akijitokeza Mfini, mara nyingi anapenda uone yeye ni bora kuliko Warusi na Waestonia.


Lakini kabla sijaendelea nimemkumbuka Peter Tosh asemavyo...

Hii mivutano ya binadamu huwa inanifikirisha sana !
Lakini kwa bahati nzuri hapa kuna Hoteli ya Kiafrika. Ugali utapatikana karibuni kwa jina la Fufu.
Ngojea nikuache na baadhi ya picha kutoka Tallin...
Photobucket - Video and Image Hosting
Hapa nafikiri unaweza kuona huu mji uko katika ukarabati.

Photobucket - Video and Image Hosting
Usistuke, wanahudumia watu weusi vizuri tu.

Photobucket - Video and Image Hosting
Samahani, hapa hawana bado makande!

Photobucket - Video and Image Hosting

Kwa wazoefu, huyu ni Mrashia au Muestoni?


Photobucket - Video and Image Hosting

Huyu jamaa anapendwa hapa , kwasababu wasichana wanamfananisha na David Beckham.

Photobucket - Video and Image Hosting

Photobucket - Video and Image Hosting

Sasa tuendeleze basi libeneke!


Watu mliokuwa FEST Afrika, kwa mfano KIBUNANGO, tuwekeeni picha la FeST.Unajuatena nimelimisi.
Haya tuendeleze, lakini du...Ali Farka Toure, unamkumbuka?

Read more...

Ashki Ya Michango!Lakini Ushachangia Nanihii?

Swali:
Hivi Tanzania tunaweza kurudia michango tuihitajio au waihitajio kikweli?



Sisi binadamu tunamapungufu yetu! Ni vigumu kila siku kuweza kufanya yote tutakayokufanya kwa nguvu zetu wenyewe. Tunahitaji misaada mara kwa mara. Tuna matatizo mengi.Na kwa bahati mbaya matatizo haya hayawezi kuisha.

Lakini.....
Naamini mara nyingine sisi wenyewe hutengeneza baadhi ya matatizo. Kwa bahati mbaya au nzuri, kitu kingine kitufanyacho sisi kuwa binadamu ni jinsi tunavyoweza kujijengea mazoea ya vitabia vyetu. Moja ya tabia ambayo ni rahisi kuzoeleka ni ile ya michango.

SISEMI KUWA MICHANGO NI KITU KIBAYA!

NAKUBALI KUNAMICHANGO NI MUHIMU KWETU KUCHANGIA.

Lakini.......

Je, hii michango tuipayo kipaumbele na yenyewe inatupakipaumbele ?

Je, hii michango inasaidia kuendeleza au inabomoa?

Je, hii michango inasaidia tuchangiapo?

Katika baadhi ya vitu binadamu afanyavyo , vimejijenga ndani ya binadamu kwa muda mrefu. Kama unamkumbuka Maslow na kile kielelezo chake cha ngazi za matakwa ya jamii na binadamu.......





......utaona kuwa, tunanasa katika ngazi nyingi tu.






Ukiniuliza kwanini tunachanga sana hata pale ambapo hatuna ujanja tunajihisi ni lazima tutoe michango, kwa kutumia Jicho la mitazamo ya Maslow,
.....nitasema kwasababu
:

  • Kupata amani(ngazi ya pili, kwenye jeduali):tunafarijika kuwa iposiku tutasaidiwa pia na watu tuwachangiao.Iwe ni familia, wafanyakazi wenzetu, nk
  • Kukubalika/kupendwa(ngazi ya tatu):kwa kawaida usipokuwa mchangiaji hukawii kuitwa bahiri na sio mtu safi
  • Staha(ngazi ya nne hapo juu kwenye jeduali): kuheshimika, inatusaidia kuwa na uhakika, na tunajisikia hali ya kufanikiwa.
  • Tunajisikia tunafanikisha maswala, tunajisikia kunakitu ambacho tunafanya .
Kwa hiyo utakuta kuwa katika kila ngazi inaweza ikawa ni mimi au wewe umenasa.Katika kila ngazi kuna kamsukumo kamsutako mtu asipo changa.

Tukiachana na Maslow na mitazamo yake , mimi naweza kusema kuwa hii hali ya michango haiko katika binadamu tu bali hata katika wanyama karibu wote wa kinyaninyani.

Kama wewe ni mfuatiliaji wa tabia za wanyama kama Chimpanzee, na hata bonobo utakuta wanakamtindokao kakushughulikia maswala ya michango. Chimps katika mengi wafanyayo , hukumbuka nani alimfadhili mwingine.Chimps aliyekuwa anamkuna mwenzie na kumtoa vidudu , huwa ni rahisi kwake kupewa chakula na aliyemkuna iwapo atakosa chakula. Bonobo wao imefikia mpaka mwanamke ndio ananguvu katika kundi kutokana na kutengeneza uhusiano kwa kupeana michango. Ndio nakubali hawatoi pesa, lakini unafikiri michango ya pesa inanunulia nini?

Ngoja niwakumbushe tofauti za hawa wanyama wawili niwazungumziao.

Huyu ndio Chimp










Huyu ndio Bonobo.

Yeye huwa mwembamba kuliko Chimp wa juu. Halafu anamidomo ya denda.





Kwanini nimewakukumbusha hawa wanyama?

Duh!
Tuache tu!

Lakini usijisikie mpweke! Si wewe wala mimi pekee katika kamchezo haka ka-maisha tunajikuta tumebanwa kona fulani, hata manyani pia.

SASA lakini.....

Kumbuka michango mingine ukweli wake ni kwamba haukusaidii wala kumsaidia yeyote yule!
Halafu kwa kuzidi kuiendekeza unajiumiza tu!

Naamini msemakweli na afanyaye kutoka moyoni ,hustukiwa tu na jamii!Sasa kama kale kamchango ka-filigisi za sikukuu ya...... hukawezi , achananako.
Ukikaendekeza kanakuumiza tu !

Halafu kumbuka haka kamchezo ka-maisha kana mambo yake mengine.Ukijiumiza kwa kufanya mambo usiyoyaweza ipo siku utaonekana mbaya na umeumia zaidi. Halafu ukionekana mbaya au umeumia zaidi , watu wanakamchezo kakukukwepa. Wataobaki ni wale tu rafiki zako wa kweli ambao,wangekuelewa hata usingechangia.

Tuchange tu tuwezapo, lakini tuangalie tusiibe tu jamani kwa kujaribu kutunza sura!

Hivi michango na minyoo vinauhusiano?

Halafu kwanini ghafla tu, michango imekuwa ndio lifestyle Tanzania?

Mimi sielewi kama nisivyoelewa hapa chini ,Franco akiwa na TP Ok anasemanini.....


Read more...

Ukiniuliza kuhusu Tanzania vitani!

>> Tuesday, February 27, 2007

Ukimsoma H.G Wells katika kitabu chake cha The war of the worlds, unaweza kufikiria kuwa ni mpaka vibwengo kutoka sayari nyingine waingiapo duniani ndio vita kabambe inaweza kutokea. Ukifuatilia jinsi vita mbalimbali, sehemu mbalimbali duniani vilivyoweza kutokea hata zile sehemu watu walipoonekana kuwa wanaishi kwa amani,Tanzania chini ya uongozi mzuri tunaweza kuanza kupigana vita wenyewe kwa wenyewe. Ukifuatilia Bosnia miaka ya tisini, Ujerumani miaka ya thelathini, bila kuwasahau Watusi na Wahutu , hapo jirani, lolote laweza kutokea Tanzania.

Kinachohitajika ilikufanikisha vita Tanzania ni uongozi bora.
Au ulitaka niseme uongozi mbaya?
..lakini tuendelee na sababu zinazoweza kuondoa amani....
Kusahau ladha ya utamu wa amani .Uchumi kuendelea kudidimia wakati viongozi kuendelea kunawili.
Duh!
Dini nazo zikiendelea kutuaminisha maswala na kutusahaulisha kutumia akili.Akili nazo zikiendelea kukosa chakula kiiakikishiayo makali yasaidiayo kutatua matatizo yatukabiliayo, na hata pia kushindwa kututuliza katika dakika ambazo maamuzi lazima yatolewe.

Tanzania pamoja na yote ni jamii iliyogawanyika ingawa mara nyingi tunapenda kubisha. Ni rahisi sana kugundua kuwa:

  • Ukabila tunao
  • Udini tunao
  • Umasikini tunao
  • Uongozi bora ambao unaendelea kutufanya masikini tunao
  • Mfumo wa kisiasa ambao haujatengemaa tunao
  • Ujinga tunao
  • na nakadhalika tunayo.
Vita nyingi duniani zilisababishwa na zinasababishwa na maswala niliyoyataja hapo juu.

Lakini vilevile naamini tunamatumaini. Hakuna haja ya kukata tamaa.

AU UNASEMAJE?

Read more...

Internet


Je, internet imeshakuwa ugonjwa kwako?
Jipime hapa

Read more...

Hivi Ushawahi kufanya matusi?

>> Sunday, February 25, 2007


Kuhusu swala hili la kuhonga, mimi nakiri nishaonga sana.Si unajua yale maswala yakutaka kuwa mstari wa mbele!Au yale yakutaka mambo yawe rahisi zaidi kidogo!
Nilimsoma Ndesanjoaliposema tuanzie nyumbani katika kusawazisha mambo. Mimi naacha hii mambo.Mimi nimeaanza muda mrefu lakini hii kitu napenda nitangaze ,ni kona yingine naanza. Lakini kabla ya yote, nakiri katika hii rushwa na mimi nilishiriki kuisaidia kinamna. Wewe Je?
Tuache haya matusi basi!

AU?
Au ulifikiri matusi ni nini?

Tuendeleze wikiendi. Namuacha Barrington Levy akikupa Murderer

Read more...

UKOKO!

>> Friday, February 23, 2007


Ushawahi kuwa shabiki wa ukoko? Utandu je? Bwana eeh!Kuna wakati nilishajenga tabia ya asubuhi kukwepa mikate na vitu vingine na kuhakikisha napata kiporo cha wali na maharage ya nazi ya jana. Hasa yale yasio na rojo sana. Basi hapo nikipata na chai basi siku imeanza.

Lakini ngojea turudi kwenye Pizza. Nisisahau na hambaga. Unajua hivi vyote ni vyakula vya walalahoi vilivyowafanya baadhi ya watu kuwa mamilionea.Sasa bongo tuna vyakula vingapi vya walalahoi hatujavifanyia kazi?.Au tunasubiri tuone mpaka Malkia akivitafuna, kama Pizza ilivyopata umaarufu ndio tuvishabikie?
Usitishike najiuliza tu!
Tuendeleze libeneke.

Namuachia stereoman..

Read more...

Kitchen Party na....

Hivi hii party imepataje umaarufu namna hii?
Siipingi!Usinielewe vibaya.

Kabla sijasema sana:
Swali:
Hivi wanawake wa kibongo wanaridhishwa kimapenzi?

Duh!
Samahani akina dada , badala ya kimapenzi kwenye swali hapo juu, nilikuwa namaanisha ngono.
Wakati ukifikiria msikilize Sade akisema smooth operator....




Naamini binadamu anaruhusiwa kujitafutia sababu za kufurahi. Na nakiri sijui ni nini kinatokea huko.Lakini nasikia kunamafunzo kibao akinadada hupata. Au ndio aina mpya ya kumfunza Mwali kama ilivyokuwa katika unyago?

Huwa sipendi kuandika mambo katika kuegemea katika jambo nisilolijua sana. Ila nachojua kuwa jamii yetu inahitaji sana mafundisho yawezayo kuokoa mahusiano ya watu. Iwe katika ndoa au hata katika urafiki wa kimapenzi.Tatizo kubwa linatokana na misingi iliyobobea hata kwenye mila zetu. Mila zetu mara nyingi zimewafunza wanawake kuridhisha wanaume na pia kuwafunza kukaa kimya pale wasipo ridhishwa.Kuna makabila machache Tanzania ambayo yalikuwa na historia ya kuwafunza wanaume kuwaridhisha wanawake katika ngono.Ni mara chache utasikia staili kama katerero nk. ambazo hubobea kumridhisha mwanamke zikizungumziwa katika mila nyingi.

Kuna hoja zinajengeka kuwa moja ya sababu kubwa ya mwanamume na mwanamke kuwa na nguvu ya kuonja nje ni hii hali yakutoridhika na kitowewo cha nyumbani.Inasemekana kuwa ingawa mahindi ya kuchoma ya mtaani yananukia zaidi na ni matamu watu wengi wangeweza kuvumilia mpaka wafikapo nyumbani kama wanauhakika mahindi ya kuchoma yale ya nyumbani yapo na yanaridhisha kubwa kuliko.

Sasa eeh! Turidhishane basi!

Ila tatizo mbinu za kuridhishana mara nyingi hakuna pakujifunzia. Sasa kama huko kitchen party kunamasomo haya basi akina dada mnawini, ngawa na mashaka kuwa somo la siku moja na la mazingira niyasikiayo ya Kitchen party latosha

SASA eeh!

Nafikiri tunaongelea sana matatizo mengi yatutatizayo Watanzania. Lakini mara nyingi tunaruka hili la mahusiano.
Kumbuka mahusiano mazuri huzaa wazazi wazuri.Husaidia kupunguza magonjwa.Husaidia kupunguza watoto wa mitaani.Husaidia ukuaji wa watoto walio lelewa vizuri. Huzaa watoto wafanyao vizuri katika shughuli zao. Hupunguza matatizo chungumzima.

Sasa kwanini hatufundishani hizi mbinu za kuridhishana?

Mimi nafikiri tunahitaji kukuza uwazi wa maswala haya. Tumeua mila za unyago na jando. Sisemi tuzirudie. Nachotaka kusema nikwamba si yote yaliyokuwemo katika mila hizo yalikuwa yanaumiza jamii. Tuchukue mazuri tuunganishe na yanayohusiana na maisha tuishio sasa hivi. Tuyafundishe yawezayo kusaidia hata ikibidi somo hili liwe kwenye silabasi za shule.

Duh!
Katika kuzungumzia kuridhishana, nimekumbuka swala la matako.
Rafiki yangu mmoja Mzungu kaniambia anapenda matako makubwa kuyaangalia tu. Kasema kinachomshinda ni pale ajaribupo chuma mboga ambayo ndio madoido apendayo akiwa katika shughuli, hawa sangara wanasababisha ajisikie hafiki ufukweni. Sasa mimi nikamsamehe kwa kuwa alikuwa mkweli.Kwa hiyo msiwalaumu sana wapendao dagaa, huwezi kujua siri ni nini.

Duh!
Na hili jina Kitchen Party, mie lanizingua. Au ndoa inauhusiano zaidi na Kitchen kuliko mambo mengine? Kwanini haikuitwa sherehe ya jikoni lakini?

Sasa kwa wale ambao wanaume wao ndio wazima zaidi katika maswala ya Kitchen, wawe na Chumbani Party nini?

Najiuliza tu!
Lakini unajuatena leo ijumaa. Nakuacha na Lagbaja


Wikiendi njema!

Read more...

Ulisherehekea sikukuu ya kuzaliwa Mugabe?

>> Thursday, February 22, 2007


Mugabe alifikisha miaka 83 jana.Halafu inasemekana bado anampango wa kuendelea katika uongozi baada ya mwaka 2008. Hivi ni kweli anaamini hakuna mwingine awezaye kuongoza nchi?

Huyu kiongozi mpiganaji ukifuatilia maswala yake utakuja gundua kwa muda mrefu ilikuwa vigumu kumbana na kumlaumu. Ukichanganya siasa za kikabila za Washona kama yeye na Wandebele, na pia siasa za Afrika Kusini kwa ujumla, utakuta kuwa mambo hayakuwa rahisi sana kisiasa. Ukija kuwaingiza na wazungu wa Zimbabwe na Waingereza basi unaweza kuona jinsi gani hali ilivyokuwa ngumu kutatua baadhi ya mambo.Lakini sasa hivi naona alishapitiza na sidhani ni msaada tena kwa watu wake.

Mimi nafikiri wakati umefika wa hawa viongozi kuwa na mikakati ya kuondokea ofisini tokea mwanzo waingiapo katika ofisi. Naamini wengi wakishaingia wanakuwa hawajui jinsi ya kutoka. Wengine wanakuwa washaiba wanajua wakitoka wanaweza kufungwa. Wengine ndio hivyo tena , wanastukia kugongana na akina Tony Blair ndio inakuwa imetoka tena, hivyo wanang'ang'ania. Hii ni sawa tu na Wamarekani walivyoingia Iraq bila kuwa na mikakati ya jinsi ya kutoka.

Lakini wajifunze kutoka kwa akina Boris Yeltsin wa russia. Yeye alihakikisha anamweka kijana wake Vladimir Vladimirovich Putin ambaye hatamgusa akimaliza ulaji. Wajifunze kutoka katika uongozi wa CCM. Wao huhakikisha anayefuata hamgusi aliyepita hata kama madhambi yake yanajulikana.

Duh! Lakini inasikitisha.Huyu ni miongoni mwa viongozi ambao kama kwenda shule tu nakuipenda shule inasaidia, yeye katika viongozi wa Afrika si mvivu.Inasemekana hivi sasa bado kuna degree anaisomea.Hizi hapa chini ndio alizonazo kwakuziendea shule na kwa masafa, ukiachana na alizopewa tu na baadhi ya vyuo...
* BA (Educ) Fort Hare;
* BSc(Econ) Fort Hare;
* BSc (Econ) University of London, by distance learning;
* BEd University of London, by distance learning;
* LLB University of London, by distance learning;
* BAdm University of South Africa, by distance learning;
* LL.M University of London, by distance learning; and
* MSc (Econ) University of London, by distance learning.
Kinasikitisha pia kuwa mke wake wakwanza Sally Hayfron, aliyekuwa Mghana, anasahaulika siku hizi kama mwanamama aliyekuwa mpigania haki hata kufungwa jela kwa hilo.

Read more...

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP