Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Kama HUNA PESA ,jinunulie Mji wa GEITA kwa Kutumia PESA za DHAHABU ya GEITA.

>> Wednesday, October 08, 2008

MAAJABU ya Musa!
Geita tajiri , watu Masikini!


Kwa mji unaotoa mabilioni ya dola kwa dhahabu yake, utashangaa kuwa kuna watu wanashindwa kuwasomesha hata shule ya msingi watoto wao, maji ya shida na sana sana ni ya visima, umeme unasura mbaya kama TANESCO na barabara yenyewe ya kufikia huko ndio hivyo tena..

Labda hilo ni jambo la kawaida Tanzania. Lakini ukawaida wake utakuzingua ukijua kuwa wahusika wafaidikao na dhahabu ambao sio watu wa Geita, wamefanikiwa kuwa na maji yasiyo katika kutoka Ziwa Viktoria, umeme usio katika na barabara zenu hawatumii kwa sababu ndege na helkopta zipo.

Samahani kidogo!
Ngoja niangalie kidogo Geita!


Photobucket
(Baadhi ya sehemu ya barabara nzuri kuelekea Geita)



Sasaaaa...
Swali:

  • Inakuwaje viongozi wetu wakubali watu waje kuchimba madini hata bila ya kufaidisha maeneo wanayochimba madini?
  • Inakuwaje waweze kupitisha bomba la maji kwenda migodini na kuvuka mji ambao unamatatizo ya maji bila maji?
  • Inakuwaje hata wanasiasa washindwe kuweka mshinikizo kuwa angalau hata kama dhahabu inachukuliwa bila sisi kuhusika angalau basi hata barabara au hospitali iwe ni moja ya faida kwa wananchi wanaoibiwa dhahabu yao?


Sasaaaa....

Chakusikitisha ni kwamba, matokeo ya kuwepo kwa migodi ya dhahabu Geita, unaambiwa asilimia 10 -15% ya watu wana vijidudu vya UKIMWI. Na hiyo ni idadi ya ambao wameenda kupima. Kama unavyojua kuwa asilimia kubwa ya waendao kupima mdudu ni wale wahisio kuwa hawana mdudu. Wanaojihisi labda wameukumba tayari , huwa hawapi UKIMWI.

Swali:
  • Umepima UKIMWI?
Lakini.......

Naweza kukiri kuwa Geita mji na ni wilaya poa!
Watu wake poa sana!
Nahisi ni kwa sababu ni Watanzania ambao cha ajabu tumefikia kujisifia wenyewe kuwa siye ni watu poa sana na nchi yetu ni poa sana kuliko nchi yao.
Swali:
  • Hivi sifa si inanoga ukisifiwa na sio ukijisifia?
  • Hivi Watanzania tunajisifu tuna amani eeh?
  • Hivi unauhakika na mtu ajisifiaye mwenyewe kuwa babu kubwa , mzuri, anaakili sana au MJINGA kidoooooooogo?
  • Unauhakika anayekusifia anakigezo gani ambacho anakulinganisha nacho ili kujua wewe zaidi kiduchu katika kufanya nanihii au katika kunanihii?
DUH!

Ngoja nisicheleweshe kukuna kipele!!!!!!!

Geita ni tajiri.

Kwa wataalamu niliokutana nao ,wanakuambia kuwa ardhi ya geita ni dhahabu.
Mpaka sasa hivi kwa makadiro ya mtaalamu mmoja niliyeongea naye kwa kina , anakuambia kuwa, akipatikana mwenye pesa ya maana , mji wa Geita unaweza kuhamishwa kwa sababu uko juu ya dhahabu.

Mpaka sasa kuna migodi ya aina mbili Geita.
Mgodi ambao unachimba juu kwa juu(hakuna mahandaki) na mgodi unaochimba chini kwa chini. Sasa unaambiwa unaoingia chini kwa chini lazima utaingia mpaka mjini Geita kwa chini, kitu ambacho kitasababisha Mji usijengeke kwa juu au baadhi ya nyumba kudidimia ardhini .

Swali:
  • Ushastuki sasa kuwa kugombea UBUNGE GEITA ni DILI ?
  • Unafikiri ni kwanini wajanja kutoka nchi kibao ambao wanamamilioni wanakwenda Geita maporini ?
  • Wewe na mimi tuko Mwanza mjini au Dar?

Chakusikitisha!

  • Ukifika Geita, huwezi kuamini ndiko dhahabu inatoka.
  • Ukifika Mererani Arusha, hutaamini kuwa ndiko Tanzanite inatoka.
Bado kidogo nami nianze kukatatamaa na kuanza kuamini kama wasemao:'AMA KWELI sehemu zenye utajiri HAZITAJIRIKI.'

Swali:
  • Hivi Tanzania ni nchi masikini eeh?
  • Unajua unaweza kuinunua Mererani kwa pesa za Tanzanite, kama vile unavyoweza kuinunua Tanzania kwa pesa ulizovuna Tanzania ,mbele ya macho ya Watanzania?
  • Hivi Watanzania ni wajanja kwa sababu wana Kiswahili Mingi?

Duh!
Basi Bwana!
MIMI na WEWE, na labdaYULE ndio WATANZANIA wenyewe, ambao labda ndio kwanza bado tunahangaikia chakula kwanza tushibe. Hatujavuka hata katika kutatua tatizo la kuwa na uhakika wa chakula mezani .

DUH!:-(

Usitishike lakini!
Naamini wewe ushastuka kama mimi!
Fanyiakazi basi kuondoa kiini macho.

AU?
Duh!

Ngoja nirudi Mwanza kwa shingo upande hivyo hivyo mikono mitupu au angalau kwa picha......:-(

Photobucket
Ndani ya Lake Victoria

Photobucket

Photobucket

Photobucket
Photobucket
Hapa ndipo TEPANYAKI ndani ya TILAPIA ukitaka kula kijapani ndani ya Mwanza
Photobucket
Kiki ndani ya Tilapia

Photobucket

Photobucket
TILAPIA.( Picha kutoka katika Pool Bar ambako hukawii kugongana na wachukua Dhahabu za Geita ambao barabara zetu mbovu hawajawahi kuzitumia .)

Ngoja nimuache SEAL atupe kile kibao alicho kikarabati cha SAM COOKE A Change is Gonna Come

Read more...

MTAZAMO wa maendeleo ya TANZANIA kwa kutembelea CHOO au VYOO ndani ya TANZANIA!

>> Tuesday, October 07, 2008

Sehemu za kutunzia kinyesi au kupunguzia LITA au kwa JINA maarufu ``CHOO´´, chaweza kukunong'oneza kitu kuhusu watumiaji wa faragha hizo hata kama watumiaji hutumia sehemu za kuheshimika hizi kwa matumizi ya kujamba tu. (Samahani kwa kutumia lugha chafu kama neno kujamba, ninamaanisha kutoa hewa inayonuka.)


Lakini.....

Sehemu babu kubwa yenye choo kichafu , hakina maji au hata makokoneo, kinaweza kuwakilisha nini wamiliki wa sehemu au waendao sehemu wanaona ni muhimu.Ingawa ni kweli kinaweza kuonyesha tu hali halisi ya ugumu au uhadimu wa kupatikana vitu fulani kama maji ya kutawadhia, debe la kutupia takataka au majivu ya kusaidia mambo fulani katika choo cha shimo, wakati Kitimoto, Bia fulani, Konyagi, Bavaria,Festival,Savanna, John Walkers......... mpaka Shampeni zipo kwenye shelfu kwa sababu ndio biashara yenyewe.

Sibishi !
Tanzania inaendelea!

(Mimi na wewe si ndio Watanzania wenyewe)


Lakini bado Tanzania kuwa na kitambi , kwa mtazamo wa wengi ni mali na sio tatizo la kiafya !
Kwa haraka haraka, nina maana .....

  • Bado KULA au KUWA NA CHAKULA ni ujanja na sio kitu cha uhakika
  • Bado tunatishana kwa muonekano.
  • Bado ukiendesha Benzi na hauna kitu benki au hata pesa ya mafuta, unaweza kuopoa ngoma kuliko ukiwa na pesa ya benzi na unapakia Bajaji.
  • Bado wewe unavutia kwa muonekano wa vazi la nje ingawa chupi chafu halafu imechanika kidooooogo.
Swali:
  • Hivi mimi na wewe tumeendelea?
Samahani kidogo!
Hebu nikuwekee baadhi ya picha za Mabloga wa Kibongo niliokutananao hivi karibuni.....
Photobucket
Mzee wa Rundugai Samaki Samaki -Mlimani City
Photobucket
Araway Kikaho Kwa Mama Perina -Morogoro

Photobucket
Photobucket
Rasta Luihamu na Mzee wa Rundugai Samaki Samaki -Mlimani CITY
Photobucket
michuzi Ofisini
Photobucket
Nikiwa na Mkuu wa Wilaya- Breakpoint katikati ya Muji

Photobucket

Rasta eeh! Nakusikiliza. Mlimani City
DUH!

Tuendelee....

Lakini sitaniii!

Matumizi ya SIFA za nguvu za akili , busara, ufanyajikazi bora, tabia nzuri, mpenda amani , sio mwizi nk, unaweza kuyashinda kwa Matumizi ya SIFA zitokanazo na unavaa nguo gani , unaendesha gari gani, unapesa bila mtu kujua unazipataje na unawatishia watu maisha kwa staili za amri zako uzitumiavyo kujihakikishia unastahili heshima.

SAMAHANI KIDOGO!
Hebu tuwacheki kidogo hawa simba niliowafumania maeneo walivyo kuwa na uhakika.Hawahitaji kukutisha ili uwaheshimu.



Photobucket

Photobucket


Sasaaaa........

Swala la chumba kipi kiwe kisafi zaidi katika nyumba chaweza kukusababishia ukasafisha zaidi chumba chakulia chakula zaidi kuliko jikoni chakula kipikiwako kwa sababu unaamini wageni hawafiki huko.

Lakini.....


Labda ni UKWELI ukiwa na njaa, cha muhimu ni chakula tu .
Maswala ya utaenda choo wapi huwa ni mbele kwa mbele au ni mambo ya baada ya kula.
Labda hata pale nyuma ya mlango wa nyumba ya jirani kama kuna giza, panaweza kufaa katika matumizi ya kushusha kilo au hata lita ukidhani hutashikwa chupi haijasitiri.

Lakini nisikuzingue!.............

KWA kifupi sehemu nyingi ziitwazo BAABU KUBWA Bongo, bado zinatimiza haja za mwenye njaa na hazijafikia kujali Mwenye Njaa akishakula atakwenda haja wapi.

Unaweza kunibishia , lakini naamini asilimia kubwa ya waitwao matajiri Bongo , bado wana tabia za wenye njaa. Mwenye njaa asiye nauhakika na tajiri mwenye uhakika unaweza usiwatofautishe kutokana na kufanana kwao kisaikolojia. Utakuta tajiri mzima naye hajiamini, aliyeelimika(tajiri wa elimu) naye hajiamini. Atataka kukutisha akijua unatishika na hakuna kujiamini ambako kunaweza kumfanya asione sababu ya kukutisha kwa sababu anajua hauwezi kumfanya kitu kwa sababu wewe huna. Mwenye nacho anaweza akawa anashindana na wewe usiyenacho ili tu ajisikie kuwa anacho badala ya kwenda hatua ya mbele itakayo mfungulia yeye mambo mengine na kukusaidia usiyenacho kuvuta hatua mbele badala ya kupiga makitaimu.

Mimi na ogopa utajiri wa GARI KUBWA, SEBULE SAFI chooo KICHAFU!:-(
Swali:
  • Kama matajiri bongo wanatabia za wenye njaa unafikiri masikini wenye njaa wawe na tabia gani?
  • Au mwenzangu unaweza kutofautisha tabia za tajiri mwenye njaa lakini anauhakika na kula na masikini mwenye njaa na asiye na uhakika na kula ndani ya bongo ,ukiwakuta wanawania ubwabwa?

Samahani turudi kwenye Choo....

Kirahisi sehemu ambazo tokea maili kumi zinaonyesha kuwa Mafisadi hawaendi hapo, basi uwe na uhakika kuwa unaweza kupata matatizo ya uchambie nini au hata utumie staili gani ya kupunguza kilo kama sio lita . Na ukitoka huko msalani ,sina uhakika utanukia a pafyumu gani kwenye vazi au puani.

Swali:
  • Ushastukia kuwa harufu mbaya inaweza kukuganda puani tu mpaka ukafikiri unanuka kichoochoo mwili mzima na kumbe bado unanukia manukato?
  • Hivi akinadada wastaarabu waendao sehemu babu kubwa walioko kwenye hedhi mnakumbukwa hata huko katika vyoo vya sehemu baabu kubwa sehemusehemu za kuhifadhi mambo ya kikubwa ya kike baada ya kubadilisha?(Naamini sehemu nyingi meneja ni mwanamume ambaye labda hajawahi hata kuona chupi ya dada yake imeanikwa)
Swali jingine ngojea nimuulize George W Bush

DUH!

Tuendelee.........au tuanze upya.......


Kama umezoea choo cha kukaa ukienda cha shimo, unaweza ukawa na matatizo ya kulengesha nanihii! Na labda miguu itakuuma.

Kwa Mtanzania Mweusi kama MIE, kama umezoea kuwa wengine ndio wanavyo, wanajua na wanastahili, hutashangaa kujikuta unashuhudia tu wenzako nyumba ya jirani wanavyojinoma katika mambo wewe uhisiyo kuwa hustahili kwa sababu zako fulani kama vile sehemu yenyewe ni kwaajili ya wenyenazo na labda hata Watanzania Wazungu au Wazungu Wazungu, hapo ikiwa kama umeshawazoeaWatanzania Wahindi,Wahindi , Watanzania Waarabu,Waarabu au WatanzaniaWachina, Wachina , ambao kuna maeneo mengi ndio wanaaminika kuwa wanavyo, wanaweza, au hata kustahili.

Utasikia kuwa bongo ni Tambarare kwa watu fulani!
NI KWELI HIYO!

Lakini muonekano wa utambarare wa bongo unastaili zake.
Bado kwa mengi ambayo utayaita ni tambarare , yuko atakayeona ni sawa tu na kuona hoteli nzuri lakini choo kichafu na hakuna maji! Hasa kutokana na mapungufu ambayo yanatatulika kama watu watakuwa makini kukuna muwasho kwenye kipele.

Tatizo ni kwamba ni MIMI na WEWE tunaohitajika katika kutatua na wala sioYULE
:-(


KAZI IPO!
USICHUKIE!Mimi nawaza tu hapa MKUU, kinamna!

Pata kidogo picha nyingine zangu na wadau kinamna kama hujali .
Samahani lakini!
AU?

Photobucket
Papa manento

Photobucket

Photobucket
Rose Garden hapa. FJ unakitenga kijiwe hiki lakini!

Photobucket

Photobucket
Maisha Club na Muzee Tiba...

Photobucket
Rasta Haji -Rock Garden
Photobucket
Mimi na Kaka zangu

Photobucket
Merinyo- Africa Sana

Photobucket
Bro Davie na Luta


Baadaye Basi!

Twende South Africa kidogo tujikumbushe mambo na Mzimbabwe/Mzambia/Msauzi DOROTHY MASUKA katika tamutamu ya zilipendwa iitwayo..Kwa Nhingirikiri

Read more...

(Tangazo)WELCOME to MOROGORO and TANZANIA

Dear Visitor,

Welcome to Morogoro and Tanzania.



NAPAC is a company based in the Morogoro Municipal, now offers a variety of cultural programmes for adults and special programmes for children, upon request.

Since Tanzania is multicultural society, these programmes are aimed at providing information on various cultural topics. Below are the choices of programmes. Every session is designed to take two hours per day; the whole course is designed to be ten hours.

1. Lectures on various cultural matters in Tanzania

o Cultural based information o Cultural affairs consultation o Cultural based tour guiding

2. Traditional African (Tanzanian) music classes
* Theory and practical sessions * The sound of drums and their occupational and occasional roles o Other instruments such as xylophones, bamboo flutes, shakers etc.



3. Traditional and contemporary African (Tanzania) dance classes

o Theory and practical session o Dance movements and their occupational and occasional roles o Making of African dances (choreography)

4. Classes on the use of community based African theatre for communication of educational or promotional programmes, this is for both urban and rural areas. Suitable for NGOs and Development Institutions.

NOTE: This can also be a very good way to practice your Kiswahili while being treated culturally! Hotel reservation can be made for those far from Morogoro upon request.

For more information on the time tables and registration, please contact us through:

Physical Address: MOECO building-Mazimbu area. Turn right before the main gate to Sokoine University (Solomoni Mahlangu Cumpus)

Call us through: 0787-292982, 0714-679162, OR 0732-930019
Email: napactz@yahoo.com,

Mail Address: P. O. Box 1446, Morogoro, Tanzania, EA Welcome to Morogoro The heart of Tanzanian cultural hospitality

Read more...

Raymond H. Hall seeks YOUR support

>> Monday, October 06, 2008

I am writing this special e-mail to seek support for my brother's (Raymond) hospital bill.

My brother has been ill for the past one year, treatment was not the best back home in Tanzania and he was referred to India. However, at the time of his referral his condition was very critical so much that he could not be flown straight to India. He had to be air-lifted to Aga Khan Nairobi (Kenya) to stabilize his condition before being taken to India. The Doctors in Nairobi have done a wonderful job despite the fact that he had to have both his legs amputated to save his life.They did only what was best for him. He did not have to go to India again. The Doctors themselves say that Raymond is a Testimony... a True Miracle!

Raymond is currently doing fine although he is a bit depressed and the doctors feel that it is only dawning to him now what has actually happened, and especially the amputation of his second leg which was done without his consent as he was not in a conscious state to make a choice...it was a matter of life and death! He has had some Professional Counselling since the 30th Sept 2008 which we hope and believe will be fruitful.

Raymond had a Medical Cover (AAR) of Tshs. 100m (USD. 100,000) through his employer (Plan International) which has been exhausted. The Excess Bill comes to about USD. 80,000. As a family we are seeking other means available of raising the outstanding balance to enable us settle the bill as soon as possible.

Being close friends, I/we plead for your financial support (whatever the amount) towards the Medical Cost Outstanding. Do not hesitate, nothing is too small everything is much appreciated. I have also approached my Parish and explained the situation to them. I am optimistic assistance is on the way.

Thanking you in advance for your anticipated support. I/we cannot thank you enough but God will reward you accordingly.

Kind Regards,

M.H. Magori



Raymond is my blood brother, Our First Born in a family of 3

His number is +255 754 884 591 / Mama: +255 766 05 38 06

He is currently in Aga Khan Nairobi, Kenya. Both are reachable on their local numbers.

He is now communicating well so anybody may try to call his number.

Full Name: RAYMOND HENRY HALL
WORK: PLAN INTERNATIONAL (T) LIMITED

Read more...

NDANI ya sekunde fulani TANGU nilipoandika MARA ya MWISHO hapa KIJIWENI!

>> Sunday, October 05, 2008

Mambo vipi wadau!
Shikamoo wakubwa!

Nimerudi kinamna!
Nimejifunza na naendelea kujifunza kinamna.
Nilifurahi , kusikitika na kutokuwa na uhakika wa nini mshawasha kinamna.
Nilifiwa na kushuhudia waliozaliwa kinamna.


Ngoja nikuache na baadhi ya picha za msiba wa babu yangu aliyefariki akiwa na miaka 105.

Photobucket

Bibi akimuaga BABU kwa mara ya mwisho.

Photobucket

Photobucket

Mpaka sasa nimefanikiwa kutembelea Mikoa TISA ndani ya BONGO nyoso.

  • Dar es Salaam
  • Morogoro
  • Kilimanjaro
  • Pwani
  • Dodoma
  • Singida
  • Tabora
  • Shinyanga
  • Mwanza
Kwa ambao hamjafika kwa muda mrefu, kuna mabadiliko mengi karibu kila sehemu ndani ya BONGO.

Yapo mazuri na mabaya kama ......

Tofauti ya masikini na tajiri inazidi kukua.
Simu za mkononi si ajabu kuziona mpaka vijijini.
Barclays Bank inashindana na benki za Kitanzania mpaka kijijini kwenu na huwezi kumtisha mtu na Credit Card yako.

Kwa Dar es Salaam si muda mrefu kutakuwa na Wachina wafundishao watoto wako TUISHENI ya lugha ya KISWAHILI. Kwani sasa kuanzia Wamachinga, Mwenye Baa ya kwenye kona ya mtaani kwenu, mpaka mwenye kumiliki migodi, tayari anaweza akawa ni yule Mchina uliyempita bila kumuangalia juzi kwa kisingizio huvutiwi na Wachina hata ukiwa unaota zile ndoto uotazo wakati muda mrefu umepita bila ya kutekenywa, kuguswa, kufanya mazoezi ya kutengeneza watoto au hata kuvunja amri fulani iliyokatazwa kwenye baadhi ya vitabu maarufu vitakatifu na YULE .

Swali:
  • Hivi ni kweli asilimia kubwa ya watu weusi hawavutiwi kimapenzi na Wachina ?
  • Hivi unavutiwa na bidhaa za Kichina lakini eeh?

Nitaendelea zaidi kukusimulia kuhusu BONGO baadaye!



Hebu pumzika na Ryan Leslie akiwa Studio akikutengenezea kibao DIAMOND GIRL

Dar es Salaam BAJAJi kibao kama unaogopa taxi na ndio usafiri wangu...
Photobucket

Baadaye basi!

Asanteni wote ambao bado mnanitembelea hapa kijiweni!

Asanteni marafiki wote !

Nitaweka baadhi ya picha zenu niliokutananao baadaye!

Tulia na ASA basi akukumbushe JAILER

Read more...

Niko TANZANIA , najifunza KWA muda KIDUCHU kunanihii!

>> Wednesday, July 30, 2008

Niko BONGO nyoso , bado sijajulia.

Unawezakunipata kwenye namba:+255765855382

Usipoangalia, NITAKUJIBU!
Nikichelewa kurudi hapa kijiweni, NAOMBA MSAMAHA!

BAADAYE BASI!

Read more...

SIKUBALIANI na WEWE kuhusu UKOKO, dini au M-BINYO kama tu NIKUKUBALIAVYO kuhusu MAISHA!

>> Monday, July 21, 2008

WEWE si YULE!

Kuna ambacho YULE anaweza akakudanganya UKAAMINI!
:-(

Wakati unamkubalia, unaweza ukawa unauhakika ANAKUDANGANYA ingawa unapenda tu SAUTI ya SENTENSI.

Wakati unakataa , unaweza ukawa na sura ya FURAHA ingawa labda UNGEKUBALI, ungekula PILAU, kama wewe ni MPENZi wa PILAU.

SWALI:

  • Unafikiri umekataa mara ngapi kuliko ulivyokubali KUONJA?
  • Unafikiri unakubali kuliko KUKATAA ukiNYOLISHWA?
Naacha basi hii topiki!
-------------------------------------------------------------------------------------------------
Ngoja Morgan HERITAGE watukumbushe kurudi kazini katika LONGOLONGO iitwayo READY TO WORK.

au SANTANA ambaye pia amenisaidia KUPITILIZA wiki hii atukumbushe ENZI za WOODSTOCK 1969 katika SOUL SACRIFICE.


BAADAYE BASI!
AU?

Read more...

JEMADARI HAMU!

>> Sunday, July 20, 2008

Ukiwa na HAMU!
Akili yako itajaribu kukutimizia HAJA za HAMU.


Ukiwa na haja, ni rahisi kufikiria kuwa kuna staili BOMBA za kutimiza HAJA yako kama YAKE.


Kutimiza haja yako ,inawezekana kuwa ni WEWE PEKEE unaweza kusawazisha kwa sababu UKWELI ni kwamba haja yako unaijua vizuri wewe MWENYEWE.

Swali:

  • UNAFIKIRI kuna staili nzuri ya kuongelea haja ambayo inadaka yote yaliyo kwenye MIMBA ya HAJA yako?

SIKU NJEMA!
------------------------------------------------------------------------------------------------

NAKUACHA na JESS MATADOR akija na dawa iitwayo Décalé Gwada

AU pata picha fulani KADHAA zangu na WADaU kadhAA!
Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket


Photobucket

Photobucket


Photobucket



Photobucket

Photobucket


Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket
Photobucket

Photobucket


Photobucket



Photobucket


Photobucket




Photobucket



Photobucket

Photobucket

Photobucket



Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket


Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket
PUMZIKA na NINA SIMONE kiduchu akija na dawa iitwayo FOUR WOMEN

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket


Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket


Photobucket

Photobucket

Photobucket


Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket


Photobucket

Photobucket

Photobucket
SAMAHANI!

FilmLOOP inanizingua kiduchu, KWAHIYO inawezekana ikawa nimeweka picha NYINGI kadhaa wa kadhaa na HEADMASTER huwa anafikiria kuwa SI mchezo MZURI kuweka PICHA ambazo labda haziFUNDISHI KIPENYO ni sawasawa na nini katika TUNDU.


:-(

Lakini nitajaribu KUSAWAZISHA!

Ziruke tu PICHA kama zinaKUZINGUA!


HALAFU ni KWELI .....


MARY J BLIGE, SHAGGY , DJ CLIFF na.....
......wamenisaidia sana kupitiliza, kama UONAVYO kwenye PICHA......
:-(



Mpate SHAGGY aendeleze DAWA iitwayo BONAFIDE MSICHANA

Read more...

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP