Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Uwezo na Mapenzi ya MUNGU katika kumsaidia MWIZI kuiba, MZINZI kuopoa NGOMA au Mfuata dini KUFARIJIKA leo na ahadi za akishaKUFA.

>> Monday, October 13, 2008

Tusichojua TUMSINGIZIE MUNGU!
AU?

Labda ni mapenzi ya Mungu mimi na wewe hatujui!
Labda ni mapenzi ya Mungu kuwa hakuna asiyeugua!
Labda ni mapenzi ya Mungu wewe na mimi hatuna kile na tuna hiki.

Lakini utamu waulichonacho INGAWA UPO , labda unapatikana zaidi pale ukijua uchungu wakutokuanacho.

Kwa akili za kibinadamu , labda Mbinguni kunavutia kwa sababu tu unaamini au hata kujua kuwa duniani kunatesa au KUNA MAPUNGUFU. Na labda kama unanogewa na ya dunia, unaweza usivumilie UCHUNGU wa mbinguni ambao kwa wengine ni UTAMU.

Inawezekana kabisa kwa upeo wangu na wako wa kibinadamu kwa matumizi ya huu huu ubongo UTAFSIRIO kuwa CHIPSI MAYAI ni tamu, MBINGUNI KUNABOA.

Au......

Labda wanasayansi wanasema kweli kuwa mwili wa binadamu bila kusahau UBONGO wa BIN ADAMU ndio unatafsiri sana jinsi unavyojinoma au kuumia hapa duniani. Kemikali na homoni zinasababisha upende, unogewe au hata utake zaidi kunanihiii, bila kusahau jinsi MISHIPA ya FAHAMU (nerves) iunganishavyo UJUMBE MWILINI, mpaka unaweza kujisau kuwa utamu wa ngono, kutekenywa au hata chakula UKO kwenye UBONGO na sio kwenye sehemu zako za faragha, kwenye kidongoloso au kwenye ULIMI wako uutumiao kulamba nanihii.


Sasaaa......

Tunachojua ni kwamba, MIMI na WEWE tukifa, MWILI pamoja na UBONGO utarudi kuwa UDONGO. Inamaana karibu kila utumiacho , kupapasa , kuonja kuibia, mpaka kikusaidiacho kutafsiri kuwa wewe KIBOKO na mambo yako kwa tafsiri yako ni MSWANO , kitageuka KUWA udongo na labda kitakuwa kinarutubisha tu mazao fulani kama tu MBOLEA ya MAVI YA KUKU.


Lakini.......

Tunachosikia ni kwamba, binadamu ana ROHO .
Tusichojua ni jinsi gani roho inatafsiri UTAMU au UCHUNGU ikiachana na hilo LIMWILI LAKO au LANGU ambalo tunalazimika tulichambe baada ya kwenda HAJA KUBWA.!

Swali:

  • Unafikiri roho ya binadamu inajua utamu wa BIA, Ngono au utamu wa kumpiga mwenzio?
  • Kama wewe ni mwanamume au mwanamke , unajua uhusiano wa kutaka kwako sehemu za siri za wenzio ufanyikavyo UBONGONI na UONGEZEKO wa mjao wa damu katika sehemusehemu zako za faragha?


Lakini tusiyojua anajua MUNGU!


Narudia kinamna.........

Mapenzi ya binadamu matamu na yanaweza kukusaidia kupata GONO.

Kama wewe ni mwanasayansi utadai kuwa unajua kuwa kemikani na homoni zako ndio zinazosababisha uhisi utamu au uchukie kutokana na tukio.

Kama wewe unaamini katika sayansi utadai kuwa ni kemikali na hormoni mwilini na ubongoni ndio visababishavyo uingie ukichaa wa KULIPENDA na KUENDELEA kukaa na LIMTU LAKO ambalo limesababisha uone ni kitu cha kawaida na ni USAFI kugusanisha VIKOJOLEO VYENU ingawa unadai MKOJO ni uchafu na harufu ya mkojo unaichukia kama tu HARUFU ya SAMAKI MAREHEMU mwenye mafinyofinyo.

lakini.....

Utafiti wa mambo ya ubongo unaonyesha kuwa wale binadamu waitwao wanaakili sana au Majiniasi, bado wanatumia sehemu ndogo sana ya ubongo.

Na inasemekana watumiao UBONGO wakipata jibu la swali, huacha kumlaumu Mungu kwa hilo.
Malaria huacha kuonekana kuwa anayeumwa kalaaniwa , wanampa Kloroquini au hata Muarubaini CHAUMBEA na anapona. Inawezekana pia anayeumwa kichwa akapewa tu dawa na bila ya watu kukumbuka kuomba Mungu amponye. Hata yule kibibi mwenye macho mekundu asingiziwaye uchawi kwa sababu jirani yake ana ukoma, husamehewa chanzo cha kuwa kwake na macho mekundu kijulikanapo, chanzo cha UTASA kijulikanapo kuwa si kweli KALOGWA ndio maana HAPATI MIMBA, na ni lidume lake NDILO linafyatua risasi tupu.

Swali:
  • Si inasemekana Mungu ndiye aliyeruhusu Magonjwa duniani kutokana na upotofu wa binadamu?
  • Ukisha muombea mtu apone kwa Mungu halafu akafa ingawa hukutaka afe, sini mapenzi ya MUNGU?

Lakini tusiyojua anajua MUNGU!



Binadamu ni kiumbe cha ajabu na kigumu kukielewa ujenzi wake kama tu SISIMIZI au MENDE na ujuzi wao wakustukia ulipoacha kiporo tamu tamu ingawa huoni pua zao.

Sawa basi.......!
Labda ni kweli binadamu ndio kiumbe BAABU KUBWA kuliko MENDE ,kwa mtazamo wa binadamu, ingawa hata ndege wanatushinda kwa ujuzi wa Jiografia ya dunia. (Si unakumbuka kuwa ndege wamekuwa wanasafiri kutoka bara moja mpaka jingine kwa miaka kibao kabla hata binadamu hawajajua kuwa Dunia imegawanyika katika mabara na ni ya mviringo?)




Lakini........

MUNGU ni MKUBWA!
Labda ndio maana mambo yakitushinda siye binadamu , tunadai kuwa ni MAPENZI ya MUNGU!

Na ni kweli MAPUNGUFU ya binadamu ni makubwa kiasi kwamba , BINADAMU kumuelewa BINADAMU mwenzie IMESHINDIKANA.

AU?

Swali:
  • Kama unaamini MUNGU anajua yote na amepanga yote, UNAUHAKIKA gani hajapanga kuwa MIMI na WEWE tutaenda jehanamu, kama unaamini kuna jehanamu?
  • Unapozungumzia mapenzi ya MUNGU , UNAUHAKIKA unayajua mapenzi ya BINADAMU?
Lakini tusiyojua anajua MUNGU!

Ila kama wewe huamini MUNGU, labda tusiyojua tutajua kesho!

Tatizo ni......

Hatujui kama tuna kesho.


Kwa hiyo, labda ndio IMETOKA HIYO ,kama hujui na wala hujaonja.

Na labda kama hujui na hujaonja ndio imetoka hiyo, kwani hautakuwa na kitu cha kufananishia kautamu au kauchungu upatako.

Kama hujawai kuonja vitu viwili na hauna cha kufananisha, labda ni kitu kizuri kama uambiwavyo kuwa SUBIRI mpaka UOE ndio UONJE WAKUBWA waonjavyo KWA KISINGIZIO cha KUTAFUTA MTOTO au kiburudisho.

Swali:
  • SI kuna dini maarufu zishaurizo kuwa UKISHAOA hakuna kuliacha hilo LIMTU katika SHIDA na RAHA, na kama ni maandazi na chai ni mwiko kutaka kuonja togwa kwa vitumbua?


Lakini tusilo lijua , ANALIJUA MUNGU!


Na kama kuna mbinguni , labda tujuavyo VITAKUFA na LIUBONGO hili lisababishalo tufikiri tunajua.

DUH!
Naacha hii topiki!

Ngoja nikakague Nyati kidogo.........(usishuke mbugani kama mimi nilivyofanya lakini)


Asanteni tena WADAU!
Baadhi ni hawa katika picha zangu ambao hamkunitenga.....

Photobucket
Stephano


Photobucket

Super Ngedere

Photobucket

Danny

Photobucket
Jacky


Photobucket
Vitali MAEMBE Nanenane MORO

Photobucket
Vitali- Bagamoyo

Photobucket
Jonas na Salim- ZE CLUB , Morogoro
Photobucket

JHIKOMAN


Photobucket
The CHEF--Peace of Mind

Photobucket

Morogoro

Photobucket
Bagamoyo

Photobucket
Dada Yulia

Photobucket
Heri na Mrinde

Photobucket
KC Msiba

Photobucket
Mhina wa Tanzanite na DJ Peter Moore
Photobucket
DJ Peter Moore kazini
Photobucket
Tanzanite Band kazini- Mzalendo Pub, Millenium Tower

Nakuacha na muziki aina ya QAWWALI ukiletwa na USTAD NUSRAT FATEH ALI KHAN akikupa kibao ALLAH HOO au GOD is ONE.


AU ngoja tu PUBLIC ENEMY wakupe HE GOT GAME

Read more...

Ni starehe KUANGALIA video/picha za NYUCHI au taarifa za MJUMBE wa NYUMBA kumikumi kwenye INTERNET Tanzania?

>> Friday, October 10, 2008



Starehe ya kumuangalia MNENGUAJI wa SEBENE katika Video ni kuangalia ANAVYOPEKECHA mpaka moto unawaka na SIO kuangalia AKIPEKECHA NUSUNUSU kwa sababu video ina kwamakwama.

Kwa mtafuta elimu isemekayo hutafutwa zaidi na WATUMIA internet Bongo na DUNIANI, watumiao GOOGLE kutafuta busara kwa kuandika neno kama; 'MATAKO, uke(kwa jina lake maarufu) , Uume (kwa kale kajina kake) au hata kwa jina la kitundu kitoleacho mabaki ya chakula katika mwili wa binadamu, mbele ya neno SEARCH, nafikiri elimu inanoga zaidi kama unachotafuta KITAKUJA Haraka au MARA MOJA mbele ya macho yako ili ukitolee macho, kuliko ukae kukisubiria huku ukiwa na wasiwasi na mtu aliyekaa kwenye komputa ya pembeni yako, asije akastukia kuwa unasoma BIBLIA , KORANI na sio staili za MIKAO kwenye KAMASUTRA.

Nacho jaribu kusema ni kwamba........



  1. Internet Tanzania, kwa ujumla inakwenda mwendo wa KONOKONO(Very slow)
  2. Internet Tanzania, bado ni ghali sana kwa mtu wa kawaida.

Unaweza kubisha!

Lakini, watumiaji wazuri wa internet Tanzania, wanatumia katika maofisi walikoajiriwa au wanakofanyia kazi. Kwenye internet cafe, labda kama ndio ofisi yenyewe au kwa adoado sana.

Kama huna Laptop yako na unategemea Internet cafe ,basi uwe na bahati sana kupata sehemu ambayo uki ''CLICK'' tu e-mail yako inafunguka bila kusubiria sana au kuanza kuangaika labda FIREWALL ndio inazingua kwanini hii picha KITOVU tu ndio kinaonekana, lakini huoni mpaka kule chini NJIA PANDA.

DUH!

Kwa ujumla......

Tanzania inazidi kuwa nchi ya ajabu kwa jinsi matabaka yanavyojengeka.

Sasa hivi unaweza ukajisahau kuwa uko Tanzania upande mmoja wa barabara kwa kusikia watu wanalalamika jinsi walivyokula PIZZA mbaya , halafu ukivuka tu barabara ukakuta wanao lalamika hawajui watakula wapi.

Kuna watakaokuambia kuwa ukitaka kuongea na watu watakaokuelewa , uende vijiwe fulani fulani siku hizi, hasa kama wewe ndio wale ambao moja ya tatizo lako, ni kujua nini kinaendelea New York , London au hata Beijing sasa hivi kama tu uangaikavyo kutafuta CIDER kwa sababu hupendi BIA Morogoro.


Unaweza kubisha!

Hasa wewe ambaye unanisoma hapa kwenye net hivi sasa hivi, lakini Internet bado si jambo linalojulikana na hata kutumiwa na asilimia kubwa ya watu Tanzania.

Unaweza kubisha!

Asilimia kubwa ya yaandikwayo kwenye net kuhusu Tanzania ni mambo ambayo hayawafikiii Watanzania walio wengi Tanzania.

Unaweza kubisha!


Kwa walalamikao kuwa wengi watumiao internet Tanzania hutumia kutafuta mambo ya sio kuwa na maana, ukweli ni kwamba asilimia kubwa ya hao watu ni hao waitwao watu wa maana, wenye akili kama vile wanafunzi wa vyuo, walimu , maprofesa na wenye unafuu katika maisha . Na kama sikosei labda ni mimi na wewe ndio mabingwa wa kutaka kujua;'' hakuna picha za uchi za Rais kwenye net na wala sio hivi sera za Rais na Chama chake za kuendesha nchi zinatupeleka wapi. ''

Swali:

  • Haujawahi kutafuta picha za uchi kwenye net?
  • Hivi kutafuta maswala ya ngono kwenye net ni UJINGA?
  • Ukiandika mtandaoni unafikiri ni nani anasoma?

DUH!


Naacha topiki basi!


Ingawa cha kusikitisha ni kwamba ,hapa huwa napenda kuunga video kutoka YOUTUBE na kwa mmtandao bongo , KUFUNGUKA KWAKE, KAZI IPO.

Usinielewe vibaya!
Tanzania BOMBA!

Usije ukadhani nalalamika tu kwa sababu CHUNGU inazidi TAMUTAMU . Tamutamu ni nyingi kuliko chungu Tanzania. Na naamini ni mimi na wewe tunaotakiwa kuendeleza kuongeza TAMUTAMU Tanzania.

UKWELI ni kwamba maswala ya INTERNET hapa bongo bado yanazingua !:-(



AU?
Lakini pata MOTIVATION na TONY ROBBINS



Au pumzika na Henri Salvador akupe Jazz Méditerranée




Nakuacha na BAADHI ya picha za NDUGU na MARAFIKI kiduchu tena, ambao ni baadhi ya wanisaidiao katika Shida na Raha!


ASANTENI SANA!

Unaweza kuziangalia kama huzinguki!
Samahani lakini kama unazinguka!

Photobucket
Eli

Photobucket
Kusirie

Photobucket

Hassan na CO
Photobucket

Paul
Photobucket

Gayo na Katizu
Photobucket
FJ na Masandika

Photobucket
FJ na Nderima

Photobucket

Mrinde
Photobucket
Mr DJ

Photobucket
Master Marcus

Photobucket
Sisi

Photobucket
Irioko , Manento na KIKI

Photobucket
Adelino


Photobucket
Luta

Photobucket

Mchezo wa kuigiza Kale KAKUKU

Photobucket
Mimi , Maya , Davie na Mari

WIKIENDI NJEMA!

Read more...

KAMA wewe ni PROFESA, unaweza pia KUKUBALI kusema ; ''ZIDUMU KAULI za Rais KIKWETE '',kama ZINAKUKUNA.

>> Thursday, October 09, 2008

Naamini binadamu hupenda asikilizwe na ikiwezekana aeleweke.
Bahati mbaya si wote tumebarikiwa KUJUA KITU na kuweza kufikisha ujumbe ukaeleweka na kukubalika.Ndio maana tuko wengi tunajua kuwa TUNAMPENDA na KUMTAKA yule NANIHINO, lakini jinsi yakumtupia KAULI au hata kumsababisha aje nawe migombani kwa hiari kulionja TUNDA , inakuwa SHUGHULI.

Labda ndio maana utasikia fulani kwa KUTONGOZA au mwanadada yule KWA......KIBOKO , kutokana na kuwa wengine siye, KAULI ZETU hazifiki kwa tumlengae, au zikifika, hazisababishi MTU MZIMA na akili zake aamue kuwa atakuvulia nguo, mpaka KIFICHA MBILIMBI wewe BINADAMU mwenziye BILA HAYA.

LOOOOH!

Swali:

  • Unauhakika ujumbe wako unataka umfikie nani?
  • Wewe kama Bloga unafikiri UJUMBE wako unamfikia nani?
Katika pitapita zangu ndani ya BONGO, hasa katika siku ambazo Rais KIKWETE anaongea, nimefanikiwa kugundua kuwa kuna matabaka mawili yanayo sikia tofauti kauli za huyu Mheshimiwa.

Kuna kundi la waitwao WASOMI na Kuna WASIOTAJWA JINA liashiriyo uhusiano wao na shule au masomo ya shule ambayo sio Elimu Dunia. (Sina maana kuwa kuna UKUTA unaotenganisha makundi haya mawili)

Mara nyingi Kikwete akiongea, nimestukia kuwa kuna ambao watadai kitu kama 'HE DOESN'T SOUND PRESIDENTIAL' na ambao watasikia , ' Umemsikia Kikwete mwenyewe kakuambia KABLA HUJALA lazima ULIWE!'


Kuna kitu ambacho naamini kuwa hata kama humpendi Kikwete inabidi ukichukulie maanani.
JARIBU.... Ujiulize kuwa;
  1. ' Hivi KIKWETE akiongea, anaongea na nani na anayemlenga anafikiria nini?'
  2. Je, anafikisha ujumbe atakao kwa anaowalenga?


Kabla sijaendelea......
' Kuna Rafiki yangu KWEBA pale UHOLANZI alishanikalia kooni kuhusu swala hili, kwa kudai kuwa tokea niko TANZANIA, nimegeuka CCM kutokana na mtazamo wangu kuhusu Kikwete akiongea.'


DUH!
Tuendelee....

Mimi naamini Kikwete ni Rais wa pili Tanzania baada ya Nyerere ambaye anajua jinsi ya kufikisha ujumbe wake kwa anaowalenga.
Lakini KUMBUKA ANAOWALENGA INAWEZA KUWA SIO WEWE.


Na naamini kama wewe ni mwanasiasa Tanzania au tu ni Mtongozaji , jifunze kitu kutoka kwa Kikwete , hasa katika kuchagua unamlenga nani na kujua ni kauli gani utumie ili upewe kifuko cha DHAMBARAU.

Simsifii Kikwete, lakini, asilimia kubwa ya watu kwa uchunguzi wangu ambao wanampigia kura Kikwete , Kikwete anajua jinsi ya kuongea nao na kuwafikishia kauli au hata ujumbe ambao kawaandalia.

Naamini kabisa pamoja na kuwa Kikwete yuko ndani ya Mashine Kubwa iitwayo CCM , ila bado ni mtu ambaye akikupania kuja kukukopa unaweza kumpa pesa yako ya kodi ya mwezi ujayo kwa kuamini kuwa baadaye kidogo atairudisha.


Asilimia kubwa ya niliokuwa nawatolea macho na kuwadadisi ambao ndio wapiga kura , watakuambia , hakuna mwanasiasa ambaye amebakiza Uraisi/Raisi au amelikuwa Raisi, ambaye yuko hai Tanzania, ambaye anaongea lugha yao na wanamuelewa kuliko Kikwete hivi sasa.

Profesa Lipumba na wengine wengi , kuna watu kibao niliokutana nao na kuwasikiliza kutoka vijiwe vya kila aina vya watu wa kawaida ambao ndio wapiga kura ,watakuambia husikika kama MWALIMU FULANI ambaye unasubiri tu kipindi chake kiishe anaongea na anachoongea hakikuingii MUKICHWA.

Ndio kuna watu kama Kabwe ambao wanajua kulistukia kundi walilengalo na wakajua nini na kwa staili gani watafikisha ujumbe, lakini staili ya Kabwe imekaamkao wa kunoga ukiwa nje ya Mfumo . Inaweza ikawa ngumu Kabwe akiwa Rais Kabwe au kama tu Mchungaji Mtikila baada ya kamuda fulani kuongezea maji juisi.

KUMBUKA sijasema FIKIRA za Raisi KIKWETE zidumu, lakini nafikiri kuwa unaweza kujifunza kitu hata kama wewe ni mtaalamu wa mambo ya siasa hapo Chuo kikuu kwa kumsoma tu Kikwete Hata kama ni kweli hukubaliani na aidia ya RAIS MSHIKAJI!

Sina uhakika lakini kuwa wanasiasa Tanzania huwa wanatumia WATAALAMU au UTAALAMU katika kujaribu kuangalia kundi walitakalo na jinsi ya kulifikishia UONGO au huwa wanabahatisha tu .

Naanza kuamini Mchungaji Mtikila hatumii utaalamu ndio maana kwa navyojua uwezo wake WAKUFIKISHA UJUMBE ulivyokuwa mkubwa , UJUMBE wake hata kama ule wa chuki kwa aliowaita jina ambalo laweza kuchukuliwa kama tusi ,'MAGABACHORI 'hauwafikii tena walengwa na makali yake kutokana na KUBAHATISHA KWINGI , kutegemea sana HISIA na kutokuwa na kundi maalumu lilengwalo.

Sawa, unaweza kusema kuwa ukiwa mwanasiasa Tanzania ,WALENGWA wako ni Watanzania wote.


Lakini jiulize kitu ......

  • Unafikiri Watanzania wote ni sawa?
  • Unafikiri Kikwete anaathirika nyie wasomi mkidai kuwa anapigaalinacha na anaongea kama mtoto wa kijiweni tu ?
  • Unafikiri Watanzania waliowengi wanaelewa hata kuwa Rais ni timu na sio mtu mmoja?
  • Unafikiri Watanzania wangapi wana DATA ambazo zinaweza kuwajulisha kuwa unawadanganya hata UKIWA unajulikana kama Mengi na unadai utawajaza MAPESA?

DUH!

Ngojea niache hii topiki.

BAADAYE BASI!


Lakini kama unanguvu kidogo ......

Katika pitapita nilikutana na hawa Taifa la kesho...
Photobucket
Mitaa ya Sinza
Photobucket
Huyu Dogo aliniua kwa jinsi alivyo zama kwenye kitabu. Mpaka msamaria mwema akamuomba aende akasome nyumbani maana atagongwa na magari.

Photobucket
Mitaa ya Mikocheni.
Photobucket


Ndio, nilikuwa na Bajaji kama kawa.......
Photobucket

Photobucket


Nilifika Bagamoyo kwa JHIKOMAN pia.
Mpate kidogo akiwa nyumbani na marafiki.


Ilibidi niguse bahari kwa upande wa Bagamoyo kiduchu pia.....



Photobucket
Nilikutana na Ogola .-Holiday Inn

Photobucket

Photobucket
Michuzi -kwa Wachina akiwa na LadyJAYDEE

Photobucket

Lady
Photobucket
Machozi Band

Photobucket

Photobucket

Photobucket
Agapiti

Photobucket

Magusa

Photobucket

Photobucket
Machozi Band


Swali:
  • Hivi unauhakika Profesa unayemuita Profesa anajua nini?
  • Ushawahi kukutana na Profesa mjinga?


Nakuacha na Talib Kweli akikupa kitu Hostile Gospel

Read more...

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP