Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Roho ya Kwanini!

>> Friday, April 06, 2007

Sijui kwanini
Nani na nani ana nini
haiepuki mimi na ninyi
Ya washawasha maini

Matajiri kwa masikini
roho ngumu kama nini

Lakini kwanini?

Ni nini kiini?

Wataka yote maini

Tugaiane kwa makini
Yatutosha wote hiyo nini
Sasa, nini?
Na:Simon Kitururu

--



6 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Anonymous 2:37 am  

Kuna washairi waliojifichaficha huku bloguni. Huwa wanajitokeza hapa na pale. Huko nyuma tulikuwa na magwiji wa ushairi ila wakatokomea. Haya, tuendeleze fani hii ya kucheza na lugha na maudhui.

Simon Kitururu 12:02 pm  

@Ndesanjo:si utani. huwa kuna baadhi ya siku hujisikia kucheza na lugha.La kini ugwiji sijaufikia. Sijui kwanini sioni mashairi ya Mwandani siku hizi.Kwa sababu yeye kwa mtazamo wangu ni gwiji.

mjengwa 2:54 pm  

Ongera Kaka haina haja ya kuwa gwiji.. kwangu mimi shairi lako ni super tu.

Anonymous 4:50 pm  

Umesema sawa Simon. Mwandani gwiji. Mashairi yake niliyapenda zamani kabisa kabla hata blogu kuzaliwa.

Mwandani: tunakusihi...tupe aya.

Je aya hizi za mwanablogu wa Kenya umeziona? Wakenya hawajui Kiswahili? Tazama aya hizi uniambie:
http://serinaserina.wordpress.com/

Simon Kitururu 1:44 am  

@Halifa: asante kwa kunitembelea. Nashukuru kwa kunipa moyo katika anga ya ushairi.
@Ndesanjo: Nimecheki pale.Mara nyingi ni rahisi kwa Watanzania kudai kuwa Wakenya hawajui kiswahili. Nahisi hii ni sawa tu na Wakenya wapendavyo kudai Watanzania hawajui Kiingereza. Hili jambo ukiliamini utashangaa mwenyewe jinsi gani unavyoweza ukawa umekosea.

Simon Kitururu 1:45 am  

@Halifa:Tunasubiri blogu yako.

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP