Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Nafikiria nini kuhusu Krismasi na Mwaka Mpya!

>> Monday, December 25, 2006


Nafikiri binadamu mara nyingi hutafuta sababu ya kusherehekea.Hii ni kawaida.Tanzania katika mila zetu utakuta sherehe hizi nyingi tu. Kuhusu Krismas kama siku ya kusherehekea kuzaliwa kwa yesu ni tarehe iliyo buniwa tu. Tafiti nyingi zinadai kuwa kwa kufuata kalenda tuitumiayo na mambo mengi yaliotokea kipindi cha kuzaliwa kwa yesu inawezekana kabisa ikawa Aprili ndio kipindi.Hata hivyo hakuna uhakika asilimia mia wa siku hiyo.Na nukuu nyingi hizi zilizoko kwenye biblia ziliandikwa miaka mingi baada ya kufariki kwa yesu.

Kuhusu mwaka mpya ndio hivyo tena ukifuatilia historia ya kalenda na ukajiuliza kwanini watu wengi walikuwa na kalenda tofautitofauti, na bado wana kalenda tofautitofauti utapata jibu.

Kuhusu Santa Klaus au Saint Nicholaus- askofu wa mji wa Myra,Uturuki na kuibiwa na Waitaliano waliomhamishia mji wa Bari na kuingia dili na kanisa ilikukuza utalii kwa kumtangaza. NAfikiri unajua nafikiria nini. Lakini Cocacola Kampani ilimtafutia vazi zuri ilikupendeza akitangaza Coca cola.

Tukiachana na hilo, nadhani asilimia kubwa yetu tunapenda sherehe na tunapenda zawadi.Nafikiri hakuna haja ya kufuatilia sana mambo haya maana utaondoa utamu wa sherehe yako. Heri ya Krismas na Mwaka Mpya, lakini kumbuka siku ya krismas na mwaka mpya zaweza kuwa ni siku yoyote ile uamkapo, na hizi siku tusheherekeazo ni binadamu kama mimi na wewe waliozitunga.

1 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

luihamu 7:40 am  

Kweli umenena.Haya ndo mambo yakuzungumza.

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP