Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Sukari HUZUNI, kabla ya KULIA!

>> Thursday, December 18, 2008

Kifungua kinywa ni huzuni
...kama chakula NI mwenye huzuni KULIA

Furaha kushoto ukilia ..
...ingawa huzuni si lazima KULIA.

Ingawa kwa furaha......
....unaweza KULIA.

Huzuni ni siri ya utamu wa furaha
...ukiacha KULIA

Utamu wa huzuni,
...chukua muda kabla ya KULIA.


_______________ __________________ _____________

Nawaza tu MKUU!

Swali:

  • SI unajua huwezi kuharakisha HUZUNI hata kama UNATAKA au UKO TAYARI kulia?
Tubadili topiki au tupumzike kwa kumsikiliza Malcolm Gladwell atumie mfano wa SPAGETI katika : What we can learn from spaghetti sauce



Au Lord Kitchener aje na - Old Lady Walk Ah Mile



Au tu Lord Kitchener aendeleze tu muziki wa aina ya SOCA katika "kaka roach"...

8 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Unknown 5:52 am  

AMBIERE, E VAVA,
NIMEPITA TENA LEO ALFAJIRI KUKUJULIA HALI.
KAZI NZURI NA IMEJAA UBUNIFU WA HALI YA JUU.

Simon Kitururu 6:59 am  

@Ambiere:E vava hi aho!:-)Asante kwa kutonitenga hapa kijiweni!

Yasinta Ngonyani 10:36 am  

Simon! kuna watu wanaweza kulia kwa sababu wana furaha, machozi ya furaha. Au nimechemsha?

Simon Kitururu 10:38 am  

@Yasinta:Ndio maana nimeandika...:


´´Ingawa kwa furaha......
....unaweza KULIA.''

Christian Bwaya 11:45 am  

Kazi nzuri sana. Nimependa tungo yako kaka. Inanitafakarisha. Nitarudi kusema nilichowaza.

Simon Kitururu 2:52 pm  

@Bwaya:Karibu tena Mkuu na asante kwa kutonitenga!Nashukuru kama imegusa kitu Mkuu!

Mzee wa Changamoto 7:09 pm  

Haya tena nanukuu. Na safari hii ni kutoka kwa Lucky Dube aliyesema "tears can not bring you joy, but joy can bring you tears. Even though i cry today, i will not hide it. It's for a different reason. JOY" (na hili si watu wa malezi na jinsia zote wanaweza kukubaliana nalo hivyo kama hudhani ni kweli usibishe maana yawezekana ni malezi na jinsia yako vikuaminishivyo hivyo). Lakini ukweli utabaki uleule kuwa ukiona mtu analia usianze kumpa pole. Pengine ahitaji hongera. Na usimpe hongera pia maana yawezekana ahitaji faraja. Kuna haja ya kutafakari kabla hujaamua kutatua tatizo maana si mara zote twawa sahihi katika kuamua juu ya tuonayo, kwani namna tuonavyo .......

Simon Kitururu 8:13 am  

@Mzee wa Changamoto: Si utani!

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP